Bezaleli Media Tanzania

Bezaleli Media Tanzania Ungana nasi YouTube|TikTok|Facebook|Instagram|Kwa Habari Picha na Matukio ya Injili|Jumbe za Neno la Mungu|Mahusiano
¶Sisi ni Habari Njema

ya Neno la Mungu, Mafundisho na Injili ya Wazi
za Kiofisi: Photocopy & Printing, Scanning, Lamination na Vifaa Vyote Muhimu

Safari ya staa wa muziki wa pop duniani, Justin Bieber, ni kielelezo tosha cha jinsi kipaji kikubwa kinavyokutana na uma...
21/07/2026

Safari ya staa wa muziki wa pop duniani, Justin Bieber, ni kielelezo tosha cha jinsi kipaji kikubwa kinavyokutana na umaarufu mzito akiwa mdogo na hatimaye kupata matumaini na utambulisho mpya ndani ya Yesu Kristo. Ingawa alilelewa katika misingi ya Kikristo na mama yake Pattie Mallette, presha za umaarufu na tasnia ya burudani katika ujana wake zilimuingiza kwenye msongo wa mawazo na matumizi makubwa ya dawa za kulevya zilizomfanya ajione k**a "bidhaa" tu na kufikia hatua ya kukata tamaa kabisa ya maisha.

​Mabadiliko makubwa ya kiroho yalianza mnamo mwaka 2014 alipofikia hatua ya mwisho ya uvumilivu na kuamua kubatizwa kwa dharura Usiku wa manane ndani ya beseni la kuogea (bathtub) la mchezaji wa NBA Tyson Chandler, akisaidiwa na Mchungaji Carl Lentz na Judah Smith. Tangu wakati huo, Bieber amekuwa akieleza jinsi Mungu alivyomwezesha kupona majeraha ya nafsi na kumrejeshea utambulisho wake k**a mwana wa Mungu, badala ya kutawaliwa na matakwa au matarajio ya tasnia ya muziki.

​Imani hiyo imekuwa nguzo kuu iliyomvusha kwenye changamoto mbalimbali za maisha, ikiwa ni pamoja na skendo za kijamii, matatizo ya kiafya k**a vile kupooza uso kutokana na Ramsay Hunt syndrome mwaka 2022, na ubatizo wa pamoja na mke wake Hailey Bieber mwaka 2020. Hivi sasa, Bieber anaendelea kutumia jukwaa lake kubwa kuuhubiri ulimwengu kuhusu pendo lisilo na masharti, msamaha, na matumaini anayoyapata kupitia Yesu Kristo.

“Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.”  — Marko 16:16 TOCC DODOMA
20/07/2026

“Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.”
— Marko 16:16

TOCC DODOMA

Kilele cha wiki ya Idara wa Muziki na uimbaji, DMS.TAG DMS
14/07/2026

Kilele cha wiki ya Idara wa Muziki na uimbaji, DMS.

TAG DMS

12/07/2026

Tunamtaka Bwana na nguvu zake

11/07/2026

11/07/2026

Utaratibu!!

07/07/2026

: Wanaume Wakiamua jambo lao, Hakuna wa Kuwazuia!

Hawa ni CMF_@TAG TOCC BAHI DODOMA

_KAZI ZA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO_1. Kukuongoza (Warumi 8:14, Matendo 16:6)2. Kukufundisha neno la Mungu au kukutia kwe...
04/07/2026

_KAZI ZA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO_

1. Kukuongoza (Warumi 8:14, Matendo 16:6)

2. Kukufundisha neno la Mungu au kukutia kwenye kweli yote ya Mungu (Yohana 16:13-14, 1 Wakorintho 2:12-15)

- Kweli ni neno la Mungu (Yohana 17:17)

3. Kukulinda (1 Petro 1:5)

4. Kukusaidia udhaifu wako wa kutojua kuomba (Warumi 8:26)

5. Kutia nuru macho yako ya rohoni (Waefeso 1:18)

6. Kukusaidia kuyaweza yale mambo magumu yasiyowezekana kwa wanadamu (Wafilipi 4:13, Mathayo 19:26)

7. Kuijenga nafsi yako (1 Wakorintho 14:4)

8. Kukupa roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha Bwana (Isaya 11:2)

9. Kukupa tunda la Roho mtakatifu (Wagalatia 5:22-23)

10. Kukusaidia usitimize tamaa za mwilini (Wagalatia 5:16-17)

11. Kukupa karama mbalimbali za rohoni (1 Wakorintho 12:4-11)

12. Kukusaidia kumwabudu Mungu katika roho na kweli (Yohana 4:24)

- Hakuna siku utamwabudu Mungu katika roho na kweli k**a ndani yako huna Roho mtakatifu..

13. Anakupa ujasiri wa kuishuhudia habari njema ya ufalme wa Mungu mbele za mataifa yote (Matendo 1:8, Matendo 4:31)

14. Kukusaidia kujitambua kuwa wewe ni mwana wa Mungu (Warumi 8:16)

_HIZI NI MOJA YA KAZI ANAZOZIFANYA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO, HIVYO TAFUTA SANA KUJAA NGUVU ZA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO KWA FAIDA YA UTU WAKO WA NDANI_

Whatsapp/ Call +255657117595

Mwl.Joseph Leonard

 : TAZAMA MKUTANO WA INJILI UNAVYOTIKISA HAPA  Hàkika, Yesu anayo Mamlaka!“Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu a...
04/07/2026

: TAZAMA MKUTANO WA INJILI UNAVYOTIKISA HAPA
Hàkika, Yesu anayo Mamlaka!
“Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza),”
— Marko 2:10

Leo Tena TUNAENDELEA, WOTE MNAKARIBISHWA!!



Mch.Anas Boazi
: Mwinjilisti, Ev.Geofrey Mourice_Kutoka Dar

Address

Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bezaleli Media Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Bezaleli Media Tanzania:

Shortcuts

Share