Pastor Erasto Msuka

Pastor Erasto Msuka ▪️ Apostle,Pastor & Teacher at MAABARA YA YESU CHURCH - Dodoma, Tanzania
▪️Mentor
▪️Life Coach.

HAPPY ABSENCE DAY Leo *4.4.2026* ingekuwa *Birthday* yako mke wangu kipenzi, lakini kwa mapenzi ya *MUNGU* akaona vyema ...
04/04/2026

HAPPY ABSENCE DAY

Leo *4.4.2026* ingekuwa *Birthday* yako mke wangu kipenzi, lakini kwa mapenzi ya *MUNGU* akaona vyema ukaisherehekee *PARADISO*.

Kwa mara ya kwanza, ninasherehekea siku yako ya kuzaliwa bila uwepo wako mama wa watoto wangu wazuri.

Siku k**a hii, tulizoea kuitumia kwa pamoja kumtafakari MUNGU kwa zawadi ya maisha kwetu.

Endelea Kumsifu MUNGU huko uliko, endelea kuinama na kuinuka mbele za MWANA-KONDOO WA BWANA pamoja na Makerubi, Maserafi na Malaika, ukiuimba wimbo wa *Musa*, "Wastahili MWANA-KONDOO uliyechinjwa.

Bado nitaendelea kukuenzi kwa kuwa mwaminifu kwa maisha yangu yote, mpaka hapo MUNGU atakaponifungulia mlango wa agano jingine kwa UAMINIFU wangu. Vitoto vyako *Miracle na Melvin* wanakukumbuka, ila picha zako kwenye SIMU zetu imekuwa faraja kwao, Miracle anauliza baba *"mama atarudi lini?, akipona atarudi?".* Watoto hawa wananifariji sana mke wangu.

"*_Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika k**a na wengine wasio na matumaini. Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye_ "* (1 The 4:13-14)

Tunakukumbuka mama yetu.

04/04/2026
05/03/2026

Ministering and Mastering Birthday Ceremony.

*MC kazini.*

Shepherd Erasto

HAPPY BIRTHDAY HELLEN (MRS OMAR) 1/3 miaka kadhaa iliyopita, ndio siku iliyokubali kukuleta duniani mtoto wangu mrembo  ...
04/03/2026

HAPPY BIRTHDAY HELLEN (MRS OMAR)

1/3 miaka kadhaa iliyopita, ndio siku iliyokubali kukuleta duniani mtoto wangu mrembo HELEN binti JOSEPH.... Masha'Allah.....

K**a Mchungaji wako na baba yako wa Kiroho, ninayo furaha kubwa sana kwa Neema ya MUNGU kukuona ukiongezewa mwaka (1+ ) mwingine tena.

Najua mwanangu umepitia nyakati nyingi za furaha, maumivu, misukosuko, amani, magonjwa, mafanikio, kudharauliwa na kuthaminiwa n.k.

Umekuwa na nyakati pia za kumiliki vitu vingi vizuri na vya thamani kwenye maisha yako ikiwemo mume, watoto, fedha, nyumba, mavazi, biashara n. k, hakika hayo yote ni mema sana mbele za MUNGU, lakini nikuhakikishie tu, siku uliyofanya maamuzi ya kupokea "WOKOVU (YESU)" ndicho kitu cha THAMANI sana ulichokipokea katika maisha yako yote MWAKA JANA. Ninakufurahia sana mwanangu kukuona ukizidi kuongezeka kumpenda YESU kwa IMANI ya MATENDO na unazidi kumtegemea Yeye kila iitwapo leo.

Yeremia 17:7

“Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake”

Umefanyika BARAKA kubwa kwenye Kanisa lako la CMF-MAABARA YA YESU PENTECOST CHURCH , SADAKA zako na majitoleo yako yote ni HARUFU NZURI YA MANUKATO YA KUPENDEZA MBELE ZA MUNGU. MUNGU azikumbuke SADAKA zako na kuyaangaza maisha yako k**a tafsiri ya jina lako " Helen/Hellen" - yaani mwangaza au Nuru au mng'ao(Light or Shining).

Abarikiwe mume wako kipenzi Mr. Omar , wabarikiwe mabinti zako wazuri, Mariam na Zuhura (Zuu).

Umemheshimisha MUNGU na familia yako kwa kufanyia BIRTHDAY PARTY yako ndani ya KANISA. Libarikiwe tumbo lililokuzaa.

Hesabu 6: 24-26

“Bwana akubarikie, na kukulinda; Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili; Bwana akuinulie uso wake, na kukupa amani”

Happy birthday to you my lovely spiritual daughter, mwanangu kipenzi, Hellen wangu, kipenzi cha Omar mwenyewe, shangazi na bibi wa MIRACLE na MELVIN. Melvin ameniambia akija nyumbani akute misosi ya kutosha na masotojosotojo yake.... 😂😂😂. Enjoy your day daughter.

