Glory to God /Mwl Mwambeso

Glory to God /Mwl Mwambeso Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Glory to God /Mwl Mwambeso, Religious organisation, Dodoma.

13/03/2026

SOMO: *"MADHARA YA KUACHA KUOMBA KWASABABU YA KUKATA TAMAA"*

*📖Luka 18:1........ imewapasa kumwomba Mungu siku zote, wala wasikate tamaa.*

*Sehemu ya 2*

✍️Katika utangulizi wa somo hili, nilisema kwamba kuna madhara makubwa ya kuacha kuomba kwasababu ya kukata tamaa, ingawa si watu wengi wanajua jambo hili.

✍️Katika sehemu sehemu ya 1 ya somo hili, tulianza kuangalia madhara ya kuacha kuomba kwasababu ya kukata tamaa. K**a haujapata nafasi ya kufuatilia sehemu ya 1 ya somo hili, jitahidi ufuatilie kwasababu kuna vitu muhimu ambavyo nilifundisha.

✍️Siku ya leo naomba tuangalie madhara mengine ya kuacha kuomba kwasababu ya kukata tamaa 👇👇

*MADHARA YA 2: KUKOSEKANA KWA NGUVU AMBAYO INAHITAJIKA NA MUNGU ILI AITUMIE KATIKA KUJIBU MAOMBI YAKO*

✍️Unapokuwa unaomba, kuna kiasi/kiwango fulani cha nguvu za Mungu zinazotoka ndani yako (kiwango fulani cha nguvu za Mungu zinazofanya kazi muda huo kutoka ndani yako), na hicho kiwango cha nguvu za Mungu ndicho ambacho Mungu anakitumia katika kujibu maombi yako.

✍️Kwahiyo ukikata tamaa na kuacha kuomba, maana yake ni kwamba, *kunakosekana nguvu za Mungu kutoka ndani yako ambazo zipo kazini, ambazo Mungu ndizo anazotakiwa kuzitumia katika kujibu maombi yako.*

📖Waefeso 3:20 *Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu.*

*MSISITIZO:* Msisitizo mkubwa kwenye huo mstari sio tu nguvu, bali nguvu itendayo kazi ndani yetu (nguvu iliyopo kazini).

✍️Kwenye huo mstari, unaona wazi kabisa kwamba Mungu anafanya mambo ya ajabu mno kuliko yale tuyaombayo au tuyawazayo, *kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu.*

✍️Nguvu itendayo kazi ndani yetu, ni kiwango cha nguvu za Mungu kilichopo kazini wakati husika. Yaani kiasi cha nguvu za Mungu kutoka ndani yetu ambacho kinatumika wakati husika.

*✍️Hiyo nguvu itendayo kazi ndani yetu, ndiyo nguvu ya Mungu ambayo Mungu anaitumia katika kujibu maombi yetu wakati tunaombea jambo fulani.*

*KUMBUKA:* Wakati wewe umekata tamaa na kuacha kuomba na huku unasema kwamba unamuachia Mungu, fahamu ya kwamba kunakuwa hakuna kitu kinachoendelea ambacho kitasukuma majibu ya maombi yako kuja kwako. Maana kunakuwa hakuna nguvu itendayo kazi ndani yako, ambayo Mungu ataitumia katika kujibu maombi yako.

‼️Ni hasara kubwa sana kukata tamaa na kuacha kuomba, na huku unasubiri majibu kutoka kwa Mungu, wakati hakuna nguvu ya Mungu kutoka ndani yako ambayo itasukuma majibu yako kutoka kwa Mungu kuja kwako.

🔺Mara nyingi mtu ukikata tamaa na ukaacha kuomba, Roho Mtakatifu anakuwa anakuletea himizo la kukutaka uendelee kuomba, kwasababu anajua kwamba hakuna kitakachoendelea, zaidi ya kujichelewesha tu kuja kupata majibu ya maombi yako.

* AKIWA GEREZANI*
✍️Petro akiwa gerezani na amefungwa minyororo, alikuwa amekata tamaa na anasubiri tu kuuwawa na Herode.

✍️Kutokana na kwamba Petro alikuwa amekata tamaa ya kuishi, hivyo kule gerezani alikuwa haombi, bali analala tu.

✍️Kitendo cha Petro kutokuomba, maana yake ni kwamba kilikuwa hakifungui mlango wa msaada wa Mungu kuja kwake.

* ya juhudi ya Kanisa kwa ajili ya Petro:*
✍️Kilichomsaidia Petro kutoka gerezani ni *maombi ya juhudi,* ambayo kanisa liliomba kwa ajili yake.

📖Matendo ya Mitume 12:4-5
[4] Alipokwisha kumk**ata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu. [5] Basi Petro akalindwa gerezani, *nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.*

✍️Maombi ya juhudi, sio maombi ya kawaida, bali ni maombi ambayo ndani yake yamebeba bidii, kuomba bila kukoma na kutokata tamaa, haijalishi mazingira ya anayeombewa yakoje au jambo linaloombewa yakoje.

✍️Maombi ya juhudi ambayo yaliombwa na kanisa kwa ajili ya Petro, ndiyo yaliyoachilia nguvu za Mungu kutoka ndani ya waombaji, ambazo Mungu alizitumia katika kumtoa Petro gerezani kwa kumtuma malaika.

