Efatha Church kimara

Efatha Church kimara Efatha Church Kimara, located at Kimara Mwisho opposite with Midlands High School.You 're all welcome

31/05/2026

GLOBAL COMMUNION SERVICE.

MEZA YA BWANA.Yohana 6:33-35 “Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.  ...
31/05/2026

MEZA YA BWANA.

Yohana 6:33-35 “Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima. Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki.”

Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.”

Yohana 1:1-5 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.”

Tunapokubaliana na neno tunakuwa tunapata uzima wa milele, tunaporuhusu Neno ndani yetu tunaruhusu Yesu akae ndani yetu, kwa maana Yesu ndiye uzima wetu. Tukikubali Neno tumemkubali Yesu, na hapo ndipo tunalinda imani yetu, ukiilinda imani yako itakupa kuponyeka, ukiamini kile unachokiamini mtu asikiondoe wala kukiharibu ndipo uponyaji unatokea kwako, Yusufu alilinda imani yake japokuwa alitupwa gereani lakini akaishia kuwa mtu mkuu, Daudi pia alilinda imani yake na akaishia kuwa mfalme. Imani ukiilinda unakuwa salama na kwako kunakuwa kwema.

Zaburi 128:1-4 “Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake, Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema…”

Yule amchaye Bwana atabarikiwa. Kumcha Bwana ni kulinda kile unachokiamini, unapolinda unachokiamini maisha yako yanaonekana yana mpangilio na ndipo Mungu anakufurahia, kwa maana unapolinda hicho unajiponya na mambo au ulimwengu huu na ndipo Mungu anakufurahia na kuruhusu mema yakujilie na kwako kunakuwa kwema.

Zaburi 126:6 “Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.”

Tunapolinda imani kuna magumu, machungu kudharauliwa na kusukumwa lakini usiangalie yale yanayoendelea bali angalia kile unachokiamini ili kikupe kile unachokitaka, hakikisha unalinda kile unachokiamini na ndipo kwako kutakuwa kwema na Mungu atakushangaza na kila mtu atakushangaa.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

SOMO: KUFANYA MAPENZI YA MUNGU.ISAYA 9:6.“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa ki...
31/05/2026

SOMO: KUFANYA MAPENZI YA MUNGU.

ISAYA 9:6.
“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”

Kwa ajili yetu, na kwa faida yetu na kwa ajili ya maisha yetu mtoto amezaliwa, siyo kwa ajili ya Mungu, la! bali ni kwa ajili yetu, usisahau hilo. Watu wanaishi maisha haya ya wokovu k**a vile kamwe hawatakaa wafe, kwamba wataishi duniani milele, la! Lazima ufe, labda tu Yesu aje mapema, lakini k**a sivyo kufa utakufa tu, lakini lazima uelewe unakufaje, kwamba unakufa na utukufu au laana.

Biblia inasema “Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani” tulipewa mtoto mwanaume ambaye alikuwa na majina manne:-

Mshauri wa ajabu; akikushauri, akikusaidia na kukuongoza wewe, akikunyoosha ili uende kule Mungu anataka uwe.

Mungu mwenye nguvu; hii ina maana kuwa kuna miungu mingine lakini Mungu huyu ni Mungu mwenye nguvu, kwa nini mwenye nguvu? Ili kukusababisha wewe uweze kushinda, ili aweze kushinda miungu mingine yote kwa ajili yako. Mungu anapokupa mtu kusimama kwa ajili yako kumbuka anampa huo uweza ili akukomboe kutoka kwenye miungu mingine.

Baba wa milele: hii ina maana kuwa ubaba wake hauna mwisho, Mungu anapokupa baba wa kiroho huo ubaba kamwe hautakaa uishe, kwamba amekufa au yupo hai. Mungu anapokupa baba wa kiroho unapaswa kujua kuwa huo wajibu hautakaa uishe kwa maana siku tutakapofika mbinguni ni Yeye baba wa kiroho atakayesimama kwa ajili yako.

Mfalme wa Amani: Yeye amebeba mambo yote yanayohusu amani, maana yake ni pamoja na mafanikio yako. Yesu alizaliwa katika ushindi wa namna hii akibeba majina haya, kwa nini? Kwa sababu alikuwa kwa ajili yetu.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

31/05/2026
ZABURI 100:1-2, "Mfanyieni BWANA shangwe, dunia yote; Mtumikieni BWANA kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba."
31/05/2026

ZABURI 100:1-2, "Mfanyieni BWANA shangwe, dunia yote; Mtumikieni BWANA kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba."

IBADA YA MEZA YA BWANA, JUMAPILI TAREHE 31/05/2026 KANISA LA EFATHA KIMARA.Maombolezo 3:22-23, "Ni huruma za BWANA kwamb...
31/05/2026

IBADA YA MEZA YA BWANA, JUMAPILI TAREHE 31/05/2026 KANISA LA EFATHA KIMARA.

Maombolezo 3:22-23, "Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi. Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu."


It's the day of completion of fasting and praying for 31 days. GLORY TO GOD.
31/05/2026

It's the day of completion of fasting and praying for 31 days. GLORY TO GOD.

Ibada imekwisha kuanza, jiunge nasi kumfanyia Mungu ibada mubashara kupitia
31/05/2026

Ibada imekwisha kuanza, jiunge nasi kumfanyia Mungu ibada mubashara kupitia

Address

Kimara
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church kimara posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church kimara:

Share