Kanisa La TAG OCC BAHI Dodoma

Kanisa La TAG OCC BAHI Dodoma Tunakukaribisha Katika Jina la Yesu!

Huu ni Ukurasa Rasmi wa Kanisa letu zuri la TOCC DODOMA linalopatikana Mji WA BAHI, MAGHARIBI Mwa Jiji la Dodoma, Tanzania.
“Nasi TU mashahidi wa Injili katika Mji WA Bahi, na katika Dodoma Yote, Tanzania na hata mwisho wa nchi.”
— Matendo 1:8

  WA MUME MKRISTO NA MKE MKRISTO KIBIBLIAMnenaji: Mwl.Imani Mwanyingi| FGG|Bezaleli Media Tanzania|IBADA YA JUMAPILI| TO...
28/01/2026

WA MUME MKRISTO NA MKE MKRISTO KIBIBLIA
Mnenaji: Mwl.Imani Mwanyingi| FGG|Bezaleli Media Tanzania|IBADA YA JUMAPILI| TOCC DODOMA|Januari 04, 2025
Rejea:
- BIBLIA
- Wajibu wa Mme Mkristo (Frank R. Parish - 2003)
""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""
Familia ni taasisi ya kwanza kabisa aliyoanzisha Mungu, na ili iwe imara, kila mwenza anapaswa kutimiza wajibu wake kikamilifu. Baba na mama wana nafasi za kipekee katika malezi, uongozi, ujenzi p mm maadili, na ustawi wa kiroho, kijamii na kiuchumi wa familia. Biblia inaelekeza wazi majukumu yao, huku jamii ikitegemea mchango wao katika kuunda kizazi chenye heshima, bidii na kumcha Mungu.
~ Uongozi wa Ki-Mungu huanzia nyumbani; Kwa ajili hiyo maandiko yote yanayohusu maisha ya Ukristo yamekusudiwa yaonekane kwanza NYUMBANI.
“tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane k**a na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.”
— Waefeso 4:32

A: WAJIBU WA MUME MKRISTO (BABA)

1. KUMTII KRISTO KWA BIDII ILI KUPATA MSAADA WA KUONGOZA FAMILIA (KICHWA)
“Kumcha Bwana ndio mwanzo wa hekima, Wote wafanyao hayo wana akili njema, Sifa zake zakaa milele.”
— Zaburi 111:10
“Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, k**a chombo kisicho na nguvu; na k**a warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.”
— 1 Petro 3:7

2. KUMPENDA MKE WAKE NA KUMPA HESHIMA KWA MOYO WA KUJITOA
• K**a Kristo alivyoipenda Kanisa.
“Enyi waume, wapendeni wake zenu, k**a Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;” — Waefeso 5:25 (22-33)

• Kutenda Kila jambo Kwa Upendo
“Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.”
— 1 Wakorintho 13:13

• Kumpenda Mke SI Kwa jinsi anavyotii au asivyotii; Bali KWA KULITII LILE AGIZO LA MUNGU.
Angalia HAPA, maneno KUMPENDA MKE yanarudiwa mara Tatu k**a msisitizo!
Waefeso 5:25,28, 33
²⁵ Enyi waume, wapendeni wake zenu, k**a Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
²⁸ Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao k**a miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
³³ Lakini kila mtu ampende mke wake k**a nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.

• Kwa KUAMUA (UAMUZI), Siyo KUJISIKIA
Kumpenda Mke kunapaswa kufanyika Kwa uamuzi wa dhati kutoka moyoni badala ya kuongozwa na Hisia.
K**a vile Kristo alivyolipenda Kanisa, akautoa upendo wake Wote bila kujali kungetokea NINI.
“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”
— Yohana 3:16
“Ninyi waume, wapendeni wake zenu msiwe na uchungu nao.”
— Wakolosai 3:19

• Kuwa tayari KUMSAIDIA MKE KATIKA HALI ZOTE
Mfano:
- Mahitaji ya Kimwili: madeni, kuyumba biashara, matatizo ya kifamilia kwao, nk.
- Shughuri za nyumbani: Kufua, kupika, kumwagilia bustani, kwenda sokoni, nk Kila inapobidi.