📖Matendo ya Mitume 12:7-8
*[7] Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka mikononi. [8] Malaika akamwambia, Jifunge, kavae viatu vyako. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, Jivike nguo yako, ukanifuate.*

✍️Kumbuka ile Waefeso 3:20 ya kwamba *"Mungu anajibu yale tuyaombayo au tuyawazayo kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu"*. Kwahiyo Mungu alitumia nguvu zilizokuwa kazini wakati kanisa linaomba kwa juhudi, kwa ajili ya kumwokoa Petro dhidi ya mikono ya Herode.

*ZINGATIA:* K**a kanisa lisingemwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili ya Petro, ni wazi kabisa kwamba Petro angeuwawa na Herode, kwasababu yeye binafsi alikuwa amekata tamaa na haombi, *hivyo hakukuwa na nguvu zilizokuwa kazini kutoka ndani yake, ambazo Mungu angezitumia katika kujibu maombi yake na kumwokoa.*

🔺Hili jambo la Mungu kujibu maombi yako kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yako, ni moja ya kanuni za kiroho, ambazo zinahusisha ushirikiano wa Mungu na mwanadamu kiutendaji.

✍️NI HASARA KUBWA SANA KUKATA TAMAA NA KUACHA KUOMBA, HALAFU HUKU UNAJIFARIJI KWAMBA MUNGU ATAJIBU TU KWA WAKATI WAKE.

✍️KUSUBIRI MAJIBU KWA MUNGU WAKATI UMEKATA TAMAA NA HAUOMBI, NI SAWA NA KUENDELEA KUJIPOTEZEA MUDA WAKO.

🔺KILA WAKATI INAPOKUJA HALI YA KUKATA TAMAA NA KUACHA KUOMBA, NI LAZIMA UJIULIZE KWAMBA SASA MUNGU ATAJIBU MAOMBI YANGU KWA KUTUMIA NGUVU GANI WAKATI HAKUNA NGUVU INAYOACHILIWA, AMBAYO MUNGU ANATAKIWA AITUMIE KUJIBU MAOMBI YAKO??

🔺K**A KUNA JAMBO ULIKUWA UMELIKATIA TAMAA NA UMEACHA KULIOMBEA, NAKUSHAURI ANZA KULIOMBEA TENA KWA JUHUDI KUBWA, BADALA YA KUSUBIRI MAJIBU HEWA.

*Somo litaendelea sehemu ya 3......*

ujumbe huu, nina amini umepata kitu cha kukusaidia.

+Mungu akupe nguvu ya kuendelea kuombea vitu bila ya kukata tamaa.

°Ni sisi ndugu zako katika mwili wa Kristo,
* , Mwl Mandela & Devotha Mwambeso*
0752197065
Dodoma, Tanzania
Email: [email protected]

10/03/2026

SOMO: *"MADHARA YA KUACHA KUOMBA KWASABABU YA KUKATA TAMAA"*

*Sehemu ya 1*

✍️Watu wengi wanapopitia mahali pagumu au wanapoona majibu ya maombi yao hawajayapata kwa wakati ambao walitarajia, huwa wanakata tamaa na kuacha kuomba.

✍️Katika mazingira k**a hayo ya kukata tamaa na kuacha kuomba, sio watu wengi wanajua kwa upana juu ya madhara ya kuacha kuomba kwasababu ya kukata tamaa.

✍️Ni kweli kabisa neno la Mungu liko wazi kabisa kwenye Mithali 13:12 ya kwamba *"Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua.* Lakini madhara ya kukata tamaa na kuacha kuomba ni makubwa zaidi.

✍️Madhara ya kukata tamaa na kuacha kuomba ni makubwa sana, ndio maana Yesu alisema maneno yafuatayo👇👇
📖Luka 18:1......*imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.*

✍️Yesu asingeweza kusema hayo maneno, k**a hakuna madhara ya kukata tamaa na kuacha kuomba.

* YA 1: KUKATIKA KWA MAWASILIANO YAKO NA MUNGU.*

✍️Njia mojawapo ya kuwasiliana na Mungu ni maombi. Hivyo ukikata tamaa na kuacha kuomba, maana yake unakuwa umekata mawasiliano yako na Mungu.

✍️Mawasiliano yako na Mungu yakikatika ni hatari sana na itakuwa ni vigumu sana kupata msaada wa Mungu juu ya jambo ambalo umelikatia tamaa.

✍️Shetani anatumia sana mbinu hii ya kuwakatisha watu tamaa na kuwafanya waache kuomba, ili wapoteze mawasiliano yao na Mungu.

* :*
Mawasiliano yako na Mungu yakikatika kwasababu ya kukata tamaa kwako na kuacha kuomba, Mungu anaweza akakuotesha ndoto kwamba umepoteza simu.

✍️K**a ambavyo simu inatumika kwa ajili ya mawasiliano, Mungu anatumia lugha ya picha ya kupoteza simu, ili kukupa taarifa kwamba mawasiliano yangu na wewe yamepotea.

✍️Wakati mwingine unaweza ukaota kwamba simu yako imeibiwa. Hii maana yake unakuwa unajulishwa kwamba shetani amehusika katika kupoteza kwako mawasiliano yako na Mungu.

*Kumbuka;* Kazi mojawapo ya shetani ni kuiba.
📖Yohana 10:10 *Mwivi haji ila aibe* na kuchinja na kuharibu;....

*Mwivi anayezungumzwa hapo ni shetani.

‼️Jihadhari kuacha kuomba kwasababu ya kukata tamaa, maana mawasiliano yako na Mungu yakikatika itakuwa ni vigumu sana sana kupata msaada wa Mungu juu ya ulichokuwa unakiombea.

