Huduma Ya Bonde La Baraka

Huduma Ya Bonde La Baraka Huduma ya Bonde la Baraka ni huduma huru ya kutangaza Neno la Mungu kwa watu wote makabila yote na Ulimwenguni kote kadri atakavyo tujalia Roho Mtakatifu.

12/11/2017

NAIBARIKI JUMAPILI YAKO.

Bwana Yesu Asifiwe, Leo ni siku njema yenye Utukufu kwa Bwana Yesu.
Kumbuka kumkumbuka Mungu na kumshukuru kwa wiki zima ulilopita salama umelindwa na vitu vingi ikiwemo ajali, magonjwa na mikosi ya kila namna.

Ni kweli kuwa hatujamuonga Mungu atupe uzima na ulinzi na afya hivi leo Ni Neema zake na Rehema zake tu kwamba Tuna uzima na Amani.

Nasimama Kuibariki Siku yako hii iwe ya mafanikio kwako Kiroho na Kimwili.

Bwana Yesu akakutane na haja za moyo wako na akutendee k**a alivyokusudia kwako.

MUNGU AKUBARIKI SANA

NOVEMBER ITAKUWA NJEMA KWAKO K**A UTAFANYA HAYA;Bwana Yesu Asifiwe unaendeleaje na majukumu yako ya kila siku? Natumai k...
02/11/2017

NOVEMBER ITAKUWA NJEMA KWAKO K**A UTAFANYA HAYA;
Bwana Yesu Asifiwe unaendeleaje na majukumu yako ya kila siku? Natumai kuna namna ambavyo una uzima.

Naomba niseme kila mmoja anatamani huu mwezi uwe mwezi wa Tofauti na Neema kubwa ndani yake na uwe mwezi wa kifikia malengo fulani, nitakupa mambo machache ambayo hayo yataifanya NOVEMBER YAKO KUWA NA ALAMA KATIKA MAISHA YAKO.

1. KUJIKANA NA KUJIINGIZA KWA NGUVU.
Mwezi huu wenye wiki nne utumie kwaajili ya kujikana wewe na nafsi yako, kana zile tabia mbaya ambazo zimekuwa changamoto, kana kupitishwa kwenye shida na adui zako, kana maneno ya kurudishwa nyuma yaliyotamkwa kwako, kana hali ya kufeli na kurudi nyuma.
Jiingize katika Neema na maendeleo mazuri kiroho na kimwili usitazame wingi wa adui zako jiingize kwa nguvu katika ushindi, Usitazame sana hali ngumu inayokuzunguka hila jiingize kwa nguvu katika hali nyepesi.
Unapojiingiza kwa nguvu hakikisha haumkosei Mungu kwa kila unapotaka kujiingiza.
Mfano: Mwanamke aliyetokwa na damu kwa miaka mingi alijipenyeza na kujiingiza alipo Yesu naye akawa mzima.

2. KUAMINI NA KUTEMBEA
Unapaswa kuamini katika mambo mengi mwezi huu moja AMINI KATIKA YULE ALIYEKUUMBA hapa unapaswa kuwa na huakika na yule aliyekuumba, Kuwa na huakika wa 100% na YESU KRISTO /MUNGU ALIYE HAI unaye mwabudu kila siku.
Mbili Amini kuwa ni wewe na si mwingine anayepaswa kubadili mazingira magumu yenye changamoto yanayokuzunguka.
Tatu Amini katika muda ulionao kuwa ndio huo na hauna mwingine tena utumie ukubadilishe.
Tembea katika vitu vitatu nilivyovitaja hapo juu unavyopaswa kuviamini ndipo utaona njia.

3. KUTHUBUTU NA KUFANYA
Mwezi huu thubutu kufanya mambo ya msingi na ya kimaendeleo kiroho na kimwili.
Fanya yale ambayo unasukumwa kudhubutu kufanya, ENVIRONMENT IS CAPITAL IF USED ACCORDINGLY- Suleiman Shedrack Swai November 2018
Tumia mazingira yanayokuzunguka kubadilisha mfumo wa maisha yako. Kuna baraka kubwa sana Mungu ameachilia hapo ulipo tafuta hiyo Baraka ili Ikubariki.

