Bezaleli Media Tanzania

Bezaleli Media Tanzania Ungana nasi YouTube|TikTok|Facebook|Instagram|Kwa Habari Picha na Matukio ya Injili|Jumbe za Neno la Mungu|Mahusiano
¶Sisi ni Habari Njema

ya Neno la Mungu, Mafundisho na Injili ya Wazi
za Kiofisi: Photocopy & Printing, Scanning, Lamination na Vifaa Vyote Muhimu

_KANUNI 5 MUHIMU ZA KUZINGATIA SIKU YA IBADA_1. Kuupumzisha moyo wako, yaani moyo wako haupaswi kuwaza madeni, kazi zako...
31/05/2026

_KANUNI 5 MUHIMU ZA KUZINGATIA SIKU YA IBADA_

1. Kuupumzisha moyo wako, yaani moyo wako haupaswi kuwaza madeni, kazi zako, mahusiano yako, biashara zako, marafiki zako, mali zako n.k bali unapaswa kumuwaza Mungu tu 'na hii ndiyo maana ya KUPUMZIKA (Kutoka 34:21

- Moyo wako ukikosa utulivu wa ndani hauwezi kumwabudu Mungu katika roho na kweli (Yohana 4:23)

- Kwahiyo ili umwabudu Mungu katika roho na kweli unapaswa upate utulivu wa ndani (uupumzishe moyo wako) ili upate nafasi ya kukutana na Mungu bila kubanwa na kitu chochote..

2. Nenda ukajihudhurishe nyumbani mwa Bwana (Waebrania 10:25, Zaburi 122:1, Zaburi 100:1-5)

- Siku ya ibada si siku ya kukaa tu nyumbani bali ni siku ya kwenda kujihudhurisha nyumbani mwa Bwana (kanisani), ni siku ya kukaa hemani mwake na kumwabudu kwa unyenyekevu, sifa na usafi wa moyo (Zaburi 135:1-3)..

3. Hakikisha una sadaka ya kwenda nayo kwenye madhabahu ya Mungu (Kutoka 23:15b)

- Sadaka itaifanya madhabahu iseme kitu kwaajili ya maisha yako (Ufunuo 16:7, Mwanzo 22:10-18)

4. Hakikisha Mungu ameutia wimbo mpya wa sifa moyoni mwako (Zaburi 40:3, Zaburi 96:1-13)

- Ukiukosa wimbo mpya wa sifa kwenye kinywa chako hutamsifu Mungu wala kumwabudu Mungu katika roho na kweli, hutamwabudu Mungu k**a wanavyofanya wenye uhai 4 na wazee 24 huko mbinguni (Ufunuo 5:8-14)

5. Hakikisha una biblia na unaongozwa na Roho mtakatifu kwenye ibada yako (Warumi 8:14, Yoshua 1:8, wakolosai 3:16)

- Biblia na uongozi wa Roho mtakatifu vitakusaidia kumthibitisha Mungu wa kweli unayepaswa kumwabudu kwenye ulimwengu wa roho, bila Biblia na uongozi wa Roho mtakatifu utamwabudu Mungu yoyote hata usiyemjua 'CHUNGA SANA' (Matendo 17:11)

_NIKUTAKIE IBADA NJEMA, NA UWE NA IBADA YA NEEMA NA BARAKA KWA JINA LA YESU_

Whatsapp/ Call +255657117595

Mwl.Joseph Leonard

31/05/2026

MAOMBI Mazuri ya Kufunga Ibada
TBT GUNGU_KIGOMA

_TABIA 11 ZINAZOFANYA USHINDWE KUFANIKIWA KIROHO NA KIMWILI_1. Usingizi wa kiroho, mfano 'kutokuwa na muda wa kuomba, ku...
30/05/2026

_TABIA 11 ZINAZOFANYA USHINDWE KUFANIKIWA KIROHO NA KIMWILI_

1. Usingizi wa kiroho, mfano 'kutokuwa na muda wa kuomba, kutokuwa mtu wa ibada, kutokuwa na muda wa kusoma biblia yako, kutotembea kwenye mapenzi ya Mungu na kutokumtii Mungu kabisa (Waefeso 5:14-17)

