24/11/2024
JUMAPILI ASUBUHI 24.11.2024.
SOMO: UMUHIMU WA KUA NA MCHUNGAJI
UTANGULIZI.
-Wote ambao tunamwamini Mungu tunahitaji kua na mchungaji k**a kiongozi wetu na mtu wa kutuhudumia.
-Sababu ni nyingi na faida ni nyingi za wewe kua na mchungaji.
-Mchungaji hatumtazami kwa muonekani au umri au namna ya jinsi ilivyo bali tunatazama namna ambavyo Mungu amempa hiyo nafasi kusimama kwetu.
-Mchungaji kwako anasimama k**a kiongozi kwako na kwaajili ya kigezo cha kimbingu.
-Mungu huwachagulia watu wachungaji kwa kusudi lake Mungu yeye mwenyewe.
-Wajibu wetu ni kutii na kuitikia kile ambacho Mungu ametupa.
Waefeso 4:11 Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;
-Mungu ndie anayechagua mchungaji licha ya mifumo ambayo binadamu huitumia kujipatia wachungaji.
Yeremia 3:15-16 nami nitawapa ninyi wachungaji wanipendezao moyo wangu, watakaowalisha kwa maarifa na fahamu.
16 Kisha itakuwa, mtakapoongezeka na kuwa wengi katika nchi hiyo, asema Bwana, siku zile hawatasema tena, Sanduku la agano la Bwana; wala halitaingia moyoni; wala hawatalikumbuka, wala hawatalizuru, wala hayatafanyika hayo tena.
-Mungu anapohitaji mtu akue na kuongeza humuwekea kwake mbele mchungaji ilikusudi apandwe kwake na kuona na kujua kile kilichomo ndani yake kwaajili ya kukua na kustawi kwa mtu huyo.
-Ukikataa kua na mchungaji kwenye hilo eneo maana yake umekataa kustawi na kuongezeka na kukua pia.
Yeremia 23:4 Nami nitaweka juu yao wachungaji watakaowalisha; wala hawataona hofu tena, wala kufadhaika, wala hatapotea hata mmoja wao, asema Bwana.
-Mungu ndie anaeweka wachungaji juu yetu na jukumu lao kuu ni kutulisha kwa mafundisho mazuri.
NINI WAJIBU WA MSHIRIKA KWA MCHUNGAJI.
1. Kuwatii.
Waebrania 13:17 Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, k**a watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.
-Biblia inatia msisitizo wa kuwa tii na kuwaheshimu wachungaji wetu aliwaweka mbele yetu na huo ndio moyo wa mshirika kwa Mungu.
Waefeso 6:1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.
2. Kuwaombea.
Wakolosai 4:2 Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani;*
3 mkituombea na sisi pia, kwamba Mungu atufungulie mlango kwa lile neno lake, tuinene siri ya Kristo, ambayo kwa ajili yake nimefungwa
-Ilikusudi wadumu na kubaki kwenye maono na maeneo ambayo Mungu amewapa.
-Ni wajibu wetu k**a washirika kusimama na kuomba kwaajili ya wachungaji wetu.
-Maombi yetu yanaweka hekima kwao na kuisema ile siri ya Mungu kwa ujasiri.
Wakolosai 4:4 ili niidhihirishe, k**a inipasavyo kunena.
-Ni wajibu wetu kuwaombea hawa watu ambao Mungu amewaweka mbele yetu.
3. Kuwaheshimu.
1 Petro 2:17 Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mcheni Mungu. Mpeni heshima mfalme.
-Tuwaheshimu wachungaji wetu hata k**a hatuko karibu nao lazima tuwajibike katika hilo.
-Weka mipaka ya kimahusiano wewe na mchungaji wako mazoea yasipite zaidi.
4. Kuwahudumia.
Wafilipi 4:14-19 Lakini mlifanya vema, mliposhiriki nami katika dhiki yangu.
15 Nanyi pia, ninyi wenyewe mnajua, enyi Wafilipi, ya kuwa katika mwanzo wa Injili, nilipotoka Makedonia, hakuna kanisa lingine lililoshirikiana nami katika habari hii ya kutoa na kupokea, ila ninyi peke yenu.
16 Kwa kuwa hata huko Thesalonike mliniletea msaada kwa mahitaji yangu, wala si mara moja.
17 Si kwamba nakitamani kile kipawa, bali nayatamani mazao yanayozidi kuwa mengi, katika hesabu yenu.
18 Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.
19 Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.
-Shiriki katika matukio yao,changamoto zao au mahitaji yao kwa kuwahudumia vyema.
-Matokeo ya huduma nzuri kwao kwa kugusa mioyo yao huleta furaha na amani mioyoni mwao.
-Sisi k**a vyombo vya Mungu tutumike kuwahudumia wachungaji wetu.
NINI HUTOKEA TUNAPOTAMBUA NAFAZI YA MTUMISHI WA MUNGU KWENYE MAISHA YETU.?
1. Unakua umegusa moyo wa Mungu.
2. Lango la baraka kutoka kwa Mungu.
-Na ndipo wanapobariki watu kwa kutamka na baraka hizo huja.
Hesabu 6:22-24 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
23 Nena na Haruni na wanawe, uwaambie, Hivi ndivyo mtakavyowabarikia wana wa Israeli; mtawaambia;
24 Bwana akubarikie, na kukulinda;
-Mchungaji ni lango la baraka kwako maana yeye ndie anachofungua kile ambacho Mungu amekusudia kifike kwako.
Waebrania 7:7 Wala haikanushiki kabisa kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa.
-Wachungaji ni wakubwa kwetu,wazazi na walezi wetu wao huachilia baraka kwetu sisi wadogo.
3. Kifuniko/ulinzi kwako wa Kiroho.
-Itambue nafasi ya mchungaji kwemye maisha yako kwa kushikisha wao mema na changamoto zako.
4. Mchungaji ni utambulusho wako kwake katika ulimwengu wa Roho.
Matendo ya Mitume 19:14-16
[14]Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, kuhani mkuu, waliofanya hiv
[15]Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani?
[16]Na yule mtu aliyepagawa na pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.
-Kuna namna tu ambavyo kwenye maisha yako unahitaji mchungaji na maisha yako yanakupa dhamani pale tu unapotambua nafasi ya wachungaji kwako.
-Tambua nafasi ya mchungaji kwenye maisha yako na kwa kadri amabavyo Mungu anakupa nafasi na kufanya kwenye maisha yako.
-Nguvu ya mchungaji ni washirika na viongozi wake na sisi tunao wajibu wa kua bora kwa watumishi wa Mungu.
HITIMISHO.
Mawasiliano: 0757754176