Utukufu Life Ministry

Utukufu Life Ministry Utukufu is the Swahili word meaning Glory, at Utukufu Life Ministry we live by glorifying Lord Jesus in everything we do or that happen under the sun.

ShalomSomo letu la UHUSIANO WA NDOTO NA MAISHA YAKO HALISI KIBIBLIA linaendea leo WhatsApp group na linakujia kwa njia y...
26/04/2021

Shalom

Somo letu la UHUSIANO WA NDOTO NA MAISHA YAKO HALISI KIBIBLIA linaendea leo WhatsApp group na linakujia kwa njia ya Voice note. Leo ndo tunaanza kuweka msingi wa somo letu
Karibu upokee maarifa ya kimungu kuhusu ndoto unazoota.

Kujiunga link bonyeza link hapo chini

WhatsApp Group Invite

Darasa la masomo ya neno la Mungu linaendelea kwa njia ya WhatsApp Voice note. Tupo na somo zuri sana linalozungumzia "U...
22/08/2020

Darasa la masomo ya neno la Mungu linaendelea kwa njia ya WhatsApp Voice note. Tupo na somo zuri sana linalozungumzia "UJUE WITO WA MUNGU KWAKO KABLA YA KUOMBA MTU/WATU WA KUAMBATANA NAO". Ni somo ambalo limewafungua wengi sana.

Kujiunga bonyeza link hapo chini.

Barikiwa

WhatsApp Group Invite

26/05/2019

SOMO: MAPITO YANAYOWEZA KUKUFANYA UHISI MUNGU AMEKUACHA NA MAMBO YA KUFANYA WAKATI HUO(WA MAPITO).

Sehemu ya kwanza

Na Mwl Ansbert Justus
+255759947276

Bwana wetu Yesu Kristo asifiwe sana ndugu zangu. Ni matumaini yangu kuwa mu wazima kabisa kiroho na kimwili. Namshukuru Mungu nimwabuduye kwa kutupa kibali cha kukaribia mezani kwake ili tupate kula na kunywa kile alichotuandalia kupitia somo hili. Hili ni somo ambalo linamgusa kila mtu aliyeokoka na ambaye hajaokoka, kwa hiyo naweza kusema ni somo ambalo Roho Mtakatifu ameliachilia kwa wakati sahihi.

Msingi wa somo letu unatoka katika andiko la Mathayo 27: 45-46 "Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa. Na k**a saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?"

Utangulizi wa somo.
Kila somo ambalo Roho Mtakatifu uwa anaachilia kwangu ili niweze kulileta kwenu uwa lina lengo. Sasa malengo ya Roho Mtakatifu kuachilia somo hili ni:
1. Kukusaidia kujua jinsi ambavyo Mungu ufanya kazi kulingana na nyakati
2. Kukusaidia kujua jinsi Mungu anavyozungumza kulingana na nyakati unazopitia
3. Kukusaidia kutambua majira na nyakati yanavyobadirika na jinsi ya kuenenda.
4. Kukufunulia akili za kujua jinsi ya kutembea katika mapenzi ya Mungu wakati wa mapito.
5. Kuimarisha uhusiano wako na Mungu katika Kristo Yesu.

Somo hili tutajifunza kwa mtindo wa vipengele, ambapo tutatazama vipengele vifuatavyo;
1. Maana ya mapito
2. Ishara zitakazokufanya utambue ya kwamba upo kwenye kipindi cha mapito
3. Kazi ya mapito katika maisha ya mwanadamu
4. Matokeo ya mapito ndani ya moyo wa mwanadamu
5. Vyanzo vya mapito/ Aina za mapito
6. Mambo ya kufanya uwapo kwenye kipindi cha mapito.

Turudi kidogo kwenye msingi wa somo ili tupate kujifinza jambo mahali hapa. Biblia inasema Yesu pale msalabani alipaza sauti akasema Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha? Hiki ni kipindi ambacho Yesu alihisi Mungu amemuacha. Ni kipindi ambacho alikuwa anapitia mapito magumu sana tangu alipokuwa kwenye mlima wa Gethsemane kuomba, biblia inasema aliomba mpaka matone ya damu yakatoka, kwanini? Kwa sababu mwili ulikuwa umegoma kwenda msalabani, ndiyo maana alikuwa akiomba anasema "Baba yangu ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke, walakini si k**a nitakavyo mimi, bali k**a utakavyo wewe"(Mathayo 26:39) lakini baba yuko kimya, ikafika hatua akashuka kuwaangalia akina Petro waombaji wake akakuta wamelala, akawauliza "Petro, Je hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? Kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni, roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu" (Mathayo 26:40-41). Akarudi tena mara ya pili na ya tatu kuomba lakini biblia inasema Mungu alikuwa kimya. Akak**atwa akateswa, akavikwa taji la miiba kichwani, akapigwa kwa muanzi, akahukumiwa kwa uongo, akapigwa mijeredi, akadungwa misumari, akasurubiwa msalabani, muda wote huo Mungu yuko kimya. Akapandishwa msalabani saa tatu, akajitia moyo akajua Mungu atazungumza, saa sita, saa saba, saa nane, saa tisa, Mungu yuko kimya. Ikabidi apaze sauti amuite na kumuuliza "Mungu wangu, Mungu wangu mbona umeniacha?" lakini bado Mungu yupo kimya. Mpaka akaitoa roho yake Mungu yuko kimya.