4. KUSAMEHE NA KUVUMILIA
Tafuta kuwa na amani na watu wote, wewe uliyesema hutamsamehe huyo ebu msamehe uone mambo yatakavyonyooka kwako, Bwana Yesu anataka mwezi huu uwaachilie wakosaji wako wote hili hili ayaongoze maisha yako.
Uvumilivu huleta Saburi, Vumilia kwa kiwango cha juu bila kuchoka.

MWEZI NOVEMBER NA UKUPE ALAMA NJEMA KATIKA MAISHA YAKO

Mtumishi Suleiman S Swai
Huduma ya Bonde la Baraka Tanzania
Dodoma
0621066205
[email protected]

19/10/2017

MSIKIAJI NA MTENDAJI
Bwana Yesu Asifiwe Wapendwa wa Mungu aliye Hai Natumai mpo wazima kabisa.

Ninamshukuru sana kwa siku hii ya leo ambapo ametupa kwaajili ya kujifunza Neno lake, Siku ya leo tutajifunza kwa habari ya Msikiaji na Mtendaji.

Msikiaji ni mtu anayesikiliza jambo pasipo kulichukulia hatua.
Mtendaji ni mtu anayesikia jambo na kulitendea kazi inavyotakiwa.

Wengi tunashindwa kutofautisha kati ya Kusikia na Kutenda.
"Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu".
Yakobo 1 :22

Neno linatuagiza kuwa WATENDAJI(DOERS) na si WASIKIAJI(LISTENERS) sasa utajuaje kuwa mimi ni Mtendaji au msikiaji wa Neno la Mungu?
Kuna utaratibu watu wamejiwekea baada ya mahubiri au mafundisho ya Neno la Mungu UTASIKIA WAPENDWA WANASEMA NENO LA LEO LIMENIBARIKI.
KUBARIKIWA KWA NENO HAKUNA MAANA K**A HUTOLIISHI HILO NENO.
Hii ina maana kuwa MTENDAJI wa Neno la Mungu ni KULIISHIA /KULIISHI NENO LA MUNGU kinyume na hapo ndipo tunabaki kuwa wasikiaji.

"Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni k**a mtu anayejiangalia uso wake katika kioo, Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo." Yakobo 1 :23-24

Hapa ndipo pale tuposema tumebarikiwa na Neno wakati tunatenda kinyume na Neno tulilobarikiwa nalo. ndio kule kujiangalia katika kioo na kuondoka punde unasahau ulivyo.

" Lakini aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake."
Yakobo 1 :25

Hapo nataka ujifunze jambo katika utendaji wa Neno la Mungu, Kuwa kwa kiwango unachosikia Neno la Mungu na kulitenda ndicho kiwango ambacho NENO LA MUNGU LINABADILISHA MFUMO WA MAISHA YAKO.

Jiulize maswali yafuatayo hili uweze kutambua unasikia au unatenda Neno la Mungu.

1. JIULIZE UNAPOSIKIA NENO LA MUNGU LINAKUBADILISHA?
2. UNATEMBEAJE KULINGANA NA NENO UNALOLISIKIA?
3. NI KWA KIASI GANI NENO LINAKUWA MAISHA YAKO.

TENDEA KAZI NENO LA BWANBWANA NA SI KUSIKIA NA KULIACHA MADHABAHUNI NA KWENYE MIKUTANO YA INJILI AU KWENYE MADAFTARI.

Mtumishi Suleiman S Swai
Huduma ya Bonde la Baraka Tanzania
Dodoma
0621066205- Andika sms utajibiwa

05/10/2017

TUJIFUNZE PAMOJA LEO:
Ufalme wa Mungu ni nini?
Kwanini Ufalme wa Mungu upo?
Unafikiri Ufalme wa Mungu una umuhimu gani kwa Mtu?

Comment majibu kulingana na unavyoelewa ni vyema ukatumia maandiko ya Biblia.

Jambo lingine Kwanini jambo la Wadada kushika mimba limekuwa changamoto na nini kifanyike?

Hii ni kwa wadada na wamama k**a unapata ndoto za kufanya tendo la ndoa na watu unaowafahamu na usio wafahamu baasi mwezi huu nipo kukusaidia niandikie Sms facebook halafu nitakujulisha cha kufanya.

Athari ya ndoto za kufanya Tendo la Ndoa.
1. Kuanguka kiroho.
2. Kukosa Uzao
3. Kuvunjika kwa ndoa kwa walioolewa/kuoa
4.Kutumika kuongeza jeshi la shetani kupitia uzazi wako.
5. Kuwa na Maisha yasiyo na Amani.

