04/03/2026
HAPPY BIRTHDAY HELLEN (MRS OMAR)
1/3 miaka kadhaa iliyopita, ndio siku iliyokubali kukuleta duniani mtoto wangu mrembo HELEN binti JOSEPH.... Masha'Allah.....
K**a Mchungaji wako na baba yako wa Kiroho, ninayo furaha kubwa sana kwa Neema ya MUNGU kukuona ukiongezewa mwaka (1+ ) mwingine tena.
Najua mwanangu umepitia nyakati nyingi za furaha, maumivu, misukosuko, amani, magonjwa, mafanikio, kudharauliwa na kuthaminiwa n.k.
Umekuwa na nyakati pia za kumiliki vitu vingi vizuri na vya thamani kwenye maisha yako ikiwemo mume, watoto, fedha, nyumba, mavazi, biashara n. k, hakika hayo yote ni mema sana mbele za MUNGU, lakini nikuhakikishie tu, siku uliyofanya maamuzi ya kupokea "WOKOVU (YESU)" ndicho kitu cha THAMANI sana ulichokipokea katika maisha yako yote MWAKA JANA. Ninakufurahia sana mwanangu kukuona ukizidi kuongezeka kumpenda YESU kwa IMANI ya MATENDO na unazidi kumtegemea Yeye kila iitwapo leo.
Yeremia 17:7
“Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake”
Umefanyika BARAKA kubwa kwenye Kanisa lako la CMF-MAABARA YA YESU PENTECOST CHURCH , SADAKA zako na majitoleo yako yote ni HARUFU NZURI YA MANUKATO YA KUPENDEZA MBELE ZA MUNGU. MUNGU azikumbuke SADAKA zako na kuyaangaza maisha yako k**a tafsiri ya jina lako " Helen/Hellen" - yaani mwangaza au Nuru au mng'ao(Light or Shining).
Abarikiwe mume wako kipenzi Mr. Omar , wabarikiwe mabinti zako wazuri, Mariam na Zuhura (Zuu).
Umemheshimisha MUNGU na familia yako kwa kufanyia BIRTHDAY PARTY yako ndani ya KANISA. Libarikiwe tumbo lililokuzaa.
Hesabu 6: 24-26
“Bwana akubarikie, na kukulinda; Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili; Bwana akuinulie uso wake, na kukupa amani”
Happy birthday to you my lovely spiritual daughter, mwanangu kipenzi, Hellen wangu, kipenzi cha Omar mwenyewe, shangazi na bibi wa MIRACLE na MELVIN. Melvin ameniambia akija nyumbani akute misosi ya kutosha na masotojosotojo yake.... 😂😂😂. Enjoy your day daughter.
Pastor Erasto Msuka