‼️Mawasiliano yako na Mungu yakikatika, huo ndio mwanzo wa wewe kupoteza mwelekeo kabisa.

‼️Utaanza kufanya maamuzi ambayo yatakugharimu vibaya sana.

‼️Utaanza kupita njia ambazo zitakupeleka mahali pabaya.

‼️Utatumbukia kwenye mashimo ambayo yatakusumbua sana kutoka.

✍️Mawasiliano yako mazuri na Mungu ni mlango mkubwa sana wa kupatia na kupokelea msaada kutoka kwa Mungu juu ya jambo ambalo umekuwa ukiliombea au juu ya mahali pagumu ambapo umekuwa unapita.

‼️KUACHA KUOMBA KWASABABU YA KUKATA TAMAA, NI JAMBO LA HATARI SANA.

❌KAMWE USIKUBALI MAWASILIANO YAKO NA MUNGU YAKATIKE KWA KUACHA KUOMBA KWASABABU TU MAHALI PAGUMU UNAPOPITA AU KUTOPATA MAJIBU YA MAOMBI YAKO KWA WAKATI AMBAO ULITAMANI WEWE.

*Somo litaendelea sehemu ya 2......*
Bwana Yesu akubariki na akutunze.

* , Mwl Mandela & Devotha Mwambeso*
0752197065
Dodoma, Tanzania
Email:[email protected]

03/10/2025

*"USIIGE MFUMO WA WATU AMBAO HAWAOMBI, LAKINI MAMBO YAO YANAONEKANA KWENDA TU"*

✍️Kati ya kosa mojawapo ambalo hautakiwi kulifanya, ni kujaribu kuiga mfumo wa watu ambao hawaombi na mambo yao yanaonekana kwenda tu.

✍️ Hilo kosa litakugharimu vibaya sana mwana wa Mungu.

✍️Siku zote ni lazima ujue kwamba hatufanani huku duniani.
*1. Hatma zetu hazifanani*

*2. Aina za vita tulizonazo hazifanani.*

*3. Idadi ya maadui hatufanani.*

*4.Jamii na koo tulizotoka hazifanani.*

*5.Maono tuliyonayo hayafanani.*

*6.Tulichobebeshwa na Mungu kwa ajili ya familia, kanisa, Taifa, hatufanani.* n.k

✍️K**a mambo mengi hatufanani, basi itakuwa ni hatari sana kwako kutaka kuishi kienyeji k**a watu wengine, ambao hata wasipoomba mambo yao yanaonekana kwenda tu.

✍️Itakuwa ni hatari sana kwako wewe ambaye una maadui wengi na una vita nyingi, kutaka kuishi kienyeji bila kupambana kwenye maombi.

* *
✍️Daudi alikuwa na maadui wengi na vita nyingi kwenye maisha yake, kiasi kwamba ilimlazimu kuishi maisha ya maombi kila siku, tena maombi ya mara 3 kwa siku.

📖Zaburi 55:17 *Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua, Naye ataisikia sauti yangu.*

✍️ Kuomba mara 3 kwa siku kulimsaidia sana Daudi kufanikiwa katika kutimiza kusudi la Mungu kwenye maisha yake.
13:36

* *
✍️Ili Danieli aweze kutimiza kusudi la Mungu kwenye maisha yake, ilimlazimu kuishi maisha ya maombi, yaani kuomba mara 3 kwa siku maana alizungukwa na watu wenye wivu, wachawi na waganga katika eneo lake la kazi.
6:1-10

❌ACHA KUIGA MFUMO WA WATU WENGINE AMBAO HAWAOMBI LAKINI MAMBO YAO YANAENDA TU.

‼️MWENZANGU NA MIMI USIPOPAMBANA KWENYE MAOMBI, MAISHA YAKO YATATAWALIWA NA MIKWAMO YA KILA AINA, MAANA HATMA YAKO NI KUBWA NA MAADUI ZAKO NI WENGI.

‼️ MWENZANGU NA MIMI AMBAYE UNATAKA KUTIMIZA KUSUDI LA MUNGU KWENYE DUNIA HII, NI LAZIMA UPAMBANE SANA KWENYE MAOMBI MAANA SHETANI HAWEZI KUKUBALIANA NA HILO.

‼️K**A KWELI HAUTAKI KUISHI MAISHA YA HASARA KWENYE DUNIA HII, MAOMBI NI LAZIMA, TENA MAOMBI YA KUMAANISHA KWELI KWELI.

‼️WEWE AMBAYE UNA MAADUI WENGI NA UNA VITA NYINGI HALAFU HAUTAKI KUOMBA, NAKUAMBIA HATA MAISHA YAKO YANAWEZA YAKAWA MAFUPI NA YALIYOJAA TABU NYINGI.

✍️WEWE AMBAYE UNAJUA KABISA KWAMBA HAPO ULIPOFIKA MAOMBI YAMEHUSIKA SANA, KAMWE USIJE UKAINGIA KWENYE MFUMO WA WATU WASIOOMBA NA MAMBO YAO YANAONEKANA KWENDA TU. UTAPATA HASARA KUBWA SANA.

* , OMBA, OMBA*

* ,Mwl Mandela & Devotha Mwambeso*
0752 197065
Dodoma, Tanzania

27/08/2025

* YAKO*
✍️Usiyachukie mapito yako, wala usimkasirikie Mungu kwa kuruhusu upitie mahali pagumu ulipopita/unapopita.

