03/02/2024
Kunako majira Fulani Bwana huwainua watu ili wawe kielelezo Cha Watu wengine Mbele za Mungu. Ni wajibu wangu kuyahubiri na kuyaishi Yale Bwana Yesu ananifundisha, ili niwe mwanafunzi wa Yesu kwelikweli huku nikiujenga msingi Kwa kuwafanya wengine kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo. Nikitoa Historia ya maisha ya utumishi wangu na jinsi nilikotolewa na Bwana Yesu jinsi ilivyokuwa ni vigumu na mbali sana kiasi ambacho hata ukiniacha au ukininyima maji ya kunywa ama tu vile ukashindwa kumwelewa Enock, ila ukweli ni kwamba Siku Ile nilipoondoka nyumbani nilikua sijui niendako lakini nilijua nilikotoka na Mahali nilipo nachojua ilikuwa sio mipango yangu Wala Kwa nguvu za akili zangu. Kwahio nathubutu kusema K**a SI Bwana aliyekuwa pamoja Nami Nisimgelikuwa hivi nilivyo. Nimekuchagua Eee Bwana wangu(Yesu Kristo ) uliyezifikirisha akili zangu na kuzifanya ziwaze k**a uwazavyo wewe ili niwe kielelezo chako Kwa watu wako.
Nawakaribisha nyote tusali, tumwabudu Mungu pamoja na tujifunze Yale yaliyo ya Mbinguni. Basi tukiishi, twaishi kwaajili yake Kristo na ikiwa twafa,twafa kwaajili ya mambo ya dhambi na twafanywa hai kwaajili ya mambo ya umilele ambayo katika hayo twautazamia ujio wa Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudi mara ya pili kutuchukua. Je,watamani kuwa miongoni mwao? Basi nikukaribishe uungane nami katika kulitangaza Neno la Bwana, karibu tuabudu sote tumfanyie Bwana shangwe.
Evangelist Enock Jacob
A Pastor of the AZAZELI Evangelistic Gospel Group(Church).