28/07/2026
Tunamshukuru Mungu kwa mafanikio ya Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Field ya Arusha. Kuanzia tarehe 1–3 Julai 2026, Mkutano Mkuu wa Uchaguzi ulifanyika Maji ya Chai, makao makuu ya Field ya Arusha, ukisimamiwa na wawakilishi kutoka Union ya Tanzania, Mch. Bartholomew James na Mch. Peter Paulo.
Baada ya usomaji wa taarifa za viongozi na maafisa wa Field, vipindi vya maswali na majibu pamoja na uvuaji wa ofisi, wajumbe kutoka makanisa mbalimbali walikamilisha zoezi la uchaguzi wa viongozi watakaoiongoza Field kwa kipindi cha miaka mitatu yaani 2026 hadi 2029.
Katika ibada ya Sabato, tarehe 4 Julai 2026, waumini kutoka makanisa ya Field ya Arusha walikusanyika kanisani Maji ya Chai, ambapo viongozi wapya walitambulishwa na kuapishwa rasmi kwa ajili ya kuanza majukumu yao.
Sambamba na viongozi wa idara na majukumu mbalimbali, viongozi wakuu waliochaguliwa ni:
• Kiongozi wa Field: Mch. Enock Ndimangwa
• Makamu Kiongozi: Mz. Mweta Kajiru
• Katibu: Prosper Mbwambo
• Mtunza Hazina: Seth Mbwambo
Pichani ni kusanyiko la ibada ya Sabato lililowakutanisha waumini, wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi, viongozi na maafisa waliomaliza muda wao wa uongozi, pamoja na viongozi na maafisa wapya waliochaguliwa wa Field ya Arusha.
Tunaendelea kuwaombea viongozi hawa pamoja na timu nzima ya uongozi ili Mungu awaongoze, awajalie hekima na uaminifu wanapoendelea kulitumikia Kanisa na kuendeleza utume wa Injili.