✍️Mapito yana faida kubwa sana, hata k**a ndani yake yamebeba machungu, maumivu na kila aina ya mateso.

✍️K**a Mungu anakuandaa na kitu kikubwa huko mbele, mapito ni sehemu ya maisha/darasa lako.

✍️Njia za kuuendea ukuu, hazijawahi kuwa nyepesi. Jipe moyo mkuu mwana wa Mungu.

*1.Ndani ya mapito, kuna kufinyangwa, ili uweze kufaa zaidi.*
°Wewe ni udongo mikononi mwa Mungu.
{Yeremia 18:1-6}

*2.Ndani ya mapito, kuna kutengenezwa.*
°Yusufu alitengenezewa moyo wa huruma kwa watu, akiwa kwenye mapito.
{Mwanzo 40:1-8}
{Zaburi 105:19}

*3.Ndani ya mapito, kuna kurekebishwa.*
°Mapito yanakuonyesha njia sahihi za kupita.

*4.Ndani ya mapito, kuna kufundishwa.*
°Huwezi kuwa Mwalimu mzuri na mshauri mzuri k**a darasani haujapita.
°Yesu alijaribiwa na akashinda, ndio maana ana uwezo wa kuwasaidia wanaojaribiwa.
{Waebrania 2:18}

*5.Ndani ya mapito, kuna kuondolewa tabia zisizofaa, ili thamani yako ipande/iongezeke.*
°Wewe ni Sawa na dhahabu, unapochomwa ni kwa lengo la kukuondolea uchafu ili thamani yako ipande.
{Ayubu 23:10}

*6.Ndani ya mapito, kuna kutengenezewa nidhamu.*
°Jangwani ilikuwa inawatengenezea nidhamu Wana wa Israeli jinsi ya kuishi wakifika Kanaani (nchi ya maziwa na asali).

*7.Ndani ya mapito, kuna kuimarishwa.*
°Mapito ya Daudi maporini, yalimwimarisha na kumfanya kuwa jasiri, na hatimaye akawa msaada kwa Taifa lake.

*8.Ndani ya mapito, kuna kukuzwa.*
°Utakuzwa kiakili, kiufahamu na kiusemi. Pia utakuzwa katika kumjua Mungu.
{1Wakoritho 13:11}
{2Petro 3:18}

*9.Ndani ya mapito, kuna kukomazwa.*
°Unakomazwa ili huko mbele usiyumbishwe na tufani na dhoruba za kila aina.
{Mathayo 7:24-27}

*10.Ndani ya mapito, kuna kukamilishwa.*
{Yakobo 1:2-4}

_📖Waebrania 5: *[7]Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;[8]na, ingawa ni Mwana, alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata;[9]naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii.*_

* ZA KUUENDEA UKUU HAZIJAWAHI KUWA NYEPESI.*

* MOYO MKUU MWANA WA MUNGU. UKIVUKA HAPO, UTAKUWA MTU BORA SANA.*

, Mwl Mandela & Devotha Mwambeso
0752 197065
Dodoma, Tanzania
Email:[email protected]

27/08/2025

*"JARIBU NA MLANGO WA KUTOKEA"*

*1.Jaribu ni kipimo*
✍️Unapojaribiwa maana yake ni kwamba unakuwa unapimwa.

✍️Kwenye jaribu, unaweza ukapimwa na Mungu au shetani au tamaa zako mwenyewe.

*2.Jaribu linakuwa ni jaribu hadi limekufikisha njiapanda kimaamuzi.*
✍️Usipofika njiapanda, hilo sio jaribu bali ni changamoto tu.

*3.Mungu anaporuhusu jaribu lije kwako, ni kwa lengo la kukuimarisha.*
{Yakobo 1:2-4}

✍️Mungu aliporuhusu Roho Mtakatifu ampeleke Yesu nyikani kujaribiwa na Ibilisi, ilikuwa ni kwa lengo la kumuimarisha zaidi, anapoingia kwenye utumishi wake.
{Luka 4:1,2}

*4. Shetani anapokuletea jaribu, ni kwa lengo la kukuangusha.*

✍️Shetani alipokuwa analeta majaribu kwa Ayubu, lengo lake lilikuwa ni kumwangusha Ayubu katika imani na si vinginevyo.
{Ayubu 1:7-11}

✍️Shetani alipokuwa analeta majaribu kwa Yesu, lengo lake lilikuwa ni kumwangusha Yesu k**a alivyomwangusha Adamu wa kwanza.
{Luka 4:1-13}

*5. Kila jaribu ambalo Mungu analiruhusu lije kwako, liko ndani ya uwezo wako.*

✍️Mungu hawezi kuruhusu jaribu ambalo liko nje ya uwezo wako, lije kwako.

✍️Kila jaribu ambalo Mungu analiruhusu lije kwako, ni size yako kabisa.

📖1 Wakorintho 10:13 *Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu;*.......

*6. Kila jaribu ambalo Mungu analiruhusu lije kwako, lina mlango wake wa kutokea.*

❌ Hakuna jaribu ambalo halina mlango wa kutokea.

📖1Wakorintho 10:13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; *lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea,* ili mweze kustahimili.

*7. Si kila mlango ni mlango sahihi wa jaribu lako kutokea.*

✍️Unatakiwa kuwa mwangalifu sana, unapokuwa kwenye jaribu na unataka kutoka, maana sio kila mlango ni mlango sahihi wa jaribu lako kutokea.

