09/11/2023
KIWEKEE AZINA KWA SIKU YA TAABU YAKO
"Utukufu wangu utakuwa mpya kwangu, Na uta wangu hurejezwa upya mkononi mwangu."
Ayubu 29:20
- Kila ukitendacho duniani unaniwekea hazina Yako
- Kusitiriwa kwa mtu kunategemea Jinsi Yeye anavgosimama kusitiri wengine
- Kiwango chako Cha kuwatendea wengine kinaamua Nini utendewe na kwa Kiwango Gani
- Kadri mtu anavyowatendea watu yaliyo mema ujiwekea ulinzi, akiba ha mema na Azina ya kurejeza utu wake
- Biblia inasema Ezekia alimkumbisha Mungu mema aliyowahi kiyatenda, Mungu akamsikia akamwongezea Miaka 15
Isaya 38:3
Kumbe wema ni akiba na ubaya ni akiba pia.
Mwandishi wa kitabu Cha Ayubu anajaribu kutukumbusha Tumaini la Ayubu siku ya TAABU yake
- Ayubu alitumainia wema wake kwa watu Kuwa msaada kwake siku ya TAABU yake.
Na alitarajia kurudishiwa utukufu na heshima aliyokuwa nayo mara dufu kwa azina aliyoiweka kwa watu
Anasema
"Utukufu wangu utakuwa mpya kwangu, Na uta wangu hurejezwa upya mkononi mwangu. Ayubu 29:20
KWA NINI AYUBU ALIPATA UJASIRI KUTARAJIA
KURUDISHIWA HESHIMA NA UTUKUFU ALIOKUWA NAO?
Ayubu 29:11
11 Maana sikio liliponisikia, ndipo likanibarikia; Na jicho liliponiona, likanishuhudia.
12 Kwa sababu nalimwokoa maskini aliyenililia; Yatima naye, na yule asiyekuwa na mtu wa kumsaidia.
13 Baraka yake yeye aliyekuwa karibu na kupotea ilinijia; Nikaufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
14 Nalijivika haki, ikanifunika, Adili yangu ilikuwa k**a joho na kilemba.
15 Nalikuwa macho kwa kipofu, Nalikuwa miguu kwa aliyechechemea.
16 Nalikuwa baba kwa mhitaji, Na daawa ya mtu nisiyemjua naliichunguza.
17 Nami nilizivunja taya za wasio haki, Na kumpokonya mawindo katika meno yake.
21 Watu walitega masikio kunisikiliza, na kungoja, Wakanyamaa kimya wapate sikia mashauri yangu.
22 Hawakunena tena baada ya kusikia maneno yangu; Matamko yangu yakadondoka juu yao.
23 Walikuwa wakiningojea k**a kungojea mvua; Wakafunua vinywa vyao sana k**a mvua ya masika.
24 Walipokata tamaa nikacheka nao; Na mwanga wa uso wangu hawakuuangusha.
25 Niliwachagulia njia, nikakaa k**a mkuu wao. Nikakaa k**a mfalme katika jeshi la askari, Mfano wa awafarijiye hao waombolezao.
KATIKA MAANDIKO HAYO TUNAPATA SIFA ZA AYUBU ZILIZOSABABISHA KURESHWA
KWA UTUKUFU NA HESHIMA YAKE
1. Aliwasaidia maskini na Yatima
2. Aliwafariji wajane na kuwatunza
3. Alikuwa mteteze wa haki na alisimamia maadili
4. Alifanya kazi ya advocacing, kuwasemea wasioweza kusema, kuwaonesha na kuwaongoza wasioweza kuona Ili wapate kuona.
5. Aliwasaidia wahotaji, Tena si tu wale aliowajua bali hata wale hasiowajua aliwasaidia
6. Alitetea waliodhurumiwa na kulinda haki zao
7. Aliwashauri watu wakamsililiza
8. Alicheka na waliokata tamaa wakapata tumaini la kurejezwa kwa furaha yao
9. Aliwaongoza watu katika mema hata walayafikia.
10. Aliwafariji waombolezao.
KURURUDISHWA KWA UTUKUFU KWA AYUBU KULITEGEMEA SANA AZINA YAKE NA IVUMILIVU WAKE WAKATI WA TAABU.
Rejea
Mathayo 19:21
Marko 10:31
Luka 18:22
Mathayo 6:14-20
HITIMISHO
".. jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi; "
Mathayo 6:20