2. Kutokuwa na maono, mikakati, mipango au vipaumbele vya maisha (Mithali 29:18)

3. Kutokuwa na maarifa sahihi ya kiroho na kimwili (Hosea 4:6, Wagalatia 4:1-2)

4. Kutokuwa na ushirika na Mungu kiroho au kutokumjua Mungu kabisa (Ayubu 22:21,

5. Kutumia zaidi unachokipata kuliko kuzalisha au kukiendeleza (Mathayo 25:14-30)

6. Kushindwa kujua uwezo ulionao au kipawa ulichonacho (Waefeso 4:11

7. Hofu ya kulipa gharama (Luka 14:28-30)

8. Kutojua yale uliyokirimiwa na Mungu ndani yake Kristo (1 Wakorintho 2:12, Waefeso 1:3)

9. Kuambatana na watu wasio na ndoto yoyote ya maisha ( 2 Wakorintho 6:14, Mithali 27:17, Mithali 13:20)

10. Kutumia muda wako mwingi kwenye mambo yasiyo na faida kwenye maisha yako (Isaya 48:17

11. Uvivu uliopitiliza (Mithali 12:27, Mithali 13:4, Mithali 20:4)

_HIZI NI TABIA UNAZOPASWA KUZISHINDA KWENYE MAISHA YAKO ILI UFANIKIWE KIROHO NA KIMWILI_

Whatsapp/ Call +255657117595

Mwl.Joseph Leonard

 : Jumapili hii katika ibada zetu zote tatu, kwa neema ya Mungu tutakuwa na mtumishi wa Mungu Mwinjilisti Johannes Amrit...
29/05/2026

: Jumapili hii katika ibada zetu zote tatu, kwa neema ya Mungu tutakuwa na mtumishi wa Mungu Mwinjilisti Johannes Amritzer. Naomba nikukaribishe kwako uliyeko Dar, karibu tuabudu pamoja. Ratiba za ibada zipo hapo chini 👇
Mungu akubariki

  NINI TUYAONAPO HAYA?🇰🇪 Viongozi wa makanisa ya Kiinjili nchini Kenya wameanzisha rasmi harakati mpya ya maombi iitwayo...
28/05/2026

NINI TUYAONAPO HAYA?
🇰🇪 Viongozi wa makanisa ya Kiinjili nchini Kenya wameanzisha rasmi harakati mpya ya maombi iitwayo Kenya National Prayer and Transformation Movement (KNPTM), wakilenga kuandaa zaidi ya waombezi milioni 1 kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.

Harakati hiyo ilizinduliwa Mei 4 jijini Nairobi chini ya kaulimbiu “My Country, My Responsibility”, ikiwakutanisha maaskofu, wachungaji, waombezi na viongozi wa Kikristo kutoka madhehebu mbalimbali.

Viongozi hao wamesema Kenya inapitia kipindi kigumu cha kupanda kwa gharama za maisha, ukosefu wa ajira kwa vijana, migawanyiko ya kisiasa na ongezeko la rushwa, hali ambayo imeongeza hofu na kukata tamaa kwa wananchi wengi.

Kupitia KNPTM, makanisa yanapanga kuanzisha mitandao ya maombi katika kaunti zote 47 za Kenya, mikutano ya maombi ya kila wiki na mfumo wa maombi hadi ngazi ya familia.

Apostle Peter Kinyanjui alisema harakati hiyo siyo ya kisiasa bali ni “mwito wa kiroho” kwa taifa. Naye Bishop Calisto Odede wa CITAM alisema Wakristo hawapaswi kuogopa uchaguzi wa 2027 bali waendelee kuombea amani, umoja na mabadiliko ya taifa.

Uzinduzi huo umefanyika wakati Kenya ikikabiliwa na ongezeko kubwa la bei ya mafuta na gharama za maisha, huku viongozi wa kanisa wakisisitiza kuwa taifa linahitaji toba, uwajibikaji na maombi ya pamoja kwa ajili ya uponyaji na mabadiliko ya kweli.



  GUNGU_KIGOMA: IBADA YA PENTEKOSTE|SIKU YA JUMAPILI|Mei 24, 2026|Ujumbe: SIKUKUU YA PENTEKOSTENa: Rev.Julius D. Kiyoho•...
27/05/2026

GUNGU_KIGOMA: IBADA YA PENTEKOSTE|SIKU YA JUMAPILI|Mei 24, 2026|
Ujumbe: SIKUKUU YA PENTEKOSTE
Na: Rev.Julius D. Kiyoho
•••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••
Kabla ya PENTEKOSTE, hakukuwa na Kanisa. WANAFUNZI waliiitwa Thenashara, na WANAFUNZI waliiitwa TU mitume.