: *Mlango mwingine unaweza ukakuingiza kwenye matatizo makubwa zaidi ya hilo jaribu. Badala ya kutoka, ukajikuta ndio umepotea zaidi.*

* :*
✍️Ibrahimu na Sara wakiwa kwenye jaribu la kutopata mtoto kwa muda mrefu, walitafuta mlango wa kuzaa mtoto kupitia mjakazi wao (Hajiri) na kweli wakampata mtoto (Ishmaeli).

✍️Lakini yule mtoto alikuwa chanzo kikubwa sana cha ugomvi kwenye ndoa na familia ile, tangu mimba yake ilipotungwa tu.
°Mwanzo 16:1-6
°Mwanzo 21:8-12

*8. Ukiwa kwenye jaribu, kuwa mwangalifu sana na ushauri unaopewa na watu, ili uweze kutoka kwenye hilo jaribu.*

✍️Sio kila ushauri ni mzuri na unafaa kukusaidia kutoka kwenye jaribu. *Ushauri mwingine utakupoteza kabisa na pengine kukupeleka mbali na uso wa Mungu.*

✍️Mara nyingi sana shetani huwa anatumia watu(washauri) kwa ajili ya kukupoteza.

* :* Ayubu akiwa ndani ya majaribu mazito, mke wake alimpa ushauri ambao haukuwa mzuri, kwamba ni heri amkufuru tu Mungu na afe.
{Ayubu 2:9,10}

* :* Shetani alimwingia Petro kwa ajili ya kumpa Yesu ushauri ili asipite msalabani.
{Mathayo 16:21-23}

‼️UNISIKILIZE VIZURI MWANA WA MUNGU; *Sijajua unapitia jaribu la namna gani, lakini nakushauri siku ya leo, kwamba kuwa mwangalifu sana sana na ushauri wa watu.*

*9. Anayefanya mlango wa jaribu lako kutokea sio wewe bali ni Mungu.*

📖1Wakorintho 10:13..... *lakini pamoja na lile jaribu atafanya(Mungu) na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.*

✍️Mungu aliyeruhusu jaribu lije kwako, ndiye anayefanya na mlango wa kutokea kwa hilo jaribu, na sio wewe unayefanya mlango.

*✍️Ukiwa ndani ya jaribu, wewe muombe Mungu akuonyeshe na akufanyie na mlango wa kutokea kwa hilo jaribu, kwasababu yeye anaujua huo mlango.*

*10. Ukiwa ndani ya jaribu, acha kulaumu watu na kugombana na watu.*

✍️Kulaumu watu na kugombana na watu, inaweza ikawa ni sababu mojawapo ya jaribu lako kuendelea kuwa gumu na pengine kukupeleka kuingia kwenye majaribu mengine.

*11. Ukiwa ndani ya jaribu, acha kumkasirikia na kumnung'unikia Mungu.*

✍️Tafsiri mojawapo ya Kibiblia ya kumnung'unikia Mungu ni *kumdharau na kutomwamini Mungu.*

✍️Wana wa Israeli walipokuwa wanamnung'unikia Mungu baada ya kupewa taarifa mbaya na wapelezi 10, *Mungu alisema wanamdharau na hawamwamini.*
°Hilo likamkasirisha sana Mungu na akawashughulikia kweli kweli.
{Hesabu 14}

*KUMBUKA: Ukimkasirikia Mungu k**a Mwalimu, hauwezi kuelewa anachokufundisha ndani ya hilo jaribu.*
°Kumkasirikia na kumchukia Mwalimu, ni mlango mkubwa sana wa kufeli na somo lake.

*12. Ukiwa ndani ya jaribu, tafuta kujua Mungu anakufundisha kitu gani?*

*✍️Mungu hataki kukutoa kwenye jaribu, bila ya wewe kupata somo ndani ya hilo jaribu.*

✍️Ukidaka somo mapema ndani ya jaribu lako, inakuwa ni rahisi pia kutoka kwenye jaribu mapema.

✍️Ukishindwa kupata somo ndani ya jaribu lako, hilo jaribu linaweza kuchukua muda mrefu zaidi.

✍️Ukiwa ndani ya jaribu, *Jifunze kumuomba Mungu, ili akujulishe sababu za wewe kupitia hilo jaribu.* Hii itakusaidia kupata somo mapema.

* **A UPO KWENYE JARIBU NA HAUJUI KUSUDI LA MUNGU KURUHUSU HILO JARIBU, NAKUOMBEA ILI MUNGU AKUPE UFAHAMU JUU YA HILO; KATIKA JINA LA YESU KRISTO.*

* **A UPO KWENYE JARIBU NA UMECHOKA SANA, NAMUOMBA MUNGU KWA AJILI YAKO ILI AKUPE NGUVU YA KUSONGA MBELE; KATIKA JINA LA YESU KRISTO.*

: *USIYACHUKIE MAJARIBU AMBAYO MUNGU ANAYARUHUSU YAJE KWAKO, KWASABABU YAPO KWA AJILI YA KUKUFANYA UWE BORA ZAIDI KIROHO NA KIMAISHA.*

+Mungu akutunze na akubariki.
* ,Mwl Mandela & Devotha Mwambeso*
0752 197065
Email:[email protected]
Dodoma, Tanzania

27/08/2025

*"UAMINIFU WA MUNGU ALIYE HAI KATIKA KRISTO YESU"*

✍️Ongeza ufahamu wako kuhusu Mungu aliye hai katika Kristo Yesu na uaminifu wake, ili unufaike kupitia huo ufahamu 👇

*1. MUNGU JINA LAKE NI MWAMINIFU.*

✍️Mungu sio tu kwamba ni mwaminifu, bali mwaminifu ni jina lake pia.

