Agape Bethel Majengo

Agape Bethel Majengo Karibu Ujifunze Masomo ya Biblia katika Ukurasa Huu. Tafadhari SHARE ukurasa huu Neno lifike Mbali 🙏

07/05/2023

SOMO: MAOMBI NA SADAKA
Zaburi 24:1-6
Mithali 8:34
Wakorintho 14:40
Yohana 16:13-14
Zaburi 1:1-3
Hesabu 12:1...

23/04/2023

SOMO: PANGA CHINI YA USIMAMIZI WA MUNGU
Mathayo 6 : 25-34
25 Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?

26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?

27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti

29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri k**a mojawapo la hayo.

30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?

31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.

Zaburi 37 : 3-4
3 Umtumaini Bwana ukatende mema, Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.

4 Nawe utajifurahisha kwa Bwana, Naye atakupa haja za moyo wako.

Luka 10 : 41....

PLAN UNDER THE GUIDANCE OF GOD

09/04/2023

HE HAS RAISEN

Luke 24:1-12, 50-53
Mathew 28:16-20

02/04/2023

THEME: CONFESION OF TRUST IS TO THE LORD
SOMO: KUKIRI IMANI YETU KWA MUNGU

Zaburi 121 :1-8
1 Nitayainua macho yangu niitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi?

2 Msaada wangu u katika Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.

3 Asiuache mguu wako usogezwe; Asisinzie akulindaye;

4 Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

5 Bwana ndiye mlinzi wako; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.

6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.

7 Bwana atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.

8 Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.

Isaya 40 : 10
Tazameni, Bwana Mungu atakuja k**a shujaa, Na mkono wake ndio utakaomtawalia; Tazameni, thawabu yake i pamoja naye, Na ijara yake i mbele zake.

Kumbu kumbu la Torati 28 : 6
Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo.

Psalm 128 : 5-6
Bwana akubariki toka Sayuni; Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;

Naam, ukawaone wana wa wanao. Amani ikae na Israeli.

Zaburi 89:11

THEME: JESUS WILL ASTOUND YOUSOMO: YESU ATAKUSHANGAZATeacher: Pastor J LekeniLuka 5 :1-11 (Luke 5 : 1 -11)1 Ikawa makuta...
12/02/2023

THEME: JESUS WILL ASTOUND YOU
SOMO: YESU ATAKUSHANGAZA
Teacher: Pastor J Lekeni

Luka 5 :1-11 (Luke 5 : 1 -11)
1 Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,

2 akaona vyombo viwili vimekaa kando ya ziwa, lakini wavuvi wametoka, wanaosha nyavu zao.

3 Akaingia katika chombo kimoja, ndicho chake Simoni, akamtaka akipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano ali chomboni.

4 Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.

5 Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.

6 Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika;

7 wakawapungia mikono washirika wao waliokuwa katika chombo cha pili, waje kuwasaidia; wakaja, wakavijaza vyombo vyote viwili, hata vikataka kuzama.

8 Simoni Petro alipoona hayo, alianguka magotini pa Yesu, akisema, Ondoka kwangu, kwa kuwa mimi ni mtu mwenye dhambi, Bwana.

9 Maana alishikwa na ushangao, yeye na wote waliokuwa pamoja naye, kwa sababu ya wingi wa samaki walioupata;

10 na kadhalika Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, waliokuwa washirika wa Simoni. Yesu akamwambia Simoni, Usiogope, tangu sasa utakuwa ukivua watu.

11 Hata walipokwisha kuviegesha pwani vyombo vyao, wakaacha vyote wakamfuata.

Wafilipi 4:6 (Philipians 4:6)
Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.

Zaburi 34:4 (Psalm 34:4)
Nalimtafuta Bwana akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote.

Zaburi 37:5 (Psalm 37:5)
Umkabidhi Bwana njia yako, Pia umtumaini, naye atafanya.

Zaburi 55:22 (Psalm 55:22)
Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza, Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.

Zaburi 123:1-4 (Psalm 123:1-4)
1 Nimekuinulia macho yangu, Wewe uketiye mbinguni.

2 K**a vile macho ya watumishi Kwa mkono wa bwana zao K**a macho ya mjakazi Kwa mkono wa bibi yake; Hivyo macho yetu humwelekea Bwana, Mungu wetu, Hata atakapoturehemu.