∆YOELI_Ni Jina la nabii Yoeli(Joel) lenye maana kwamba "Yehova ni Bwana". Huyu anajulikana k**a nabii wa PENTEKOSTE Kwa kuwa alitabiri mengi sana kuhusu ujio wa Roho MTAKATIFU!
Naye k**a nabii, anatabiri;
“Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono;”
— Yoeli 2:28
“tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu.”
— Yoeli 2:29
• Unabii huu Unatumia siku ya PENTEKOSTE! Angalia HAPA Katika Kitabu Cha Matendo ya Mitume 2:1-4; MAANDIKO yanaweka wazi;
¹ Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. ² Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi k**a uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. ³ Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, k**a ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. ⁴ Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, k**a Roho alivyowajalia kutamka.

~ MAANA YA PENTEKOSTE KIBIBLIA
• Katika agano la kale, PENTEKOSTE ilikuwa ni SIKUKUU YA MAVUNO YA NGANO.
Kumbukumbu 16:9-12
⁹ Jihesabie majuma saba; tangu wakati uanzao kutia mundu katika mmea utaanza kuhesabu majuma saba.
¹⁰ Nawe sikukuu ya majuma umfanyie Bwana, Mungu wako, kwa kutoa sadaka ya hiari ya mkono wako, utakayotoa kwa kadiri akubarikiavyo Bwana, Mungu wako..."
Kwa faida ya msomaji wangu, hebu niweke sawa maana za maneno haya;
Sabato = juuma/wiki Moja
Iddi = SIKUKUU

Siku hii ya PENTEKOSTE zamani, ilikuwa Siku ya KUSHEREHEKEA, ilifanyika Katika siku ya hamsini baada ya MAVUNO.
“Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili baada ya Sabato, tangu siku hiyo mliyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa; zitatimia Sabato saba;”
— Walawi 23:15
“hata siku ya pili ya hiyo Sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka ya unga mpya.”
— Walawi 23:16

• MUNGU aliibadilisha SIKUKUU ya MAVUNO na SIKUKUU ya Ujazo wa Roho MTAKATIFU na MAVUNO ya Roho za watu!
“Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?”
— Matendo 2:37
“Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”
— Matendo 2:38-42

JE, KANISA LA PENTEKOSTE LILIZALIWA LILIKUWA LINAITWAJE?
JE, TAG? EAGT? FPCT? ROMAN CATHOLIC AU LINGINE LOLOTE?
Kiukweli, Kanisa la kwanza ni lile lililozaliwa baada ya Ujazo wa Roho Mtakatifu pale Yerusalem. Hata Kanisa la Roma ni matokeo ya Injili ya Petro pale Rumi.
Kumbe, Kanisa la kwanza halitatazamwa Kwa Historia ya madhehebu yetu, hapana! Bali, Kanisa la kwanza ni lile la PENTEKOSTE na hata Sasa Kanisa la kweli ni Kanisa lenye Ujazo na nguvu za Roho Mtakatifu; linalonena Kwa lugha, linalozaa Matunda ya Roho na kuwaleta wengi Kwa Yesu Kwa usahihi Wote! MUNGU Atusaidie kuelewa!

2. UHUSIANO WA UTABIRI WA YOELI NA PENTEKOSTE YA AGANO JIPYA
• MUNGU alimtumia Nabii Yoeli kumfikisha Ujumbe WA PENTEKOSTE Kwa Kanisa la Leo.
Yoeli 2:28-29

• Unabii huo ulitimia siku ya PENTEKOSTE Katika agano JIPYA!
Matendo 2:14-21
¹³ Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.
¹⁴ Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

JINSI YA KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU
1. Kwa NJIA YA KUISHI MAISHA MATAKATIFU
Hebu tafakari! JE, mtu mzinzi, msengenyaji, mchawi, mwizi, mnafiki, nk aweza kujazwa nguvu za MUNGU WA kweli? BIBLIA INASEMAJE?
Matendo 2:37-38
³⁷ Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? ³⁸ Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Kumbe, Kukosekana Kwa UTAKATIFU Ndani ya Kanisa la Leo ni SABABU ya Kukosekana Kwa nguvu za MUNGU Katika IBADA na maisha ya mtu MMOJA MMOJA. Ukame wa KIROHO ni mwingi Kwa SABABU waamini wengi hawajapokea kipawa hiki!

2. KUAMINI AHADI ZA MUNGU KWAKO
“Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.”
— Matendo 2:39

3. KUWA NA SHAUKU NA KIU YA KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU (MHITAJI)
Yohana 7:37-40
³⁷ Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe. ³⁸ Aniaminiye mimi, k**a vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
³⁹ Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.
Mfano:
• Bidii Katika MAOMBI Kila wakati; mifungo ya Siku Tatu, sana, 21, 40, nk.
• Kusoma na kujazwa Neno la Mungu

4. KUDUMU KATIKA MAOMBI YA DHATI
“Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.”
— Luka 11:9 (5-13)
“Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”
— Luka 11:13

Itaendelea...!