✍️Hiyo inatosha kabisa kukupa picha kwamba hautakiwi kuwa na mashaka ya aina yoyote kuhusu uaminifu wa Mungu, maana uaminifu wake unaanzia kwenye jina lake lenyewe.

📖Ufunuo wa Yohana 19:11 Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye *Mwaminifu na Wa-kweli,* naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

*2. MUNGU NI MWAMINIFU KWENYE AHADI ZAKE.*

✍️Siku zote fahamu ya kwamba, *Ahadi za Mungu ni kweli tupu. Hakuna uongo ndani yake.*

*KUMBUKA: Mungu hawezi kuahidi kitu ambacho hakitimiziki. Ukiona Mungu ameahidi, ujue ameipima hiyo ahadi kwamba inatimizika.*

📖2Samweli 22:31 Mungu njia yake ni kamilifu;
*Ahadi ya BWANA imehakikishwa;*
Yeye ndiye ngao yao
Wote wanaomkimbilia.

✍️Mungu akiahidi anatimiza. Sulemani alikiri hilo jambo kwa kinywa chake, baada ya kuona Mungu anatimiza yale ambayo alimwahidi baba yake Daudi.

📖1Wafalme 8:24 *Umemtimizia mtumishi wako, Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidia; naam, ulinena kwa kinywa chako, ukayatimiza kwa mkono wako, k**a ilivyo leo.*

✍️Ibrahimu kwa kujua uaminifu wa Mungu kwenye ahadi zake, kulimfanya aendelee kusubiri kwa miaka mingi utimilifu wa ahadi ya Mungu kumpa mtoto.

📖Warumi 4:20-21
*[20]Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini, bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu; [21]huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.*

* KABISA MASHAKA JUU YA UAMINIFU WA MUNGU KWENYE AHADI. K**A AMEKUAHIDI, UWE NA UHAKIKA KWAMBA ATATIMIZA. AMINI HIVYO NA KUWA NA UVUMILIVU NDANI YAKO.*
📖Waebrania 6:15 *Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi.*

*3. MUNGU NI MWAMINIFU KWENYE MAAGANO.*

✍️Mungu ni Mungu wa maagano.

✍️Mungu ni mwaminifu sana kwenye maagano anayoyafanya na watu wake.

✍️Ukifanya agano na Mungu, uwe na uhakika kwamba hilo agano atalifuatilia siku zote.

✍️Mungu anauwezo wa kufuatilia agano kwa vizazi na vizazi, maana yeye ni Mungu ashikaye maagano.

✍️Mungu alifuatilia agano alilofanya na Ibrahimu kuhusu uzao wake, baada ya miaka mia nne (400)
Mwanzo 15:13-21
Kutoka 2:23-25
Kutoka 12:36,41

✍️Sulemani alikiri jambo hili la Mungu kushika maagano.

📖2 Mambo ya Nyakati 6:14 akasema, Ee BWANA, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu k**a wewe, mbinguni, wala duniani; *ushikaye maagano* na rehema kwa watumishi wako, waendao mbele zako kwa moyo wao wote;

✍️Danieli k**a mwombaji, alijua jambo hili pia kwamba Mungu anashika maagano na akatumia kwenye maombi yake.

📖Danieli 9:4 Nikamwomba BWANA, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, *ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake.*

*4. MUNGU NI MWAMINIFU KWENYE NENO LAKE.*

✍️Mungu ni mwaminifu sana kwenye neno lililotoka kwenye kinywa chake.

✍️Mungu akitoa neno kwenye kinywa chake, siku zote anakuwa mwaminifu kulitimiza. Ndio maana alimwambia hivyo Yeremia.

📖Yeremia 1:12 Ndipo BWANA akaniambia, Umeona vema, kwa maana *ninaliangalia neno langu, ili nilitimize.*

📖Zaburi 89:34 Mimi sitalihalifu agano langu, *Sitalibadili neno lililotoka midomoni mwangu.*

📖Isaya 55:11 *ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.*

*ZINGATIA: Neno alilolisema Mungu, ndivyo lilivyo. Wewe lipokee tu, liamini na kuliweka kwenye matendo.* Utapata matokeo tu.

*5. UAMINIFU WA MUNGU UNAFIKA HATA MAWINGUNI.*

✍️Hii ni ishara kwamba uaminifu wa Mungu una uwezo wa kwenda umbali mrefu sana. Kutoka kwenye ardhi hadi kwenye mawingu, kuna umbali mrefu sana.

📖Zaburi 36:5 Ee BWANA, fadhili zako zafika hata mbinguni, *Uaminifu wako hata mawinguni.*

*6. UAMINIFU WA MUNGU UMEMZUNGUKA.*

✍️Mungu sio tu kwamba ni mwaminifu, bali uaminifu wenyewe umemzunguka. Hii inathibitisha kiwango cha juu sana cha uaminifu wa Mungu.

📖Zaburi 89:8 BWANA, Mungu wa majeshi,
Ni nani aliye hodari k**a Wewe, Ee YAHU?
*Na uaminifu wako unakuzunguka.*

*KUMBUKA:* Mungu amezungukwa na uaminifu, ndio chochote anachokifanya, huwa anakifanya kwa uaminifu.
33:4

*7. UAMINIFU WA MUNGU HAUZUILIWI NA MAZINGIRA.*

✍️Mazingira sio kikwazo kwa Mungu kuonyesha uaminifu wake.

