Harufu ya Uzima

Harufu ya Uzima Harufu ya Uzima ni huduma yenye lengo ya kuidhihirisha harufu ya kumjua Kristo Yesu kila mahali.

KUHUSU IMANI"Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo." Warumi 10:17Somo la imani bado li...
16/05/2024

KUHUSU IMANI

"Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo." Warumi 10:17

Somo la imani bado linaonekana gumu na tata sana kwa wengi, ingawa ni rahisi. Utata wake umefichwa katika urahisi wake. Wengi husema hawana imani au wana imani ndogo; hata hivyo, unawakuta watu hao hao wanaamini mambo mengi sana isipokuwa Neno la Mungu.

Leo, nimeongozwa kuzungumzia suala linalohusu imani.

Baada ya wengi kusikia wahubiri wakizungumzia imani na umuhimu wake; walihisi hitaji la imani, na hivyo walitaka kuwa nayo. Walitaka kuitengeneza imani ndani yao, na wengine kuiongeza. Lakini, wengi hawafahamu wafanye nini ili wawe na imani, hivyo hitaji lao la 'imani kubwa' limewafanya kupoteza hata imani ile ndogo waliyokuwa nayo.

Fahamu hili kuhusu imani. Hakuna imani inayojiumba yenyewe. Imani yote hutolewa na hupokelewa; rahisi namna hiyo. Neno linapopokelewa, ndani yake imani inapokelewa. Neno la madaktari kwa mgonjwa hubeba imani katika dawa; mwongozo wa watengenezaji gari hubeba imani katika gari yao. Unaweza hata kumwamini rubani na maisha yako kwa kumwona tu akiwa amevalia sare. Vipi kuhusu Neno la muumba wako?

Mioyo yetu ni udongo mzuri ya kupandia imani, lakini tunachagua mbegu tunazoruhusu kukua k**a imani ndani yetu. Wengine wamewaamini wazazi wao kuwapatia msaada, zaidi ya wanavyoweza kumwamini Mungu; wengine wana imani na ripoti ya daktari na maagizo yake, kuliko Neno linavyosema (ripoti ya Mungu).

Changamoto ya mtu yeyote anayehangaika na imani ni kwamba, bado hajamjua Mungu katika kweli, wala Neno lake.

Usihangaike kujitengenezea imani yako, pokea tu neno la Mungu zaidi; ndani yake ni imani. Imani imefungwa ndani ya Neno. Kadiri unavyopokea Neno, ndivyo imani inavyoongezeka ndani yako. Baada ya kuwa na imani yote unayohitaji, ifanyie kazi ili kuifanya iwe na imara zaidi.

- Harufu ya Uzima

Na D. K. Davis
0713816586

JILINDE KATIKA UPENDO"Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya u...
28/02/2024

JILINDE KATIKA UPENDO

"Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya; tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane k**a na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi."
Waefeso 4:31‭-‬32

Katika kitabu cha Mithali 4:23 tunapata maelekezo ya muhimu kuhusu uzima na ustawi wetu: "Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima." Moyo wako haukukusudiwa kubeba vitu visivyofaa k**a uchungu, ghadhabu, hasira, kelele, matukano, dharau, ubaya, au kutokusamehe.

Uchunguzi wa kisayansi umegundua kwamba afya ya mtu huharibiwa kutokana na mtu kubeba moyoni, vitu visivyofaa (vimetajwa hapo juu). Na hivyo ndivyo Biblia inafundisha.

Bwana Yesu akitoa mfano wa mtu asiyesamehe, alisema, "Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji..." (Mathayo 18:34‭). Kuna mateso kwa mtu asiyesamehe.

Chuki na uchungu vinakuathiri wewe zaidi ya wale unaowachukia. Hii ndiyo sababu lazima uamue kuziacha kumbukumbu mbaya, na uchague kuishi kwa upendo.