3 Uturehemu, Ee Bwana, uturehemu sisi, Kwa maana tumeshiba dharau.

4 Nafsi zetu zimeshiba mzaha wa wenye raha, Na dharau ya wenye kiburi.

THEME: LOVE AND DEVOTION FOR JESUS (UPENDO NA KUJITOA KWA YESU)Tech: Pastor J LekeniUpendo unaoendelea na wenye nguvuMar...
29/01/2023

THEME: LOVE AND DEVOTION FOR JESUS (UPENDO NA KUJITOA KWA YESU)
Tech: Pastor J Lekeni
Upendo unaoendelea na wenye nguvu

Marko 14 : 1-9

1 Baada ya siku mbili ilikuwa sikukuu ya Pasaka, na mikate isiyochachwa; wakuu wa makuhani na waandishi wakatafuta njia ya kumk**ata kwa hila na kumwua.

2 Kwa maana walisema, Isiwe kwa wakati wa sikukuu, isije ikatokea ghasia katika watu.

3 Naye alipokuwapo Bethania, nyumbani mwa Simoni mkoma, ameketi chakulani, alikuja mwanamke mwenye kibweta cha marhamu ya nardo safi ya thamani nyingi; akakivunja kibweta akaimimina kichwani pake.

4 Palikuwa na watu waliochukizwa katika nafsi zao wakisema, Kwani kupoteza marhamu namna hii?

5 Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa dinari mia tatu na kuzidi, wakapewa maskini. Wakamnung'unikia sana yule mwanamke.

6 Yesu akasema, Mwacheni; mbona mnamtaabisha? Amenitendea kazi njema;

7 maana sikuzote mnao maskini pamoja nanyi, na kila mpendapo mwaweza kuwatendea mema; lakini mimi hamnami sikuzote.

8 Ametenda alivyoweza; ametangulia kuupaka mwili wangu marhamu kwa ajili ya maziko.

9 Amin, nawaambia, Kila ihubiriwapo Injili katika ulimwengu wote, na hili alilotenda huyu litatajwa kwa kumbukumbu lake.

Mwanamke alijitoa na kuonesha upendo wake kwa Yesu
Hakuna mtu alimuunga mkono wala kumtia moyo. Unaweza fanya vizuri kwa Bwana na asiwepo hata mmoja wa kukutia moyo, usifadhaike endelea na upendo wako kwa Bwana Yesu bila kujali

THEME: HE SEND HIS WORD TO HEALSOMO: ANATUMA NENO LAKE ILI TUPOBEMungu anatuma neno lake ili tuponeLuka 7 : 11-17(Luke 7...
15/01/2023

THEME: HE SEND HIS WORD TO HEAL
SOMO: ANATUMA NENO LAKE ILI TUPOBE
Mungu anatuma neno lake ili tupone

Luka 7 : 11-17(Luke 7 : 11-17)
11 Baadaye kidogo alikwenda mpaka mji mmoja uitwao Naini, na wanafunzi wake walifuatana naye pamoja na mkutano mkubwa.

12 Na alipolikaribia lango la mji, hapo palikuwa na maiti anachukuliwa nje, ni mwana pekee wa mamaye ambaye ni mjane, na watu wa mjini wengi walikuwa pamoja naye.

13 Bwana alipomwona alimwonea huruma, akamwambia, Usilie.

14 Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, Kijana, nakuambia, Inuka.

15 Yule maiti akainuka, akaketi, akaanza kusema. Akampa mama yake.

16 Hofu ikawashika wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, Nabii mkuu ametokea kwetu; na, Mungu amewaangalia watu wake.

17 Habari hii yake ikaenea katika Uyahudi wote, na katika nchi zote za kando kando.

Yesu alikikataa kifo maana haukuwa mda wa kijana Yule kuzikwa; Sio mda wako kuingia kaburini, una Nguvu ya kukipinga kifo ambazo ni Jina la Yesu. Kwa kila shida yako mwite yeye naye atayanyoosha mapito yako.

Yesu anapoingia katika Maisha huondoa huzuni ya mwanzo na kuleta Furaha iliyotoweka

Zaburi 107 : 20(Psalm 107:20)
Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao.