3. KUTUNZA NA KUMHESHIMU AGANO TAKATIFU LA NDOA
Mwanaume anapoamua kuoa, anafanya AGANO LA KUJITOA KWA MKEWE mbele za MUNGU. Huu unafananishwa na mkataba wa kimbingu ambao kamwe hautanguki. Ni jukumu zito ambalo mwanaume hapaswi KUINGIA bila maandalizi ya Kutosha!
Angalia,
“Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.”
— Mwanzo 2:24
“Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
— Marko 10:9
“Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema Bwana wa majeshi; basi jihadharini roho zenu, msije mkatenda kwa hiana.”
— Malaki 2:16

4. KUTOA UONGOZI WA KIROHO/DIRA KWA MKE NA FAMILIA
– Kuwaongoza kwa hofu ya Mungu.
“Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, k**a Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.”
— Waefeso 5:23
“akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo”
— Waefeso 1:22
“Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.” — 1 Wakorintho 11:3

5. KUWAFUNDISHA WATOTO KUMPENDA MUNGU (IMANI)
– Kupandikiza maadili, misingi ya Imani na kumcha Mungu.
“nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.”
— Kumbukumbu 6:6-7
“Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.”
— Mithali 22:6
Mfano: MAOMBI, Utoaji, Adabu na Heshima Kwa WATU wengine, Ukarimu, Matunda ya Roho Mtakatifu, Umuhimu wa ELIMU(maarifa), nk.

6. KUWAPENDA NA KUWAHESHIMU WATOTO
– Kuwapenda na Kuwalea kwa nidhamu na maonyo ya Bwana.
“Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.”
— Waefeso 6:4
- Kuwaletea Zawadi Mke na Watoto ili wafurahie kukupokea unapokuja nyumbani. SI TU upokelewe Kwa kuwa una zawadi, lakini kwamba Watoto na mke wafurahie unapoonekana kwamba wewe ndiye mtunzaji wa Familia Katika Hali zote!

- Kuwaadabisha Kwa Fimbo ya adhabu. Unapomchapa Mtoto Kwa kuwa amekosa, unadhihirisha kwamba unampenda na unataka aje kuwa Mtu mzuri.
“Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema.”
— Mithali 13:24

- KUTOA adhabu Kwa Hekima na Kiasi, WASIJE Wakakata Tamaa!
“Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.”
— Wakolosai 3:21

7. KUTUNZA NA KULEA FAMILIA(MKE NA WATOTO)
MUME MKRISTO anawajibika Kutoa mahitaji ya kifamilia; kuhangaikia mahitaji ya nyumba na familia.
“Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.”
— 1 Timotheo 5:8
KUTUNZA: Kuileta mahitaji ya nyumbani na mahitaji ya familia mfano: SAMANI ZA NDANI, CHAKULA,MAVAZI, CHAKULA, MALAZI, ELIMU NA MATIBABU.

KULEA: Ni kusimamia tabia na mwenendo wa familia (Mke na Watoto).
Mfano:
• Kufundisha Watoto tabia njema, bidii ya kazi, Adabu na Heshima, nk
• Kusimamia tabia ya Mtoto: Kupongeza anapofanya vizuri(zawadi) na kuadibu anapokengeuka!
• Kuangalia na Kusimamia mwenendo wa Mke na KUMSAIDIA inapobidi.
Mfano: Anarudi nyumbani Usiku, anachelewa Kanisani, anakwepa MAOMBI, hatoi fungu la kumi, anavaa isivyofaa, nk. Mme ana nafasi kubwa ya kusaidia, Kwa MAOMBI, maonyo na mafundisho Katika neno la Mungu!

8. KUSAMEHE NA KUWA MVUMILIVU
– Afundishe familia neema na upendo wa kweli.
Wakolosai 3:12-13
¹² Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,
¹³ mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; k**a Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.

9. KUDUMISHA TABIA NJEMA (MFANO WA KUIGWA) NYUMBANI NA KATIKA JAMII
– Kwa tabia njema, uadilifu na maisha ya kiroho.
“Mnifuate mimi k**a mimi ninavyomfuata Kristo.” — 1 Wakorintho 11:1
Mfano:
TUNDA LA ROHO
"Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo k**a hayo hakuna sheria"
--- Galatia 5:22-23

10. KUWA MLINZI WA FAMILIA
Hili linawezekana Kwa MAOMBI, ili MUNGU aistawishe familia na kuiepusha na Majanga! Mfano: UGOMVI, KUTOELEWANA, TALAKA, nk.
• Mme MKRISTO anapaswa kuwa chanzo na SABABU ya familia kuwa na amani!
Waebrania 12:14-15
¹⁴ Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;
¹⁵ mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.

