16/04/2026
MWALIKO WA KONGAMANO LA MAASKOFU,WAANGALIZI,WACHUNGAJI NA WENZI WAO.TAR.16 NA 17 /04/2026
Mpendwa Baba Ask./Mw./Mch.
Salamu kupitia jina la Bwana Yesu.
Kwa heshima na unyenyekevu mkubwa,tunakuandikia kukualika rasmi kushiriki katika Kongamano la Maaskofu,Waangalizi,Wachungaji pamoja na wenzi wao.lililoandaliwa na CPCT Mkoa tukishirikiana na k**ati kuu ya CPCT Taifa.
Lengo kuu la kongamano hili ni kuimarisha umoja na mshik**ano k**a wapentekoste, kutiana moyo katika huduma, kuchochea uamsho wa kiroho, pamoja na kushiriki Chakula cha mchana kwa pamoja k**a ishara ya upendo na ushirika.
Washiriki wa kongamano hili watakuwa ni Maaskofu,Kamati kuu ya CPCT- Taifa,Mkoa, viongozi wa CPCT Wilaya zote za mkoa wa Arusha,Waangalizi,Wachungaji na wake zao.
kwa nafasi yako tunakuomba uwajulishe wachungaji walio karibu na wewe wahudhurie.
Aidha,tunatarajia kongamano hili litafunguliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa.
MUDA: ni saa 3:00 hadi saa 10:00
MAHALI:Kanisa la TAG - Betheli Kijenge kwa Askofu Oral Sossy
Uwepo wako na umuhimu wako utakuwa faraja sana kwetu na katika kufanikisha kongamano hili.
Tafadhali Baba Mtumishi wa Mungu kwa unyekevu mkubwa pokea Mwaliko huu kwa moyo wa upendo.
wako katika huduma ya Bwana
Bish.Rogers R.Shemtambo
Mwenyekiti wa CPCT Mkoa wa Arusha.