19/09/2023
*HEAVEN LIGHT MINISTRIES INTL*
Shalom Nakusalimu kwa jina lipitalo majina yote ninayo Mambo machache natamani tuaangalie leo...
*NIFANYE NINI NINAPOMTUMIKIA MUNGU CHINI YA MTUMISHI MWINGINE WA MUNGU ALIYENITANGULIA KIHUDUMA*
Nianze kwa kumshukuru Mungu kwa Neema yake ya Ajabu na kunipa kupita chini ya Huduma kadhaa na mpaka leo bado natumika na Huduma pia na humu ndani nimepewa kujifunza mambo kadhaa ya muhimu sana kwenye Maisha ya UTUMISHI na Mimi leo nataka nishare na wewe Mambo machache ya Msingi ambayo yatakusaidia sana.
*HAPA NASEMA NA WATU HAWA*
1/WATOTO WA KIROHO WANAOLELEWA NA MTUMISHI.
2/ASKARI WENGINE WANAOHUDUMU PAMOJA NA MTUMISHI KWENYE HUDUMA(WATUMISHI WA MUNGU WANAOTUMIKA CHINI YA KIONGOZI)-NASEMA NA WATENDA KAZI WOTE WANAOFANYA HUDUMA CHINI YA MTUMISHI YEYOTE WA MUNGU.
-Wenye Huduma za masaidizano i.e waombaji waimbaji, partners,K**ati n.k
*MAMBO YA MUHIMU YA KUJIFUNZA UNAPOTUMIKA CHINI YA MTU*
1/Muheshimu na Hakikisha unakuwa MTII juu ya Maelekezo Mtu wa MUNGU anayatoa ili uwe salama katika leo yako na kesho yako ya Huduma.
Naelewa kibinadamu kuna wakati unaweza kuona k**a amekosea mambo lakini lazima ujue hajifanyii tu ila na Yeye anapokea Maelekezo kutoka kwa aliyemuita incase unapata shida na Maamuzi au Maelekezo nenda peke yako kazungumze kwa kumshauri k**a unaona kuna namna ingefanyika na kuleta ufanisi zaidi na akikataa tii na mwisho ukumbuke mwenye huduma ni Yeye(Yeye ndiye Mungu amemwamini na kumpa na wewe pale upo kujifunza)
MFANO:Elisha na Geazi
-Geazi Mtumishi wa Elisha alipatwa na ukoma kwa kutokutii Neno lililosemwa na Mtumishi la kutokupokea Fedha kutoka kwa Naamani.K*tii ni tabia ya Watu wanyenyekevu
Akamrudia yule mtu wa Mungu, yeye na mafuatano yake yote. Akaja, akasimama mbele yake; akasema, Sasa tazama, najua ya kwamba hakuna Mungu duniani mwote, ila katika Israeli; basi nakuomba upokee mbaraka kwa mtumwa wako. Lakini akasema, K**a BWANA aishivyo, ambaye nimesimama mbele yake, sipokei kitu. Akamshurutisha apokee; lakini akakataa. Naamani akasema; K**a sivyo, lakini mtumwa wako na apewe mzigo wa udongo wa baghala wawili; kwa maana mtumwa wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa wala dhabihu kwa miungu mingine, ila kwa BWANA. Jambo hili BWANA amwachilie mtumwa wako; bwana wangu akiingia nyumbani mwa Rimoni ili aabudu humo, naye akitegemea mkononi mwangu, nami nikijiinama nyumbani mwa Rimoni, hapo ninapojiinama nyumbani mwa Rimoni, BWANA amwachilie mtumwa wako jambo hili. Akamwambia, Enenda kwa amani Basi akamwondokea mbali kidogo. Lakini Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akasema, Tazama, bwana wangu amemwachilia huyo Naamani Mshami, asivipokee mikononi mwake vile vitu alivyovileta; k**a BWANA aishivyo, mimi nitamfuata mbio, nipokee kitu kwake. Basi Gehazi akamfuata Naamani. Naye Naamani, alipoona mtu apigaye mbio anakuja nyuma yake, alishuka garini amlaki, akasema, Je! Ni amani? Akasema, Amani. Bwana wangu amenituma, kusema, Tazama, sasa hivi wamenijia kutoka milimani mwa Efraimu vijana wawili wa wana na manabii; uwape, nakuomba, talanta ya fedha, na mavazi mawili. Naamani akasema, Uwe radhi, ukatwae talanta mbili. Akamshurutisha, akafunga talanta mbili za fedha ndani ya mifuko miwili, na mavazi mawili, akawatwika watumishi wake wawili; nao wakayachukua mbele yake. Naye alipofika kilimani, alivitwaa mikononi mwao, akaviweka nyumbani; akawaacha wale watu kuondoka, nao wakaenda zao. Lakini yeye akaingia, akasimama mbele ya bwana wake. Elisha akamwambia, Watoka wapi, Gehazi? Akanena, Mtumwa wako hakuenda mahali. Akamwambia, Je! Moyo wangu haukuenda na wewe, hapo alipogeuka yule mtu katika gari ili akulaki? Je! Huu ndio wakati wa kupokea fedha, na kupokea mavazi, na mashamba ya mizeituni, na mizabibu, na kondoo, na ng’ombe, na watumwa, na wajakazi? Basi ukoma wa Naamani utakushika wewe, na wazao wako hata milele. Naye akatoka usoni pake mwenye ukoma k**a theluji.