Kuna mwenendo wa maisha kwa ajili ya watoto wa Mungu; ni mwenendo tofauti na wanadamu wengine. Biblia inasema, "Hivyo mfuateni Mungu, k**a watoto wanaopendwa; mkaenende katika upendo, k**a Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato" (Waefeso 5:1‭-‬2). Tunamfuata Mungu kwa kuenenda katika upendo.

Upendo ni mwenendo wa maisha ya kila mtoto wa Mungu. Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo (1 Yohana 4:8). Ondoa uchafu wote moyoni mwako, kwa kuamua kutembea katika upendo. Daima tazama na tafuta mambo mazuri kwa watu; watazame k**a Mungu anayowatazama, "Ndipo nuru yako itakapopambazuka k**a asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako itakutangulia; utukufu wa BWANA utakufuata nyuma ukulinde" (Isaya 58:8).

Na D. K. Davis
WhatsApp: 0713816586
Email: [email protected]
Telegram: https://t.me/darasa_la_uanafunzi

Kitabu pichani kinapatikana kwa Tsh. 10,000/= tu

NIDHAMU ZA KIROHO"Mimi, BWANA, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha ma...
06/02/2024

NIDHAMU ZA KIROHO

"Mimi, BWANA, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake."
(Yeremia 17:10)

Mtu mmoja aliwahi kunukuliwa akisema, "Mafanikio ni pale fursa inayotarajiwa inapokutana na maandalizi". Fikiria kuhusu hilo, lina ukweli kiasi gani. Je, haifanani na kile kilichoandikwa katika Mhubiri 9:11, kwamba "...wakati na bahati huwapata wote"? Wanaofanikiwa ni wale ambao huwa tayari pale wakati na fursa zinapokuja kwao.

Udhihirisho wa matokeo ya KiMungu kwenye eneo lolote hapa duniani, ni matokeo ya yale ambayo Mungu ametufunulia mioyoni mwetu kwa Roho wake na nidhamu tunayopaswa kuwa nayo ili kuleta katika udhihirisho kile kilichofunuliwa.

Kushindwa kutii kanuni hii, kunaleta simanzi, lawama na kukata tamaa katika kutembea kwetu na Mungu. Lakini, mtembeo wetu na Mungu haupaswi kuwa wa kukatisha tamaa au kushindwa; unapaswa kuwa wa furaha na mafanikio daima.

Katika mstari wetu wa ufunguzi, Biblia inamnukuu Mungu akisema, "Mimi, BWANA, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake." Mungu hampi mtu kitu, kwa sababu tu ana moyo mzuri, bali njia zake (nidhamu yake), na matunda ya matendo yake yakimpendeza Bwana. Moyo mzuri jumlisha uwezo vitaamua utapokea kwa kiwango gani kutoka kwa Bwana.

Baada ya Mungu kuuangalia moyo wako mzuri, huwa anachunguza utayari na umahiri wa kiuno chako. Unaweza kuhimili mangapi? Unaweza kubeba mambo mazito kwa kiwango gani? Umejiandaa kwa kiasi gani na jambo hilo unaloliomba?

Wakati ukiendelea kuuweka safi moyo wako ili umwone Bwana, endelea kuandaa kiuno chako ili Bwana anapokuja aweze kukupa alichonacho kwa ajili yako.

- Harufu ya Uzima Vol 5

Na D. K. Davis
WhatsApp: 0713816586
Email: [email protected]
Telegram: https://t.me/darasa_la_uanafunzi
Website: www.harufuyauzima.org

It's my birthday!‭‭Kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu si bure, bali ninazidi sana kufa...
26/11/2023

It's my birthday!

‭‭Kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu si bure, bali ninazidi sana kufanya; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.

Namshukuru Mungu kwa neema yake!

Jana ilikuwa na utukufu, leo ina utukufu na kesho ina utukufu mwingi zaidi.

