07/05/2026
Nimesikia yale maneno yaliyotoka kinywani mwake kwenye ukumbi huko JNICC alipokuwa na Ruto. Maneno ya kipuuzi, maneno machafu, maneno ya kejeli na unyama! Anasema wamezungumza na Ruto: “Wakija kwangu nachapa mikwaju! Wakija kwako uwachape mikwaju!” Kwa sababu tu ya kuzungumzia demokrasia? Kwa sababu tu ya kudai haki? Kwa sababu tu ya kupinga dhuluma?
Mikwaju gani hiyo? Ni nini mikwaju? Ni kuchomwa sindano? Ni kubakwa? Ni kuteswa kingono k**a walivyomfanya Boniface Mwangi? Ni kumteka nyara na kumtupilia mpakani? Hii ndiyo lugha ya rais wa nchi? Hii ndiyo kauli ya kiongozi anayetakiwa kutuongoza?
Jamani, hii ni aibu kubwa! Aibu isiyokuwa na kifani katika historia ya Tanzania! Haijawahi kutokea rais akazungumza maneno machafu k**a haya hadharani. Mtu anayejiita mwana CCM, anayejiita kiongozi wa taifa, anaropoka vitu vya kipuuzi, vya kijinga, vya kinyama k**a hivyo!
Hakuna mtu karibu yake anayemshauri? Hakuna mshauri mmoja anayesema “Samia, hii lugha haifai kwa ofisi ya urais”? Au wote wamefumba macho na kuwa vibaraka?
Hii inamaanisha nini? Inamaanisha kwamba wameamua kushirikiana na Ruto kuwapiga watu mikwaju wote wanaodai demokrasia halisi. Wanataka kulibariki unyama. Wanataka kufanya mateso na ukatili kuwa mfumo rasmi wa serikali zao. Hii si uongozi — hii ni udikteta uliofichwa kwa suti na tie!
Watanzania, tumefika wapi? Tumefika level gani mbaya hivi kwamba rais anatishia kuwapiga raia wake na wageni mikwaju kwa sababu tu ya kutaka uhuru wa kujieleza?
Demokrasia si Coca-Cola, anasema. Sawa. Lakini je, mateso na ukatili ni “demokrasia yetu”? Je, kubaka na kuteswa ni mila yetu? Je, kuwanyamazisha wapinzani kwa nguvu ni “amani”?
Hii ni fedheha! Hii ni aibu kwa taifa zima! Rais anapata kiburi cha ajabu. Anazungumza k**a mtu ambaye amesahau kwamba madaraka yanatoka kwa wananchi, si kwa silaha au sindano za mateso.
Ndugu zangu, wakati umefika wa kufakari kwa kina. Ikiwa tumefika hapa — rais akizungumza lugha chafu, akishirikiana na wenzake kuwatesa wanaodai haki — basi nchi yetu iko hatarini kubwa. Hatutaendelea kaa kimya. Hatutaendelea kuteswa na kuogopwa.
Tumechoka na maneno matupu na vitendo vya unyama!
Tumechoka na viongozi wanaotutishia mikwaju badala ya kutuletea maendeleo!
Tumechoka na serikali inayowinda raia wake badala ya kuwalinda!
Inatosha!
Wananchi, simameni kidete. Sauti zenu ziweze kusikika. Usikubali kufanywa kitoto na kauli za kejeli chafu. Demokrasia halisi inajengwa na watu, si kwa mikwaju na vitisho.