2 Fal 5:15-27 SUV
-Kosa dogo la kutokutii kukamcost akapata ukoma na hakupokea tena hata upako uliokuwa juu ya Elisha(Kosa likamcost Maisha usifanye hili kosa)
-Hapa ndipo nilijifunza hata k**a Mtumishi atakukwaza kiasi gani na kukuumiza nitaenda kulia kwa Bwana ila nitajitahidi sana kunyamaza ikibidi kuondoka kabisa hilo eneo ili usije ukakosea Nakwambia tena ni mambo ya kujifunza
*As we learn we grow in it(Tunapozidi kujifunza tunakuwa)*
-Neno la MUNGU linasema kutii ni bora kuliko dhabihu
1Samweli 15:22
Unapogusa Eneo la fundisho la Utii moja ya jambo utagundua ni kwamba Mungu kwenye maandiko yake matakatifu amekuagiza kuwatii na kuwaombea wale wanaotuongoza
Warumi 13:1-
K*tokutii ni dhambi na ndio dhambi waliyoitenda Adamu na Hawa pale bustanini shida haikuwa kula ila shida ilikuwa walikula walichoambiwa wasile umeipata Point yangu hapo...Ukiambiwa usifanye alafu wewe ukafanya maana yake umeasi au haujatii agizo/Neno....Umekaidi
Na kwenye UTUMISHI ni hivyo KIONGOZI Mkuu ni mmoja Yeye ndiye anatoa Maelekezo wengine tunafuata maelekezo yaliyotolewa unless k**a alikukaimisha na hapo lazima utafute kujua anasemaje juu ya kile unataka kukifanya...Maana yake lazima uwajibike kumpa taarifa.
2/. TEMBEA/TUMIKA KATIKA UNYENYEKEVU, UAMINIFU NA UPOLE.
-Biblia inamuonyesha Elisha akimimina maji juu ya mikono ya Elia na huoni akinung'unika Mahali popote.... Au kaangalie Nafasi alikuwa nayo Daudi baada ya kupelekwa Ikulu alikuwa ni mbeba silaha lakini wakati huo huo MUNGU alikuwa anampa shule kuhusu Ikulu.
Hapa namaanisha k**a unataka kupokea kile kilichoko juu ya Mtumishi lazima Ujifunze kumtumikia na kuwa Mwaminifu ndipo Bwana atakupa cha kwako.
Maana yake unapoona Mungu amekupeleka sehemu lazima utambue moja ya sababu za msingi za Mungu kukuweka chini ya Mtumishi mwingine ni wewe kujifunza na hakikisha kwa jitihada zote unawekeza katika kujifunza sana.Moja ya mambo utajifunza ni mwendo wa namna ya kutumika n.k
Mtumishi wa Mungu T.D Jakes aliwahi kusema You can't Receive the Anointing that you don't serve(Huwezi kupokea Upako wa Mtumishi ambaye hujautumikia/Hujatumikia chini ya Mtumishi aliye nae huo upako).
