16/04/2022
*JUMAMOSI KUU*
*Kusubiri katika Ukimya!*
Kwa kifo chake, viumbe vyote vimefanywa upya. Dunia ilitetemeka, giza likaijaza nchi yote, jua likafifia (Lk 23: 44-45) kila kitu kipo katika utulivu. Leo Kanisa linatualika tusubiri kwenye kaburi la Bwana, tukitafari mateso yake, kifo na kushuka kwake kuzimu, tukisubiri katika sala na kutarajia ufufuko wake. Mama Maria yupo nasi, yeye ambaye aliyaweka yote moyoni mwake (Lk 2:19). Leo hii katika miji yetu, kuna kelele za kila aina. Angani kuna kelele, barabarani kuna kelele, kelele nyumbani na hata katika Makanisa. Na zaidi ya yote kuna kelele katika akili zetu na mioyo yetu. Tunapaswa kujenga ukimya, kwa sababu neno la Mungu halisikiki katika kelele za siku hizi. Hakuwezi kuwa na uhusiano wa kweli na Mungu k**a hamna ukimya. Siku hizi watu wanaogopa ukimya hata katika sala. Katika ukimya tutagundua mengi sana kuhusu nafsi zetu, udhaifu wetu, na uzuri wetu. Tusubiri na Maria katika kaburi la Yesu kwani Yesu anatuambia kitu cha pekee na muhimu kabisa. Pengine ni kitu ghaniβ¦..? Ngoja nimsikilize kwa makini kabisa. Pengine ananiambia mimi, mwanangu NAKUPENDA SANA