15/09/2024
MAVAZI? SURUALI? SKETI? 😀😀
Biblia inafundisha kuvaa kwa kujisitiri na kwa heshima.. (modest dressing) wala haifundishi vazi gani livaliwe.
Kujisitiri ni swala la utamaduni..
Tafsiri ya kujisitiri kwa wamasai na Wachaga hazifanani. Kwa Wahadzabe na Wahaya hazifanani. Kwa wazungu na Waafrika hazifanani.
Kwa waafrika wengine kutoa "maziwa" na kumnyonyesha mtoto kwenye daladala ni jambo la kawaida... kwa wazungu ni "taboo" ni jambo la aibu sana. Lakini kibongobongo mtu anatoa "maziwa" yake kwenye daladala na kumnyonyesha mtoto na hakuna kinyaa wala mtu anawaza ujinga.. tunaona tu mtoto anapata dinner yake.
Lakini nchi za Magharibi hiyo ni issue kubwa.
Ndiyo maana ni ngumu kuona filamu za kizungu wanaonyesha mtoto anaponyonya waziwazi. Ni jambo la kukosesha heshima kabisa... lakini watu hao hao watavaa "bikini" na kujisambaza bustanini wakati wa "summer".. au kiangazi..
Na bado asilimia ya ubakaji (r**e) ikawa kidogo kuliko wale wanaojifunika "gubigubi"... hii isiwe tabu sana.. tuendelee..
Kile ambacho mmasai anaita nguo ya heshima sicho anachokiita mnyakyusa.
Tafsiri ya kujisitiri pia inategemea umbo la mtu..
Usipigilie mavazi mpaka kila mtu anatokwa na mate mdomoni. Unatafuta nini?
😀
Mtu mmoja kwa speed atanukuu 👉🏽Kumbukumbu la Torati 22:5
[5]Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa BWANA, Mungu wako.
Hapa kuna ugonjwa mkubwa wa kunyofoa mistari nje ya muktadha ili mtu alazimishe iseme kile anataka.. NI UOVU WA KIWANGO CHA PhD..
Lakini mtu huyo hatasoma Mistari inayofuata k**a ataweza kuyatendea kazi.
Okay hii hapa vipi? Kumbukumbu la Torati 22:9
[9]Usipande shamba lako la mizabibu aina mbili za mbegu; yasije yakaondolewa matunda yote, mbegu ulizopanda na maongeo ya mizabibu yako.
Unafanyia kazi?
Unachanganya mazao shambani? Unafanya "mixed cropping"?
Vipi kuhusu hii?
Kumbukumbu la Torati 22:10
[10]Usilime kwa ng’ombe na punda wakikokota jembe pamoja.
Hapa kwenye kuchanganya nguo na vishada?
Kumbukumbu la Torati 22:11-12
[11]Usivae nguo iliyochanganyikana sufu na kitani pamoja.
[12]Ujifanyizie vishada katika pembe nne za mavazi yako ya kujifunika.
Hapa wote tungevaa makanzu tu hahaha.
Nimechukua tu baadhi ila watu wanapenda sana kukazia mstari wa 5 ila sura ya 22 yote wanajua hawawezi kutendea kazi.
Ili uweze kutendea kazi inabidi mambo yafuatayo.
1. Aina za sheria za Musa.
2. Lengo la sheria za Musa.
Usipojua utapata tabu sana.
Wakati Musa anawapa sheria hii.. hawakuwa na sketi na suruali k**a mavazi yao rasmi.
Nguo zao ni makanzu au jamii ya nguo za kufunika juu mpaka chini. Ni rahisi kabisa mwanamke kujivalia vazi la mwanaume. Siku hizi kuna mbwembwe zimewekwa kutofautisha.. lakini ilikuwa ngumu kuzitofautisha. Kiasi kwamba mwanaume akichukua nguo za mwanamke (akiwa kwenye siku zake) anakuwa NAJISI.. akaingia nayo kwenye HEMA YA KUKUTANIA ujue anaenda kufa. 😀
Njia rahisi ya kuwasaidia.. WASIVALIANE.
Leo ukienda umasaini.. Rubega ya k**e na ya kiume haipo..
Huo mstari wa Kumb 22:5 utautumiaje?
Maana kinachotofautisha ya "kiume" na ya "k**e" siyo mavazi.. bali namna atakavyofunga hiyo rubega (nguo iko k**a shuka tu).
Vipi kuhusu suruali kutajwa kwenye Biblia.. Oh ipo na imetajwa kwenye Biblia ya Kiswahili Standard Union Version mara 7 kwenye Agano la Kale.. tena kitabu cha KUTOKA, MAMBO YA WALAWI, EZEKIELI na DANIELI.
Maelezo ya nguo hiyo yako.. kwenye Kutoka peke yake na ilikuwa spesho kwa haruni..
Angalia.. Kutoka 28:42
[42]Nawe wafanyie SURUALI za nguo ya kitani, ili kufunika tupu ya miili yao; suruali hizo zitafika tangu kiunoni hata mapajani;
And thou shalt make them linen BREECHES to cover their nakedness; from the loins even unto the thighs they shall reach:
HIZI NI NGUO ZA KUTOKA KUNONI HADI MAPAJANI.. Actually ni nguo ya ndani ya KUHANI MKUU (enzi hizo Haruni). Haruni akivaa mavazi ya KIKUHANI nguo hiyo haionekani. 😀😀
Inakuwa UNDERWEAR.. (Picha na maelezo ninazo)..
Hili vazi "BREECHES" kwa lugha ya siku hizi ni suruali fulani wanavaa watu wanaopanda farasi ambapo wanakuwa wamevaa viatu fulani vinakuja mpaka magotini.
Google: breeches.
Sasa mavazi ni jambo la utamaduni..
NCHI YA FIJI, Raisi na Waziri mkuu anavaa sketi inaitwa KILN.. tena kwenye sherehe maalumu anatokeza na sketi.. 😀 baadhi ya nchi askari wanavaa sketi k**a baadhi ya askari Scotland..
Askari wa Kirumi walikuwa wanavaa nini? 🤷🏽♂️
Ukiacha kufikiri kidini na kimapokeo hili jambo.
Sasa k**a kwenu suruali inawakwaza... katazeni tu lakini acheni kusema Biblia imesema..😎 SEMA HAYA NI MAPOKEO YETU na watu wenu WATAYAPOKEA k**a mapokeo yenu ikiwa ni lazima kufanya hivyo na k**a kuna sababu za msingi..
The bottomline is...
VAA, PENDEZA, HESHIMIKA KULINGANA NA MAZINGIRA YAKO.
Katika mazingira yako yote... LENGA KUMTUKUZA BABA YETU (MUNGU) NA KUHAKIKISHA HAUWI KWAZO LA INJILI KWENYE MAZINGIRA HAYO..
Nikienda umasaini na hawawezi kupokea Injili nikiwa nimevaa suruali.. nitavaa nguo zao.
Anyway. Wakati tunabishana juu ya suruali na sketi kuna ndugu (WAMISIONARI) wako mbigani huko wamevua nguo zao.. wamevaa majani na kufunika sehemu fulani tu ili wahubiri Injili... maana kuna makabila huwezi kuwafikia huko porini ukiwa na sketi au suruali..
Nimepita tu!.
Ap Shemeji Melayeki
Global Family Gatherings
"God's Standards"