27/05/2026
GUNGU_KIGOMA: IBADA YA PENTEKOSTE|SIKU YA JUMAPILI|Mei 24, 2026|
Ujumbe: SIKUKUU YA PENTEKOSTE
Na: Rev.Julius D. Kiyoho
•••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••
Kabla ya PENTEKOSTE, hakukuwa na Kanisa. WANAFUNZI waliiitwa Thenashara, na WANAFUNZI waliiitwa TU mitume.
∆YOELI_Ni Jina la nabii Yoeli(Joel) lenye maana kwamba "Yehova ni Bwana". Huyu anajulikana k**a nabii wa PENTEKOSTE Kwa kuwa alitabiri mengi sana kuhusu ujio wa Roho MTAKATIFU!
Naye k**a nabii, anatabiri;
“Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono;”
— Yoeli 2:28
“tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu.”
— Yoeli 2:29
• Unabii huu Unatumia siku ya PENTEKOSTE! Angalia HAPA Katika Kitabu Cha Matendo ya Mitume 2:1-4; MAANDIKO yanaweka wazi;
¹ Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. ² Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi k**a uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. ³ Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, k**a ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. ⁴ Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, k**a Roho alivyowajalia kutamka.
~ MAANA YA PENTEKOSTE KIBIBLIA
• Katika agano la kale, PENTEKOSTE ilikuwa ni SIKUKUU YA MAVUNO YA NGANO.
Kumbukumbu 16:9-12
⁹ Jihesabie majuma saba; tangu wakati uanzao kutia mundu katika mmea utaanza kuhesabu majuma saba.
¹⁰ Nawe sikukuu ya majuma umfanyie Bwana, Mungu wako, kwa kutoa sadaka ya hiari ya mkono wako, utakayotoa kwa kadiri akubarikiavyo Bwana, Mungu wako..."
Kwa faida ya msomaji wangu, hebu niweke sawa maana za maneno haya;
Sabato = juuma/wiki Moja
Iddi = SIKUKUU
Siku hii ya PENTEKOSTE zamani, ilikuwa Siku ya KUSHEREHEKEA, ilifanyika Katika siku ya hamsini baada ya MAVUNO.
“Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili baada ya Sabato, tangu siku hiyo mliyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa; zitatimia Sabato saba;”
— Walawi 23:15
“hata siku ya pili ya hiyo Sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka ya unga mpya.”
— Walawi 23:16
• MUNGU aliibadilisha SIKUKUU ya MAVUNO na SIKUKUU ya Ujazo wa Roho MTAKATIFU na MAVUNO ya Roho za watu!
“Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?”
— Matendo 2:37
“Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”
— Matendo 2:38-42
JE, KANISA LA PENTEKOSTE LILIZALIWA LILIKUWA LINAITWAJE?
JE, TAG? EAGT? FPCT? ROMAN CATHOLIC AU LINGINE LOLOTE?
Kiukweli, Kanisa la kwanza ni lile lililozaliwa baada ya Ujazo wa Roho Mtakatifu pale Yerusalem. Hata Kanisa la Roma ni matokeo ya Injili ya Petro pale Rumi.
Kumbe, Kanisa la kwanza halitatazamwa Kwa Historia ya madhehebu yetu, hapana! Bali, Kanisa la kwanza ni lile la PENTEKOSTE na hata Sasa Kanisa la kweli ni Kanisa lenye Ujazo na nguvu za Roho Mtakatifu; linalonena Kwa lugha, linalozaa Matunda ya Roho na kuwaleta wengi Kwa Yesu Kwa usahihi Wote! MUNGU Atusaidie kuelewa!
2. UHUSIANO WA UTABIRI WA YOELI NA PENTEKOSTE YA AGANO JIPYA
• MUNGU alimtumia Nabii Yoeli kumfikisha Ujumbe WA PENTEKOSTE Kwa Kanisa la Leo.
Yoeli 2:28-29
• Unabii huo ulitimia siku ya PENTEKOSTE Katika agano JIPYA!
Matendo 2:14-21
¹³ Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.
¹⁴ Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.
JINSI YA KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU
1. Kwa NJIA YA KUISHI MAISHA MATAKATIFU
Hebu tafakari! JE, mtu mzinzi, msengenyaji, mchawi, mwizi, mnafiki, nk aweza kujazwa nguvu za MUNGU WA kweli? BIBLIA INASEMAJE?
Matendo 2:37-38
³⁷ Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? ³⁸ Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Kumbe, Kukosekana Kwa UTAKATIFU Ndani ya Kanisa la Leo ni SABABU ya Kukosekana Kwa nguvu za MUNGU Katika IBADA na maisha ya mtu MMOJA MMOJA. Ukame wa KIROHO ni mwingi Kwa SABABU waamini wengi hawajapokea kipawa hiki!
2. KUAMINI AHADI ZA MUNGU KWAKO
“Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.”
— Matendo 2:39
3. KUWA NA SHAUKU NA KIU YA KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU (MHITAJI)
Yohana 7:37-40
³⁷ Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe. ³⁸ Aniaminiye mimi, k**a vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
³⁹ Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.
Mfano:
• Bidii Katika MAOMBI Kila wakati; mifungo ya Siku Tatu, sana, 21, 40, nk.
• Kusoma na kujazwa Neno la Mungu
4. KUDUMU KATIKA MAOMBI YA DHATI
“Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.”
— Luka 11:9 (5-13)
“Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”
— Luka 11:13
Itaendelea...!
Jamani MUNGU AWABARIKI! Awajaalie na Ujazo wa Roho MTAKATIFU Katika Jina la Yesu, Amina!
Media Tanzania|Sisi niHabari Njema|Facebook|YouTube|Instagram|TikTok|WhatsApp+255763946411
•••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••