Efatha Church Dodoma

Efatha Church Dodoma EFATHA CHURCH DODOMA WE BRING THE WORLD TO JESUS

04/06/2026
ALHAMISI YANGU IMEBARIKIWAVyakula Vinono na Vitamu, Utele, Karamu, Tafrija, Furaha, Sherehe, Kicheko KWANGU HAVITAPUNGUA...
04/06/2026

ALHAMISI YANGU IMEBARIKIWA

Vyakula Vinono na Vitamu, Utele, Karamu, Tafrija, Furaha, Sherehe, Kicheko KWANGU HAVITAPUNGUA.

Alhamisi Yangu Imebarikiwa na BWANA.

YESU ni Mzuri.

JUMATANO YANGU IMEBARIKIWA.Ni Siku ya Kuchukua Urithi wangu. Mimi ni Mmiliki na Nitamiliki pamoja na Wamiliki. Sitakaa u...
03/06/2026

JUMATANO YANGU IMEBARIKIWA.

Ni Siku ya Kuchukua Urithi wangu. Mimi ni Mmiliki na Nitamiliki pamoja na Wamiliki. Sitakaa uchochoroni wala kuwa mpangaji bali Nitapangisha. Mimi nimebarikiwa na BWANA.

YESU ni Mzuri.

JUMANNE YANGU IMEBARIKIWA.Furaha, Amani, Afya Njema, Kicheko, Ustawi, Baraka, Maisha Marefu, Upendo vitajaa katika Famil...
02/06/2026

JUMANNE YANGU IMEBARIKIWA.

Furaha, Amani, Afya Njema, Kicheko, Ustawi, Baraka, Maisha Marefu, Upendo vitajaa katika Familia yangu; Mimi na Familia yangu Tumebarikiwa na BWANA.

YESU ni Mzuri.

JUMATATU YANGU IMEBARIKIWA.Mimi ni mbarikiwa wa BWANA, nimebarikiwa mjini na mashambani, uzao wangu umebarikiwa na uzao ...
01/06/2026

JUMATATU YANGU IMEBARIKIWA.

Mimi ni mbarikiwa wa BWANA, nimebarikiwa mjini na mashambani, uzao wangu umebarikiwa na uzao wa wanyama wangu umebarikiwa. Kazi za mikono yangu zimebarikiwa. Adui zangu watapigwa mbele yangu. Mimi ni mtu mkuu na mataifa yote wataniona kuwa mimi ni mtakatifu wa BWANA.

IBADA YA PAMOJA KANISA LA EFATHA DODOMA | 31.05.2026Zaburi 133:1"Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pa...
31/05/2026

IBADA YA PAMOJA KANISA LA EFATHA DODOMA | 31.05.2026
Zaburi 133:1
"Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, kwa umoja."

MEZA YA BWANA
31/05/2026

MEZA YA BWANA

MEZA YA BWANAMungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yak...
31/05/2026

MEZA YA BWANA
Mungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yako ndipo dhambi, magonjwa, shetani wachawi, njaa na hata dhiki zitakukimbia na ndipo utakapoona mema yakikujilia. Ayubu anasema utakusudia neno nao litatimia. Ukilinda imani yako isiyumbe hautasikia njaa wala kiu, maana yake mahitaji yako yatatimizwa.
Haya yote yatatokea kwako k**a utalinda imani yako. Tunapomega mkate na kunywa mvinyo, yale yaliyoshindikana yakawezekane, Biblia inasema “Imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo” mwana wa Mungu Neno hili litatimia kwako, hutaona kiu wala njaa maana mahitaji yako yatatimilizwa, unaenda kula na kunywa vile vitamanikavyo.
Biblia inasema Mungu ndiye uzima wako, baada ya kula na kunywa (meza ya Bwana) ule ugonjwa uliyokukandamiza utaondoka. Kwa mamlaka niliyonayo utaenda kutamka Neno leo na litakwenda kutimia, yule mgonjwa aliyekuwa kitandani kwamba ni mkubwa au mdogo anakwenda kuinuka, kwamba ulikuwa unaumwa na kansa, TB, presha, kisukari au aina yoyote ya ugonjwa leo huo ugonjwa umeondolea maana Bwana amesema amekuja ili sisi tuwe na uzima tele, leo unakwenda kuwa na uzima tele. K**a umekuja hapa ulikuwa na maswali yanayokusumbua umepata majibu yake. Mwanangu wacha ikawe hivyo kwako.
@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

MEZA YA BWANAYohana 6:33-35 “Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.  B...
31/05/2026

MEZA YA BWANA
Yohana 6:33-35 “Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima. Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki.”
Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.”
Yohana 1:1-5 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.”
Tunapokubaliana na neno tunakuwa tunapata uzima wa milele, tunaporuhusu Neno ndani yetu tunaruhusu Yesu akae ndani yetu, kwa maana Yesu ndiye uzima wetu. Tukikubali Neno tumemkubali Yesu, na hapo ndipo tunalinda imani yetu, ukiilinda imani yako itakupa kuponyeka, ukiamini kile unachokiamini mtu asikiondoe wala kukiharibu ndipo uponyaji unatokea kwako, Yusufu alilinda imani yake japokuwa alitupwa gereani lakini akaishia kuwa mtu mkuu, Daudi pia alilinda imani yake na akaishia kuwa mfalme. Imani ukiilinda unakuwa salama na kwako kunakuwa kwema.
Zaburi 128:1-4 “Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake, Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema…”
Yule amchaye Bwana atabarikiwa. Kumcha Bwana ni kulinda kile unachokiamini, unapolinda unachokiamini maisha yako yanaonekana yana mpangilio na ndipo Mungu anakufurahia, kwa maana unapolinda hicho unajiponya na mambo au ulimwengu huu na ndipo Mungu anakufurahia na kuruhusu mema yakujilie na kwako kunakuwa kwema.
Zaburi 126:6 “Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.”
Tunapolinda imani kuna magumu, machungu kudharauliwa na kusukumwa lakini usiangalie yale yanayoendelea bali angalia kile unachokiamini ili kikupe kile unachokitaka, hakikisha unalinda kile unachokiamini na ndipo kwako kutakuwa kwema na Mungu atakushangaza na kila mtu atakushangaa.
@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Address

KISASA/IPAGALA MWISHO
Dodoma
41000

Telephone

+255787432633

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Dodoma posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Dodoma:

Share