Pastor Erasto Msuka

NINI KINATAWALA AKILI YAKO?Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu.” Yakobo ...
24/02/2026

NINI KINATAWALA AKILI YAKO?

Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu.” Yakobo 1:22

Mojawapo ya funguo muhimu ya kuishi maisha ya ushindi ni kuwa mtendaji wa Neno la Mungu. Kwa maana yeyote aliyelisoma neno kisha akalichukua Neno na kuliishi,alitembea kwenye baraka siku zote za maisha yake. Faida ya Neno la Mungu haipo katika kusoma na kutafakari pekee,bali faida ipo katika kuliishi Neno la Mungu.

Neno la Mungu likitawala akili yako, litaathiri mwenendo na tabia yako.

Kuwa mtendaji wa Neno ni:

•Kuweka Neno katika matendo ya kila siku
•Kuishi kulingana na mapenzi ya Mungu
•Kutii hata sauti ya Mungu
•Kuruhusu Neno litawale maamuzi na tabia

Luka 11:28 “Heri walisikiao neno la Mungu na kulishika.”

Kumbuka;

Silaha na funguo kubwa ya ushindi ni kuwa mtendaji wa Neno. Hebu kumbuka kile ambacho Bwana alichowaambia Israeli kwenye Kutoka 19:5, aliwaambia ikiwa wataitii sauti yake kweli kweli, na “kulishika agano langu,” hapo ndipo watakapokuwa tunu kwake kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yake.

Vita na Mapigano ni ya kawaida. Imani ni tofauti. Wale wasio na Neno hutukuza adui lakini wale walio na Neno hutangaza ahadi za ushindi.

Acha mazoezi ya kushindwa bali anza kutangaza ushindi. Mfariji yuko pamoja nawe. Ahadi yake bado ipo.

Ushindi wako unaanza pale Neno linapotawala akili yako.

Shepherd Erasto Msuka

24.2.2026.

Yamkini Mwaka 2025  haukuwa mzuri kwako  ulipata MISIBA Umelia sana 😭😭.......... Umehuzunika Sana kiasi cha Imani yako k...
23/12/2025

Yamkini Mwaka 2025 haukuwa mzuri kwako ulipata MISIBA Umelia sana 😭😭..........

Umehuzunika Sana kiasi cha Imani yako kwa Mungu kutikiswa hata kushuka kabisa kwa sababu ya mapito mengi lakini, naomba kusema neno Moja NAWE rafiki yangu......

MUNGU BADO YUPO NA WEWE, ANAJUA MAPITO YAKO YOTE uliyopitia, unayopitia na yajayo, HIVYO HATA K**A HAJAJIBU UNAVYO TAKA YEYE BABO NI BABA YAKO.

Jambo moja jema kwako ni kwamba, 2026 ni MWAKA BORA ZAIDI KWAKO......... NEEMA MPYA, KIBALI KIPYA, MIPENYO MIPYA , BARAKA MPYA ZIPO NJIANI ZINAKUJA. AMINI TU.

Isaya 43:19

"Tazama, nitafanya jambo jipya! Sasa litachipuka, je, hamtalitambua? Nitafanya njia jangwani na vijito vya maji katika nchi kame".

👉Mwaka 2026 Simama na MUNGU....... UTAFANIKIWA KILA JAMBO UTAKALO LIFANYA KWA IMANI.

✍️Andika "NINAPOKEA"

Erasto .

UMELALA MKE WANGU😭💔?*  UMELALA USINGIZI WA GIZA MAMA MCHUNGAJI💔😭?.....UMEPUMZIKA MCHAGA WANGU. PUMZIKA KATIKA BWANA mke ...
04/11/2025

UMELALA MKE WANGU😭💔?*
UMELALA USINGIZI WA GIZA MAMA MCHUNGAJI💔😭?.....UMEPUMZIKA MCHAGA WANGU.

PUMZIKA KATIKA BWANA mke wangu Grace V. George kipenzi changu.

Ni nyakati ngumu sana kwenye maisha yangu ambazo sikutaraji k**a nitakutana nazo, na hata k**a zingenipata si mapema namna hii.

Familia ya mke na mume yenye umri wa miaka 5 tu...Mbona ndoa changa sana yenye umri wa mtoto wa chekechea tu unalala jumla mke wangu?😭💔

Ulinipa nafasi ya kuwa "baba na mama" yako, nikikuonesha upendo wote ulioukosa kwa wazazi wako waliotangulia mbele ya haki, ukiwa mdogo sana wewe na wadogo zako 2, ambapo wawili mmeshatangulia mbele za Baba yetu wa mbinguni na kumuacha mdogo wenu wa mwisho Barnaba kwenye lindi zito la upweke pasina ndugu wa damu. It hurts me a lot 💘.

