06/11/2023
Shalom Shalom Shalom
Natumai Nyote Ni Wazima Wa Afya
Uongozi Wa Kwaya Ya Safina Na Wanakwaya Wote Kwa Ujumla Tunapenda Kuchukua Nafasi Hii Na Kwa Heshima Kabisa Kuwashukuru Wakristo Wenzetu Wote Ambao Jana Mlitenga Muda Wenu Na Kuja Kusheherekea Nasi Kwenye Sikukuu Ya Kwaya Yetu Ya Safina ( SAFINA DAY
Kipekee Tutoe Shukrani Zetu Za Dhati Kwa Mgeni Rasmi Rev.Can. Thomas Mwayela Kwa Kukubali Ombi Letu La Kuwa Mgeni Rasmi Na Kutuchangia Kwenye Shughuli Yetu, Pia Tunatoa Shukrani Zetu Kwa Uongozi Wa Kanisa Chini Ya Mchungaji Rev.Fr. Gerikoshua Baliko Kwa Kushirikiana Nasi Kuanzia Maandalizi Ya Tukio Mpaka Tulipokamilisha Tukio Letu. Tunashukuru Waumini Wote Wa Mt.Aidano Kwa Kuwa Nasi Mwanzo Mpaka Mwisho Wa Tukio Letu.
Pia Tuchukue Nafasi Hii Kuzishukuru Kwaya Zote Ambazo Zilikubali Mwaliko Wetu Wa Kuja Kushiriki Nasi Kwenye Tukio Letu Wakiwemo: The Winners Choir Kutoka Mbezi, Kwaya Ya Vijana Kutoka Malamba Mawili, Sinai Kwaya Kutoka Kijichi, Paradiso Kwaya Kutoka Buza, The Corner Stone Band Kutoka T/Kisukuru, Sifuni Kwaya Kutoka T/Kinyerezi, Sinai Kwaya Kutoka Karakata, N.k
Mungu Awabariki Sana Pale Pote Mlipotoa
Wenu Katika Bwana
Joseph Hillary Indidi
M/Kiti Safina Kwaya
Kwa Neema Ya Mungu