Inawezekana ata wewe ndugu unapitia mapito ya namna hii ambayo umefika hatua unahisi Mungu amekuacha, umeomba mpaka fahamu zako zinakwambia acha kujisumbua Mungu hakusikii. Umefika hatua ata kuomba hutaki tena. Usife moyo somo hili linaenda kufufua na kurudisha uhusiano wako na Mungu. K**a vile ambavyo siku ya tatu Mungu baba alimtembelea Yesu kaburini na kumfufua vivyo hivyo kupitia somo hili Mungu anaenda kufufua uhusiano wako na yeye ili apate kuachilia neema zake kwako.

Usikose sehemu ya pili ya somo hili jumatano.

Barikiwa sana.

Karibu darasa la WhatsApp k**a unataka kupata somo hili kwa njia ya audio.

Link:

25/05/2019

MEZANI KWA BWANA YESU
Zaburi 23:5

Shalom ndugu zangu.
Nichukue nafasi hii kiwajulisha kuwa kuanzia jumatatu tutaanza kupata somo la "MAPITO YANAYOWEZA KUKUFANYA UHISI MUNGU AMEKUACHA NA MAMBO YA KUFANYA WAKATI HUO". Ni somo aliloliachilia Roho Mtakatifu kwa wakati sahihi maana hata halikuwa kwenye ratiba zangu ila Roho wa BWANA ndiye ajuaye zaidi. Na nisomo linalomgusa kila mtu kwa hiyo nakushauri usilikose.

Lakini pia somo hili hili linafundishwa kwa njia ya sauti (audio) katika darasa la huduma hii WhatsApp na limeshaanza. K**a ungependa kujifunza kwa njia ya sauti, basi jiunge na darasa letu kupitia link iliyopo hapo chini.

Mungu akubariki.

Link:

07/05/2019

MEZANI KWA BWANA YESU
Zaburi 23:5

Bwana Yesu asifiwe ndugu zangu. Nawasalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo aliye hai. Ni matumaini yangu kuwa mu wazima kabisa kiroho na kimwili. Wiki hii ilikuwa tuanze somo la "MAPITO YANAYOWEZA KUKUFANYA UHISI MUNGU AMEKUACHA NA MAMBO YA KUFANYA WAKATI HUO" lakini hatukuweza kutoka na ratiba kuingiliana, kwa hiyo somo hili litaanza wiki ijayo. Na somo hili linafundishwa kwa njia ya audio huko daradani whatsapp, lakini na hapa tutakuwa tunakuletea kwa njia ya maandishi. Kwa hiyo k**a unaitaji kujiunga darasa la whatsapp tuma neno ndiyo kwenda namba 0759947276 au bonyeza link hiyo hapo chini kujiunga moja kwa moja.

Barikiwa sana, tukutane darasani

Mwl Ansbert Justus

Link https://chat.whatsapp.com/3mhvONhTWbF23jnBDwHcdH

01/04/2019

DARASA LA WHATSAPP
Unaota ndoto hujui tafsiri yake?? Wakati mwingine unayoyaota yanatokea na hujui kwanini??? Uliota ndoto ambayo tangu siku hiyo kila kitu kilikwama??? Hivi unajua k**a shetani anatumia ndoto pia kupandikiza vitu maishani mwako??? Na unajua k**a Mungu anatumia ndoto kuzungumza na watu lakini waliowengi hawatambui???
Haya yote utajifunza whatsapp group ya huduma ya Utukufu Life Ministry.
Jiunge mapema maana wiki hii tutaanza hili somo la ndoto. Tumia link hiyo hapo chini kujiunga.

Barikiwa🙏

24/03/2019

Shalom wapendwa. Wakati tunaanzisha ukurasa huu, watu wengi mliomba tuwe na group whatsapp kwa ajili ya kujifunza zaidi, nikawaambia tusubiri tu wakati wa Mungu, sasa napenda kuwaambia kuwa tumepata kibali kwa Bwana kuwa na group la whatsapp. Unaweza kujiunga kwa kutumia link hiyo hapo chini. Mwambie na mwingine unayejua kuwa group hili litafanyika baraka kwake. Hatuna dini wala madhehebu, hii ni kwa watu woooote, hapa tunajifunza neno la Mungu kibiblia sio kidini wala kidhehebu.

Karibu

04/03/2019

UMEFIKA HATUA YA KUHISI MUNGU AMEKUACHA KATIKA MAISHA YAKO??? (Pokea ujumbe wako).

Bwana Yesu asifiwe.

