15/05/2026
MABADILIKO YA TAREHE ZA MKUTANO MKUU WA UCHAGUZI.
Ofisi ya Katibu Mkuu, inawajulisha wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi 2026 kuwa sasa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi utafanyika Tarehe 18 na 19 Juni 2026 na sio tarehe zilizopangwa hapo awali, Jijini Dodoma.
Hii ni kutokana na uwepo wa Mkutano wa CPCT TAIFA katika tarehe zilizokuwa zimepangwa hapo awali.
Endelea kuombea mkutano huo na Karibu sana Dodoma.