The Mantle is transferable(Vazi/Upako unamishika)Ila hauendagi kwa yeyote.Kumbuka wana wa Manabii walikuwepo ila aliyepokea upako uliokuwa juu ya Elia ni mmoja tu Elisha chanzo ni nidhamu aliyokuwa nayo.
3/Hakikisha unapata MUDA wa Kumuombea na kutoa Mali au fedha zako(sadaka) kutegemeza HUDUMA YAKE.
Nisikilize k**a Yeye anakesha kukuombea nawe muombee tena kwa bidii sana....KUMUOMBEA NI LAZIMA SIO OMBI HATA K**A HUTAKI MUOMBEE
Pia Neno linasema atampiga Mchungaji na kondoo watatawanyika...
Marko 14:27
Shetani akitaka kuwavuruga anampiga Kiongozi wenu,na akipigwa kundi lote hutawanyika na hamtaendelea Mbele tena...
kwahiyo kumuombea kwenu ndio usalama wenu pia.Kumuombea kutawafanya mmpende na kunyenyekea zaidi...K**a hujui moja ya jambo Maombi hufanya ni kushughulikia hali yako ya ndani(Mtu wako wa ndani pia)
Kasome namna Paulo alikuwa anayaombea makanisa yaliyoenda kuhubiri pamoja nae kwa Mali zao Mfano Kanisa la Filipi nilikuwa nasoma mpaka Nashangaa... anawatamkia Maneno Mazito ya Baraka
Unajua Mungu anatufundisha ni hili Jifunze kujiungamanisha na SADAKA kwenye HUDUMA ya MTUMISHI unayetumika chini yake.Kuna wakati unakuta umepata kujua kuna Mambo yanamsumbua na anahitaji FEDHA au assistance fulani be there saidia pasipo kutaka kuonekana na Watu uone k**a kutakuwa na Milango iliyofungwa Mbele yako.
Usisubiri partners watoke Nje kuja kusupport HUDUMA yenu lakini anzeni nyinyi kujitoa watu wa nje wakija waje kusupport tu.Chota Baraka chap chap hahaa hapa najua kuna aina ya watu hawapendagi kusikia habari za Sadaka ila kasome biblia yako Zawadi itakupa kibali mbele za wakuu Wewe endelea kwendaga mikono mitupu tu hayaa sisi Wengine haya tulijifunza in a hard way hatukupataga Mtu wa kutuambia mapema ila Namshukuru Mungu amenipaga nidhamu ya kujifunza kwa watu iwe kwa kutazama au hata kuuliza inapobidi na hiki moja ya watu walitumika kupanda mbegu ni Mke wangu pamoja na Mtumishi wa Mungu Rehema tena huyu ndio aliniambia wazi wazi Mungu awabarikini sana kokote mlipi
Ile kwamba mpo ndani ya Huduma sio guarantee ya ninyi kupokea kile alichobeba Mtumishi hata k**a atawawekea mikono kila Mara na kuwaombea.
Nakwambia ukweli Mtu yeyote anayesimama na Mtumishi kwenye jambo lolote analolifanya huwa anaenda pamoja nae kokote aendapo, na kiukweli huwa anakuwa kwenye Moyo wa Mtumishi kasome habari za Mama Mshunami na Elisha nawaza tu k**a yule mama asingelipata wazo la kujenga kile chumba yamkini Elisha asingelipata mzigo wa kumuombea ili apate Mtoto.
*Iguse madhabahu nayo ikuguse*
Madhabahu ambayo huipelekei sadaka haiwezi kukusaidia.Iguse madhabahu ya Mtumishi unayetumika nae kwa SADAKA ZAKO acha kupeleka Nje au Mbali majibu yako yapo hapo hapo Tulia Unless umeongozwa na Bwana...Hii inaenda mpaka kanisani maana wengi hiwa wanawadharau wachungaji wao sana leo upone kwa jina la Yesu.
Jifunze kujichotea baraka,kwani hujawahi kufwatilia na kujiuliza kwanini watu wa nje ndio hubarikiwa/kupata msaada kwa wepesi kuliko walioko ndani ya Huduma/Kanisa
4/KATAA KUJILINGANISHA NAE HATA K**A NA WEWE NI MTUMISHI.
-Upako huwa hautembei horizontal (ulalo) ila Vertical (kutoka juu kwenda chini).Ukitaka kupokea jishushe kujishusha sio dhambi ila itakufaidia wewe ujishushae.
