01/08/2019
AUGUST2019.
MWEZI WA MUNGU KUTEMBEA KATIKATI YETU.
"K**a Mungu alivyosema,ya kwamba,Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea,nami nitakuwa Mungu wao,nao watakuwa watu wangu."(2koritho6:16b).
Huu ni mwezi wa mtembeo wa Mungu katika maisha yako.Mungu anataka atembee kupitia miguu yako,anataka kugusa vitu mbalimbali kwenye maisha yako na ya wengine kupitia mikono yako.!
Ukiwa mwenyewe tu ukitembea hakuna matokeo,ukishika vitu wala huoni badiliko lakini kwa imani ukijua kuwa si wewe tena bali ni Kristo ndani yako,ukitembea Mungu anatembea,ukigusa vitu Mungu ameshika,ukisema ni Mungu amesema,utaona matokeo ambayo hujawahi kuyaona,na siyo wewe tu utakaye yaona bali hata wanaokuzunguka wataona!
Ngoja nikuoneshe matokeo ya Yesu kuwa anatembea:-
Katika nchi ya wagerasi kulikuwa na mtu mwenye mapepo mengi(region)na makao yake yalkuwa makaburini na hakuna mtu aliyeweza kumfunga tena ,hata kwa minyororo.kwasababu alikuwa mara nyingi kwa pingu na minyororo lkn aliikata ile minyororo,na kuzivunjavunja zile pingu na minyororo,wala hakuna mtu aliyeweza kumshinda!
Lakini siku Yesu amakanyaga tu katika aridhi kwa miguu yake biblia inasema"Alipomwona Yesu kwa mbali ,alipiga mbio,akamsujudia"!(marko5:1-13).
Yesu akianza kutembea ndani yako impact yake itasababisha yaliyoshindikana kwa wanadamu yawezekane kwako,Mungu amekufanya kuwa jawabu la matatizo ya watu katika Jina la Yesu.
Unaweza ukatumia ufunuo huu kuombea nyumba yako,ofisi yako,mashamba yako,na chochote kwa kutembea maana ukikanyaga si wewe unayekanyaga bali ni Kristo ndani yako,na kwa njis ya Kristo,miguu yako imepewa mamlaka ya kukanyaga nge na yoka na nguvu zote za yule adui(luka10:19),kila mahali zitakapokanyaga nyayo za miguu yako nimewapa kumiliki(joshua1:3)-miguu yetu imepewa umiliki kwa jina la aliye ndani yetu.Miguu yetu inafanya mazingira yasiyovukika yaweze kuvukika mbele yako kwa jina la Yesu,mfano katiƙa mto yordani maji yalitii wakavuka salama"basi hao waliolichukua hilo sanduku,walipofika yardani,na nyayo za makuhani waliolichukua sanduku zilipotiwa katika maji ya ukingoni,ndipo hayo maji yaliyoshuka kutoka juu yakasimama,yakainuka yakawa kichuguu mbali sana....
Watu wakavuka kukabili yeriko"(yoshua3:15-17).
Nakuombea kwa jina la Yesu,kokote utakapokanyaga wakajue kuwa umefika siyo watu tu bali ata ufalme wa giza wakajue kuwa amafika aliyemkuu kuliko sisi na wakusujudie siyo wewe ila Yesu Kristo ndani yako,Kila mikono yako itakachogusa,Mungu amegusa,ukinena ni Kristo amenena,maneno yako yawe na neema huku yakiwa yamekolea munyu yamfae kila muhitaji katika jina la Yesu.
Yesu Kristo atembee ndani yako,katikati yako na kwa watu kupitia wewe katika jina la Yesu!
Shalom.