Talanta za BWANA YESU

Talanta za BWANA YESU Wokovu ni matumizi ya kipawa ulichonacho, ushuhuda, kutangaza habari njema na kuishi kitakatifu

Anaandika Jennifer Mgendi JINSI YA KUFANYA USAFI AKILINI MWAKO1. Kila siku linda akili yako dhidi ya mawazo mabaya.2. Us...
11/05/2026

Anaandika Jennifer Mgendi
JINSI YA KUFANYA USAFI AKILINI MWAKO
1. Kila siku linda akili yako dhidi ya mawazo mabaya.

2. Usikae na maumivu moyoni kwa muda mrefu, yajengee uponyaji.

3. Epuka watu wenye sumu wanaochafua amani yako ya ndani.

4. Kusamehe ni njia ya kusafisha moyo na akili.

5. Usifikirie sana mambo usiyoweza kubadilisha.

6. Jaza akili yako kwa maneno mazuri na yenye tumaini.

7. Pumzika vizuri, akili iliyochoka hujaza mawazo mengi.

8. Omba na kumtumaini Mungu unapohisi umelemewa.

9. Ondoa hofu kabla haijajenga utando ndani ya maisha yako.

10. Amani ya kweli huanza pale unapojisafisha ndani kwanza.

TABIA 10 MBAYA ZILIZOZOELEKA MAKANISANI MWETU: 1️⃣ Kuchati au kubofya bofya simu wakati wa Ibada. 2️⃣ Kukataa kuketi mah...
05/05/2026

TABIA 10 MBAYA ZILIZOZOELEKA MAKANISANI MWETU:

1️⃣ Kuchati au kubofya bofya simu wakati wa Ibada.

2️⃣ Kukataa kuketi mahali umeelekezwa na wahudumu uketi.
Hii inaonyesha jinsi gani ulivyomkaidi na hufuati utaratibu.

3️⃣ Upo kwenye Ibada ghafla unakimbia nje kupokea simu Huku ikiita kwa sauti za juu.
Hii ni kukosa utii kwa Mungu wako.

4️⃣ Kuchelewa Ibadani.
Kuna watu hii imekua tabia sugu.

5️⃣ Kusinzia, kunong’onezana au kupiga story za chinichini wakati wa Ibada.

6️⃣ Kukaa chini bila sababu za msingi wakati wa vipindi vya Kusifu na kuabudu.
Hii ni kudharau huduma lakini pia inaonyesha huna maadili kwa waongoza vipindi.

7️⃣ Kuangalia saa ya ukutani au saa ya mkononi wakati mahubiri yakiendelea.

8️⃣ Kutoshiriki kikamilifu kwenye huduma mbalimbali za kanisani.
Mfano wenzio wanaimba wewe unaangalia watu huyu kavaaje nk.u

9️⃣ Kuondoka Ibadani kabla Ibada haijaisha.
Tabia hii inaondoa uwepo kwa waumini wengine walio ibadani. Kumbuka pia ibada ni Alfa na Omega

🔟 Kukusanyika nje ya kanisa wakati wa Ibada mkijadili mambo yenu.

Apostle Arome Osayi Talanta za BWANA YESU Pastor Imran Fazal & Mehwish Imran

23/04/2026

1 like. "pokea maonyo ......"

SIFA ZA WATU WENYE DAMU GROUP “O”*BLOOD GROUP “O”*-Huwa Mara nyingi wanajitahidi kuwa mahodari na mashujaa katika Mambo ...
19/02/2026

SIFA ZA WATU WENYE DAMU GROUP “O”
*BLOOD GROUP “O”*
-Huwa Mara nyingi wanajitahidi kuwa mahodari na mashujaa katika Mambo Tofauti.
-Mara zote kiu yao ni kuwafurahisa na kuwapendeza watu wengine in wenye Moyo wa Uongozi.
-Wenye kiu ya kuona Rafiki zao wanakuwa wenye furaha wakati wote.
-Sio wagumu wa Mabadiliko,wako tayari kubadilika.
-Ni wenye mawazo mapana na ya wazi.
-Sio wagumu kifikra na ni Marafiki Wazuri(Comrades).

