26/03/2026
KINGDOM PRIORITY MISSION CHURCH
SEMINA YA NENO LA MUNGU MTANDAONI
MACHI 24-27, 2026 (JUMANNE - IJUMAA)
SOMO: THE MIGHT OF GOD IS UNQUESTIONABLE / UWEZA WA MUNGU SI WA KUULIZA
MNENAJI: DR. MWAMTOBE AAM - ASKOFU MKUU WA KPMC NA MCHUNGAJI KIONGOZI WA KANISA LA KPMC DODOMA
SIKU YA PILI - JUMATANO MACHI 25, 2026
Watumishi wa Mungu, ninawasalimuni nyote katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Bwana na mwokozi wa maisha yetu. Bwana Yesu Asifiwe sana! Hallelujah!
Ninamshukuru sana Mungu tena kwa neema hii kwamba ametupa siku ya pili ili tuweze kuendelea na semina yetu ambayo Tulianza Jana. Semina yetu ina ujumbe THE MIGHT OF GOD IS UNQUESTIONABLE ambao niliutolea maana yake siku ya Jana. Pamoja na hiyo, pia niliweza kukueleza andiko moja la msingi la semina yetu ambalo ni Luka 1:37.
Siku ya leo tena, siku ya pili niko hapa kwa ajili ya mwendelezo wa semina yetu na leo tutaanza kuangalia kwa kina lile andiko la msingi la pili la semina yetu ambalo ni
“Akasema, Yasiyowezekana kwa wanadamu yawezekana kwa Mungu.”
— Luka 18:27 (Biblia Takatifu)
Karibu sana tujifunze pamoja, karibu sana tule na kunywa pamoja mezani pa Bwana Yesu.
Wanadamu tuna mahangaiko mengi sana, tumejaliwa ufahamu mkubwa sana wa kufanya mambo yatokee hapa duniani. Mungu aliumba vyote alivyoumba pasipo kutumia kitu chochote ambayo kwa Kigiriki inaitwa "creatio ex nihilo" yaani creating something from nothing.
Sisi wanadamu tunaumba vitu kutoka kwenye vitu ambavyo vilikuwepo yaani "nihilo" yenye maana ya creating something from something that exist. Mfano, Daktari anapotengeneza dawa kutumia miti anaumba dawa ambayo haikuwepo lakini hutumia miti ambayo hakuiumba yeye. Huu ni uwezo ambao wanadamu tumepewa.
Si wote tunafanana, kila mtu anao uwezo fulani wa kufanya mambo yatokee (ubunifu na IQ). Wengine wana uwezo mkubwa sana huku wengine wakiwa na uwezo mdogo kabisa.
Lakini pia maeneo ya ubobevu hutofautiana, anayeweza kutengeneza ndege siyo lazima aweze kujenga nyumba, siyo lazima, aweze kutengeneza simu au saa au magari nk. Kwa hiyo kila mtu ana maeneo yake fulani, Daktari mmoja bingwa wa kufanya upasuaji ofisini anaogopa kuchinja kuku nyumbani kwake. Akipanga kula kuku lazima atafute mtu wa kumsaidia kuchinja.
Pamoja na ubunifu mkubwa, mahangaiko mengi sana, bado Kuna mambo hayawezekani kabisa kwa upeo wa Mwanadamu. Ndiyo, uwezo wa Mwanadamu kufanya mambo yatokee una ukomo wake. Mwanadamu hata akihangaika awezavyo Kuna mambo hawezi kabisa kuyafanya yatokee.
Miaka mitatu iliyopita nilikutana na mama mmoja ambaye wakati anajifingua alipata kifafa cha mimba. Kwa bahati mbaya mtoto wake alifariki muda mfupi baada ya kujifungua, na kile kile kifafa kulikuwa kinamtia ukichaa yule mama baada ya muda fulani Kaa siku 2 mpaka 3 hivi.
Madaktari walipambana walivyoweza lakini waliishi kusema ile hali hawailelewi sawasawa na namna pekee waliyokuwa wamebakia nayo ni kumpa vidonge vya ku*ima (siyo kuondoa) ile hali ya ukichaa ambapo utaratibu ulikuwa kwamba atume vidonge 2x3 kila siku kwa maisha yake yote.
Ukiambiwa hivi Unaelewa kwamba maisha yako yote yatakuwa ni maisha ya vidonge tu mpaka pale utakapokufa. Mwanzoni Kuna wakati alikuwa anajisahau, ile hali ya ukichaa ilikuwa ikimpata hata k**a amejisahau awamu moja lakini baadaye alizoea kunywa hizo dawa kila siku.
Mimi nilipata neema ya kukutana naye nilipoalikwa kuendesha semina ya siku tano kanisani kwao. Mungu akikusudia jambo huwa hakuna wa kuzuia kabisa. Nilipofundisha siku ya kwanza, wakati wa MAOMBEZI alipita nikamwombea na nilimuuliza shida yake.