Jamani MUNGU AWABARIKI! Awajaalie na Ujazo wa Roho MTAKATIFU Katika Jina la Yesu, Amina!

Media Tanzania|Sisi niHabari Njema|Facebook|YouTube|Instagram|TikTok|WhatsApp+255763946411
•••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••

  GUNGU_KIGOMA: IBADA YA PENTEKOSTE|SIKU YA JUMAPILI|Mei 24, 2026|Ujumbe: SIKUU YA PENTEKOSTENa: Rev.Julius D. Kiyoho•••...
27/05/2026

GUNGU_KIGOMA: IBADA YA PENTEKOSTE|SIKU YA JUMAPILI|Mei 24, 2026|
Ujumbe: SIKUU YA PENTEKOSTE
Na: Rev.Julius D. Kiyoho
•••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••
Kabla ya PENTEKOSTE, hakukuwa na Kanisa. WANAFUNZI waliiitwa Thenashara, na WANAFUNZI waliiitwa TU mitume.

∆YOELI_Ni Jina la nabii Yoeli(Joel) lenye maana kwamba "Yehova ni Bwana". Huyu anajulikana k**a nabii wa PENTEKOSTE Kwa kuwa alitabiri mengi sana kuhusu ujio wa Roho MTAKATIFU!
Naye k**a nabii, anatabiri;
“Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono;”
— Yoeli 2:28
“tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu.”
— Yoeli 2:29
• Unabii huu Unatumia siku ya PENTEKOSTE! Angalia HAPA Katika Kitabu Cha Matendo ya Mitume 2:1-4; MAANDIKO yanaweka wazi;
¹ Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. ² Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi k**a uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. ³ Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, k**a ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. ⁴ Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, k**a Roho alivyowajalia kutamka.

~ MAANA YA PENTEKOSTE KIBIBLIA
• Katika agano la kale, PENTEKOSTE ilikuwa ni SIKUKUU YA MAVUNO YA NGANO.
Kumbukumbu 16:9-12
⁹ Jihesabie majuma saba; tangu wakati uanzao kutia mundu katika mmea utaanza kuhesabu majuma saba.
¹⁰ Nawe sikukuu ya majuma umfanyie Bwana, Mungu wako, kwa kutoa sadaka ya hiari ya mkono wako, utakayotoa kwa kadiri akubarikiavyo Bwana, Mungu wako..."
Kwa faida ya msomaji wangu, hebu niweke sawa maana za maneno haya;
Sabato = juuma/wiki Moja
Iddi = SIKUKUU

Siku hii ya PENTEKOSTE zamani, ilikuwa Siku ya KUSHEREHEKEA, ilifanyika Katika siku ya hamsini baada ya MAVUNO.
“Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili baada ya Sabato, tangu siku hiyo mliyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa; zitatimia Sabato saba;”
— Walawi 23:15
“hata siku ya pili ya hiyo Sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka ya unga mpya.”
— Walawi 23:16

• MUNGU aliibadilisha SIKUKUU ya MAVUNO na SIKUKUU ya Ujazo wa Roho MTAKATIFU na MAVUNO ya Roho za watu!
“Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?”
— Matendo 2:37
“Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”
— Matendo 2:38-42

JE, KANISA LA PENTEKOSTE LILIZALIWA LILIKUWA LINAITWAJE?
JE, TAG? EAGT? FPCT? ROMAN CATHOLIC AU LINGINE LOLOTE?
Kiukweli, Kanisa la kwanza ni lile lililozaliwa baada ya Ujazo wa Roho Mtakatifu pale Yerusalem. Hata Kanisa la Roma ni matokeo ya Injili ya Petro pale Rumi.
Kumbe, Kanisa la kwanza halitatazamwa Kwa Historia ya madhehebu yetu, hapana! Bali, Kanisa la kwanza ni lile la PENTEKOSTE na hata Sasa Kanisa la kweli ni Kanisa lenye Ujazo na nguvu za Roho Mtakatifu; linalonena Kwa lugha, linalozaa Matunda ya Roho na kuwaleta wengi Kwa Yesu Kwa usahihi Wote! MUNGU Atusaidie kuelewa!

