24/10/2025
Bwana Yesu asifiwe hapo ulipo ndugu yangu!
Tunamshukuru Mungu tena kwa kutupa nafasi ya kusikia kutoka kwake.
Ujumbe Mungu aliyotupa leo, unasema
Usiruhusu nuru yako izimishwe na nyakati unazopitia.
shetani anashida na nuru yako kuliko kile unachopitia. Anatafuta kuzima nuru yako iliafanye kazi kwa uhuru bila kuonekana.
Mara nyingi huju panya wanafurahi kwa kiasi gani taa ikizimila nyumbani. Kwasababu taa nitishio kwa shuhulizao.
Tutazame Ile;
Mathayo 5:14-16, unasema hivi
[14]Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.
[15]Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.
[16]Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
Nataka useme maneno haya wakati tunaweka utangulizi wa somo hili,
Sema "Mimi ni nuru mahali Mungu aliponiweka na ulimwengu mzima."
Mistari hii inatuwekea muunganiko mzuri sana kati ya nuru na matendo na utukufu wa Mungu. Kwa muunganiko huu, unaona nuru inamatendo (yanayoitwa mema). Ukifanikiwa kuzima nuru umezima matendo yanayotegemea nuru kuonekana.
Kwahiyo ukizima nuru unazima na matendo yake, yanayofanya Mungu asionekane na atukuzwa na watu. Unapoamua kuficha nuru unaficha matendo ya nuru ili nuru isiwafikia watu.
Ujawahi kuona mtu akiwa na rafiki zake na wanfanya vitu ambavyo havijakaa sawa, Ili asigombane nao au kutendana nao anaamua kutokufanya au kusema kile kinachopingana na dhambi yao.
Au mtu akiwa na shida anaamua kuficha nuru yake asijulikana k**a ameokoka Ili apate msaada.
Hivi ni vitu vipo na madhara yake ni makubwa.
Haijalishi nyakati unazopitia hakikisha Nuru yako haizimikia kabisa. Kumbuka u apopoteza nuru yako unapoteza na muelekeo wa maisha yako. Bwana Yesu asifiwe Sana.
Tutazame jambo la,
1) Wako wanaotegemea nuru yako, hata k**a wote mnapita mahali pa kufanana.
Mungu anapokupa kuwa nuru mara nyingi siyo kwaajili yako peke yako. Hivyo ni muhimu kuwa makini na mamuzi unayofanya unapopita kwenye nyakati ngumu.
Tutazame mfano huu wa Yesu akiwa malabani pamoja na wale wanyang'anyi wawili, ile Luka 23:39-43
[39]Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.
[40]Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
[41]Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
[42]Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
[43]Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.
Unaposoma habari hii, unamuona Yesu amesulubiwa msalabani pamoja na Wany'ang'anyi wawili, tunaweza sema wote walipita kwenye hali za kufanana.
Wote tunajua Yesu ni nuru na mwokozi wa ulimwengu, usingefikiri angepita kwenye mazingira ya namna hiyo pamoja na watu aliopita nao.
Sasa tazama wale wanyang'anyi walichokiona kwa Yesu waliekuwa wanapita nae kwenye nyakati ngumu, ule mistari wa [39]"Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi".
Mmoja aliamua kumtukana akifikiri ile kwamba anapita mahali wanapopita hawezi kuwamsaada kwao pia.
Sasa angalia Yule wa pia kitu alisema, " [40]Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
[41]Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
[42]Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. "
Wa pili alijua kabisa hata k**a tunapita na Yesu katika mazingira ya kufanana, hatufanani nae kunamsaada aliobeba kwaajili yetu . Alimjua Yesu anapita anapopita kwaajili yao waokolewe, kwahiyo alijua anaweza kumsaidia katikati yamazingira yaleyale wanayopitia.
Alijua wote wanapita kwenye giza lakini Yesu ni nuru yao.
Unajua ni kazi kuomba masaada kwa mtu amabae wote mnapita kwenye hali ngumu. Lazima Mungu akufunulie uone kilichondani yake. Na ukiona mtu anaomba msaada kwa mtu ambae anapita kwenye hali hiyo hiyo, ujue kunakitu maeona kwake k**a msaada.
Yesu angeamua kunyamazi ombi la yule mnyang'anyi kwasababu ya hali anayopitia, lakini alijua alichobeba kwaajili yao. Hivyo hakuruhusu Hali anayopitia izimishe kile alichobeba kwaajili yao.
Ile kwamba unapita kwenye hali ngumu haina maana huwezikuwa nuru kwa wengine. Ndiyo maana ni lazima kulinda Sana moyo wako, Ili Hali unazopitia isizimishe Nuru yako na watu wanaokutegemea wakakosa msaada wa Mungu. Ukosoma habari ya Naomi na wakwe zake kwenye kile kitabu cha Ruthu 1-2, utaona Naomi alijaribu kufanya kosa la kujaribu kumzuia Ruthu asipate msaada Mungu alioweka ndani yake.