Kujilinganisha nae wakati wengine huwa ni matokeo ya kiburi cha uzima/Ujeuri n.k
Kuna Watu wa Mungu wana mahusiano ya ndani sana unaposhindana nao Bwana atakachokuja kufanya ni kukublock wewe ukajikuta hukui wala uendelei kamwe au hata kupigwa kabisa na Mungu kwa ujinga wako.
MAFANO:
MUSA /HARUNI V.S AKINA KORA
Hesabu 16:
-Kora alimchallenge Musa na Haruni kwamba na wao ni makuhani Mungu hawezi kusema na akina Musa tu peke yao na wao ni Watumishi ...alafu aliyeita akaja kuamua kesi ndipo Ardhi ikafunguka na ikawameza akina Kora na wenzie wote.
Soma hapa....
nao, pamoja na watu kadha wa kadha wa wana wa Israeli, watu mia mbili na hamsini, Wakuu wa mkutano, waliokuwa wateule wa mkutano, watu wenye sifa, wakainuka mbele ya Musa; nao wakakusanyika kinyume cha Musa na Haruni, na kuwaambia, Ninyi inawatosha, kwa kuwa mkutano wote ni mtakatifu, kila mmoja miongoni mwao, BWANA naye yu kati yao; n’nini basi kujitukuza juu ya mkutano wa BWANA? Musa aliposikia maneno haya, akapomoka kifudifudi; kisha akanena na Kora na mkutano wake wote, akawaambia, Asubuhi BWANA ataonyesha ni kina nani walio wake, kisha ni nani aliye mtakatifu, tena ni nani atakayemkaribisha kwake; maana, yeye atakayemchagua ndiye atakayemsongeza kwake. Fanyeni neno hili; twaeni vyetezo, ninyi Kora na mkutano wake wote; vitieni na moto, mkaweke na uvumba juu yake mbele za BWANA kesho; kisha itakuwa ya kwamba mtu BWANA atakayemchagua, yeye atakuwa mtakatifu; inawatosha ninyi, enyi wana wa Lawi. Je! Mwaona kuwa ni jambo dogo kwenu, kuwa Mungu wa Israeli amewatenga ninyi na mkutano wa Israeli, ili apate kuwakaribisha kwake; ili mfanye utumishi wa maskani ya BWANA, na kusimama mbele ya mkutano ili kuwatumikia; tena ya kuwa amekuleta uwe karibu, na ndugu zako wote wana wa Lawi pamoja nawe? Nanyi, je! Mwataka na ukuhani pia? Kwa sababu hii wewe na mkutano wako wote mmekusanyika kinyume cha BWANA; na Haruni, je! Yeye ni nani hata mkamnung’unikia? Musa akakasirika sana, akamwambia BWANA. Usiikubali sadaka yao; mimi sikutwaa hata punda mmoja kwao, wala sikumwumiza hata mtu mmoja miongoni mwao. Kisha Musa akamwambia Kora, Wewe na mkutano wako wote iweni hapa mbele ya BWANA kesho, wewe, na wao, na Haruni; mkatwae kila mtu chetezo chake, na kutia uvumba juu yake, mkavilete mbele za BWANA, vyetezo mia mbili na hamsini; wewe pia, na Haruni, kila mtu na awe na chetezo chake. Basi wakavitwaa kila mtu chetezo chake, wakatia na moto ndani yake, wakatia na uvumba juu ya moto, na kusimama pale mlangoni pa hema ya kukutania, pamoja na Musa na Haruni. Kisha Kora akakutanisha mkutano wote kinyume chao mlangoni pa hema ya kukutania; na utukufu wa BWANA ukatokea mbele ya mkutano wote. Kisha BWANA akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia, Jitengeni ninyi mkaondoke kati ya mkutano huu, ili nipate kuwaangamiza mara moja. Nao wakapomoka kifudifudi, wakasema, Ee Mungu, Mungu wa roho za wenye mwili wote, je! Mtu mmoja atafanya dhambi, nawe utaukasirikia mkutano wote? BWANA akasema na Musa, na kumwambia, Nena na mkutano, na kuwaambia, Ondokeni ninyi hapo karibu na maskani ya Kora, na Dathani, na Abiramu. Basi Musa akainuka na kuwaendea Dathani na Abiramu; na wazee wa Israeli wakaandamana naye. Akasema na