Wewe unajua Grace, tulipanga mengi yahusuyo huduma na Kanisa, yahusuyo familia ya watoto wetu wadogo hawa, yahusuyo ndugu wa familia zetu mbili na jamaa, lakini taa yako imezimika ghafla mama yangu kipenzi changu.

Nakuhakikishia mke wangu, Moyo wako wa IBADA NA KUMPENDA MUNGU, UPOLE, HESHIMA NA NIDHAMU YAKO KWA KILA MTU, MSAMAHA, UKARIMU, UPENDO, IMANI, UAMINIFU WAKO, UJASIRI na KUJITOA kwako, vyote nitavienzi maisha yangu yote yaliyobaki hapa duniani na kuwarithisha uzao wa tumbo lako.

Watoto wako wazuri MIRACLE na MELVIN wanakulilia, Miracle ananiuliza baba "mama yuko wapi?", mwanzo alijua "mama yuko Moshi kwa bibi" k**a tulivyomhadaa akiamini utarudi tena nyumbani, asijue uwepo wako hospitalini kwa maumivu makali, lakini baadaye akakukuta kwenye Wodi ya Benjamin Mkapa Hospital ukiwa umelala taabani hujiwezi tena.... Alizoea kumbato lako, lakini hukuwa na nguvu za kumkumbatia tena kipenzi binti yako wa pekee.

Melvin shujaa wako wa kiume, nguvu zako mwenyewe......Kwa nini umemwacha bado kichanga hivi? ... Ooooh! Mwanangu wa viuno vyangu Melvin, katika jumla ya maneno kinywani mwako ni 3 tu unayoweza kuyatamka, yaani Mama... Baba.... Dada.......Mama yako amekuacha mwanangu ungali kinda, hata hujafurahia kifua na mgongo wake kwa kumbato la mama na mtoto😭😭.

Kanisa linakulilia mlezi wao, ulilipenda Kanisa, uliwapenda washirika wako, ulijitoa kwa hali na mali zako ili kuwahudumia washirika Kanisan

YESU ANAOKOA na KUSAMEHE Dhambi kabisa na kutoa UZIMA wa MILELE kwa NEEMA kwa wewe unayeamini habari hizi. Ikiwa umeamin...
27/10/2025

YESU ANAOKOA na KUSAMEHE Dhambi kabisa na kutoa UZIMA wa MILELE kwa NEEMA kwa wewe unayeamini habari hizi.

Ikiwa umeamini basi, unao wajibu wa kuwaeleza wengine HABARI NJEMA (Injili) ZA WOKOVU upatikanao kwa njia ya YESU KRISTO (YOH. 3:16).

Umebarikiwa.

EJM.

MADHARA ya CHANJO ya COVID-19 ndo haya. Ukombozi wa Tanzania tuitakayo bado una safari ndefu sana. Enyi waombaji walinzi...
03/09/2025

MADHARA ya CHANJO ya COVID-19 ndo haya. Ukombozi wa Tanzania tuitakayo bado una safari ndefu sana.

Enyi waombaji walinzi, tuendelee kuliombee Taifa letu lisichezewe na wenye tamaa ya madaraka na vyeo.

Isaya 62:6
Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha BWANA, msiwe

Ezekieli 3:17
Mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa nyumba ya Israeli; basi, sikia neno hili litokalo katika kinywa changu, ukawape maonyo haya yatokayo kwangu.

Ezekieli 33:7
[7]Basi wewe, mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi kwa nyumba ya Israeli; basi ulisikie neno hili kinywani mwangu, ukawape maonyo yangu.

Shepherd EJM
CMF- MAABARA YA YESU PENTECOST CHURCH.

3 Yohana 1:2"Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, k**a vile roho yako ifanikiwavyo". " Belove...
28/08/2025

3 Yohana 1:2
"Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, k**a vile roho yako ifanikiwavyo".

" Beloved, I wish above all things that thou mayest prosper and be in health, even as thy soul prospereth"
======================================

Happy birthday ndugu yangu, legend mwenzangu katika tasnia ya Habari (Uandishi na Utangazaji). Wewe ni chachu ya mimi kuwa Mtangazaji wa Radio, nilijifunza mengi kwako kimyakimya toka ukiwa Living Water FM na Crew ya akina Leah Ezekiel Mnyambwa, Esther Tindos Kusekwa, Ayub Dauuuuudi mzee wa Naaaaaammmmm, Macdonald Masey nk.

Umekuwa njia kwa vijana wengi kuwa waandishi na watangazaji , umekuwa Kiongozi bora kwa vituo mbalimbali vya radio. You're a blessing bro. Bahati mbaya sana hatukuwahi kuwa fellow staff , I remember 2013, when you arrived at HHC ALIVE FM is the same time I was leaving HHC to KWA NEEMA FM radio .

Today's your remembrance and memorable day . Enjoy your day shemeji. Blessings upon Blessings legend.

Happy belated birthday to you Maganga James Gwensaga .

Address

Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pastor Erasto Msuka posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Pastor Erasto Msuka:

Share