SOMO: MIMI NI RAFIKI YAKO SINTA KUDHURU(YESU NI RAFIKI YAKO, HATO KUDHURU)Mwl : Pastor James LekeniMathayo 26:17-2617 Ha...
08/01/2023

SOMO: MIMI NI RAFIKI YAKO SINTA KUDHURU
(YESU NI RAFIKI YAKO, HATO KUDHURU)
Mwl : Pastor James Lekeni
Mathayo 26:17-26
17 Hata siku ya kwanza ya mikate isiyotiwa chachu, wanafunzi wake wakamwendea Yesu, wakamwambia, Ni wapi utakapo tukuandalie uile Pasaka?

18 Akasema, Enendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie, Mwalimu asema, Majira yangu ni karibu; kwako nitafanya Pasaka pamoja na wanafunzi wangu.

19 Wanafunzi wakafanya k**a Yesu alivyowaagiza, wakaiandaa Pasaka.

20 Basi kulipokuwa jioni aliketi chakulani pamoja na wale Thenashara.

21 Nao walipokuwa wakila, alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu atanisaliti.

22 Wakahuzunika sana, wakaanza kumwuliza mmoja mmoja, Ni mimi, Bwana?

23 Akajibu akasema, Yeye aliyetia mkono wake pamoja nami katika kombe, ndiye atakayenisaliti.

24 Mwana wa Adamu aenda zake, k**a alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule k**a asingalizaliwa.

25 Yuda, yule mwenye kumsaliti, akajibu, akasema, Ni mimi, Rabi? Akamwambia, Wewe umesema.

26 Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega,

Yesu alimtambua Yuda kuwa ndiye atakaye msaliti, lakini hakumdhuru, aliendelea kuishi naye.
Yapo Mambo tunayomkosea Bwana lakini hatuachi, anaendelea kuwa upande wetu na kutupigania.

Yesu angepoteza tumaini tangu mwanzo kwa kuwa alijua binadamu hawaaminiki lakini hakufanya hivyo, alilijua jukumu lake.

Huwezi jificha kwa Mungu maana yeye hutambua nia ya ndani ya mwanadamu, Yesu alifahamu moja kwa moja Yuda ndiye msaliti ingawa Yuda alifanya siri.

MUNGU AKUBARIKI. 🙏🙏

SOMO: CHUKUA HATUA ANZA UPYA NA BWANA.Mwl: Askofu Dk Jonas Mkane Mhusika wa somo letu: YakoboMwanzo 32:22 - 3020 Tena se...
01/01/2023

SOMO: CHUKUA HATUA ANZA UPYA NA BWANA.
Mwl: Askofu Dk Jonas Mkane
Mhusika wa somo letu: Yakobo

Mwanzo 32:22 - 30
20 Tena semeni, Tazama, mtumwa wako, Yakobo, yuko nyuma yetu. Maana alisema, Nitamsuluhisha kwa zawadi inayonitangulia, baadaye nitamwona uso wake; huenda atanikubali uso wangu.

21 Basi ile zawadi ikavuka mbele yake, naye mwenyewe akakaa usiku ule kambini.

22 Akaondoka usiku ule akawatwaa wakeze wawili, na vijakazi wake wawili, na wanawe kumi na mmoja, akavuka kivuko cha Yaboki.

23 Akawatwaa, akawavusha mto, akavusha na vyote alivyokuwa navyo.

24 Yakobo akakaa peke yake; na mtu mmoja akashindana naye mweleka hata alfajiri.

25 Naye alipoona ya kuwa hamshindi, alimgusa panapo uvungu wa paja lake; ukateguka uvungu wa paja la Yakobo alipokuwa akishindana naye.

26 Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki.

27 Akamwuliza, Jina lako n'nani? Akasema, Yakobo.

28 Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda.

29 Yakobo akamwuliza, akasema, Niambie, tafadhali, jina lako? Akasema, Kwa nini waniuliza jina langu? Akambariki huko.

30 Yakobo akapaita mahali pale, Penueli, maana alisema, Nimeonana na Mungu uso kwa uso, na nafsi yangu imeokoka.

Yakobo alitambua kuwa adui wa maisha yake ni yeye mwenyewe.

MAMBO YA KUJIFUNZA KUTOKA KWA YAKOBO
1. Alikumbua juu ya ahadi ya kulindwa na Mungu. Mwanzo 32:9

2. Alionyesha Shukrani maana alijua Hakustahili.

3. Aliamua kuomba Ukombozi kwa Mungu.

Yakobo hakutaka kubaki k**a alivyokuwa, maana jina lake lilijaa undanganyifu, aling'ang'ana Bwana Mpaka alipo pata Baraka.

