04/04/2026
HAPPY ABSENCE DAY
Leo *4.4.2026* ingekuwa *Birthday* yako mke wangu kipenzi, lakini kwa mapenzi ya *MUNGU* akaona vyema ukaisherehekee *PARADISO*.
Kwa mara ya kwanza, ninasherehekea siku yako ya kuzaliwa bila uwepo wako mama wa watoto wangu wazuri.
Siku k**a hii, tulizoea kuitumia kwa pamoja kumtafakari MUNGU kwa zawadi ya maisha kwetu.
Endelea Kumsifu MUNGU huko uliko, endelea kuinama na kuinuka mbele za MWANA-KONDOO WA BWANA pamoja na Makerubi, Maserafi na Malaika, ukiuimba wimbo wa *Musa*, "Wastahili MWANA-KONDOO uliyechinjwa.
Bado nitaendelea kukuenzi kwa kuwa mwaminifu kwa maisha yangu yote, mpaka hapo MUNGU atakaponifungulia mlango wa agano jingine kwa UAMINIFU wangu. Vitoto vyako *Miracle na Melvin* wanakukumbuka, ila picha zako kwenye SIMU zetu imekuwa faraja kwao, Miracle anauliza baba *"mama atarudi lini?, akipona atarudi?".* Watoto hawa wananifariji sana mke wangu.
"*_Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika k**a na wengine wasio na matumaini. Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye_ "* (1 The 4:13-14)
Tunakukumbuka mama yetu.