26/03/2026
KINGDOM PRIORITY MISSION CHURCH
SEMINA YA NENO LA MUNGU MTANDAONI
MACHI 24-27, 2026 (JUMANNE - IJUMAA)
SOMO: THE MIGHT OF GOD IS UNQUESTIONABLE / UWEZA WA MUNGU SI WA KUULIZA
MNENAJI: DR. MWAMTOBE AAM - ASKOFU MKUU WA KPMC NA MCHUNGAJI KIONGOZI WA KANISA LA KPMC DODOMA
SIKU YA TATU - ALHAMISI MACHI 26, 2026
Watumishi wa Mungu, Bwana Yesu Asifiwe sana. Ninawasalimuni nyote katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Bwana na mwokozi wa maisha yetu. Hallelujah.
Ninazo shukrani nyingi kwa Mungu kwa kutupa neema tena ya kuendelea na somo letu na leo ni siku ya tatu. Lakini Nitumie nafasi hii kukukaribisha tena na tena kuendelea kufuatilia somo hili nikiamini kwamba kuna jambo la kwako kabisa ambalo Mungu anataka kusema na wewe.
Umekaribishwa sana.
Katika siku hizi mbili Tumefanikiwa kuona dhana za ndani kabisa za mistari yetu ya msingi ambayo ni Luka 1:37 na Luka 18:27. Mungu hasubiri tumalize somo ndiyo upate jambo la kujifunza na la kuondoka nalo, na kwa sababu hiyo naamini kwamba kupitia mistari hiyo ya msingi na maelezo yaliyotolewa vimekutoa mahali kwenda mahali pa juu na pazuri zaidi katika safari yako ya maisha na safari ya Utumishi pia.
Leo ninataka tutoke hapo sasa tuangalie jambo jingine ndani ya THE MIGHT OF GOD IS UNQUESTIONABLE. Karibu sana tuendelee kujifunza pamoja.
Katika siku hizi mbili Tumefanikiwa kuona dhana za ndani kabisa za mistari yetu ya msingi ambayo ni Luka 1:37 na Luka 18:27. Mungu hasubiri tumalize somo ndiyo upate jambo la kujifunza na la kuondoka nalo, na kwa sababu hiyo naamini kwamba kupitia mistari hiyo ya msingi na maelezo yaliyotolewa vimekutoa mahali kwenda mahali pa juu na pazuri zaidi katika safari yako ya maisha na safari ya Utumishi pia.
Leo ninataka tutoke hapo sasa tuangalie jambo jingine ndani ya THE MIGHT OF GOD IS UNQUESTIONABLE. Karibu sana tuendelee kujifunza pamoja.
SIFA ZA MUNGU (ATTRIBUTES OF GOD)
Sifa za Mungu ziko nyingi sana, katika masomo yangu ya Theolojia niliwahi kusoma kozi moja yenye Jina la ATTRIBUTES OF GOD na mwandishi wa ile manual amechambua karibu sifa 40 za Mungu. Sitaki kusema zote hizo ila nataka nikuonyeshe sifa kuu nne za Mungu ambazo humtafautisha kabisa yeye na miungu mingine.
Sifa hizi nne siyo kwamba zenyewe ni bora na muhimu kuliko zingine bali na zenyewe ni sehemu ya kuendelea kutafsiri mada yetu ambayo ni THD MIGHT OF GOD IS UNQUESTIONABLE.
SIFA YA KWANZA : YUPO KILA MAHALI (OMNIPRESENCE)
Mungu wetu yupo kila mahali, yupo hata mahali pale ambapo hatujawahi kufikiri kwamba yupo. Fikiria popote unapoweza kufikiria, Mungu yupo. Na, si tu kwamba yupo sasa bali yupo wakati wote.
Hapo ulipo Mungu yupo, hapa nilipo Mungu yupo, na, kule kwingine yupo, ile kwamba humuoni haina maana kwamba Hayupo kwa sababu ni vitu vingi sana hatuvioni lakini vipo. Ile kwamba huoni madhihirsho yake haina maana kwamba Hayupo, maana Mungu kujidhihirisha mahali ni jambo jingine tena.
Kwa kuwa Mungu yupo kila mahali, hakuna namna unaweza kumkimbia. Ndiyo, unaweza kukimbia kivuli chako lakini huwezi kumkimbia Mungu. Umewahi kujiuliza swali hili katika wakati fulani wa maisha yako?
“Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?”
— Zaburi 139:7 (Biblia Takatifu)
Mtu mmoja baada ya mambo yake kuwa magumu alikusudia kwenda mbali kabisa na wanadamu, lakini siyo mbali na Mungu kwa sababu huwezi kumkimbia Mungu.
Je wewe umewahi kufikiria kwenda wapi? Daudi aliwahi kufikiria hivi;
Zaburi 139 (Biblia Takatifu)
⁸ K**a ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko.
⁹ Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari;
¹⁰ Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika.
Daudi aliwahi hata kufikiria kwenda kuzimu, aligundua kwamba Mungu na huko pia yuko. Umewahi kukutana na hali ile wanasema unatamani ardhi ipasuke ikumeze? Ardhi inaweza kukumeza kweli lakini na huko utakakowenda Mungu yupo. Wapi tena?
Zaburi 139 (Biblia Takatifu)
¹¹ K**a nikisema, Hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku;
¹² Giza nalo halikufichi kitu, Bali usiku huangaza k**a mchana; Giza na mwanga kwako ni sawasawa.