• Kumlinda Mke na Watoto dhidi ya mashambulizi ya WATU wengine k**a vile Ndugu wabaya, majirani wabaya, mawifi wabaya, nk.
Yaani, KUMTETEA MKE HADHARANI ili KUMUONYA NYUMBANI!!

• KUWATIA MOYO MKE NA FAMILIA
Kwa kuwa wao ni mawili MMOJA, Matendo ya Mme na Mke yanaweza ama KUMTIA MOYO MKE Kujua KIROHO au Kumkwamisha!
“Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
— Waefeso 5:31
TAZAMA!
Mhubiri 4:9-10
⁹ Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.
¹⁰ Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!

B: WAJIBU WA MKE MKRISTO KIBIBLIA*
“Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.” — Mwanzo 2:18
WAJIBU KIBIBLIA:
1. Kuyatoa Maisha yake Kwa Kristo na KUMCHA MUNGU KATIKA ROHO NA KWELI
“Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.”
— Kumbukumbu 6:5
“Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.”
— Mithali 31:30
“Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani.”
— Mithali 31:10

2. KUMPENDA MUME NA WATOTO WAKE
– Maisha ya mama yaonyeshe upendo wa kweli.
"...ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao; na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe"
- Tito 2:4-5

KWA NAMNA GANI?
• Kukubali Kuongozwa na Mme wako. Kwa kutii unaonesha wazi kwamba unampenda na unatambua nafasi yake Kwa MUNGU na Kwa familia.
“Enyi wake, watiini waume zenu k**a kumtii Bwana wetu.”
— Waefeso 5:22
“Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, k**a Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.”
— Waefeso 5:23
“Lakini k**a vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.”
— Waefeso 5:24
• Kumtendea Mema k**a Ipasavyo Wajibu wa Mke Kwa Mme.
“Lakini ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema.”
— 2 Wathesalonike 3:13

• KUTUNZA Mme na Watoto: Kuandaa chakula, Kusafisha nyumba, Kufua nguo, nk.
• KULEA MME NA WATOTO: Mwanamke anawajibika kusimamia tabia na mwenendo wa Mme wake ili KUTOA USHAURI Kwa Hekima na kujenga NDOA Imara!

3. MKE NI MLEZI WA FAMILIA
MKE anapaswa Kuungana na Mme wake KUSIMAMIA TABIA ZA WANAFAMILIA Wote nyumbani.
Mama ni Mwalimu na Mlezi nambari Moja, kabla ya Mme wake k**a hakimu inapobidi.
“Mwanangu, shika maagizo ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako.”
— Mithali 6:20
“Msikilize baba yako aliyekuzaa, Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.”
— Mithali 23:22
• Kufundisha Familia UKARIMU NA KUSAIDIA WATU. Mama mtoani na mkarimu atafunza wanaye kuwa wakarimu, na kinyume chake ni kweli!
“Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu.”
— Mithali 31:27
“Huwakunjulia maskini mikono yake; Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.”
— Mithali 31:20

• Kulea watoto katika adabu ya Bwana*
– Awe mlezi wa kwanza wa kiroho kwa watoto.
*(Mithali 1:8; 2 Timotheo 1:5)*
• Mlezi wa watoto* – Kuwa mstari wa mbele kulea watoto katika maadili.
*(2 Timotheo 1:5, Mithali 1:8)*
• *Mlinzi wa afya ya familia* – Yeye hufuatikia lishe, usafi, na matibabu Kwa Watoto wakati Wote!
Mama yu karibu zaidi na Watoto na anapatika a Kwa urahisi, Hali ambayo Watoto huihitaji zaidi!

4. KUMTII MME KATIKA KILA JAMBO
Kutii MME_Ni kujiweka chini ya Uangalizi, Kuhifadhiwa na kupokea UPENDO wake na Hali yake ya Kiungu (KICHWA CHA MKE).
KUTII _Ni Kukubali kufuata uongozi.

• Neno KUTII_Latokana na maneno mawili ya Kigiriki;
~ HUPO = Chini ya
~ TASSO = Katika Utaratibu mzuri, ulioteuliwa.