✍️Ukiwa kwenye moto, Mungu ni mwaminifu. Ukiwa jangwani, Mungu ni mwaminifu. Ukiwa shimoni, Mungu ni mwaminifu.

📖Isaya 43:2 *Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.*

✍️Mungu alionyesha uaminifu kwa Danieli akiwa kwenye tundu la simba.
6:16-22

✍️Mungu alionyesha uaminifu kwa Meshaki, Shadraka na Abednego wakiwa kwenye tanuru la moto.
2:13-30

✍️Mungu alikuwa mwaminifu kwa Yusufu alipotupwa shimoni na ndugu zake na pia akawa mwaminifu akiwa gerezani.
39:20-23

*8. UAMINIFU WA MUNGU NI WA VIZAZI NA VIZAZI.*

✍️Uaminifu wa Mungu haupo kwenye kizazi kimoja tu, bali kwa vizazi na vizazi.

✍️Vizazi vinakuja na kuondoka, na Mungu ni mwaminifu kwa vizazi vyote hivyo.

📖Zaburi 119:90 *Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi,* Umeiweka nchi, nayo inakaa.

📖Zaburi 100:5 Kwa kuwa BWANA ndiye mwema; Rehema zake ni za milele; *Na uaminifu wake vizazi na vizazi.*

*9. UAMINIFU WA MUNGU NI WA MILELE.*

✍️Uaminifu wa Mungu sio tu kwamba upo kwa vizazi na vizazi, bali ni wa milele.

✍️Uaminifu wa Mungu kuwa wa milele maana yake ni kwamba *hauna mwisho.*

📖Zaburi 117:2 Maana fadhili zake kwetu sisi ni kuu, *Na uaminifu wa BWANA ni wa milele.*

*10. UAMINIFU WA MUNGU HAUTEGEMEI KUJIBU AU KUTOKUJIBU MAOMBI YAKO.*

❌Kamwe usifanye kosa la kupima uaminifu wa Mungu kwa kuangalia kujibiwa au kutokujibwa kwa maombi yako.

✍️Hii ni kwasababu kuna maombi mengine unaweza ukajibiwa nje ya mapenzi yake na ukapata shida badae.

📖Zaburi 106:15 *Akawapa walichomtaka, Akawakondesha roho zao.*

✍️Kitendo cha Mungu kutokujibu maombi yako, hakiondoi uaminifu wa Mungu.

✍️MUNGU NI MWAMINIFU NA ATAENDELEA KUWA MWAMINIFU MILELE, HATA K**A HAJAJIBU MAOMBI YAKO.

*ZINGATIA: MUNGU KUTOKUJIBU MAOMBI YAKO KWASABABU ZAKE, HUO NAO NI UAMINIFU WA KIWANGO CHA JUU SANA. HII INAONYESHA NI KIASI GANI NI MWAMINIFU KWENYE PENDO LAKE KWAKO.*

+Mungu akubariki sana. Ninaamini umepata kitu cha kukusaidia kuhusu uaminifu wa Mungu aliye hai katika Kristo Yesu.

* ,Mwl Mandela & Devotha Mwambeso*
0752 197065
Email:[email protected]
Dodoma, Tanzania

27/08/2025

*"HASIRA INAVYOWEZA KUHARIBU HATMA YAKO"*

*Sehemu ya 2:*

✍️Katika sehemu ya 1 ya somo hili, nilizungumza kwa habari za hasira kuharibu maisha ya watu wengi.

✍️Kutoka kwenye Biblia, tuliangalia habari za Kaini na jinsi hasira ilivyoharibu hatma yake.

✍️K**a haukupata nafasi ya kufuatilia somo hili sehemu ya 1, nakushauri ufuatilie kwanza, ili upate picha pana, itakayokusaidia kuunganisha na ujumbe wa siku ya leo.

✍️Siku ya leo tuangalie mfano mwingine kutoka kwenye Biblia juu ya hasira na jinsi inavyoweza kuharibu hatma ya mtu.

* #2.MUSA*
✍️Hasira ilimgharimu vibaya sana Musa, mtumishi wa Mungu.

✍️Hasira ilimpelekea Musa kufanya kitu ambacho hakutakiwa kufanya na ikamgharimu sana katika utumishi wake na maisha yake.

✍️Manung'uniko ya Wana wa Israeli ya kukosa maji, yalimkasirisha sana Musa na akajikuta amefanya makosa makubwa mawili(2);
*1. Kusema yasiyofaa.*

*2. Kufanya kinyume na maelekezo ya Mungu.*

✍️Ili wana wa Israeli wapate maji, Mungu alimwambia Musa akiwa na fimbo yake akuambie mwamba utoe maji, *lakini yeye akasema maneno yasiyofaa na akaupiga mwamba mara mbili.*

📖Hesabu 20:8-11
*[8]Twaa ile fimbo, ukawakusanye mkutano, wewe na Haruni ndugu yako, ukauambie mwamba mbele ya macho yao utoe maji yake, nawe utawatokezea maji katika mwamba,* na hivyo utawanywesha maji mkutano na wanyama wao.
[9]Musa akaitwaa hiyo fimbo kutoka mbele za BWANA k**a alivyomwamuru.
[10]Musa na Haruni wakawakusanya kusanyiko mbele ya mwamba, akawaambia, *Sikieni sasa, enyi waasi; je! Tuwatokezee maji katika mwamba huu?*
*[11]Musa akainua mkono wake akaupiga ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi,* mkutano wakanywa na wanyama wao pia.