Aliniambia, nikamwombea tena na nikamwambia uaitumie dawa hizi tena kuanzia sasa. Maswali ya imani lazima yawepo, itakuwaje? Nikamwambia fanya zoezi la imani, jioni ya leo uaitumie hizi dawa. Nikamwombea nikamwacha.
Kesho yake kwenye semina akaja na ikabidi sasa kabla sijafundisha nimuulize. Alinijulisha kuwa mpaka hiyo kesho yake hajatumia zile dawa na hajaona shida yoyote kabisa. Tukamshukuru Mungu na tukaendelea na semina.
Mpaka tunamaliza ile semina alikuwa hajatumia zile dawa kabisa na hakukuwa na shida yoyote na alikuwa amezitupa zote zilizokuwa zimebaki maana alikuwa anaenda hospital kununua kidogo kidogo ili kuepuka kuharibika.
Na yeye alikuwa ametendewa muujiza wake kwa namna hiyo. Sasa unaona wanadamu ambao tunaweza kuwategemea, ambao wao ndiyo taaluma yao, wametumia miaka mingi kusomea mambo, hayo, ndiyo kazi yako ya kila siku hawakuwa na majibu. Ndiyo ukomo wao ulikuwa umefikia hapo, lakini Mungu aliweza kufanya ndani ya muda mfupi na kwa njia rahisi namna hii. Hii ndiyo
“Akasema, Yasiyowezekana kwa wanadamu yawezekana kwa Mungu.”
— Luka 18:27 (Biblia Takatifu)
KWA NINI YESU ALISEMA HIVI
Kijana mmoja tajiri alimwendea Yesu na kumuuliza swali, nifanye nini ili niweze kuurithi ufalme wa mbinguni? Bila shaka lilikuwa swali zuri sana ila sote tunafahamu kwamba Yesu hakujishughulisha sana na maneno ya mtu bali moyo wake. Hivyo ndivyo Mungu afanyavyo hata sasa, maneno si jambo analojishughulisha nalo bali moyo wa mtu (Nia).
Akamjibu, wazijua amri? Kijana alijibu nimezishika tangu utoto wangu k**a tu ambavyo wengi tukiwa wadogo tulifundishwa amri 10 za Mungu. Mimi kule Sunday school niliwahi kupata Tsh 500 kwa kutaja amri zote kwa mpangilio mpaka kaka yangu a
Tsh 500 kwa wakati huo ilikuwa hela kubwa maana kulikuwa hadi na bidhaa za Tsh 5, kwa hiyo mwanafunzi ukiwa na 500 unampa mama akiwekee na kila siku a nakupa labda Tsh 20 au 30 kwa ajili ya maandazi shuleni.
Kushika amri tangu utoto halikuwa jambo la muhimu kwa Yesu bali la muhimu lilikuwa ni application ya zile amri. Amri zote zimefungwa na kukamilishwa na upendo kwa Mungu na kwa watu. Tajiri akaambiwa auze mali zake zote awape maskini halafu ndiyo amfuate Yesu.
Luka 18:23-25 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
²³ Lakini aliposikia hayo alihuzunika sana, maana alikuwa na mali nyingi.
²⁴ Yesu alipoona vile alisema, Kwa shida gani wenye mali watauingia ufalme wa Mungu!
²⁵ Kwa maana ni vyepesi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
Waliosikia maneno hayo ya Yesu walishangaa mpaka wakauliza k**a mambo yako hivi ni nani basi
Ni nani basi awezaye kuokoka? Kwa nini? Kwa sababu waliona kwamba jambo la ngamia kupenya katika tundu la sindano ni jambo ambalo haliwezekani kabisa.
Wewe sindano unaijua na lile tundu lake unalijua. Ngamia unamjua hata k**a siyo kumwona ana kwa ana utakuwa umemwona kwenye picha au kwenyw video. Je ngamia aweza kupenya katika tundu la sindano? Unaweza kunijibu.
Kuna watu wamejaribu kutafiti ukweli huu wa ngamia kupenya katika tundu la sindano na kusema
"Yerusalemu kulikuwa na lango dogo la dharula ambalo ngamia walilazimishwa kupita hapo na walipita kwa taabu na kwa maumivu makubwa kwa sababu lilikuwa ni lango dogo, na lilitumika wakati wa dharula tu".
Inawezekana kwamba ni kweli kule Yerusalemu kulikuwa na geti dogo la dharula, jambo ambalo obvious ni kweli maana mji mkubwa na ngome kubwa haiwezi kukosa mlango wa dharula. Na kwa sababu ni mlango wa dharula lazima utakuwa mdogo.
Lakini katika Theolojia hatusomi jambo la namna hii kwamba ndiyo Yesu alimaanisha, tunasoma kabisa kwamba Yesu alimaanisha ngamia kupenya katika tundu la sindano. Na k**a ni hivyo basi nikufikirishe mambo mawili ambayo ili ngamia apenye kwenye tundu la sindano sharti mojawapo litokee.