mkutano, na kuwaambia, Nawasihi, ondokeni penye hema za hawa watu waovu, wala msiguse kitu chao cho chote, msiangamizwe katika dhambi zao zote. Basi wakaondoka hapo karibu na maskani ya Kora, na Dathani na Abiramu, pande zote; nao kina Dathani na Abiramu wakatoka nje wakasimama mlangoni mwa hema zao, pamoja na wake zao, na wana wao na watoto wao wadogo. Musa akasema, Kwa jambo hili mtajua ya kwamba BWANA amenituma, ili nifanye kazi hizi zote; kwa kuwa mimi sikuzifanya kwa akili zangu mwenyewe. K**a watu hawa wakifa kifo cha sikuzote, k**a watu wote wafavyo, au k**a wakipatilizwa kwa mapatilizo ya watu wote; hapo basi BWANA hakunituma mimi. Lakini BWANA akiumba kitu kipya, na hiyo nchi ikifunua kinywa chake na kuwameza, pamoja na wote walio nao, nao washukia shimoni wali hai; ndipo mtatambua ya kwamba watu hawa wamemdharau BWANA Basi ilikuwa, hapo alipokwisha kusema maneno haya yote, nchi iliyokuwa chini yao ikapasuka; nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na watu wa nyumba zao na wote walioshik**ana na Kora, na vyombo vyao vyote. Basi wao, na wote waliokuwa nao, wakashukia shimoni wali hai; nayo nchi ikawafunika wakaangamia kutoka mle mkutanoni. Nao Israeli wote waliokuwa kando-kando yao wakakimbia kwa ajili ya kilio chao; kwa kuwa walisema, Nchi isije kutumeza na sisi. Kisha moto ukatoka kwa BWANA, ukawateketeza hao watu mia mbili hamsini waliofukiza uvumba.
Hes 16:2-7, 9-11, 15-35 SUV
*MFANO WA PILI NI MWENDELEZO WA HIKI NI HESABU 17*
Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia, Nena na wana wa Israeli, kisha upokee kwao fimbo, fimbo moja kwa ajili ya nyumba ya kila baba, katika wakuu wao wote, k**a nyumba za baba zao zilivyo, fimbo kumi na mbili; kisha andika jina la kila mtu katika fimbo yake. Na katika fimbo ya Lawi utaliandika jina la Haruni; maana, itakuwa fimbo moja kwa kila kichwa cha nyumba za baba zao. Nawe utaziweka katika hema ya kukutania mbele ya huo ushahidi, hapo nikutanapo pamoja nanyi. Kisha itakuwa, mtu huyo nitakayemchagua, fimbo yake itachipuka; nami nitayakomesha kwangu manung’uniko ya wana wa Israeli, wanung’unikiayo juu yenu. Basi Musa akawaambia wana wa Israeli, ndipo wakuu wao wote wakampa fimbo, fimbo moja kwa kila mkuu, k**a nyumba za baba zao zilivyokuwa, fimbo kumi na mbili; na fimbo ya Haruni ilikuwa kati ya fimbo zao. Kisha Musa akaziweka hizo fimbo mbele za BWANA katika hema ya kukutania. Ilikuwa siku ya pili yake, Musa akaingia ndani ya hema ya ushahidi; na tazama, ile fimbo ya Haruni iliyokuwa kwa nyumba ya Lawi ilikuwa imechipuka, imetoa michipukizi, na kuchanua maua; na kuzaa malozi mabivu. Kisha Musa akazileta nje hizo fimbo zote kutoka hapo mbele za BWANA na kuziweka mbele ya wana wa Israeli wote; nao wakaangalia, na kila mtu akaitwaa fimbo yake. Kisha BWANA akamwambia Musa, Irudishe fimbo ya Haruni mbele ya ushahidi, ili itunzwe iwe ishara juu ya hawa wana wa maasi; ili uyakomeshe manung’uniko yao waliyoninung’unikia, ili wasife. Basi Musa akafanya vivyo; k**a BWANA alivyomwagiza, ndivyo alivyofanya. Kisha wana wa Israeli wakanena na Musa, na kumwambia, Angalia, sisi twafa, twaangamia, sote twaangamia. Kila mtu akaribiaye, aikaribiaye maskani ya BWANA, hufa; je! Tutakufa pia sote?