Usiendelee na Madhaifu, Mng'ang'anie Bwana aondoe madhaifu Yako.

Yakobo alipo pata baraka aliona utukufu wa Bwana katika maisha yake.

SOMO: KWA AJILI YETU MTOTO AMEZALIWAIsaya 9 : 6-76 Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uw...
25/12/2022

SOMO: KWA AJILI YETU MTOTO AMEZALIWA

Isaya 9 : 6-7
6 Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.

7 Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.

Lect: Proff Solomon MwagisaTHEME: THE POWER OF MORNING                 PRAYERSEarly morning prayer means pray before 4 A...
18/12/2022

Lect: Proff Solomon Mwagisa
THEME: THE POWER OF MORNING PRAYERS
Early morning prayer means pray before 4 AM morning.

WHY TO PRAY?
1. To express our needs to God
2. Make prosperity in our ministries
3. Gives victories life
4. To hear voice of God speaking to Us

WHT TO PRAY EARLY MORNING?
1. Making our God to be number one
2. Putting our plans of the day before God
3. Easy to touch God in morning
4. Many God's people were praying in the morning.

Mark 1 : 35-36
35 Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko.

36 Simoni na wenziwe wakamfuata;

Job 1 : 5
5 Basi ilikuwa, hapo hizo siku za karamu zao zilipokuwa zimetimia, Ayubu hutuma kwao akawatakasa, kisha akaamka asubuhi na mapema, na kusongeza sadaka za kuteketezwa k**a hesabu yao wote ilivyokuwa; kwani Ayubu alisema, Yumkini kwamba hawa wanangu wamefanya dhambi, na kumkufuru Mungu mioyoni mwao. Ndivyo alivyofanya Ayubu sikuzote.

Luke 21 : 38
38 Na watu wote walikuwa wakiamka mapema waende hekaluni ili kumsikiliza.

SOMO : WAKATI MWAMINI AANGUKAPOMaandiko : 1 Wakorintho 1012 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke....
11/12/2022

SOMO : WAKATI MWAMINI AANGUKAPO

Maandiko : 1 Wakorintho 10
12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.

Marko 14:26-31,66-72
26 Nao walipokwisha kuimba walitoka kwenda mlima wa Mizeituni.

27 Yesu akawaambia, Mtakunguwazwa ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu; kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo watatawanyika.

28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.

29 Petro akamwambia, Hata wajapokunguwazwa wote, lakini siyo mimi.

30 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, Leo, usiku huu, kabla ya kuwika jogoo mara mbili, utanikana mara tatu.

31 Naye akazidi sana kusema, Ijaponipasa kufa nawe, hata hivyo sitakukana kamwe. Na wote wakasema vile vile.

66 Na Petro alikuwa chini behewani; akaja mmoja wa vijakazi wa Kuhani Mkuu,

67 akamwona Petro akikota moto; akamkazia macho, akasema, Wewe nawe ulikuwapo pamoja na yule Mnazareti, Yesu.

68 Akakana, akasema, Sijui wala sisikii unayoyasema wewe. Akatoka nje hata ukumbini; jogoo akawika.

69 Na yule kijakazi akamwona tena, akaanza tena kuwaambia waliosimama pale, Huyu ni mmoja wao.

70 Akakana tena. Kitambo kidogo tena wale waliosimama pale wakamwambia Petro, Hakika u mmoja wao, kwa sababu u Mgalilaya wewe.

71 Akaanza kulaani na kuapiza, Simjui mtu huyu mnayemnena.

72 Na mara jogoo akawika mara ya pili. Petro akalikumbuka lile neno aliloambiwa na Yesu, Kabla ya kuwika jogoo mara mbili, utanikana mara tatu. Na alipolifikiri, akalia.

1 Petro 3:15
Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.

1Petro 5 : 6-11

6 Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;

7 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

8 Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa msh*taki wenu Ibilisi, k**a simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.

9 Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.

10 Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.

11 Uweza una yeye hata milele na milele. Amina.

Address

Kanisani
Iringa
51101

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Agape Bethel Majengo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Agape Bethel Majengo:

Share