KUMBE, KUTII MME ni kuishi chini ya utaratibu maalum uliotolewa na Mungu, yaani kuishi chini ya Uongozi WA MUME wake Katika Utaratibu uliowekwa na MUNGU mwenyewe.
“Lakini k**a vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.”
— Waefeso 5:24

• KWA KUWA MME NI KICHWA CHA MKE (KIONGOZI)
"Enyi wake, watiini waume zenu k**a kumtii Bwana wetu. Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, k**a Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili"
--- Efeso 5:22-23

• ILI WASIOAMINI NENO, WAVUTWE!!
“Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;”
— 1 Petro 3:1

• ILI WATUNZWE NA KULINDWA
“Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, k**a chombo kisicho na nguvu; na k**a warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.”
— 1 Petro 3:7
“Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,”
— 2 Wakorintho 6:18

5. MSAIDIZI WA MME WAKE* – Hii ni Kazi ya awali aliyokabidhiwa na Mungu. MKE husaidia na kuhakikisha Mipango, malengo, na MAONo ya Mme wake Kwa familia yanafanikiwa.
“Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”
— Mwanzo 2:18
“Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanamume.”
— 1 Wakorintho 11:9
• KUMUOMBEA MME WAKATI WOTE
• KUMTIA MOYO MAMBO YAKE YANAPOENDA MRAMA NA YANAPOENDA VIZURI
• KUSIMAMIA SHUGHURI ANAZOAGIZWA NA MME KWA UAMINIFU, nk.

6. KUWA NA TABIA NJEMA NA KUMCHA MUNGU
• Kutafuta SIFA Njema (MKE Mwema)*(Mithali 31:10–31,
• UPENDO wa dhati Kwa Mme na Watoto.
Tito 2:3-5
⁴ ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;
⁵ na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.

7. MAMA NI FUNDI, MJENZI WA FAMILIA YENYE MAADILI MEMA
• Mama hufundisha lugha, heshima, ibada
“Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.”
— Mithali 10:1

8. *Kushiriki shughuli za kiuchumi* – Mama anaweza kufanya kazi au biashara kusaidia familia.
• Mjasiriamali, SI MVIVU/MZEMBE!
Mithali 31:16-19
¹⁶ Huangalia shamba, akalinunua; Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.
¹⁹ Hutia mikono yake katika kusokota; Na mikono yake huishika pia.

9. *Kusimamia nyumba kwa hekima*
– Mama ndiye mlinzi wa mazingira ya nyumbani.
“Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu.”
— Mithali 31:27
- Msimamizi wa nyumbani* – Kusimamia shughuli za ndani; USAFI WA MAZINGIRA, VYOMBO VYA CHAKULA, MPANGILIO WA SEBULE,

10.. *Kuwa mwenye busara, safi, mpole na mtulivu*
– Maisha yake yawe mfano kwa jamii.
*(Tito 2:5)*
• Kumstahi/KUMSITIRI MME wake.
“Lakini kila mtu ampende mke wake k**a nafsi yake mwenyewe; WALA MKE ASIKOSE KUMSTAHI MUMEWE ”
— Waefeso 5:33
KATIKA UDHAIFU, MKE amuombee Mme wake, Amtunzie Siri na Kutafuta namna nzuri ya KUMSAIDIA Mme badala ya KEJELI, DHARAU NA MASENGENYO!!
• Aweze kuwatumia Kwa Hekima maneno MATATU MUHIMU Katika NDOA
A. ASANTE
B. SAMAHANI
C. NISAMEHE

Baba na mama kila mmoja Kwa wakati wake ana nafasi ya kipekee kimaandiko, kijamii na kiuchumi. Familia ikiongozwa kwa ushirikiano wa wajibu hawa, huleta jamii imara yenye heshima kwa Mungu.

“Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.”
— 1 Petro 3:8-10

JE, NDOA yako Ina changamoto? Hakuna amani na utulivu wa kweli!? Yupo MUNGU, muasisi wa NDOA! Yeye aliyewaunganisha, Atawasaidia kuishi PAMOJA Kwa amnlani, furaha na UPENDO! Bado tunaweza kumwamini TU, nyakati nzuri zinakuja! Usiondoke! Usiombe TALAKA, SI mpango wa MUNGU!
MUNGU akujaalie Amani, UPENDO na Furaha ya kweli mwaka huu Mpya 2026

