11/08/2026
Cristiano Ronaldo afunga ndoa na msichana wake baada ya kuishi miaka mingi na kuzaa pamoja.
Jambo hili limenifanya nikatambua ubora wa Sheria za Dini ya Kiislamu ambazo haziruhusu kuanza kuishi pamoja k**a kimada na kuzaa watoto ndipo mje baadae kufunga ndoa, katika Uislamu hili ni jambo geni na la ajabu.
Uislamu unaweka ndoa mbele ya uzazi, kwa sababu ndoa ni ahadi na mkataba mtakatifu unaolinda heshima, nasaba na haki za familia. Badala ya watu kuanza kuishi k**a wanandoa na kupata watoto kisha baadaye kutafuta ndoa, Uislamu unaelekeza kwamba ndoa ifungwe kwanza, ndipo maisha ya kindoa na kupata watoto yaanze.
Tofauti kubwa ni kwamba Uislamu umeweka mfumo unaolinda mwanamume, mwanamke na mtoto. Ndoa halali huweka wazi wajibu wa kila upande, ikiwemo matunzo, heshima, uaminifu na ulinzi wa nasaba. Mtoto anazaliwa ndani ya familia yenye uhalali unaotambulika kisharia, na wazazi wanawajibika kwa malezi yake.
Qur’an inasema:
“Wao ni vazi kwenu, na nyinyi ni vazi kwao.”
(Al-Baqarah 2:187)
Hii inaonyesha uzuri wa ndoa katika Uislamu: mume na mke si watu wanaokusanyika kwa tamaa tu, bali ni watu wanaopaswa kuwa kinga, faraja, heshima na msaada kwa kila mmoja.
Allah anasema:
“Na katika ishara Zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao, na akaweka baina yenu mapenzi na rehema.”
(Ar-Rum 30:21)
Kwa hiyo, Uislamu haupingi mapenzi; bali unayapa mapenzi njia halali na yenye heshima. Mtu anaweza kumpenda mwenzake sana, lakini Uislamu unamfundisha kwamba upendo huo uwe na mipaka na uelekezwe kwenye ndoa na sio kuishi kwa kimada.
Uzuri wa Uislamu hauachi masuala ya familia yaamuliwe na tamaa, mazoea au mabadiliko ya jamii. Unaweka kanuni zinazolinda heshima ya mwanamke, wajibu wa mwanaume, haki za mtoto, nasaba na utulivu wa familia.
Katika Uislamu, tunafunga ndoa kwanza, kisha tunaanza maisha ya kindoa na kupata watoto. Huo ni miongoni mwa uzuri wa sheria ya Allah katika kulinda familia na heshima ya mwanadamu.
K**a alichofanya Ronaldo na mfano wake kinaruhusiwa katika Dini yake nakiheshimu lakini kwa mtazamo wangu utaratibu uliowekwa katika sheria ya Kiislamu uko bora zaidi.