Happy Birthday kwako D. K. Davis (Harufu ya Uzima)

UNAWAJIBIKA KWA MAISHA YAKO"Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, ...
16/11/2023

UNAWAJIBIKA KWA MAISHA YAKO

"Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako"
Kumbukumbu la Torati 30:19

Mwanadamu ni kiumbe wa kipekee sana, ana uhuru wa kufanya maamuzi; ana mapenzi yake mwenyewe, na huwajibika kwa maamuzi yake. Mungu halazimishi ajenda zake kwa mwanadamu, ametupa nafasi ya kutumia utashi wetu kufanya maamuzi yaliyo bora kwetu.

Maisha yamejaa chaguzi nyingi. Kila siku ya maisha yako ni siku ya kufanya uchaguzi, na kila chaguo unalofanya huamua mwelekeo wa maisha yako. Machaguo yako huathiri hatima yako. Chaguo moja baya linaweza kuharibu maisha yako, na chaguo moja zuri linaweza kukuweka kwenye kiwango cha juu zaidi maishani.

Mahali ulipo sasa katika maisha ni matokeo ya chaguzi ulizofanya huko nyuma, na pale unapotaka kwenda katika maisha bado iko mikononi mwako; unaweza kuchagua mahali ambapo utakuwa siku zijazo.

Kila siku, Mungu amekuwekea nafasi za kufanya chaguzi. Mbele yako kuna mauti na uzima, baraka na laana; zaidi Mungu anakupa ushauri wa kuchagua uzima. Wako wengine wamechagua mauti kwa kutojua na hivyo kuua mambo ambayo yalipaswa kuwanufaisha.

Baadhi ya huduma, ndoa, biashara, taaluma na elimu zimeathiriwa sana na chaguzi mbaya ambazo watu wamefanya.

Shukrani kwa Mungu, hakutuacha bila msaada katika chaguzi zetu. Alitupa Neno lake na Roho Mtakatifu. Neno la Mungu hutoa mwongozo bora zaidi kwa uchaguzi wetu, na Roho Mtakatifu hutuongoza katika chaguzi zetu.

Thibitisha maamuzi yako kwa Neno la Mungu na kwa Roho Mtakatifu anayeishi na kufanya kazi ndani yako. Kila siku jaza Neno la Mungu moyoni mwako, na uimarishe ushirika wako na Roho Mtakatifu, ili uweze kuishi maisha ya ushindi usio na kikomo.

- Harufu ya Uzima Vol 4

Na D. K. Davis
WhatsApp: 0713816586
Email: [email protected]
Telegram: https://t.me/darasa_la_uanafunzi

NIDHAMU NDIYO NJIA YA KWENDA JUU"Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu v...
13/11/2023

NIDHAMU NDIYO NJIA YA KWENDA JUU

"Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo."
1 Wakorintho 10:23

Mwanadamu ni wakala huru wa maamuzi, anao uhuru wa kuchagua jinsi anavyoishi maisha yake. Pamoja na kuwa Mungu ameumba vitu vyote, hamlazimishi mwanadamu ‘kuwa’ au kufanya yale Anataka; amempa uhuru wa kuchagua. Na Kila uamuzi unaofanywa una matokeo chanya au hasi.

Tunaishi katika ulimwengu wa kanuni mbalimbali zilizowekwa na Mungu. Kanuni ambazo haziwezi kuvunjwa, lakini mtu anaweza kujivunja dhidi ya hizo. Mfano, kupanda na kuvuna ni kanuni ya muda wote, wakati wote tuwapo ulimwenguni.

Nidhamu ni utiifu wa sheria na kanuni zilizopo ili kupata matokeo. Kizazi chetu kinajua kidogo sana kuhusu nidhamu. Wengi hutaka kufanya kilicho rahisi kwao, ama kile tu wanachokubaliana nacho. Kwa kuwa nidhamu ina gharama na inahitaji mtu kujituma kikamilifu, wengi huamua kuishi kwa urahisi na kuepuka gharama hiyo.