Huu mwezi Oktoba nimepewa kibali cha kuwasaidia wote wanaosumbuliwa na ndoto za KUFANYA TENDO LA NDOA.

KUMBUKA UONGOZI WA YUSUFU ULIPITISHWA KWA NDOTO.

KARIBU INBOX KWAAJILI YA HIYO NDOTO.

Unaweza ukashare ujumbe huu tuwasaidie watu wa Mungu.

MMEPEWA BURE TOENI BURE.

MWEZI OCTOBER 2017 NI MWEZI WA KURITHI AHADI.Bwana Yesu Asifiwe Mtu wa Mungu kwanza kabisa Nimshukuru Mungu kwaajili yak...
30/09/2017

MWEZI OCTOBER 2017 NI MWEZI WA KURITHI AHADI.
Bwana Yesu Asifiwe Mtu wa Mungu kwanza kabisa Nimshukuru Mungu kwaajili yako kwa kukuwezesha kuvuka kutoka September kuja October Si kwamba umetenda mambo makubwa sana hila kuna namna Bwana amezidi kukuacha uendelee kuishi kwasababu kuna jambo hujalitimiliza ndio maana upo fanya juhudi ufanye unachotakiwa usije kusema hukupewa muda wa kutosha.

Upo kwenye chumba cha mtihan na upo kwenye dakika za nyongeza unatakiwa uhakikishe unakifanya kinachotakiwa kufanywa.

Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani. Wagalatia 3 :9

Weka Imani yako katika Kristo Yesu kwasababu lazima urithi ahadi ulizo ahidiwa na Mungu mwezi huu.

Inawezekana unaona ugumu fulani katika kumiliki ahadi yako hila ipo namna ukiamini tofaut na unavyoona basi SOMETHING IS GOING TO HAPPEN TO YOU VERY SOON.

TWENDE PAMOJA KUZITEKA NA KUMILIKI AHADI ZA KIMBINGU KATIKA MWEZI HUU OCTOBER

IMANI NDICHO KINACHOTAKIWA HILI WEWE UMILIKI AHADI.

Comment najiunganisha na ahadi za mwezi October.

By Mt. Suleiman S. Swai
Huduma ya Bonde la Baraka
Dodoma
0745993259/0621066205

KUFANIKIWA KATIKA MAMBO YA YAKO KUNA HITAJI UFAHAMU WA ZIADA.Bwana Wetu Yesu Kristo Asifiwe unaendeleaje mpemdwa wa Mung...
26/09/2017

KUFANIKIWA KATIKA MAMBO YA YAKO KUNA HITAJI UFAHAMU WA ZIADA.
Bwana Wetu Yesu Kristo Asifiwe unaendeleaje mpemdwa wa Mungu, Binafsi Namshukuru Mungu kwa uwepo wako na afya yako.

Leo nasukumwa kukuambia mambo machache juu ya kutafuta mafanikio.

Ni dhaihiri kuwa kila mmoja ana kiu ya kufanikiwa na kufkia malengo mengine na wengi huwa tupambana na wengine kukata tamaa kabisa kutokana na kutofanikiwa kwao katika kutafuta.

Yawezekana unaomba saaana wakati unatafuta mafanikio yako na bado huoni njia bado hali ni ngumu na inafika wakati unajiuliza umemkosea MUNGU nini?

Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. Mathayo 6:33, Biblia inazungumza kuutafuta UFALME WAKE hapa kulikuwa kuna jambo limefichwa ndani yake n hii VYOTE TUNAVYOVIHITAJI VIMEWEMWA KATIKA UFALME WA MUNGU.

