22/04/2026
MAOMBI YA LEO โ IMANI KWA YALIYOSHINDIKANA
Baba wa mbinguni,
Nasimama mbele zako leo nikikiri kwamba Wewe ni Mungu wa yasiyowezekana. Wewe ndiye unayesema kwenye utupu na kuleta uhai palipokuwa hapana kitu.
Kuna hali katika maisha yangu zinazoonekana kuwa ngumu, zisizoeleweka, na zilizo nje ya uwezo wangu. Kuna mambo siwezi kuyatatua kwa nguvu zangu mwenyewe. Lakini leo nakumbushwa kwamba hakuna jambo gumu kwako, ee Bwana.
NENO LA MUNGU
Mathayo 19:26
โKwa wanadamu haiwezekani, bali kwa Mungu yote yanawezekana.โ
Yeremia 32:27
โTazama, mimi ndimi Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! kuna neno lolote gumu lisilowezekana kwangu?โ
MAOMBI
Ee Bwana,
Imarisha imani yangu pale mashaka yanapotaka kuingia. Nisaidie nisiangalie yale ninayoyaona kwa macho ya mwili tu, bali niamini yale uliyoniahidi.
Wakati hali zinaonekana hazibadiliki, nikumbushe kwamba bado unatenda kazi, bado unasonga, na bado una uwezo wa kufanya zaidi ya ninavyofikiri au kuwaza.
Nifundishe kukuamini kwa moyo wote, na nisaidie kuachilia mipaka yote niliyoweka juu ya uwezo wako. Ondoa mashaka yangu, ujaze ndani yangu imani thabiti.
Badilisha kusitasita kwangu kuwa ujasiri.
Badilisha hofu yangu kuwa tumaini.
Badilisha kutokuamini kwangu kuwa imani isiyotikisika.
TAMKO LA IMANI
Leo nachagua kuamini kwamba:
Mungu anafanya kazi hata nisipoona
Mungu hajachelewa
Mungu ana uwezo wa kubadilisha kila hali
Najua tayari unatenda kazi nyuma ya pazia kwa ajili yangu.
Nachagua kuamini, kuamini, na kuendelea mbele kwa imani.
Kwa maana Wewe unaweza kufanya zaidi sana kuliko yote niombayo au nifikiriyo.
Katika jina la Yesu Kristo,
Amina.
WITO WA IMANI
K**a umebarikiwa na maombi haya, andika kwa imani:
๐ โMUNGU WA YALIYOSHINDIKANA ANATENDA KAZI KWANGU SASAโ
BY PASTOR FRANK MGAYA
Huduma: Newjerusalem Church of Holy Christians
๐ Makao Makuu: Dodoma, Tanzania