Ili mtu uweze kuishi maisha ya juu tu; maisha ya mafanikio na ustawi, ni lazima uishi kwa nidhamu. Nidhamu ni njia ya kwenda juu. Mtu asiye na nidhamu hawezi kuishi maisha ya juu, na akijikuta yuko juu, muda si mrefu atashuka (ataanguka).

Kuwa na nidhamu ya kuomba, kusoma Neno, kufunga, kuhudhuria ibada, utoaji wa sadaka, fedha, kutafakari, kuzungumza, na mambo yote ya utauwa.

Jiweke chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu na kwa maongozi ya Neno kila siku. Jenga nidhamu ya kujifunza Neno na kuliishi Neno. Neno la Mungu ni kwa faida yetu; litii na kulifuata na maisha yako yatakua ya juu siku zote. Haleluya!

- Harufu ya Uzima Vol 2

Na D. K. Davis
0713816586
[email protected]

NGUVU YA MANENO"Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao wapendao watakula matunda yake."Mithali 18:21Maneno ya...
08/11/2023

NGUVU YA MANENO

"Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao wapendao watakula matunda yake."
Mithali 18:21

Maneno yana nguvu, yanaweza kuleta mauti au uzima katika hali yoyote ya maisha. Maneno yanaweza kuanzisha jambo au kulimaliza. Mungu ameweka nguvu kubwa katika ndimi zetu; na tunamshukuru kwa kuwa ametujulisha, ili tusiutumie dhidi yetu wenyewe.

Kila siku ya maisha yako, unakula matunda ya midomo yako, iwe unatambua au la. Biblia inasema hivyo. Midomo yako ina matunda: kifo au uzima, mafanikio au kushindwa, furaha au huzuni, afya au ugonjwa, utajiri au umaskini. Uchaguzi ni wako.

Maneno ni nguvu katika ulimwengu wa kiroho, yanavuta kile unachozungumza. Biblia inatangaza kwamba, kila kitu kilifanyika kwa Neno (Yohana 1:1-3); kwa hiyo kila kitu kinaitikia maneno yatokayo kinywani mwako.

Kuhusu Maneno, Bwana wetu Yesu alisema: “Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa” (Mathayo 12:37).Kila wakati unapofungua kinywa chako kuzungumza, unatayarisha matokeo ya kile unachozungumza; iwe ni haki au hukumu, kifo au uzima.

Kuwa mwangalifu jinsi unavyozungumza. Jifunze kunena sawasawa na Neno la Mungu; jifunze kutoka kwa Bwana Yesu, hakuwahi kukosea katika usemi wake mahali popote. Zungumza kile unachotaka kuona, kile ambacho ni sawa na Neno la Mungu.

Yakobo anasema, wewe ni mkamilifu ikiwa haukosei katika maneno. "Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote k**a kwa lijamu" (Yakobo 3:2).

- Harufu ya Uzima Vol 3

Na D. K. Davis
WhatsApp: 0713816586
Email: [email protected]
Telegram: https://t.me/darasa_la_uanafunzi

MAISHA YANA CHANZO‭‭"Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka ...
31/10/2023

MAISHA YANA CHANZO
‭‭
"Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo."
Mhubiri 12:1

Moja ya ukweli wa msingi, ambao kila mtu anapaswa kujua ni kwamba: Maisha yana chanzo, na chanzo hicho ni Mungu. Mwanadamu anapenda kuwa msimamizi wa kila kitu, na wakati mwingine anajidanganywa kufikiria kuwa ndiye anayeongoza kila kitu. Lakini, hii si kweli. Mwanadamu ni kiumbe aliyeumbwa, na Mungu ndiye muumbaji. Mungu ndiye mtawala, ana mpango na kusudi kwa uumbaji wake; na ili uumbaji ufanikiwe, ni lazima unyenyekee kwa muumbaji, Mungu.

