06/06/2020
Somo: Nidhamu ya maombi / ibada Kanisani.
Maelezo: Ni vema utambue kuwa, nidhamu ya maombi, au
utaratibu wa kuwa katika maombi ni jambo moja muhimu
sana. Unapoingia Kanisani ni lazima uelewe mambo ya
muhimu ya kuzingatia au kujua umuhimu wa nidhamu katika
nyumba ya Mungu au maombi.
Mambo ya kuzingatia katika nidhamu ya Maombi (au Kanisani)
k**a ifuatavyo.
1. Mavazi unayovaa. Kuvaa kwako unapokuja Kanisani au
unapokuwa katika maombi. Hakikisha unavaa mavazi ya
heshima au adabu kwani nyumba ya Mungu ni mahali pa
kuheshimika sana kuliko sehemu yoyote ile. Hivyo ni vema
mavazi yetu yawe ya heshima.
2. Zima simu, ondoa mlio wa simu, lakini hata ikiita usitoke
nje kupokea hadi umalize ibada. Unapotoka nje kupokea simu
na kuacha maombi au kuacha ibada ni kumdharau Mungu na
ni dhambi. 1 Sam. ....Kwa maana wao wanaoniheshimu nitawaheshimu, na wao wanaonidharau watahesabiwa kuwa si kitu
3. Ukichelewa kufika ibadani, unapoingia Kanisani usiburuze
miguu au viatu ukawapigia watu kelele, na k**a una
viatu vya koo koko, vua au nyata visipige kelele.
4. Unapochelewa na umewakuta watu kwenye maombi au
kuabudu, unapotaka kukaa kiti cha ndani ya mstari, ikiwa na
maana, ili ukae ni lazima umpite mtu mmoja au wawili, unashauriwa usiingie kukaa hadi wamalize maombi ili usiwasumbue na kuwatoa katika uwepo wa Mungu. 1 Kor. 14:40 Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.
5. Iwapo mtu yupo kwenye maombi nyumbani chumbani
nk. Usiingie hadi amalize kuomba au k**a utaingia basi
iwe ni kwa lengo la kuungana naye katika maombi. Aidha
mwombaji iwapo utatumia chumba chenye matumizi ya
watu wengi ni vema uwajulishe wenzako kuwa utakuwa na
maombi kwa muda fulani ili wawe na taarifa.
6. Kila kinachoagizwa au unachotakiwa ufanye wakati wa
maombi ya pamoja k**a Kanisani nk. Hakikisha unafanya
pamoja na wenzako. Kwa mfano, kiongozi anaposema tusimame basi na wewe simama, au tuimbe, tuombe nk ufanye k**a wenzako wote wanavyofanya usifanye kinyume na kiongozi wa ibada anavyokuelekeza.
Tunapoona mtu huwa hataki kufanya sawa na waumini weningine Kanisani inatosha kujua huyo mtu ana roho nyingine tofauti na waumini wengine. Biblia imeagiza kuwa tuwe na nia moja na roho moja na mapenzi mamoja. Wafilipi 2:2.3 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja. Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
1 Yohona 4:1. Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo
roho, kwamba zimetokana na Mungu;
Matendo 4: 24.31. Nao waliposikia, wakampazia Mungu sauti
zao kwa moyo mmoja, wakisema, Mola, wewe ndiwe Mungu,
ndiwe uliyefanya mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo;........................ Hata walipokwisha kumwomba Mungu, Mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.
Hapo tunaona umuhimuwa kuwa na nia moja katika maombi
au nguvu ya umoja katika maombi. Aidha kutokugawanyika
katika maombi. Kufanya kila kitu kwa pamoja. Kiongozi wa
maombi au Mchungaji awe makini sana na watu ambao wanaotofautiana na utaratibu wa maombi awasaidie au awakemee kwani mtu anayejibagua bagua mara nyingi huwa anatumiwa na adui shetani kuvuruga uwepo wa maombi.
Somo hili limetoka katika kitabu changu Kiitwacho "Omaba k**a Tai, Maombi ya Upenyo" Iwapo utahitaji kitabu hiki wasiliana na Mwandishi kwa+255717528272