Ngamia ni mnyama mkubwa na tundu la sindano ni dogo kwa sababu hata sindano yenyewe ni ndogo. Sasa ili ngamia apenye katika tundu la sindano lazima...
"Ama ngamia afanywe mdogo k**a u*i ili aweze kupita kwenye tundu la sindano" Au "Tundu la sindano litanuke na kuwa kubwa kiasi cha kuruhusu ngamia kupita kwenye hilo tundu".
Ukifikia level hii ya kufikiri utakubaliana nami kwamba kwa Mungu jambo hili linawezekana kabisa ila kwetu wanadamu ni jambo ambalo haliwezekani kabisa. Na siyo kwamba ninafikiri kwamba inawezekana, hapana, Nina uhakika kwamba linawezekana kwa sababu limewahi kutokea jambo linalofanana na hili kwenye agano la kale.
Kuna mtu anauliza, Dr. Hili jambo lilitokea wapi mbona sijawahi kukutana nalo? Inawezekana umewahi kukutana nalo lakini hukutafsiri kwa namna hii ambayo Mimi nimetafsiri. Sasa Nikukumbushe na kukuonyesha jambo lenyewe.
Ukisoma kitabu cha Hesabu sura 16 unakutana Habari ya Kora na wenzake ambao walishawishiwa kuukataa uongozi wa Musa. Jambo hili likafika mpaka kwa Mungu na k**a ujuavyo ukimkataa aliyetumwa umemkataa aliyemtuma. Kwa hiyo hii ni sawa na kusema akina Kora walimkataa Mungu maana Musa hakujichagua wala hakujituma bali alichaguliwa na kutumwa na Mungu.
Kilichotokea ni hiki hapa;
Hesabu 16 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
³¹ Basi ilikuwa, hapo alipokwisha kusema maneno haya yote, nchi iliyokuwa chini yao ikapasuka;
³² nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na watu wa nyumba zao na wote walioshik**ana na Kora, na vyombo vyao vyote.
³³ Basi wao, na wote waliokuwa nao, wakashukia shimoni wali hai; nayo nchi ikawafunika wakaangamia kutoka mle mkutanoni.
Sasa nikupe maelezo ya tukio hili, hapa hapakuwa na tetemeko la ardhi wala maporomoko ya ardhi ila Kuna tukio la ajabu nje ya Geografia lililofanywa na Mungu.
Kwenye Geografia tunajifunza kwamba ardhi hii ina matunda madogo madogo ambayo huiwezesha kupumua, na kwa yalivyo madogo hayawezi kuonekana kwa macho ya damu na nyama. Matunda haya yangekuwa makubwa sisi wanadamu pamoja na wanyama wengine tunaotembea juu ya ardhi tusingeweza kutembea juu yake maana tungetumbukia kwenye hayo mashimo. Kwa hiyo udongo wake ndiyo hutuwezesha kutembea juu yake bila shida.
Ukitaka kuthibitisha kwamba hayo matunda yapo mwaga maji hasa kipindi cha kiangazi utaona kwamba hayo maji yanapotea kwa haraka lakini pia Kuna bubbles kutoka kwenye ardhi.
Ardhi iliwamezaje watu? Ardhi iliwameza akina Kora na timu yao kwa kupanua yale matundu kiasi cha mtu kuzama na kisha kurudi katika hali yake ya kawaida. Yaani mtu unavyomuona kwa uwezo wa Mungu aliingia kwenye tundu za ardhi na kumezwa humo.
Sasa k**a Mungu alifanya hili tukio la tundu za ardhi kumeza kundi kubwa la watu kwa wakati mmoja, atashindwa kweli kupitisha ngamia kwenye tundu la sindano? K**a tundu za ardhi zilitanuka kiasi cha kumeza watu, je ni jambo kubwa tundu la, sindano kutanuka kiasi cha kuruhusu ngamia kupenya?
Mtumishi wa Mungu, sisi wanadamu tuna ukomo wa kuweza mambo lakini kwa Mungu yote yanawezekana. Inawezekana unasoma ujumbe huu lakini kuna jambo umehangaika nalo sana na umefika mahali pa kukata tamaa.
Ninazo Habari njema kwamba bado Mungu anaweza kufanya jambo kwenye hiyo hali yako. Tuna Mungu ambaye hashindwi na chochote, na lolote, yeye anaweza mambo yote. Wakati akili zetu Zikiwa na ukomo yeye za kwake hazichungu*iki; Isaya 55 (Biblia Takatifu)
⁸ Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana.
⁹ Kwa maana k**a vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.
“Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichungu*iki.”
— Isaya 40:28 (Biblia Takatifu)
Mungu hajashindwa bado, bado anaweza kukuvusha hapo na kukupeleka katika hali nyingine. Usimkatie tamaa Mungu, endelea kumwamini, anaweza na atafanya makubwa zaidi ya hilo.
Leo tukomee hapa, tukutane kesho tena kesho!
Kwa herini