Kunawatu Mungu anawapitisha pamoja na wewe kwenye hali mbayo uliyonayo siyo kwasababu wamekosea au walistahili kupita hapo, bali kwasababu yako upate msaade wa kutoka. Sasa unajua ni rahisi kuwadharau kwasababu wote mnapita kwenye hali za kufanana, ukafikiri hawezi kuwa masaada kwako. Hili ndolokosa alilofanya yule mnyang'anyi namba Moja! Usije ukaingia kwenye kosa k**a hili.
Unajua ni kwanini Yule wa kwanza alianza na kumtukana Yesu? Ili tujue yule wa pili hakuangalia yule wa kwanza anamuonaje Yesu au anamsemaje Yesu , lakini alisikia Mungu anachomsemesha moyoni mwake juu ya masaada alioweka ndani ya Yesu.
Yule mwizi wa pili angeungana na mwenzake asingepata masaada kabisa wa kutoka.
Jifunze kusema k**a yule ndugu alieponywa na Yesu,
"........Kwamba yeye ni mwenye dhambi sijui. Najua neno moja, kuwa mimi nalikuwa kipofu na sasa naona. "Yohana 9:25.
Ni rahisi sana ukawatazama watu Mungu aliowabebesha masaada kwaajili yako kwa maneno ya watu wanayosema juu yao. Jifunze kusikia moyoni mwako, Mungu anachokuwekea kuhusu mtu aliembebesha msaada wako.
Wengine wanaweza wasione masaada wao bali wewe unakaonamsaada wako, k**a yule mwizi wa pili.
Usifanye kosa k**a la yule mtu wa Isaya 53:4-5
[4]Hakika ameyachukua masikitiko yetu,
Amejitwika huzuni zetu;
Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa,
Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
[5]Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu,
Alichubuliwa kwa maovu yetu;
Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake,
Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
Wao walidhani Yesu amepigwa na Mungu, wakapishana na uponyaji wao.
Maana yake hawakuona uponyaji wao kupitia kupigwa kwake kwasababu walidhani amepigwa na Mungu. Wakati wengine wanaona uponyaji kwakupigwa kwake wao waliona anaadhibiwa na Mungu kwa makosa yake mwenyewe.
Japo Yesu alipita pamoja na wanyang'anyi msalabani lakini alikuwa nuru yao.
Jifunze kwa Yesu, mazingira yasizimishe nuru yako, Yesu alijua Yeye ni nuru hatak**a amesulubiwa katikati ya wanyang'anyi, hakuruhusu nuru yake izimishwe na mateso na kipigo na maumivu na kudharauliwa pamoja na wanyang'anyi. Yule mwizi wapili asingeona nuru kwa Yesu K**a angeamua kumezwa na hali anayopiti. Yesu alijua msaada aliobeba kwaajili yao.
Ikiwa Mungu amekubebesha masaada kwaajili ya wengine, usidharau ulichobebeshwa kwasababu ya mahali unapopita. Yesu hakudharau alichobeba kwasababu ya hali anayopitia na wewe pia uusidharau ulichobeba kwasababu ya mazingira unayopitia. Bado unaweza kuwamsaada hatak**a umewekwa msalabani na wanyang'anyi. Haleluya!!!
2) Ile kwamba mnapita mahali pa kufanana, haina maana mnafanana.
Tutazame mfano wa kutoka 14:1-31.
Hii ni habari ya wana wa Israeli walipokuwa walivuka bahari ya Shamu, bahari ya Shamu ilikuwa ni mlango wa kuvuka kwa Wana wa Israeli kutoka misri. Lipo jambo nataka tujifunze hapa. Ukosoma Ile habari utagundua,
Wamisri walipowafuatia wana wa Israeli ungefikiri k**a vile Wamisri wangevuka bahari ya shamu kwasababu walivuka pamoja na wana wa Israeli. Lakini unaona waisraeli wanatokeza upande wa pili na Wamisri wanazama baharini. Walifikiri kwasababu Israeli wamevuka bahari ya Shamu na wao watavuka bahari ya Shamu.
Wasijue bahari walipovuka Israeli inaweza ikawameza wao. Kwa sababu swala siyo kuvuka bali ni nani anaevuka pamoja na wewe. Haleluya!!
Ndiyo maana usijaribu kuiga watu wengine hakikisha una Imani yako kwa Mungu wako, atakutoa.
Ile kwamba unaona mtu anavuka mahali usiige kwanza, tafuta kujua anavuka na nani. Bwana Yesu asifiwe milele.