MUNGU AKUBARIKI, AMEN!!!
FGG|Mwalimu wa Neno la Mungu|Mwandishi| Media Tanzania| TOCC DODOMA|MAGHARIBI Mwa Jiji la Dodoma|Ibada ya JUMAPILI|Januari 04, 2025
©©©©©©©©©©©©©©©©©©©©©©©©

  TOCC DODOMA: HATA SISI HAPO ZAMANI TULIKUWA K**A VILETito 3:1-7³ Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tu...
31/12/2025

TOCC DODOMA: HATA SISI HAPO ZAMANI TULIKUWA K**A VILE
Tito 3:1-7
³ Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tulikuwa waasi, tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu na husuda, tukichukiza na kuchukiana.
⁴ Lakini wema wake Mwokozi wetu Mungu, na upendo wake kwa wanadamu, ulipofunuliwa, alituokoa;
⁵ si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu;
⁶ ambaye alitumwagia kwa wingi, kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu;
⁷ ili tukihesabiwa haki kwa neema yake, tupate kufanywa warithi wa uzima wa milele, k**a lilivyo tumaini letu.

30/12/2025

“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”
— Isaya 9:6

KARIBU TUMWADHIMISHE MUNGU PAMOJA“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme ut...
25/12/2025

KARIBU TUMWADHIMISHE MUNGU PAMOJA
“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”
— Isaya 9:6

  ZA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme uta...
24/12/2025

ZA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026
“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”
— Isaya 9:6

TUNAWATAKIA HERI YA KRISMASI!!

MUNGU WETU AMETUKUBALI TENA!!

  MOJA NZURI SANA!!Uweponi Mwa MUNGU, KUNA AMANI NYINGI!!KUFARIJIWA KWINGI!Tuseme NINI!?
23/12/2025

MOJA NZURI SANA!!

Uweponi Mwa MUNGU, KUNA AMANI NYINGI!!
KUFARIJIWA KWINGI!
Tuseme NINI!?

  NI MCHUNGAJI NA MLANGO WA KONDOO|Na.Rev.EMMANUEL CHIBWANA|Mchungaji Kiongozi| TOCC DODOMA|IBADA YA JUMAPILI|Disemba 14...
23/12/2025

NI MCHUNGAJI NA MLANGO WA KONDOO|Na.Rev.EMMANUEL CHIBWANA|Mchungaji Kiongozi| TOCC DODOMA|IBADA YA JUMAPILI|Disemba 14, 2025
*****************************************************
“Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo.”
— Yohana 10:7

“Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.”
— Yohana 10:11
• Yesu anajinena kwamba Yeye ndiye yule Mchungaji mwema aliyetajwa Katika Zaburi! Ni k**a anasema anawaangalia KONDOO Kwa upole na UPENDO wa Hali ya juu!

“Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.”
— Zaburi 23:1

“Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.”
— Yohana 10:9
• Wanaookoka kupitia Kwa Yesu wataokolewa. Yeye peke yake ndiye MLANGO wa wokovu, hapana mwingine!

Yohana 10:10-16
¹⁰ Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
¹¹ Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
¹² Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, humwona mbwa-mwitu anakuja, akawaacha kondoo na kukimbia; na mbwa-mwitu huwak**ata na kuwatawanya.
¹³ Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake.
¹⁴ Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi;
¹⁵ k**a vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
¹⁶ Na kondoo wengine ninao, ambao si wa z**i hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.

• Mchungaji wa kweli hujali KONDOO wake; lakini Mchungaji wa Mshahara Hana muda NAO, HAJALI!

• MUNGU anawajua WALIO wake, naye anajitaabisha mno Kwa ajili Yao!
“Lakini nikasema, Nimejitaabisha bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida; lakini hakika hukumu yangu ina Bwana, na thawabu yangu ina Mungu wangu.”
— Isaya 49:4

Karibu sana Katika IBADA zetu na MUNGU AKUBARIKI, AMEN!!

TOCC DODOMA| la TAG OCC BAHI DODOMA| Media Tanzania|WhatsApp +255763946411
*****************************************************

  NA KUSAMEHEANA|Na. Rev.Emmanuel Chibwana|Mchungaji Kiongozi|Makamu Askofu|Jimbo la DODOMA MAGHARIBI|IBADA YA JUMAPILI|...
23/12/2025

NA KUSAMEHEANA|Na. Rev.Emmanuel Chibwana|Mchungaji Kiongozi|Makamu Askofu|Jimbo la DODOMA MAGHARIBI|IBADA YA JUMAPILI|Disemba \1, 2025
******************************************************
“Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?”
— Mathayo 18:21
“Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.”
— Mathayo 18:22

Hebu TUJIFUNZE PAMOJA KATIKA MFANO HUU HAPA!! Mathayo 18:23-35
²³ Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake. ²⁴ Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.²⁵ Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.²⁶ Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.²⁷ Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni. ²⁸ Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamk**ata, akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho. ²⁹ Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.³⁰ Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.
³¹ Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka.
³² Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;
³³ nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, k**a mimi nilivyokurehemu wewe?
³⁵ Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.