2. UHUSIANO WA UTABIRI WA YOELI NA PENTEKOSTE YA AGANO JIPYA
• MUNGU alimtumia Nabii Yoeli kumfikisha Ujumbe WA PENTEKOSTE Kwa Kanisa la Leo.
Yoeli 2:28-29

• Unabii huo ulitimia siku ya PENTEKOSTE Katika agano JIPYA!
Matendo 2:14-21
¹³ Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.
¹⁴ Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

JINSI YA KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU
1. Kwa NJIA YA KUISHI MAISHA MATAKATIFU
Hebu tafakari! JE, mtu mzinzi, msengenyaji, mchawi, mwizi, mnafiki, nk aweza kujazwa nguvu za MUNGU WA kweli? BIBLIA INASEMAJE?
Matendo 2:37-38
³⁷ Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? ³⁸ Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Kumbe, Kukosekana Kwa UTAKATIFU Ndani ya Kanisa la Leo ni SABABU ya Kukosekana Kwa nguvu za MUNGU Katika IBADA na maisha ya mtu MMOJA MMOJA. Ukame wa KIROHO ni mwingi Kwa SABABU waamini wengi hawajapokea kipawa hiki!

2. KUAMINI AHADI ZA MUNGU KWAKO
“Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.”
— Matendo 2:39

3. KUWA NA SHAUKU NA KIU YA KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU (MHITAJI)
Yohana 7:37-40
³⁷ Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe. ³⁸ Aniaminiye mimi, k**a vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
³⁹ Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.
Mfano:
• Bidii Katika MAOMBI Kila wakati; mifungo ya Siku Tatu, sana, 21, 40, nk.
• Kusoma na kujazwa Neno la Mungu

4. KUDUMU KATIKA MAOMBI YA DHATI
“Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.”
— Luka 11:9 (5-13)
“Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”
— Luka 11:13

Itaendelea...!

Jamani MUNGU AWABARIKI! Awajaalie na Ujazo wa Roho MTAKATIFU Katika Jina la Yesu, Amina!

Media Tanzania|Sisi niHabari Njema|Facebook|YouTube|Instagram|TikTok|WhatsApp+255763946411
•••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••

27/05/2026

Kimeumana!!

MAKAMBI YA WAPI HAYA JAMANI?Kwanini Tukambike?1. Makambi Hutukaribisha Zaidi kwa Mungu.Makambi hutupa nafasi ya kuondoka...
27/05/2026

MAKAMBI YA WAPI HAYA JAMANI?
Kwanini Tukambike?
1. Makambi Hutukaribisha Zaidi kwa Mungu.

Makambi hutupa nafasi ya kuondoka kwenye pilikapilika za maisha ili tupate muda wa maombi, kujifunza Neno la Mungu, na kutulia mbele zake.

“Tulieni mkajue ya kuwa mimi ni Mungu.”
— Zaburi 46:10

2. Makambi Hujenga Imani Yetu.

Kupitia mafundisho, mahubiri, na ushuhuda mbalimbali, maisha ya watu wengi hubadilika na kuimarishwa kiroho.
“Imani chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.”
— Warumi 10:17

3. Makambi Hujenga Umoja wa Waamini

Tunapokutana pamoja kambini, tunajifunza kupendana, kusaidiana, na kuombeana k**a familia moja ya Mungu.

“Tazama jinsi ilivyo vema na kupendeza ndugu wakae pamoja kwa umoja.”
— Zaburi 133:1

4. Makambi Hututenganisha kwa Muda na Mambo ya Dunia

Makambi hutusaidia kuweka kando shughuli za kawaida ili kumpa Mungu nafasi ya kwanza katika maisha yetu.
“Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu…”
— Mathayo 6:33

5. Makambi Huleta Mabadiliko ya Maisha

Wengi wameokoka, wameponywa majeraha ya moyo, na kupata nguvu mpya kupitia makambi ya kiroho.
“Mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya.”
— 2 Wakorintho 5:17

KARIBU MAKAMBI YA MWAKA HUU
Usikubali shughuli za maisha zikakunyima baraka za kiroho.
Biashara zitakuwepo, kazi zitakuwepo, lakini nafasi ya kukutana na Mungu ni ya muhimu zaidi.
Mwaka huu njoo:
ujifunze Neno la Mungu
uombe pamoja na wengine
ujengwe kiroho
upokee faraja na matumaini mapya
“Nami nitawapa ninyi moyo mpya…”
— Ezekieli 36:26

Karibu sana kwenye makambi ya mwaka huu.Mungu ana jambo jema kwa ajili yako.
🙏🙏🙏🙏

Address

Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bezaleli Media Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Bezaleli Media Tanzania:

Share