Jambo jingine ninalotaka uwone hapa,
Mungu alipowafungulia wana wa Israeli mlango kwenye bahari ya Shamu, Wamisri walifikiri umefunguliwa na kwaajili yao pia na wanaweza kuutumia kuvuka kwenda ng'ambo nyingine.
Mlango haukuwa kwaajili ya kila mtu bali kwa Israeli peke yao.
Unajua mlango ukifunguliwa haina maana ni kwaajili ya kila mtu. Utagundua unapoona wengine wamepita wewe ukifika unafungwa, kwanini kwasababu haukufunguliwa kwaajili yako.
Vivyo hivyo mlango ukifungwa siyo kwaajili ya kila mtu.
Ndiyo maana ukiona mlango umefungwa usikasirike muulize Mungu kwanini umefunga, kwasababu unaweza kutaka kwenda kwa mkumbo au kimazoea usijue Mungu anaufungulia mlango mwingine kwaajili yako.
Tutazame tena ule mfano wa Luka 23:39-43.
Kosa alilofanya mwizi wa kwanza ni kujifananisha na Yesu kwasababu wote wanapita mahali pa kufanana. Walisulubiwa watatu msalabani lakini mbinguni walienda wawili tu!
Wote walipita msalabani lakini sio wote waliingia mbinguni.
Nirahisi ukaona wote mnapita mahali pa kufanana lakini mlivyobeba havifanani hivyo hatma zenu hazifanani pia.
Usije ukafanya hili kosa kabisa, kwakufikiri mazingira mnayopitia kwakufanana ni kwasababu mnafanana.
- Ukisikiliza yale maneno ya mwizi wa pili pale msalabani utagundu alijiua Siri ya ajabu sana,
Jambo la I) Alijua japo wamesulibiwa wote wao walikuwa na makosa kweli ila Yesu hakukosa neno lolote. Ndani yake alipata ujumbea uliomsaidia kupata msaada kwa Yesu.
Ok alipata ujumbea gani; alipata kujua hakusulubiwa kwaajili ya makosa yake bali kwaajili ya makosa yao.
Baada ya kujua hivyo akapata hekima: isemayo, huyu mtu Mungu ameamua kumpitisha mahali tunapopita na sisi Ili tupate msaada alioweka ndani yake kwaajili yetu, asingependa tuangamia hata k**a dhambi imetufikisha hatua hii Bado kunatumaini la maisha mengine baada ya hapa.
Jambo la 2) Alijua wakifa wote watatu saa ile Yesu haendi kule watakapoenda wao, bali anaenda mbinguni kwenye ufalme wake. Ndiyo maana akasema unikumbuke "...utakapoingia katika ufalme wako" niende na wewe.
Ujumbe aliopata ni kuwa! hata k**a wote tunapita mahali pa kufanana, tulichobeba havifanani na hatma zetu hazifanani (tunapoenda hakufanani)
Akapata hekima: akasema naeweza kuamua hatma yangu kwakukubali alichobeba huyu Ndugu kwaajili yangu hapa msalabani. Kwasababu hata k**a dhambi imenifikisha hatua hii ya msalaba siruhusu inifikishe jehanamu ya moto; nitaenda na wewe katika ufalme wako huko uwendako.
Ndani yake yalizaliwa maamuzi ya ajabu sana. Aliamua hata k**a Mimi na mwenzangu tumekuja wote msalabani, sikotayari kwenda anapotaka kwenda Yeye. Mimi nimeamua kwenda na wewe Yesu kwenye ufalme wako, kwahiyo nikumbuke.
Najaribu kusema kilichokuwa moyoni mwake na kupelekea maamuzi aliyofanya.
Hayasiyo mahesabu mepesi sana, lakini ni na uhakika Mungu alimsaidia kabisa.
Najaribu kufikiri yule mwizi wa kwanza laipomuona mwenzie yuko mbingu alijisikiaje? Lazima aliwaza, yaani nilifikiri wewe ni mwizi mwenzangu aisee! Akifikiri kwasababu wote wamepita kwenye uwizi basi wataenda wote jehanamu ya moto.
Imani ya yule mwizi wa pili ilimtenganisha na wizi na mwizi mweziwe na kumuunganisha na Yesu.
Imani yako kwa Yesu Kristo uliyonayo inaweza kukutofautisha na watu wengine hata k**a mnapita kwenye hali za kufanana. Unaweza kufanya maamuzi k**a yule mnyang'anyi; je mazingira ninayopitia yaamua hatma ya nuru yangu, yaamue kesho yangu au Imani yangu kwa Mungu?
Haya ni maamuzi yako binafsi usiyafanye kwa mkumbo! Tenga muda na kaa peke yako.
Na Mungu wangu awe nawe hapo! Uvukekatika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Amen.
Mungu na akubari sana.
Ninakuombea.