01/04/2024
Tarehe 31/0/2024
Na,
Rev. Zephrine Kahigwa
Ujumbe: Ushindi ulio katika Ufufuo wake Kristo
Mathayo 28:1-28, Luka 23:50-56
Utangulizi;
👉🏾Ufufuo wa Yesu Kristo ni moja ya kweli kuu za Injili. Yesu ni tofauti kabisa na mtu mwingine yeyote na utofauti wake mkubwa ni kule kufufuka na kuacha kaburi.
👉🏾Kufufuka kwake kunathibitisha kuwa, yeye ndiye mwana wa Mungu kweli kweli.
📌Matukio Makuu yanayotokana na Ushindi ulio katika kufufuka kwake Yesu;
1. Yeye Yesu, aliizika mauti na akaleta uzima alipofufuka kutoka kwa wafu.
Yohana 11:25 - 26, 32-44
👉🏾Uzima wa Yesu unafanya mambo mengi mbali na kutuingiza mbinguni, hapa duniani bado uzima huu hufanya vitu vingi vya kutufanya tuishi k**a washindi.
2. Yeye alibeba dhambi zetu ili sisi tusiishi katika dhambi tena.
Warumi 5:8, 6:6
👉🏾Dhambi hubebwa nau hukaa ndani ya utu wa kale
👉🏾Utu wa kale, ni utu wa mtu ambaye hajaokolewa, utu huu wa lake hufa pamoja na kristo msalabani ili mwamini apokee uzima mpya ndani ya Kristo.
Wagalatia 2:20
👉🏾Sisi tuliosulubiwa pamoja na Kristo, sasa tunaishi pamoja naye katika maisha yake ya ufufuo. Yeye Yesu akifanyika, chanzo na kiini cha mawazo, akili, maneno na matendo yetu.
👉🏾Ule utumwa wa mwili kutumikia dhambi, umevunjwa. 2Wakorintho 5:17,
👉🏾Ili uhamishwe kutoka kwenye utumwa huo wa dhambi, ni lazima mtu akubali kununuliwa na Kristo kwa damu yake. Ukisha kununuliwa, utawajibika kuishi maisha ya yule (yaani Mungu) aliye kununua (lazima ubadilike). Ufunuo 5:9-10
👉🏾Kuanzia sasa waamini wanapaswa kutokukubali maisha yaliyopita kutawala maisha yako ya sasa ndani ya Kristo (ishi katika maisha yaliyobadilika na yanayodhihirisha ushindi aliotupatia Yesu)