✍️Kosa alilofanya Musa lilimfanya asiingie nchi ya ahadi, wakati alikuwa amefanya kazi kubwa sana kwa ajili ya Wana wa Israeli kuanzia kule Misri.

📖Hesabu 20:12 *BWANA akamwambia Musa na Haruni, Kwa kuwa hamkuniamini mimi, ili kunistahi mbele ya macho ya wana wa Israeli, basi kwa sababu hiyo, hamtawaingiza kusanyiko hili katika ile nchi niliyowapa.*

*KUMBUKA: Kilichomgharimu Musa asiingie nchi ya ahadi kwa kufanya asichotakiwa kufanya ni hasira.*

✍️Hasira ilimwingiza Musa kwenye hasara kubwa.

📖Zaburi 106:32-33
[32]Wakamghadhibisha penye maji ya Meriba,
*Hasara ikampata Musa kwa ajili yao,* [33]Kwa sababu waliiasi roho yake, *Akasema yasiyofaa kwa midomo yake.*

* YA HASIRA YA MUSA*
✍️Musa alikuwa na hasira sana na ile hasira ilikuwa ni ya kurithi kutoka kwenye kabila lake la Lawi.
{Mwanzo 49:

📖Mwanzo 49:5-7
*[5]Simeoni na Lawi ni ndugu; Panga zao ni silaha za jeuri.*
[6]Nafsi yangu, usiingie katika siri yao, Fahari yangu usiungane na kusanyiko lao,
*Maana katika ghadhabu yao walimuua mtu,*
Na kwa ukaidi wao walikata mshipa wa ng’ombe;
*[7]Ghadhabu yao na ilaaniwe, maana ilikuwa kali, Na hasira yao, maana ilikuwa haina huruma.* Nitawagawa katika Yakobo,
Nitawatawanya katika Israeli.

✍️Ukitaka kujua zaidi kwamba Musa alikuwa na hasira sana; angalia maneno aliyomwambia Mungu baada ya baadhi ya watu (Kora, Dathani na Abilamu) kushinda nae katika utumishi wake.

✍️Musa alimwambia Mungu maneno magumu sana ya kwamba, *watu hawa wakifa kifo cha kawaida, basi Mungu hakumtuma kwenye ule utumishi.*
Hapo ndipo unapoona ardhi ikifunua kinywa chake na kuwameza watu wakiwa hai.
{Hesabu 16:28-33}

✍️Sasa ukiangalia hasira yote hiyo ya Musa, ni hasira ya kurithi kutoka kwenye kabila lake la Lawi.

✍️Ukimfuatilia vizuri Musa, utagundua kwamba *alikuwa ni mtumishi wa Mungu mzuri sana, lakini hasira ilimgharimu vibaya sana katika utumishi wake na maisha yake kwa ujumla.*

* HASIRA*
✍️Unapoombea jambo la hasira, wakati mwingine chunguza kwenye familia/ukoo uliotoka, kwasababu wakati mwingine unaweza ukakuta ni kitu ambacho umerithi.

✍️Vitu vya kurithi vinasumbua sana iwapo hautajua namna ya kuviombea.

✍️Unapoombea vitu vya kurithi, unatakiwa kutambua ya kwamba, *damu ya Yesu Kristo ina uwezo wa kushughulikia urithi mbaya.* Hivyo tumia damu ya Yesu Kristo kwa ajili kujitenga na urithi mbaya.

📖1 Petro 1:18-19
*[18]Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu;[19]bali kwa damu ya thamani, k**a ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.*

✍️Omba sana kwa ajili ya jambo hili la hasira kwasababu madhara yake ni makubwa sana, ikiwa ni pamoja na kuwa ni *mlango wa dhambi na uharibifu wa aina nyingi.*

📖Waefeso 4:26 *Mwe na hasira, ila msitende dhambi;* jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka.

✍️Kwenye huo mstari unaona wazi kabisa kwamba, *hasira ni mlango wa dhambi.* Na hata kwa Kaini, hasira ndiyo iliyofungua mlango wa dhambi ya kumuua ndugu yake Habili.
{Mwanzo 4:3-8}

*KUMBUKA:* Hata k**a hauna hasira ya kurithi, ila ni hasira ya kawaida tu, bado chunga sana hiyo hasira pia na muombe Roho Mtakatifu akusaidie pale unapoona umekasirika.

✍️Nakuachia mistari ifuatayo kutoka kwenye Biblia, ili uweze kuitafakari 👇👇

📖Mhubiri 7:9 *Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.*

📖Zaburi 37:8 *Ukomeshe hasira, uache ghadhabu, Usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya.*

📖Yakobo 1:20 *kwa maana hasira ya mwanadamu haiitendi haki ya Mungu.*

* NI MBAYA SANA.*
* NI MBAYA SANA.*
* NI MBAYA SANA.*

✍️Ninaamini ujumbe huu umekupa kitu cha kukusaidia kuhusu hasira.
Utukufu apewe Bwana Yesu.

* litaendelea sehemu ya 3.... Tafadhali usikose.*

* ,Mwl Mandela & Devotha Mwambeso*
0752 197065
Email: [email protected]
Dodoma, Tanzania

Address

Dodoma

Telephone

+255752197065

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Glory to God /Mwl Mwambeso posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Glory to God /Mwl Mwambeso:

Share