TUFANYE NINI?
1. Usiwakosee WATU Kwa makusudi Kwa kutegemea ulinzi wa andiko hili.
K**a ilivyo, taa haiwashwi ikawekwa uvunguni, Bali Katika kinara ili KUTOA mwangaza Katika nyumba, Basi nasi tumelijua neno la Mungu, hatupaswi kuwakwaza we ngi ne Kwa makusudi!
“Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.”
— Zaburi 119:105
“Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake!”
— Luka 17:1
“Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa.”
— Luka 17:2

2. Uwasamehe WATU wanaokukosea; ili MUNGU wa mbinguni akusamehe makosa yako pia.
Marko 11:24-26
²⁵ Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.
²⁶ Lakini k**a ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.]

“Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.”
— Mathayo 6:14-15
“tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane k**a na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.”
— Waefeso 4:32

TUSAMEHE MARA NGAPI?
Luka 17:3-4
³ Jilindeni; k**a ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe.
⁴ Na k**a akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.

MUNGU AKUBARIKI SANA!! JE, uko tayari kusamehe mtu aliyekukosea? Anza Sasa, Roho Mtakatifu akusaidie kusamehe, ili MUNGU wa mbinguni akusamehe wewe pia pale unapokosea!

Tumesamehewa ili Tusamehe wengine, MUNGU Atukuzwe!!

Media Tanzania
Sisi ni Habari NJEMA
*****************************************************

 : SHULE YA UANAFUNZI NA MAANDIKO| TOCC DODOMA|Kichangani, Bahi DODOMA|IBADA YA JUMAPILI|Disemba 21, 2025Somo: PAULO NA ...
23/12/2025

: SHULE YA UANAFUNZI NA MAANDIKO| TOCC DODOMA|Kichangani, Bahi DODOMA|IBADA YA JUMAPILI|Disemba 21, 2025
Somo: PAULO NA BARNABA WANATUMWA
Na: Mwanyingi FGG|Mwalimu wa Neno la Mungu
*****************************************************
Helo, Bwana Yesu asifiwe! Karibu Tena Katika mwendelezo wa masomo ya UANAFUNZI na MAANDIKO. Leo tunaangazia Wito maalum wa Paulo na BARNABA Katika Umisheni. Kwa kuwa sisi ni WAFUASI wa Kristo, ni wajibu wetu kuwatuma wamisionari Kwa WATU na MAENEO ambayo hayajafikiwa na Injili barani Afrika na mbali zaidi.
TAZAMA,
“Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.”
— Matendo 13:2

MAANDIKO zaidi: Matendo 13:1-12

NINI KATIKA HABARI HII!?
1. Ni wajibu wetu k**a Kanisa Kujali, KUMHESHIMU na Kuzingatia IBADA.
“Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema,....”
— Matendo ya Mitume 13:2
• Kuhudhuria Ibada, Semina, Mikutano, nk.
“wala tusiache kukusanyika pamoja, k**a ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.”
— Waebrania 10:25
• Tunakusanyika ili kupokea Mafundisho ya Neno la Mungu Kwa PAMOJA.
“Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.”
— Matendo ya Mitume 2:42

2. MUNGU ndiye anayechagua na kuwatia WATU Kwa ajili ya UTUMISHI.
“Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.”
— Matendo 13:2

3. Ni wajibu wa Kanisa la Mahali PAMOJA kuhakikisha linafanya Kazi ya Umisheni ili kuwafikia waliopotea(Wasiofikiwa) Kwa Injili.
WALIMU_Watafundisha WATU mahali PAMOJA Neno la Mungu Kwa KINA/Usahihi.
MANABII_Watawatia WATU msukumo wa kuyatenda mapenzi ya MUNGU.
Mfano: KUSHUHUDIA, KUHUBIRI, KUOMBA, KUTOA, KUTIA MOYO, KUTUNZA UTAKATIFU, nk.
• Mapenzi ya MUNGU wakati ule yalikuwa KUWATUMA PAULO NA BARNABA KWENYE KAZI YA UMISHENI
Maeneo: SELEUKIA, KIPRO, SALAMI, KISIWA CHA PAFO, PERGE, PAMFILIA, nk.
“Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.”
— Matendo 13:2(1-3)