Ukipata ufahamu huu ndani yako, unakufanya usiwe na wasiwasi wa kesho kwa sababu unajua Mungu ndiye mtawala. Biblia inasema, "Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo" (Waefeso 2:10). Wewe ni kazi Yake, kazi yake ya sanaa; Ana mpango kwa ajili yako; Alitayarisha njia ambayo unapaswa kuifuata. Mungu anawajibika kwa maisha yako.

Baada ya kuzaliwa mara ya pili katika Kristo, Mungu anachukua jukumu la maisha yako. Unachohitaji kufanya ni kujisalimisha kwa mpango na kusudi lake. Hapo ndipo utaishi katika utimilifu wa maisha, furaha isiyoelezeka, na utoshelevu kamili.

Biblia ni mwongozo wa maisha yako. Inatoa maagizo juu ya jinsi unapaswa kuishi, na matokeo gani yanayotarajiwa kutoka kwako. Hii ndiyo sababu ya kwa nini unapaswa kujifunza Neno la Mungu. Ni mwongozo wa maisha yako.

Lakini, kinachonigusa zaidi ni kile ambacho Mungu anafanya ndani yetu. "Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema" (Wafilipi 2:13). Mungu alituumba kwa kusudi lake, na bado anafanya kazi ndani yetu ili kulitimiza. Hii ni ajabu. Mungu amedhamiria kutimiza kusudi lake kupitia wewe; mruhusu afanye hivyo kwa Roho wake anayekaa ndani yako.

- Harufu ya Uzima Vol 3

Na D. K. Davis
WhatsApp: 0713816586
Email: [email protected]
Telegram: https://t.me/darasa_la_uanafunzi

TAKASWA KWA UPENDO "Na hii ndiyo dua yangu, kwamba pendo lenu lizidi kuwa jingi sana, katika hekima na ufahamu wote; mpa...
30/10/2023

TAKASWA KWA UPENDO

"Na hii ndiyo dua yangu, kwamba pendo lenu lizidi kuwa jingi sana, katika hekima na ufahamu wote; mpate kuyakubali yaliyo mema; ili mpate kuwa na mioyo safi, bila kosa, mpaka siku ya Kristo; hali mmejazwa matunda ya haki, kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa ya Mungu." (Wafilipi 1:9-11)

Kifungu hiki katika Wafilipi 1:9-11 kinaleta msingi wa ufahamu wa mwenendo wa maisha ya Kikristo. Ni maombi ya Mtume Paulo kwa kanisa la Wafilipi, akiongozwa na Roho Mtakatifu kuyaandika.

Roho Mtakatifu anataka tujue hili: ili kutambua na kuyakubali yaliyo mema; kuwa na mioyo safi, bila kosa, mpaka siku ya Kristo; hali tumejazwa matunda ya haki, ni muhimu na lazima pendo letu kwa Bwana lizidi kuwa jingi sana katika hekima na ufahamu wote.

Wakolosai 3:14 inasema, "Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu." Upendo ndio kifungo cha ukamilifu. Mungu alitununua kwa upendo wake; anahusiana nasi katika upendo; tumeingizwa kwenye ufalme wa mwana wa pendo lake.

Katika agano la kale, Mungu alihusiana na mwanadamu kwa sheria, lakini katika agano jipya kwa upendo wake. Sheria haikumsaidia mwanadamu kushinda dhambi; bali upendo wake ndio njia ya kumtoa mtu dhambini. Utawala wa dhambi umevunjwa baada ya sisi kuwa chini ya neema, kielelezo cha upendo wake. Imeandikwa, "Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa sababu hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema" (Warumi 6:14).

Unapozidi KUKUA katika UFAHAMU WA UPENDO WAKE kwako, unapokea uwezo wa kuishi maisha ya haki na utakatifu wa kweli. Bwana Yesu alisema: "Mkinipenda, mtazishika amri zangu (Yohana 14:15). Unaanza kumpenda kabla ya kuzishika amri; ndipo upendo wake wakubidiisha (wakutia nguvu) kuzishika amri zake.

