Azusa Bible Church ngaramtoni

Azusa Bible Church ngaramtoni Hii ni ukurasa wa kushirisha neno la Mungu, kwaiyo karibu sana, usiache kuuliza maswali yahusuyo Biblia utajibiwa na watumish wa Mungu

30/07/2023

Yesu asifiwe mpendwa Ibada ya Leo ilikuwa Njema Sana. Matangazo yalikuwa k**a ifuatavyo:
✓ Aliesimama leo ilikuwa ni familia ya Joseph David (Mkombozi) na Piniel Hosea
✓ Atakaesimama wiki ijayo Ibada ya Asubuhi ni Witness na Mchana Elibariki Saruni.
✓ Mchungaji alimshukuru Mungu K**a alivyotangaza.
✓ K**ati ya kanisa itabaki baada ya Ibada
✓ Wamama nao watanaki baada ya Ibada
✓ Mchungaji ameomba watu waende Jumuiya kwa mitaa yao.

MAHUBIRI: SOMO; KUSITASITA KTK SAFARI YA KIROHO

1Wafalme 18:21, Naye Eliya akawakaribia watu wote, akanena, Mtasita-sita katikati ya mawazo mawili hata lini? BWANA akiwa ndiye Mungu, mfuateni, bali ikiwa Baali ni Mungu, haya! Mfuateni yeye. Wale watu hawakumjibu neno.

2 Wafalme 17:41, Basi mataifa hawa wakamcha BWANA, tena wakaziabudu sanamu zao za kuchongwa; na wana wao vile vile, na wana wa wana wao; k**a walivyofanya baba zao, wao nao hufanya vivyo hivyo hata leo.
Mchungaji amendelea kwa kusema tuache kumchanganya Mungu na Miungu utachelewesha Baraka zako mwenyewe.
Tuchague tutakae mtumika K**a ambavyo yoshua alivyochagua.

UKISOMA
Yoshua 24:14, Basi sasa mcheni BWANA, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo na kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye BWANA.
15, Nanyi k**a mkiona ni vibaya kumtumikia BWANA, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia BWANA.

28/07/2023

Yesu asifiwe mpendwa, kumbuka siku ya kesho ni Jumuiya zetu, na tutafanyia kanisani Jumuiya zote, karibu Sana, Mjulishe na mwenzako

Ibada ilikuwa Njema
02/05/2022

Ibada ilikuwa Njema

01/05/2022

ATUNZAE NENO LA MUNGU ATAPATA KIBALI.

Ukitunza neno utapata kibali na mamlaka.
✓ Mungu awezi achilia Baraka kwako K**a ulitunzi neno lake.
✓ Ukifanya unachoagizwa na Mungu utapata unachotaka kwa Mungu Tena kwa Muda.
Ufunuo wa Yohana 2:26
Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa.
✓ ukiyatunza maagizo ya Mungu ata mwisho utapewa mamlaka juu ya mataifa yote ya dunia.
Zaburi 2:8
Uniombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako, Na miisho ya dunia kuwa milki yako.
Zaburi 2:9
Utawaponda kwa fimbo ya chuma, Na kuwavunja k**a chombo cha mfinyanzi.
✓ kupitia milango miwili hapo juu ya zaburi tunaona jinsi Mungu anavyozungumza na Daudi atakapo lishika neno na kulitenda.
✓Jifunze kulijua neno na kulitenda ili Mungu akubariki na kukutumikia.

01/04/2022

SOMO: MAOMBI
*kumwambia Mungu aja ya mioyo yetu na pia kumsikiliza kwa njia hii tutaweza kuwa washindi katika maisha yetu.
*Uimarisha uhusiano wetu na Mungu katika maisha yetu Luka 9:23, Mathayo 10:33
*Tunapomwendea Yesu tunamwomba awe Bwana wa maisha Yetu, maana yake atuna mamlaka na maisha Yetu ni Mungu ndie mkuu wa Maisha Yetu.
* Unajiweka chini ya uongozi na mapenzi ya Mungu.
*Tunapomwomba awe na madaraka juu yetu na pia atuongoze nasi tunatakiwa atuongoze.
*Anaweza kutuonyesha baadhi ya sehemu za maisha Yetu anazotaka yeye.
*Maombi hufanya aachilie nguvu yake katika maisha yetu. Yohana 16:23-24, 14: 13, 14:20,15:11, 1yohana 15:14
*Maombi yanaleta upako na uweza ndani yetu.
*Maombi yanaleta karama tofauti ndani yetu.
* Mungu alituadi kutupatia maitaji yetu wafilipi 4:19, Mathayo 7:7-11,.
* Mungu anasema kwamba iwapo tukiomba tutapokea, tutapata maitaji yetu Isaya 43:26.
maitaji yetu ni haki kupata kutoka kwa Mungu.

28/03/2022
06/03/2022
26/02/2022

Amosi 5:4, Maana BWANA awaambia hivi nyumba ya Israeli, Nitafuteni mimi, nanyi mtaishi, Ameen

25/02/2022

Wafilipi 4:4, Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.Mariam AsumaniMariam Asumani

Address

Emaoi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Azusa Bible Church ngaramtoni posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share