*FAIDA ZAO*
-Ni wenye Ujasiri,
Wanashindana katika mambo mengi,
Mfano:mambo ya maendeleo.
-Hufanya kazi sana na kwa Bidii.
-Ni waaminifu.
-Wanaweza kujieleza.
-Ni Marafiki wazuri.
-Wanasamehe.
-Mitazamo yao no Chanya.
-Huweza kuhisi au kuona Mambo hata kabla hayajatokea(wana maono).
-Ni wadadisi.
-Ni watu wema na Watoaji!.
*MAPUNGUFU YAO*
Mara nyingine wanaweza kuwa wenye Fujo!.
-Wanapenda Sifa.
-Huvutia vitu Upande wao.
-Wanaepuka na kukwepa majukumu yao.
-unaweza kuona k**a wanaigiza Mambo lakini wako serious.
-Wakitaka, Wametaka mpak wapate ndio watatulia!
-Ni rahisi kuwaondoa kile wanachokifanya.

*MAISH YA KIJAMII*
-Ni marafiki wazuri unaoweza kuwategemea.
-Ni waaminifu.
-Ni wawazi ,ingawa Mara nyingine wanaweza kukuudhi.
-Wakati mwingine wanahitaji kusikilizwa wao tu.

*KAZINI*
-Wana kiu ya Mafanikio.
-Hufanya kazi kwa Bidii ingawa hukatishwa Tamaa na kupoteza hamasa ya kuendelea na kazi.
-Ili wafikie Malengo Yao ni Vyema Wakasimamiwa kwenye wanayofanya badala ya kuacha wafanye wenyewe.
-Wengine hawapendi kabisa kusimamiwa.

*MAHUSIANO YA KIMAPENZI*
-Ni watu wanaoweza kuonyesha Mapenzi ya wazi kwa wale wanaowapenda,
Ila ni vyema Ukafahamu kuwa watu hawa hutarajia Upendo wa jinsi ile ile wao wanavyoonesha Upendo kwako bila hivyo utakosana nao.
*NB*
-Wanaaminika kuwa na Tabia za kijeshi.
-Wengi wao kwa asili ni watu wa kupenda Michezo.
-Wanaaminika kuwa ni watu Wema na walio tayari kusaidia Mtu yeyote.
-Katika Uchangiaji Damu watu hawa Wanaweza kumpa damu mtu yeyote yule.
wapendelea na kujisikia Raha wanapokula Nyama.(Meet lover)-Protein.

Kula chakula cha kiroho
14/02/2026

Kula chakula cha kiroho

Mavazi yamebeba maana kuu 3 1:.Tunavaa mavazi ili kustiri miili yetu, yaani watu wasione utupu wetu;2:. Mavazi ni mawasi...
10/02/2026

Mavazi yamebeba maana kuu 3
1:.Tunavaa mavazi ili kustiri miili yetu, yaani watu wasione utupu wetu;

2:. Mavazi ni mawasiliano, maana makahaba tuna watambua kwa mavazi yao yasiyo stiri mwili;
Wanafunzi tunawatambua kwa mavazi yao,Maaskari tunawatambua kwa mavazi yao, maana mavazi ni mawasiliano;

3: Mavazi ni mapambo,kwa hiyo tunavaa mavazi ili tupendeze huku tukistiri miili yetu,kwa hiyo hatuvai ili mradi tumevaa:

Pia tambua kuwa kila mavazi yana sehemu yake ya kuvaliwa, kuna mavazi ya michezo,kuna mavazi ya kuogelea,kuna mavazi ya kulalia, kuna mavazi ya kumtega mume wako chumbani;

sasa shida inaanzia hapa pale mtu anapovaa mavazi ya michezo na kuja nayo kanisani,au mtu kuvaa mavazi ya chumbani na kuja nayo kanisani, au mtu kuvaa mavazi ya kumtega mume wake chumbani na kuja kuwatega wanaume kanisani;

hii ni hatari sana kwa kizazi hiki cha uzinzi na zinaa, maana kizazi kimekosa aibu na busara,

unakuta mtu anajua fika anaenda kanisani halafu anavaa mavazi ya kikahaba, unakuta mtu anajua fika anaenda kanisani halafu anavaa mavazi ya michezo na kwenda nayo kanisani ili lengo lake awaangushe wanaume dhambini;