HAKUNA MTU aliye na ufunuo sahihi wa upendo wa Mungu, unaoonyeshwa kupitia kazi ya Yesu Kristo aliye chini ya utawala wa dhambi. Upendo Wake unakuweka huru mbali na dhambi.

NAKUOMBEA,
Pendo lako kwa Bwana lizidi kuwa jingi sana, katika hekima na ufahamu wote; upate kuyakubali yaliyo mema; ili upate kuwa na mioyo safi, bila kosa, mpaka siku ya Kristo; hali umejazwa matunda ya haki, kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa ya Mungu. Amen.
(Wafilipi 1:9-11)

- Harufu ya Uzima Vol 3

Na D. K. Davis
WhatsApp: 0713816586
Email: [email protected]
Telegram: https://t.me/darasa_la_uanafunzi

26/10/2023

UPENDO WA MUNGU

"Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi."
Warumi 5:8

Moja ya mambo ya msingi ambayo mtoto wa Mungu anapaswa kufahamu ni upendo wa Mungu, na huu sio tu kwa kuusoma katika maandiko bali kwa kuwa na uzoefu nao. Ni jambo moja kujua Mungu anakupenda kwa sababu unaambiwa na mhubiri, lakini jambo la pili ni kujionea upendo wa Mungu ukidhihirika kwako.

Kila mtoto wa Mungu anapaswa kupata uzoefu wa upendo wa Mungu; lazima uwe na hakika ya kuwa Mungu anakupenda, kwa sababu imani yako na tumaini lako vinajengwa juu ya msingi wa upendo wake. Imani yako ni imara unapofahamu upendo wake. 1 Yohana 4:16 inasema, "Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake."

Katika mstari wa 18, Roho anaendelea kusema, "Katika pendo hamna hofu; lakini pendo lililo kamili huitupa hofu, kwa maana hofu ina adhabu; na mwenye hofu hakukamilishwa katika pendo".

Ufunuo kamili wa upendo wa Mungu katika roho yako huondoa hofu, mashaka na wasiwasi. Unakufanya uwe huru; unakuwa mtoto anayemwamini kabisa Baba yake. Unakuwa na ujasiri, si kwa uwezo wako mwenyewe bali uwezo wa Mungu ndani yako.

Mungu anakupenda, na ameonyesha upendo wake kupitia Neno lake. Soma Neno lake kwa kuwa ni ujumbe wake wa upendo kwako, na umruhusu Roho Mtakatifu audhihirishe upendo wa Mungu moyoni mwako; na uhusiano wako na baba utakwenda viwango vingine vikuu.

- Harufu ya Uzima Vol 3

Na D. K. Davis
WhatsApp: 0713816586
Email: [email protected]
Telegram: https://t.me/darasa_la_uanafunzi

MAOMBI NI MAHALI PA KUPOKEA"Ombeni, nanyi mtapewa....kwa maana kila aombaye hupokea..." (Mathayo 7:7-8).Mstari wetu wa u...
23/10/2023

MAOMBI NI MAHALI PA KUPOKEA

"Ombeni, nanyi mtapewa....kwa maana kila aombaye hupokea..." (Mathayo 7:7-8).

Mstari wetu wa ufunguzi ni mwaliko wa Mungu kwetu. Anatuita tuombe, ili atupatie yote tunayoomba. Maombi ni wazo la Mungu; Anatuita tuombe kwa sababu ana kitu cha kutoa, na anakusudia kukitoa kwa njia ya maombi.

Wengi huenda mbele za Mungu bila uhakika wa kupata majibu. Lakini, fikiria hili: Je, Mungu angekualika uombe ikiwa hayuko tayari kukupa kile unachoomba?

Ukisoma maandiko utagundua kuwa Mungu anataka kukupa zaidi ya kile unachoweza kuomba, kuwaza au kufikiria. Waefeso 3:20 inasema, "Basi atukuzwe yeye aweza kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu".

