13/02/2026
NENO LA SIKU
Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha
Tarehe 13/02/2026
SOMO: NI WAKATI WA KUPOKEA BARAKA ZAKO USISINZIE
Waefeso 5: 14-17 βHivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza. Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si k**a watu wasio na hekima bali k**a watu wenye hekima; mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwanaβ.
Wakati wa Maachilio au Marejesho ya baraka zako, uponyaji, miujiza na mengine uliyotamani kwa muda mrefu umewadia. Amka kaa katika nafasi yako ili iwe rahisi kuyapokea kwa maana Mungu hatakawia na watu watajua umekutana naye. Kuwa macho ni ile hali ya kukiri Neno, kuomba bila kukoma, kutangaza Ushindi uliopata katika Yesu Kristo na kudumu katika imani.
Kusinzia ni kulala pasipo ridhaa yako kwa sababu ya nguvu inayokuzuia ushindwe kukaa macho. K**a ilivyo unaposinzia kimwili, unakuwa haujui kinachoendelea; ndivyo ilivyo kiroho unapotazamia jambo lakini unashindwa kulisubiri huko ni kusinzia. Unaweza ukasinzia katika ndoa, matoleo, kusoma au kuomba kwa sababu ya hiyo nguvu. Kusinzia huletwa na uchovu, uvivu, kutokumaanisha na kutokuzingatia jambo unalotazamia. Unasinzia kwa kuishi maisha ya kujichanganya, mashaka na kutoliamini Neno la Mungu.
Baraka au tarajio lako linapochelewa unasinzia kwa sababu moyo wako unashindwa kutazamia au kusubiri. Shetani akijua kuwa unao ufahamu kuhusu Mungu, ufahamu huo ni tishio kwake kwani anakuwa hana uwezo wa kukuzuia wala kukushambulia kwa maana ufahamu huo unakupa kuwa macho kiroho. Hivyo ili aweze kukupata atakuletea nguvu inayopingana na huo ufahamu ili usinzie kiroho, ukate tamaa na kupoteza changamko lako ili aweze kufanya kile anachokitaka katika maisha yako.
Ili kupokea uliyoandaliwa amka uwe macho wala usikubaliane na maisha duni uliyonayo maana huo siyo mpango wa Mungu kwako. Mungu anakusubiri uamke ili akupe taraja lako.