Tena ana biblia mkononi na hana hata mashipa wa aibu hii ni hatari sana kwa kanisa la sasa;

Maandiko matakatifu yanasema

Wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujistiri pamoja na adabu nzuri 1 Timoth 2:9-10

Tena maandiko matakatifu yanasema

wanawake wasivae mavazi yampasayo mwanaume na mwaume asivae mavazi yampasayo mwanamke kumbukumbuku la torati 22:5

lakini cha kushangaza wanawake wengi huvaa mavazi ya wanaume huku wakijiita wakristo hii ni hatari sana;

Inatupasa tuishi sawa sawa na maandiko matakatifu na sio kuishi sawa sawa na dunia,kwa maana dunia inapita na tamaa zake lakini Neno la Mungu halitapita kamwe

YESU NISAIDIE KUTOA KIBANZI KATIKA JICHO LANGU,,,,,!Luka 6 ;42---45¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯⁴² Au, utawezaje kumwambia ndugu yako, Ndug...
03/02/2026

YESU NISAIDIE KUTOA KIBANZI KATIKA JICHO LANGU,,,,,!

Luka 6 ;42---45
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁴² Au, utawezaje kumwambia ndugu yako, Ndugu yangu, niache nikitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako, nawe huiangalii boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe, ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi kilichomo katika jicho la ndugu yako.
⁴³ Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri;
⁴⁴ kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana, katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu.
⁴⁵ Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.

Ilikuwa ni wakati wa kuandaa msosi wa mchana, jua kali kwa ncha zake hii ilinifanya nitembee huku naangalia chini k**a mtu anayehesabia hatua

Bpiiiiiip... bpiiiiiiip...! Honi za onyo zililia . Macho yangu aliitanzama ile range rover nyeusi kuanzia chini hadi kwenye taa za mbele ... huku miguu ikikosa nguvu .. maamuzi yalichelewa kutoka..

gonga tu huyo ....!
Makusudi hayo...! Alisikika mpita njia wa baiskel,, aliyetupita hapo bado nimeduwaa...! Miguu ilikuwa mizito sana. Kutokana na kustuka na honi ya gari ile!

Dogo usiwe na makuu .. wapishe watumia barabara waendelee na mambo yao,, sogea hapa... alikuwa ni mbaba mmoja wa k**a hamsini hivi...mwenye masharubu na ndevu nyingi ila sio ndefu.
Macho yangu yalihama kutoka kwenye kumtazama usoni na kuhamia miguuni ambapo ilikuyo ilikuwa na suruali ya kaki mpauko tena mtumba ngumu viatu vya wazi na kimoja kilishapita kwa fundi ...

Hujambo rafiki,,,, unaitwa nani,,,? Haloo,,,!Aliniongelesha. Eh naam,,,! Niliitikia kwa kulopoka..." kwani una shida? Hapana sina shida!! Nilijibu kabia hajamaliza hata kuuliza,

Okay naitwa gaspari ni mwinjilisti wa kipentekoste kutoka mtaa wa nne kulia kwetu.. samahani ( inaendelea kesho.....)

2 Timotheo 4 (Biblia Takatifu)¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯² lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea,...
29/01/2026

2 Timotheo 4 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
² lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.
³ Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti;

23/01/2026

Kwa Calvary Temple Arusha – Nipo kwenye mfululizo wa ufanisi! Nimekuwa shabiki bora kwa miezi 4 mfululizo. 🎉

20/01/2026

omba Mungu wakati wote walio kwa shetani hudumu katika ibada zao kila dakika!!¡! Talanta za BWANA YESU TAG YOUTH - CA's ATUGE

Address

Ng'enza
Iringa

Telephone

+255712051702

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Talanta za BWANA YESU posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Talanta za BWANA YESU:

Share