Kuna jinsi hutaki kufanikiwa kwasababu kila siku unasikia jambo kuhusu UFALME WA MUNGU na hautaki kulichukulia maanani.
Na hayo yote mtazidishiwa ndivyo Biblia inasema haufanyi makosa kumuomba Mungu mafanikio hila umejiuliza ni vigezo gani umevitimiza hili Mungu wa Mbinguni atume hayo mafanikio yakujilie?
Umekuwa unalalamika kila unachokifanya hakifanikiwi je umefata njia gani hili kila unachokifanya ufanikiwe?
Kuna watu wasio na akili wanasema kuwa wao wanafanikiwa hata wasipoomba(wasipomuomba Mungu) Huu ni uongo na ujinga usiofikirika kwamba unafanikiwa bila kuwa na Msingi wa Mafanikio.
Kila mafanikio ya mtu yana msingi wake sasa msingi wa mafanikio ya Mtu unaweza kuwa wa aina tatu:-
1. Akili za Mtu binafsi
2. Nguvu za giza
3. Mungu aliye hai.
Ukifanikiwa kwa njia moja wapo hapo sisi tutasema umefanikiwa hila ndipo jambo linakuja sasa ni kwa WAKATI GANI UTADUMU KATIKA MAFANIKIO ULIYOYAPATA KUTOKANA NA NJIA ULIYOICHAGUA?
Njia ya kwanza ya akili yako Utafanikiwa lakini njia yako katika mafanikio yako haitakuwa nyepesi hata kidogo na hasara ni kubwa katika biashara yako au mafanikio yako kwasababu mlinzi wa biashara yako ni wewe binafsi na si mwingine.
Njia ya pili ya Giza hapa utapata mafanikio lakini yana madhara makubwa kwasababu walinzi wa mafanikio yako ndio waaribifu wa maisha yako ya sasa na baadae sasa kwenye mafanikio utaona unafanikiwa lakini kwa upande mwingine wa kifamilia, kiroho na kiafya utakuwa ni k**a marehemu anayetembea. Sababu ni hii hili upate kitu kwa giza lazima utoe kitu na sana unachokitegemea.
Njia nyingine ni kupitia MUNGU ALIYE HAI kupata mafanikio kwa njia hii kunategemea kwanza kuakikisha hakuna njia unayoitumia kati ya hizo mbili hapo juu kisha utaanza kufanya mambo yafuatayo:-
1. Kumsikiliza Mungu kwamba ni kipi anataka ufanye na kwa wakati gani anataka ufanye na wapi. Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.Kumb.28 :3
2. Kukubali na Kuzitii njia za Mungu, hili uone mafanikio lazima ukubali na uzitii njia za Mungu aliye hai, Kukubali inamaana kuwa tayari kufanya kwa furaha wajibu wako, na kutii ni kufanya bila manung'uniko na kwa furaha amri yake. K**a mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi; Isaya 1:19
3. Kuyapa kipaumbele mambo ya Mungu na muda wa Mungu kuliko muda wako, Hapa watu wengi wanashindwa unakuta unatakiwa uwe kanisani wewe upo kwenye biashara wajati huohuo unamuomba Mungu akupe mafanikio ni Mungu yupi unayemuomba wakati haujali muda wake hili na yeye awe makini kwenye muda wako? Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu. Yohana 12:26
4. Kumbuka kutoa kilicho cha Mungu katika kila hatua unayoipiga ikiwa ni 10% au malimbuko au shukrani inakupasa umpe bila kusita kwasababu Hizo ndizo zinalinda mafanikio yako. Mungu ahitaji sana kutoka kwako ebu fikiri anakupa 300000 halafu hapo unampa 30000 je ni nyingi hiyo kulinganisha na 300000? Basi sasa, Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu.Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakini hapana aonaye moto; na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka. Hagai 1 :5-6

Mpendwa mtu wa Mungu kwa mambo hayo utakuwa umejifunza jambo katika Utafutaji wenye mafanikio sasa LAZIMA UTAFUTE UFALME WA MUNGU NA UHAKIKISHE HUU UFALME UNAKUWA NDANI YAKO HAPO NDIPO UTAKUWA MWANZO WA MAFANIKIO YAKO.
Acha kuzunguka kwa Watumishi kutafuta muujiza wa mafanikio huo muujiza upo nao wewe hila utaki kuufanya ufanye kazi na udhihirike.
Ukiona umesimama kwelikwel na Ufalme wa Mungu bado mambo magumu ndipo Umuulize Mungu ufanye nini au utafute Mtumishi wa Mungu akusaidie.
Wengi tunafanikiwa nje ya mafanikio mfano Mungu alipanga wewe uwe tajiri au fanikiwe kutokana na UALIMU lakini wewe sasa hivi ni DEREVA piga mahesabu hapo tunaanzaje kumlaumu Mungu na mtu ukimuuliza kilichompelekea kuwa DEREVA BADALA YA MWALIMU NI KUTOKUVAA KIATU CHAKE WAKATI WA KUANZA KUTENGENEZA MAISHA YAKE.

KUFANIKIWA NI KANUNI (PRINCIPLES) LAZIMA USIRUKE HATA MOJA.