Hesabu 17:1-13 SUV
-Mungu akachipuza fimbo bila kupandwa wala Maji ili kusignify aliowachagua na Mungu akakomesha Maneno yote.
-Chunga sana Mdomo wako na Matendo yako ifahamu nafasi yako na tumika kwa uaminifu mahali ambapo MUNGU amekupa ukiona umeshindwa toka ila usimobilize watu against Mtumishi ili utake Nafasi aliyonayo....Hiki kitu ndio kile alichotaka kufanya shetani pale Mbinguni alitaka kufanya mapinduzi yeye ndio aanze kurun show pale kilichompata mpaka leo anasimulia,akajua yeye si chochote si lolote.
Kuna wakati Utukufu unaouona uko juu yako ni kwasababu ya Mahali ulipojiungamanisha napo Dont forget that...Siku utakapoyakoroga na ule Utukufu utaondoka juu yako maana Utukufu ni Vazi.
5/MPOKEE MOYONI MWAKO NA TAMBUA MAFUTA YALIYOKO JUU YAKE ILI UWEZE KUYAFAIDI.
-Nataka utambue Mtumishi yeyote hata yule unayemuona niaje niaje pia anamafuta ya Roho Mtakatifu juu yake na hayo Mafuta huwa hayatoki kiholela Neno la Mungu linasema Ampokeae Nabii hupata Thawabu ya Nabii
Maana yake nini hatak**a Mtumishi anaupako mkubwa kiasi gani ukimdharau huwezi kupata msaada kutoka kwake kamwe
MFANO:YESU NA WATU WA NYUMBANI KWAKE
-Wagalilaya walikosa kufaidi kile kilichokuwa juu ya Yesu kwa ajili yao kwasababu walipofushwa na roho ya mazoea (the spirit of familiarity-Walijikuta wanamjua sana wakidhani ni Mtoto wa Yusufu na ndio wakapishana na Muujiza yao)
Soma hapa...
Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, *Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii?* Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda? Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote? Wakachukizwa naye. Yesu akawaambia, *Nabii hakosi kupata heshima, isipokuwa katika nchi yake, na nyumbani mwake mwenyewe. Wala hakufanya miujiza mingi huko, kwa sababu ya kutokuamini kwao.*
Mt 13:54-58 SUV
Kwenye Mfano huu kuna Mambo mengi ya kujifunza
-Hawa ndugu hawakumuamini Yesu kisa ni walikuwa wanamfahamu pamoja na Ndugu zake.Nakwambia fwatilia Ndugu au watu wowote wanaomfahamu Mtumishi tangu akiwa mdogo k**a huwa wanapokea kile amebeba,Hawa hata akiwepo kwenye Huduma anakuja kumsupport Ndugu yake unless Mungu ameingilia kati...
GROUP jingine ambalo huwa halipokei au huwa ni kazi wao kupokea au kumpokea ni Marafiki zake ambao walikuwa wanamjua tangu zamani nakwambia fuatilia na hawa nao ni mpaka Bwana awaponde ponde kwanzaa ndio utaona kuvunjika na wanaanza kumtazama k**a Mtumishi wa Mungu.
Kamwe usiruhusu Mahusiano yako ya nje na MTUMISHI yakuzuie kupokea Neno au Upako au Thawabu aliyobeba Mtu wa MUNGU Jifunze kubadirika ili uweze kufaidia upako juu ya Mtumishi kuna Muda hata k**a ni Rafiki yako ukiona tu kaanza kuongea kwenye Nafasi ya kitumishi na Wewe hama harakaa ili uweze kupokea sawa sawa haya Mambo sio mepesi lakini jifundishe jilazimishe mpaka uweze ni Rafiki yako sawa,Ni mume wako sawa lakini bado ni Mtumishi wa Mungu na akiama Nafasi hama nae.
Ivi umegundua pia hata wake za Watumishi au Watoto(biological) na wao huwa mara nyingi hawafaidiki na upako uliopo juu ya Watumishi wa Mungu.
