13/04/2024
HAYA NDIO MAMBO ADUI HUFANYA UNAPOKUA UNAOMBA
1. Kukuaminisha kuwa hakitafanyika au hakitawezekana. Atakuonesha muda wote ukubwa wa hilo jambo na kukuambia kuwa hilo haliwezekani. Atakuonesha watu waliowahi kujaribu k**a wewe wakashindwa. Atakuonesha namna ulivyodhaifu au kukuonesha madhaifu yako. Hataweza kukuonesha namna Mungu alivyo mkubwa na muweza yote. Yeye mission yake hapa ni kukukatisha tamaa ili uone unachofanya ni kazi bure, uombee vingine. Kuna changamoto unaweza ukawa unapitia, ni kubwa mno kiasi kwamba unaona kabisa haiwezekani. Umefika hatua huamini k**a Mungu anaweza kuingilia kati na kuitatua. Ukifika hatua hii, hata ukianza kuomba adui atatumia hiyohiyo k**a njia ya kukuzuia usiombe ipasavyo. Kila ukianza kuomba tu, unakumbuka kwamba bado siku tatu kodi yako iishe na mpaka sasa huna na wala huoni dalili ya kupata. Utajikuta unaacha kuomba halafu unaanza kuwaza nifanye nini? Niende wapi? Nimtafute nani? Ndugu yangu hebu jiulize, kwani hakuna muda mwingine wa kuwaza hayo hadi wakati ukiwa unaomba ndio mawazo hayo huja tena kwa kasi? Usikubali! Hizo ni hila za adui. Kila siku jaza Neno la Mungu ndani yako, omba pia ili hata ukiwa unaomba umuone Mungu na si tatizo lako au madhaifu yako
2. Kukuondolea focus, utajikuta wakati mwingine unaacha kukiombea kitu hiko na kuombea vingine au kukufanya uache kuomba na kuanza kuwaza mambo mengine kabisa
3. Kukuondolea nguvu ya kuendelea kukiombea. Hata baada ya maombi yako, atajitahidi ukishamaliza kuomba hutaweza kuomba tena. Ndio maana watu wengi wakianza kuombea kitu fulani, siku inayofuata hawaombi tena au wataomba kikawaida sana. Adui huinuka na kuua nguvu yako ya kuendelea kukiombea kitu hiko. Usikubali hii ikupate, moto ulioanzisha uendeleze kila siku
4. Kukukumbusha dhambi ambazo ulishasamehewa na kuanza kukuhukumu kupitia hizo kuwa zinakuzuia. Inawezekana unaomba upate mtoto, na pengine zamani umewahi kutoa mimba ukatubu na kusamehewa. Kila utakaposimama kuomba kwa ajili hiyo, atakuletea Kumbukumbu hizo tu ili ujione hufai wala hustahili. Pazia la hekalu lilipasuka kumaanisha kwamba sasa tunaweza kumsogelea Mungu mwenyewe aliye Kuhani Mkuu(Ebr 9:12).Usikubali kuamini kuhusu hilo, Mungu akishasamehe haendelei kukuhukumu, wewe sasa ni kiumbe kipya kabisa. Simama kwa ujasiri uombe na usikate tamaa, atakujibu siku moja Warumi 8:1
5. Adui anaweza kukufanya ujione wewe unajitosheleza, umekamilika, kwahiyo hata usipoomba bado mambo yako yatakua sawa. Wakati mwingine unaweza kweli ukaona upo vizuri, huwa unaomba, huwa unasoma Neno, uchumi wako umekaa vizuri, ndoa yako ina amani na furaha nk. Kwahiyo wewe mwenyewe ukiona hivyo unaona ya nini kujitesa kuomba kila siku? Ya nini kufunga? Usikubali kufika huko, uwe navyo usiwe navyo bado unahitaji kuomba na kujenga mahusiano mazuri na Baba yako wa Mbinguni
Ubarikiwe
By Mathias
0766246830