Kuna jambo Mungu kanipa la kukusaidia kiuchumi na Kiroho usisite kunitafuta kwa Namba zangu tuweze kuongea na Tushauriane hili ufikie Malengo yako..
VITA VYA KIUCHUMI NI VIKALI KWA KILA MMOJA HILA YESU KRISTO AKIWA NDANI YAKO NI USHINDI.
Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia.Mithali 8:18

Mtumishi Suleiman S Swai
Huduma ya Bonde la Baraka
+255745993259/621066205
Dodoma, Tanzania.

MTAZAMO WA KIIMANI WENYE MALENGO MAKUBWA.Bwana Yesu Asifiwe Mpendwa wa Bwana natumai wewe ni Mzima wa Afya na Mungu aliy...
18/09/2017

MTAZAMO WA KIIMANI WENYE MALENGO MAKUBWA.

Bwana Yesu Asifiwe Mpendwa wa Bwana natumai wewe ni Mzima wa Afya na Mungu aliye hai anazidi kukupigania na kukuinua zaidi.

Kuna jambo nasukumwa nikuambie kwa siku ya leo natumai kuna watu watatambua jambo kupitia jambo hili ambalo Roho Mtakatifu atalifunua kwako.

Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.
2 Wakorintho 4 :17-18

Biblia inasema dhiki yetu ni nyepesi tena ya kitambo.
Naomba nikuulize kuna dhiki nyepesi?, kuna gumu lepesi? kuna umaskini mwepesi? kuna ugonjwa mwepesi? wengi hapa mnasema hapana na sababu ni kwamba kila gumu lina maumivu yake na hasara zake kubwa.

Leo Biblia inasema dhiki yetu ni nyepesi unajua hapa Paulo alitazama mazingira kwa MTAZAMO WA MBELE kwasababu alitambua mazingira ya sasa hayawezi kuzuia MAKUSUDIO MAZURI YA MBELE. Hila yeye aliona kuwa hizo dhiki nyepesi hili asitimie muda mwingi kufikiri kuhusu dhiki aliyonayo bali kufikiri zaidi ya hapo ambapo anatupa majibu mimi na wewe ni kipi kimefichwa katika dhiki. Paulo anasema dhiki INATUFANYIA UTUKUFU KUWA MWINGI.

Paulo hakulaumu mazingira ya dhiki aliyonayo kwasabu hayakuwa na chochote katika kufikia malengo mazuri mbele.
Anasema TUSIVIANGALIE VINAVYOONEKANA KWASABABU NI VYA MUDA TU.

Hapa ndipo palipobeba ujumbe wa leo kuwa Chochote unachokiona sasa hivi ni cha muda wawe ni hao wazazi wawe ni watoto awe ni mke au mume wote ni wa muda tu na wengi macho yetu yanawatazama sana hawa watu na vitu vingine vinavyofanan na hivi bila kukumbuka kuwa maisha yako yapo sehemu isiyoonekana.

TAZAMA MAISHA YAKO KWA SEHEMU ISIYOONEKANA NA WEWE WALA MTU MWINGINE HAPO PANA UTUKUFU AMBAO KILA MTU ATASHANGAA.

TAZAMA PASIPOONEKANA MAANA NDIPO NGUZO YA MALENGO YAKO YALIPO.

Usijalishwe na hali ya dhiki inayokuzunguka kwani baada ya miaka miwili au mwezi mmoja unaioona hiyo dhiki mbele?

SATAN HAS SOMETHING BAD TO DO ABOUT YOUR CURRENT SITUATION.(SHETANI ANA JAMBO BAYA LA KUFANYA KATIKA HALI YAKO YA SASA)

"GOD HAS A LOT TO DO WITH YOU IN YOUR FUTURE" (MUNGU ANA MENGI YA KUFANYA PAMOJA NA WEWE KATIKA MAISHA YASIYOONEKANA.

FUTURE IS UNSEEN LIFE

TAZAMA MAISHA YAKO KWA IMANI UFIKIE MALENGO

MT. SULEIMAN S. SWAI
HUDUMA YA BONDE LA BARAKA
+255745993259/621066205.
DODOMA

KATIKA MAGUMU NDIPO ALIPO MUNGU WA ISRAELI. Bwana Yesu Kristo Asifiwe mpendwa mtu wa Mungu ni siku nyingine tena Mungu k...
03/09/2017

KATIKA MAGUMU NDIPO ALIPO MUNGU WA ISRAELI.
Bwana Yesu Kristo Asifiwe mpendwa mtu wa Mungu ni siku nyingine tena Mungu katupa kibali cha kujifunza neno lake.
Wapendwa kuna nyakati ambazo zinatokea kwa kila mmoja hizi nyakati wengi tunakosa njia na wengi tunaomba bila kuona mafanikio na wengi tukifika katika wakati huu basi tunaona kuwa Mungu hayupo tena Upande wetu.