Nakumbuka niliwahi kusikia ushuhuda Mmoja wa Mama Mchungaji mmoja ambaye alikuwa kanisani kwenye Ibada na mume wake alikuwa akiwahudumia watu na Wingu au Upako Ulikuwa Mkubwa sana na watu walisaidika sana wakawa wanatoa shuhuda kuu yule mama akainuka katikati ya ibada akarudi nyumbani akapika chakula kizuri akipendacho Mume wake na akatoa sahani za wageni akatenga Mezani akimsubiria Baba Mchungaji arudi...Sasa na Baba Mchungaji kule akawa anahudumu huku akitafakari kuna kitu gani kimetokea mbona Wife kaondoka ghafla alipofika nyumbani akakuta yale Mazingira akakaribishwa na kuketishwa Mezani...Sasa familia yao ilikuwa inapitia changamoto fulani na walikuwa wameomba lakini hakuna Matokeo yeyote yule Mama akapiga magoti akamwambia Baba Mchungaji familia yangu inapitia hili naomba uniombee yule Pastor anasema Upako ule ule uliokuwa kanisani ukashuka juu yake saa ile ile pale nyumbani akaweka mikono juu ya mke wake nae akaenda chini kwa Nguvu za Mungu...Hapa nikajifunza Upako wa Roho Mtakatifu unatabia usipomheshimu Mtumishi haukusaidii kamwe....
Unajua kilichotokea ni hivi yule Mama alitambua Nafasi ya Mume wake k**a Mtumishi wa Mungu na kwamba Mungu ameweka kitu juu yake kwa ajili ya watu na yeya ni mmoja ya watu waliowekwa chini yake....Mama akaama kutoka kwenye Nafasi ya mke wa Mtumishi akawa Kondoo katika kundi la Bwana ambalo Mtumishi ameaminiwa kwalo akahusiana na Mume wake k**a Mtumishi wa Mungu na alipofanya hivyo Mungu akayasikia Maombi yake.
Umenielewa ewe Mama Mtumishi si ndio ? Ubarikiwe sana
SOMA PIA MFANO HUU:
➡️MUSA, HARUNI NA MIRIAM
Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi. Wakasema, Je! Ni kweli BWANA amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? BWANA akasikia maneno yao. Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi. BWANA akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje. BWANA akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili. Kisha akawaambia, Sikizeni basi maneno yangu; Akiwapo nabii kati yenu, Mimi, BWANA, nitajifunua kwake katika maono, Nitasema naye katika ndoto. Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote; Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa? Hasira za BWANA zikawaka juu yao; naye akaenda zake. Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe k**a theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma. Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi. Nakusihi, asiwe k**a mmoja aliyekufa, ambaye nyama ya mwili wake nusu imelika hapo atokapo tumbo la mama yake. Musa akamlilia BWANA, akasema, Mpoze, Ee Mungu, nakusihi sana. BWANA akamwambia Musa, Je! K**a baba yake angalimtemea mate usoni tu, hangaliona aibu muda wa siku saba? Na afungwe nje ya kambi muda wa siku saba, kisha baada ya hayo ataletwa ndani tena. Basi Miriamu alifungwa nje ya kambi muda wa siku saba; wala watu hawakusafiri hata Miriamu alipoletwa ndani tena.
Hes 12:1-15 SUV
-Nataka nikuonyeshe Ndugu za Musa ambavyo walijikwaa kuhusu kuoa kwa Musa na wakamsema na Mungu akasikia na akaja kuamua jambo hili Miriam akapigwa na ukoma Haruni akanusurika kwasababu alikuwa na Mafuta ya kikuhani siku ile juu yake
tena Chunga kimya chako sometimes unaweza kuumizwa lakini jizuie usiongee kwa watu kaongee kwa Mungu hata k**a unaona madhaifu yake jitahidi kuyaficha unayaona kwasababu upo karibu na Mungu ameruhusu uyaone ili umuombee sawa sawa Acha Maneno Maneno.
Kumbuka hata WATOTO wa Nuhu kuna mmoja aliufunua uchi wa Baba yake badala ya kuufunika k**a wale wawili waliopata Hekima akapokea Laana kwa generation yake na wenzie wakavuna baraka kwasababu walimstahi Baba yao na kufunika uchi wake.
not Unveil the Nakedness of Your father/Man of God (Usifunue uchi wa Baba yako... Mtu wa Mungu)
Kumbuka kwasababu ya ukaribu ulionao nae ndio maana umeyajua hayo Madhaifu k**a unaona huwezi kuhandle(kustahimili) jiweke mbali sio lazima umzoee na sio dhambi kujiweka mbali ni nidhamu njema kwa ajili ya afya yako ya kiroho.