Unapokuwa na ufahamu huu katika roho yako, maombi yanakuwa mahali pa kupumzika; imani yako huinuka na kilio chako kinaisha.

Mtazamo wako katika maombi lazima ubadilike. Usifikiri maombi ni fursa tu ya kuomba na kusubiri majibu ikiwa ombi lako limekubaliwa. Fikiri k**a mahali pa kupokea, kwa sababu Mungu unayemwomba, anajua hitaji lako na yuko tayari kutoa kile unachotaka.

Bwana wetu Yesu alizungumza juu ya muundo huu rahisi, Alisema, "Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote mtakayoyaomba mkisali, amini ya kwamba mmeyapokea, nayo yatakuwa yenu." ( Marko 11:24 NEN). Mara tu, baada ya kufanya ombi lako, pokea majibu yako kwa shukrani na sifa, na yatakuwa yako.

Ni rahisi sana, lakini ni vigumu kwa mtu ambaye hajajizoeza katika imani.

Maombi ni mahali ambapo Mungu hutoa, na sisi tunapokea.

- Harufu ya Uzima Vol 3

Na D. K. Davis
WhatsApp: 0713816586
Email: [email protected]
Telegram: https://t.me/darasa_la_uanafunzi
Website: www.harufuyauzima.org

NENO NI LA SASA"Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena...
16/10/2023

NENO NI LA SASA

"Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo" (Waebrania 4:12).

Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu. Neno ni kweli ya sasa; hubeba uzima na hudumu kuwa kweli milele.

Duniani kuna historia nyingi zilizokufa kwenye rekodi, ambazo zinaelezea mambo yaliyotokea au yaliyosemwa zamani, bila uhai wala uwezo wa kiutendaji katika maisha ya sasa. Lakini, Neno la Mungu si historia mfu au jambo la zamani. Neno la Mungu ni la sasa, liko hai na lenye nguvu k**a lilivyokuwa lilipozungumzwa miaka mingi iliyopita.

Mungu wetu ni wa milele, na Neno lake ni la milele; k**a vile Yeye asivofungwa na wakati, neno Lake haliwezi kufungwa na wakati, kwa sababu Yeye ni mmoja na Neno lake.

Mstari wetu wa ufunguzi unasema, "Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu..." Hii ndiyo tabia ya Neno la Mungu: uhai na nguvu. Neno ni hai na limejaa nguvu, na linafanya kazi sasa k**a lilivyonenwa.

Mungu aliposema, "..atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini..." (Kumb 28:13). Neno hilo bado liko hai sasa na limebeba uwezo kamili wa kulidhihirisha ikiwa unaliamini na kulichukulia k**a lako.

Maneno ya Yesu yaliyoandikwa katika Biblia ni hai, na yana mamlaka na nguvu sasa, sawa na alipoyanena.

Tunaponya wagonjwa, tunatoa pepo, tunafufua wafu na kutakasa wenye ukoma, kwa sababu alitupa neno lake: "Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure" (Mathayo 10:8). Maagizo haya ni hai na yenye nguvu k**a Yesu anayazungumza sasa.

Neno la Mungu ni jipya, haliwezi kuzeeka au kuacha kuwa halali.

Amini Neno, lichukue k**a ukweli wako wa sasa. Liruhusu likuhudumie wewe binafsi, kwa sababu lilitumwa kwako na kwa ajili yako.

Liamini Neno la Mungu zaidi kuliko ukweli wowote wa kisayansi au nadharia zilizothibitishwa za kidunia, kwa sababu NENO LA MUNGU NI KWELI. Hakuna ukweli mwingine wowote juu ya Neno.

- Harufu ya Uzima Vol 3

Na D. K. Davis
WhatsApp: 0713816586
Email: [email protected]
Telegram: https://t.me/darasa_la_uanafunzi
Website: www.harufuyauzima.org

Address

Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Harufu ya Uzima posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share