Siku ya leo natamani Roho Mtakatifu akufunulie jambo la tofauti na mitazamo yetu tunapokuwa katika wakati mgumu kupita uwezo wetu.

Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa.Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini Bwana humponya nayo yote. Zaburi 34 :18-19
Kupitia Zaburi aliyoiandika Daudi anatueleza kuwa BWANA YU KARIBU NAO WALIOVUNJIKA MOYO, hili jambo wengi sana hatulijui labda nikuulize wakati mgumu unakufanya unajengeka moyo au unavunjika moyo? K**a jibu ni ndio ni mara ngapi umevunjika moyo? ni mara ngapi umekuwa katika wakati huo mgumu na unaona kuwa Mungu hayupo katika hilo? sasa hili ndilo jambo Roho Mtakatifu anataka ujue leo kuwa Hakuna Nyakati ambayo Mungu anakuwa karibu na wewe k**a wakati wa Magumu, vita, huzuni, tabu, shida na dhiki nyakati hizi Mungu anakuwa karibu na wewe maana kwa kipindi hiki moyo wako unakuwa umevunjika kwa kiasi chake.
Mstari wa 19 unasema MATESO YA MWENYE HAKI NI MENGI LAKINI BWANA HUMPONYA NAYE YOTE. sasa k**a Bwana anakuponya na mateso yote je ni jambo gani basi litakuwa limesalia je ni kitu gani kitakuwa bado hakijatimia kwa wakati huo? Kumbuka Mungu kile unachotaka anakupa unachostahili kwa wakati na sekunde husika.

Sasa mfano upo kwenye wakati mgumu na wewe unamuomba Mungu akutoe katika wakati huo Mgumu na Mungu yeye anaona kuwa La muhimu kwako ni WEWE KUISHI BILA KUFA KATIKA WAKATI HUO MGUMU SASA NDIO UNAKUJA WAKATI TUNAISHI NA TUNAMLAUMU MUNGU KUWA AMETUACHA.
Umepitia magumu mangapi ambayo ulipaswa uwe marehemu lakini leo bado unapumua na umepata neema ya kusoma ujumbe huu? je kipi ambacho kilikuwa cha Muhimu wewe kubaki unaishi au Kutolewa kwenye ule wakati mgumu?
Hatua za mtu zaimarishwa na Bwana, Naye aipenda njia yake.Ajapojikwaa hataanguka chini, Bwana humshika mkono na kumtegemeza. Zaburi 37 :23-24
Hatua zako zinafanywa imara na Mungu na yeye wewe unapaswa kupendezwa na njia ya Mungu na anasema ujapojikwaa katika magumu na hali yoyote unayoisi ni ngumu kwako yeye atakuacha uanguke maana yupo karibu na wewe akushike mkono.

Tunaelewa huwezi kumshika mtu mkono k**a haupo karibu naye hii inatupa mwanga kuwa Mungu anaposema humshika mkono ni kwasababu yupo karibu sana na yeye na wewe pia.
Wakati wa njaa atakukomboa na mauti; Na vitani atakukomboa na nguvu za upanga.Ayubu 5 :20
Ayubu anakiri kuwa wakati wa njaa, mauti na vitani yupo Munguvaliye karibu na wewe kuliko mpendwa wako ambaye ndiye anaweza kukutoa hapo kwa njia nyepesi au ngumu hila atakacho hakikisha lazima Utoke.

Nami nitakuokoa na mkono wa watu wabaya, nami nitakukomboa katika mkono wao wenye kutisha. Yeremia 15 :21
Bado Mungu anazungumza kuwa katika magumu ya namna gani na mazingira ya hali ipi na watu wenye sura au vitisho vya namna gani bado yupo karibu nawe kwaajili ya kukusaidia kwaajili ya kukuvusha hayupo mbali na wewe k**a unavyowaza mpendwa.

Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.Maombolezo 3 :33
Hii ndio sababu ya Mungu kuwa hapo kwenye ugumu unaokupata katika maisha yako maana hapendezwi sana na mateso yako hapendezwi sana na huzuni na kukosa raha kwako anatamani na kupenda tufurahi kumfurahia yeye na Utukufu wake.
Kwa mantiki hii Roho wa Mungu ananishuhudia ndani yangu hakuna ambapo Mungu anatuacha hila sisi ndio TUNAMUACHA MUNGU KWA SABABU YA YALE TUNAYOYAKIRI KWA VINYWA VYETU NA KUWAZA KWA MAWAZO YETU.

Nikupe siri hivi unajua kwanini AYUBU alipewa mara Mbili ni kwasababu ukiri wake ulikuwa si wa kawaida hakuwahi kukiri kuachwa na Mungu hila ukiri wake ulikuwa kumsifia Mungu aliye hai kuwa anaweza kumtoa alipo ndipo akapata mara mbili.
TUMIA WAKATI MGUMU ULIONAO KUNUFAISHA MAISHA YAKO KWA KUTAFUTA KUPATA MARA MBILI (DOUBLE)

Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao. Yakobo 1 :12
Kumbe ni jukumu langu na lako kustahimili/kuvumilia nyakati na vipindi vyooote vigumu kwanini kwasababu kuna vitu vinatafutwa katika kipindi hicho kigumu na ukisoma vizuri katika Yakobo 1:12 utaona neno KUKUBALIWA.

KUKUBALIWA ni hali ya kufaulu na kukidhi vigezo vyote vilivyowekwa na anayetaka jambo kwako au unayetaka afanye jambo kwako.
Tunamtazamia Mungu atukubali na kutupa uzima katika nyakati ngumu Je umejiuliza umekidhi vigezo hili akupe unavyotazamia?
Kila gumu lililo mbele yako lina vipimo vyake hili upewe upendeleo yaani mara mbili.

Jifunze haya uwapo katika hali ngumu.
Msifu Mungu Aliye Hai
Kiri Ushindi kila wakati
Vumilia
Weka Tumaini kwa Kristo Yesu
Kuwa Msiri Mungu
Tabasamu lako ni Muhimu Kufucha yaliyo ndani.
Sikia Mengi chukua machache yenye faida.

KUMBUKA MUNGU WA MBINGUNI YUPO UPANDE WAKO HILI AKUOKOE.

MUNGU AKUBARIKI.

Suleiman Shedrack Swai
Huduma ya Bonde la Baraka Tanzania.
0745993259, 0653053514 na 0621066205
Dodoma.

SIRI ILIYOFICHWA KATIKA TALANTABwana Yesu Asifiwe mpendwa wa Mungu leo ni siku nyingine ambayo Mungu katupa kibali kujif...
31/08/2017

SIRI ILIYOFICHWA KATIKA TALANTA
Bwana Yesu Asifiwe mpendwa wa Mungu leo ni siku nyingine ambayo Mungu katupa kibali kujifunza Neno lake katika siku hii ya le.

Kila Mtu ameshawahi kusikia na kusoma habari na mfano alioutoa Yesu Kristo kuhusu Talanta na watumwa, Leo tumepata Neema nitakueleza siri iliyopo katika Mfano wa Talanta.

Unaweza ukakubaliana nami kuwa BIBLIA NI UNABII KWA YALE YALIYOTOKEA, YALIYOPO NA YAJAYO.

Talanta Kibiblia imezungumzwa k**a Fedha hila leo Tutaiangalia Talanta k**a Huduma, Karama au wito wa Kristo.

Tutaanza Kuangalia Mstari hu, Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita watumwa wake, akaweka kwao mali zake. Mathayo 25 :14
Mfano wa Mtu atakaye kusafiri hapa ni Yesu Alikuwa anajizungumzia mwenyewe kabla ya kurudi kwa Baba na akawaita WATUMWA WAKE( WATEULE&WATUMISHI) na kuweka kwao mali zake,Kibiblia tunaona Yesu Kristo aliweka kwa watumishi wake mali yake na zaidi ya alivyo navyo ndio I maana akasema NILIYOYAFANYA NANYI MTAYAFANYA NA KUBWA ZAIDI YANGU.