Kwa nini maovu mengi hufanyika usiku? Hata hivi ninavyoandika Kuna watu na inawezekana wengine wanapitia ujumbe huu wanasubiri usiku uingie vizuri ili waweze kufanya maovu yao kwa Uhuru. Ni kwa sababu wakati wa giza/usiku ni ngumu kuonekana na watu, lakini siyo ngumu kuonwa na Mungu kwa sababu kwake yeye ni mwanga na giza ni sawasawa.
Kwa hiyo unaweza kudhani kwamba umefanya kwa siri kabisa lakini ninakupa uhakika kwamba wakati unafanya Mungu alikuwepo na amekuona. Ndiyo, hata k**a ulikuwa peke yako.
Daudi alipozini na mke wa Uria maandiko hayatuelezi kwamba Kuna mtu yeyote aliyeshuhudia kile kitendo, lakini tunaelezwa Mungu akimtuma Nathani kwenda kuzungumza na Daudi juu ya tukio lile lililofanyika kwa siri sana.
Nataka kusema nini? Hakuna mahali ambapo Mungu Hayupo, yupo kila mahali. K**a Kuna jambo baya umefanya na ukafikiri kwamba uko salama kwa sababu mchungaji wako hajui, wazee wa kanisa hawajui, wazazi na watu wengine hawajui, ninakufahamisha kwamba hauko salama. Salama yako ni kutubu tu.
Hii sifa ya Mungu kuwa kila mahali inaendelea kuatamia uweza wa Mungu na kuufanya uwe unquestionable. Sasa k**a anaweza kuwa kila mahali kwa wakati wote ni jambo gani litamshinda kulifanya? The Might of God is UNQUESTIONABLE.
SIFA YA PILI: MUNGU ANAJUA MAMBO YOTE (OMNIPRESENCE).
Wanadamu tumepewa uwezo fulani wa kujua mambo, lakini hatujui mambo yote. Ndiyo, hata tunfeunganisha fahamu na uelewa na ujuzi na elimu zetu wote kabisa, bado Kuna mambo mengi sana ambayo hatuyajui. Ndiyo, Kuna mambo mengi sana yasiyo na idadi ambayo hatuyajui, labda tutayajua tukifika mbinguni.
Nabii Isaya anapoandika kwa ulinganifu yale ambayo sisi tunayajua na yale ambayo Mungu anayajua anasema hivi.....
Isaya 55 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁸ Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana.
⁹ Kwa maana k**a vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.
Mimi Nimesoma Geography, haya mambo ya umbali tulisoma sana mpaka umbali wa kutoka kwenye jua mpaka kwenye dunia kwamba ni takribani kilometa million 149.6. Ni umbali mrefu sana lakini hak
Lakini umbali kati ya dunia na mbingu hakuna anayejua isipokuwa Mungu mwenyewe. Kwa hiyo Mungu anaposema kwa kinywa cha Isaya kwamba mawazo (Biblia zingine zimeandika though, knowledge, power, plans) yake yako mbali sana la mbingu ilivyo mbali na dunia maana yake uwezo wake wa kujua mambo ni mkubwa kiwango ambacho hausemeki zaidi ya kusema anajua mambo yote.
Daudi anasema...
Zaburi 139 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
² Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu; Umelifahamu wazo langu tokea mbali.
³ Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, Umeelewa na njia zangu zote.
Zaburi 139 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁴ Maana hamna neno ulimini mwangu Usilolijua kabisa, Bwana.
⁵ Umenizingira nyuma na mbele, Ukaniwekea mkono wako.
⁶ Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi, Hayadirikiki, siwezi kuyafikia.
Je Mungu anayejua mambo yote kutakuwa na jambo la kumshinda kweli? Ni muhimu ufahamu kwamba uwezo wa kufanya mambo umefungwa kwenyw uwezo wa kujua mambo, yule anayejua zaidi atafanya mambo mengi na makubwa zaidi.
Sifa hii nayo inaendelea kuatamia the Might of God is UNQUESTIONABLE.
SIFA YA TATU: WA MILELE ASIYEBADILIKA (ETERNAL AND UNCHANGING)
Kitu chochote ambacho wewe unakijua kina mwanzo wake, na chenye mwanzo lazima kitakuwa na mwisho wake (kanuni ya asili). Chochote chenye mwanzo kina historia yake ambayo inaweza kwenda umbali mrefu inavyowezekana lakini kuna wakati utafika mwisho. Pia chenye mwanzo kina tabia ya kubadilika kulingana na mazingira na muda.
Lakini kuna Mungu ambaye hana mwanzo, habadilili, hakui, hazeki, na nini Tena? Ni yeye yule Jana Leo na hata milele.
“Kwa kuwa mimi, Bwana, sina kigeugeu; ndio maana ninyi hamkuangamizwa, enyi wana wa Yakobo.”
— Malaki 3:6 (Biblia Takatifu)
“Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele.”
— Waebrania 13:8 (Biblia Takatifu)
Umewahi kufikiria mtu ambaye ameishi miaka mingi zaidi? Methusela aliishi miaka 969. Waswahili husema kuishi kwingi ni kuona mengi, na k**a ni hivyo basi kuishi kwingi ni kuweza mengi yaani kuwa na uwezo mkubwa. K**a hii ni kweli basi Methusela kwa kizazi chake alikuwa na uwezo mkubwa kuliko walio wengi.
Sasa Kuna Mungu ambaye hana mwanzo na hana mwisho, hii nayo inaendelea kuatamia the Might of God is UNQUESTIONABLE.
Sifa ya nne tutaangalia kesho ambapo tutahitimisha na mambo mengine makubwa ambayo yanaendelea kukoleza the Might of God is UNQUESTIONABLE.
Bwana Yesu akubariki sana.