4. Kazi ya UMISHENI(KUPANDA MAKANISA) inataka UTHUBUTU_Kwanza, Kuamua Kwenda KUHUBIRI Injili, Pili Kuwafungulia Kanisa(Jengo la Kuabudia/Mahali) na Tatu, KUWEKA MWALIMU/MCHUNGAJI atakayeendekea Kuwalea Kiroho.
• Kanisa linapaswa Kumtii Roho Mtakatifu ambaye ananena Kwa Vinywa vya manabii waliopo Kanisani. Na ili wawepo, lazima Kanisa liwekeze nguvu Katika IBADA na MAOMBI.
“Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.”
— 2 Petro 1:21

5. Kanisa letu la ASSEMBLIES OF GOD Duniani KOTE limepokea Kwa Unyenyekevu kazi hii ya UMISHENI. Hata MAKANISA mengine yanalitaja Kanisa letu k**a dira na mfano wa kuigwa kuhusu KUUFIKIA ULIMWENGU KWA INJILI NA KUPANDA MAKANISA.
Mfano:
• Kanisa letu Lina MAKANISA ya mahali PAMOJA zaidi ya 10,000 Nchi nzima ili kuwafikia WATU Kwa Injili.
• Kanisa letu barani Afrika na Duniani KOTE linatuma Wamishenari Kwa Nchi mbalimbali na makabila/maeneo yasiyofikiwa na Injili ili kumetea Bwana, MUNGU wetu mavuno!
“Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.”
— Warumi 1:16
“Basi usiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu, wala usinionee haya mimi mfungwa wake, bali uvumilie mabaya pamoja nami kwa ajili ya Injili, kwa kadiri ya nguvu ya Mungu;”
— 2 Timotheo 1:8
“Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.”
— Marko 8:38

“Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako.”
— 2 Timotheo 4:5

K**a alivyotumwa Paulo na BARNABA na wengine wengi hata siku za Leo,Bwana anakuhitaji wewe pia Katika UTUMISHI huu! Bado angali na mavuno mengi mno!
“Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache.”
— Mathayo 9:37
“Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.”
— Luka 10:2

Anza Sasa! Bado hujachelewa! Ishirikishe Jamii kuhusu Injili na Utoe sadaka ili kufanikisha mpango wa Umisheni wa Kanisa lako na TAIFA Kwa Ujumla!

JE, Unapata changamoto Katika Mpango huu wa Umisheni?
Unaweza Kutuandikia, nasi tutarudi Kwa ajili ya Ujumbe wako na MUNGU AKUBARIKI!

Unaweza kuungana nasi Katika Mitandao ya Kijamii Kwa ajili ya masomo mengine, Habari na Matukio zaidi kuhusu Injili kupitia Viunganishi hivi HAPA chini,
Media Tanzania||TAG TOCC DODOMA||WhatsApp +255763946411
S I S I N I H A B A R I N J E M A
*****************************************************

ASANTENI KWA KUQBUDU NASI!!TUNAWAPENDA MNO!!
30/11/2025

ASANTENI KWA KUQBUDU NASI!!

TUNAWAPENDA MNO!!

Address

Dodoma
+255755166293

Telephone

+255767166293

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kanisa La TAG OCC BAHI Dodoma posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Kanisa La TAG OCC BAHI Dodoma:

Share

TUNAKUTAKIA HERI YA MWAKA MPYA - 2019; MWAKA WA KUPOKEA NEEMA NYINGI ROHONI NA MWILINI KWA JINA LA YESU!!

Inawezekana umekuwa na wakati mgumu katika Mwaka 2018 Unaoisha masaa machache yajayo; lakini sasa Mwaka huu wa 2019 ni Mwaka mwingine Mpya wenye Baraka na Majibu yako mengi kwa Jina la Yesu wa Nazareti! Usirudi nyuma! Songa Mbele! Tunza Utakatifu, Mpinge shetani naye Atakukimbia!

Mungu akubariki!