Baada ya Yesu kutaka kusafiri alianza kugawa mali kwa watumwa wake na ilikuwa hiv, Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri-Mathayo 25 :15
Hapa Yesu Kristo alitoa Talanta kwa kila mtu kulingana na UWEZO WA UWEZO WA MTU. Halafu yeye akasafiri hii safari ni ya yeye kurudi kwa Babaye Mbinguni. Nini kiliendelea kwa wote waliopewa Talanta? Fatana nami, Mara yule aliyepokea talanta tano akaenda, akafanya biashara nazo, akachuma faida talanta nyingine tano.-Mathayo 25 :16
Huyu aliyepokea Talanta 5 kutoka kwa Yesu Kristo alifanya biashara nazo akazalisha zingine tano,Vile vile na yule mwenye mbili, yeye naye akachuma nyingine mbili faida.-Mathayo 25 :17 Unaona mtu wa pili naye alichuma zingine Mbili mbali na alizopewa.

Shida inaanzia hapa sasa Lakini yule aliyepokea moja alikwenda akafukua chini, akaificha fedha ya bwana wake.-Mathayo 25 :18
Huyu baada ya kupewa akaificha chini binafsi wengi sana tupo kwa huyu aliyefukia talanta yake chini na kujiona kuwa tupo sawa na hakuna shida kabisa tunaishi maisha ya Amani.
Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao.Mathayo 25 :19

Siku iliwadia sasa wakati ambao mwenye mali anakuja kuchukua mali zake ambaye huyu anayekuja si mwingine ni YESU KRISTO WA NAZARETH. Huyu Yesu anakuja kufanya hesabu na WOTE ALIOWAPA TALANTA SAWA UWEZO WAO.
Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida.-Mathayo 25 :20 Waoooooo Huyu alimpendeza Yesu sana kwa hicho alichopewa na kukizalisha na mwisho anarudisha vile alivyopewa na faida juu.
Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.Mathayo 25 :21

Sasa tunaenda kwa aliyepewa mbili, Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida, Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.Mathayo 25 :22-23
Sasa hao tunaona Yesu anawakaribisha hao waliopewa talanta na kuzalisha.

Tumuangalie huyu aliyepewa Talanta moja na akaifuki, Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya; basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako.Mathayo 25 :24-25
Umeona majibu ya huyu mtu yani alipewa kitu kwaajili ya kuzalisha yeye anafanya akiinacho ni sawa ambocho ni tofauti na alichopewa nini matokeo yake?

Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya; basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.Basi, mnyang'anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi. Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang'anywa.Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.Mathayo 25 :26-30

Nafikiri umeona adhabu iliyomtokea aliye fukuia Talanta yake.
Awali nimesema Leo tunaangalia Talanta k**a Huduma, Karama, Kusudi au Wito ambao ulipewa na Yesu Kristo na Mungu ukiwa Tumboni mwa mama yako na baada ya kumpokea Roho Mtakatifu. Je hiyo umeifukia au umeiwekeza izae mara mbili? wako wengi wanaishi k**a hawakupewa Talanta na Yesu Kristo wanasema wanawasindikiza wengine hii si kweli kila mmoja kapewa kulingana na uwezo wake, wewe uwezo wako ni wa 5,2 au 1? Je Talanta yako inakua au inasubiri kufufuliwa? haya maswali tunapaswa kujiuliza sote.

Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu. Yohana 15 :8
Unaona kuwa Mungu anapendezwa na namna ambavyo watu wanamzalia matunda?
Hiyo huduma uliyopewa unaifanya ni ya familia shauri yako vunja mipaka mzalie Mungu aliye hai matunda ya kiroho yaani umsogezee watu zaidi ya aliokupa.

HUDUMA KARAMA NI KWAAJILI YA WATU NA HUO NI MKOPO AMBAO YESU ALIKUKOPESHA URUDISHE NA RIBA NA HAKUNA MSAMAHA WA RIBA KATIKA MKOPO HILA KUNA FIDIA YA KULIPA KWA KUCHELEWESHA AU KUTOKUTOA MKOPO.

MUNGU AKUBARIKI NAKUTAKIA UVUNAJI WA MAZAO MEMA.
Mt. Suleiman S Swai
HUDUMA YA BONDE LA BARAKA TANZANIA.
0745993259/0653053514

Address

Dodoma

Opening Hours

Monday 06:00 - 00:00
Tuesday 06:00 - 00:00
Wednesday 06:00 - 00:00
Thursday 06:00 - 00:00
Friday 06:00 - 00:00
Saturday 06:00 - 00:00
Sunday 06:00 - 00:00

Telephone

255621066205

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Huduma Ya Bonde La Baraka posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share