Soma hapa...
Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu; akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake. Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao. Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea. Akasema, Na alaaniwe Kanaani; Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake. Akasema, Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu; Na Kanaani awe mtumwa wake. Mungu akamnafisishe Yafethi. Na akae katika hema za Shemu; Na Kanaani awe mtumwa wake. Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini. Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa.
Mwa 9:20-29 SUV
*UNAPOTUMIKA MAMBO HAYA NAOMBA USIAYASAHAU*
1/Unapotumika kuna Kitu k**a Kiongozi unatakiwa kukiachilia kwa walio chini yako
MFANO Yesu aliaachilia NENO LA MUNGU kwa Mitume 12 na PAULO pia aliachilia NENO LA MUNGU kwa akina Timotheo tena akawaagiza na wao wawafundishe watu wengine waaminifu lile Neno.
Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.
2 Timotheo2:2 SUV
-Nataka Ufahamu wewe k**a Kiongozi ni kielelezo kwa walio chini yako kuna watu wanakufwata na wanajifunza chini yako.
Wewe ni barua kuna watu wanakusoma kwa kadiri unavyoonyesha ubora katika UTUMISHI wako unafanya na Watu walioletwa chini yako Kesho kuja kuwa bora zaidi yako maana wamejengwa kwenye Msingi bora.
Jambo la Mwisho wekeza kwa kuwafundisha NENO LA MUNGU kwa ufasaha kumbuka MUNGU amekuamini na amekupa dhamana na kuna muda akiwataka anategemea wawe wameiva na wamekomaa.
hayo tu
2/Kwa wale wanaotumika chini yako(Mtumishi ) naomba niwaambie Mambo mawili ya kutoa
-Moja Muda wako na kupokea kile unapewa yaani Neno ukiwa na mtazamo kwamba unabeba NENO kwa ajili ya generation itakayofuata...Unabeba NENO kulipeleka kwa Watu wengine watakaokuwa waaminifu.
Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine.
2 Tim 2:2 SUV
Jambo la Pili ujitoe Kwa Vitu vyako Mali kuhakikisha unasupport Huduma ambayo unamtumikia Mungu kwayo
na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, *waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.*
Luka 8:3 SUV
-Je Wewe unamtumikia Mtumishi Kwa Mali zako(unatumika pamoja nae kwa fedha zako?)
-Kwasababu ya Uwepo wako hakikisha kuna maeneo Mtumishi wa Mungu asistruggle ndio maana Mungu alikupeleka hapo ili Yeye akupandie vya Rohoni naye avune vya Mwili ni Kanuni ya kimungu though Paulo akasema aliamua kufanya kazi ili asije akamlemea Mtu yeyote umenielewa
1Wakoritho 9:11
ANGALIZO LA MUHIMU:
-Jifunze kujitoa zaidi Mfano ni kweli umekuja k**a Partner wa Huduma ila kuna muda unaona kuna kitu/Vitu unaweza kufanya na wanahitaji mtu hakikisha unakuwa tayari kujitoa kwa hari yote na kuyafanya yote kwa uaminifu na kwa moyo wako wote k**a kwa Bwana.Maana wengi wanaotoa Fedha huwa hawajitoi.... 2Wakoritho 8:5
Tena walitenda hivi si k**a tulivyotumaini tu, bali kwanza walijitoa nafsi zao kwa Bwana; na kwetu pia, kwa mapenzi ya Mungu.
2 Kor 8:5 SUV
na kishaToa
Nimekupa baadhi tu ya Siri za ndani ila naamini yapo mengi waweza kujifunza kutokea kwa Watumishi Wengine na kwenye Neno la Mungu na kuweka kwenye Matendo kile tunajifunza ili kuwa bora Asante kwa kukaa Darasani kujifunza pamoja nami.Umebarikiwa sana Mtumishi wa Mungu.
Chambua generations
Kelvin & Jenipher Chambua CK
Heaven Light Ministries Intl
Dodoma.
Tanzania.