Katika nchi za Asia na Africa kuna mti unaitwa MUANZI. Mti wa muanzi ukipandwa uchukua miaka mitano ya kumwagiliwa, kupaliliwa na kuwekewa mbolea ili uchipue, na ukichipua, ndani ya wiki tano ukua kwa urefu wa futi tisa(9). SWALI; Je huu muanzi ukua futi tisa ndani ya miaka mitano au wiki tano? Jibu liko wazi, ukua futi tisa ndani ya miaka mitano, maana ndani ya miaka mitano huyu mkulima akiacha kuumwagilia, na kuuwekea mbolea hakika utakufa.

Umekuwa na ndoto na maono katika maisha yako lakini hauoni jambo lolote likizaliwa? Umekuwa na ndoto ya kufanya biashara lakini haujui utaanzaje ama umeanza lakini uoni faida wala biashara haikui? Umekuwa na ndoto ya kuoa/kuolewa lakini kila ukitazama umri unaenda lakini mambo hayaeleweki mpaka imefika hatua ndugu wanakuandama?? Umeolewa lakini hujapata mtoto na muda unazidi kwenda, umeomba mpaka unahisi Mungu akusikii mpaka ndugu/ wifi zako wamekuita kila aina ya majina???, umekuwa ukihudumu mwaka wa tano sasa, vipingamizi ndo kwanza vinaongezeka, unaomba sana mpaka wingu la Bwana linashuka na watu wanapokea haja za mioyo yao lakini huduma haikui???, unapenda sana kuimba kwa ajili ya ufalme wa Mungu lakini haujui utafanyaje???, familia yako vurugu ni kila kukicha, hamuelewani na mume/mke wako???, umeomba kwa ajili ya wanao lakini hauoni mabadiliko, mwanao wa kiume ndo kazidi uhuni wa k**e ndo ashikiki kabisaaa???

Sikia neno la Mungu mpendwa, anasema hivi yeye hajakuacha bado yupo na wewe. Endelea kumwagilia ndoto/maono yako, haijalishi watu wanasema nini juu yako, endelea kumwagilia ndoto/maono yako, husikubari kukatishwa tamaa na watu, wala husiipe akili yako nafasi ya kusema haiwezekani. Inawezekana watu wasione ama wewe usione matokeo kwa sasa, endelea kumwagilia ndoto/maono yako kwa njia ya maombi. Haimsumbui Mungu kutimiza ndoto/maono yako wala hana shida na hilo ila UMEJIANDAAJE KUPOKEA NDOTO/MAONO YAKO kwake ndo jambo la msingi zaidi, ule UTU, TABIA, UDHUBUTU, FIKRA, FAHAMU, UVUMILIVU NA IMANI vinavyojengeka wakati wa mchakato kwake na kwako ni muhimu zaidi kuliko ndoto/maono yenyewe. Husikubari kukata tamaa pambana, push, puush, puuush mpaka uone kitu kinazaliwa. Mwamini Mungu kwa wakati atatimiza ahadi yake kwako. Haijalishi umesubiri kwa miaka minne k**a mkulima wa muanzi, tambua mwaka wa tano ndoto yako inaenda kuzaliwa na ndani ya wiki tano waliokubeza watasema hakika unaye Mungu ajibuye kwa vitendo.

Mungu akubariki sana.

23/02/2019

AINA TATU(3) YA WATU WANAOKUZUNGUKA.

Bwana Yesu asifiwe.

Nakusalimu katika jina lipitalo majina yote mtu wa Mungu. Leo nataka niongee nawe aina tatu ya watu wanaokuzunguka katika ulimwengu huu.

Linapokuja swala la mafanikio ya kiroho ama kimwili hapa duniani, watu wanaokuzunguka wana mchango mkubwa mno. Mara nyingi tumekuwa tukirudi nyuma kimaendeleo ama hatufikii hatima ya mafanikio kwa sababu ya watu tulionao/wanaotuzunguka. Abrahamu alichelewa kupokea nchi ya ahadi kwa sababu ya kuambatana na Lutu (Mwanzo 12 na 13). Kwa hiyo katika maisha yako kuwa makini na nani unamwambia ndoto ama siri zako, ama nani unaambatana naye.

Sasa nataka tuone kwa undani aina hizi tatu za watu wanaokuzunguka;

1. WASIRI: Hawa ni aina ya watu ambao wapo kwa ajili yako, ni aina ya watu wanaokupenda bila kutegemea jambo lolote kutoka kwako. Uwe juu ama chini kimaisha, uwe sahihi ama umekosa bado watakuwa na wewe muda wote. Ni aina ya watu ambao wamejiunganisha na maisha yako haijalishi ni ya namna gani. Watakusifia utakapofanya vizuri na ukikosea watakukosoa, watakukaripia pale utakapofanya mambo ya kipuuzi, siku zote watakushauri mambo ya mafanikio. Ukiumia wataumia na wewe, ukifurahi watafurahi na wewe, ukiwa na uzuni watakupa faraja, wapo tayari kuingia gharama ama kwenye matatizo kwa ajili yako. Mara nyingi watu wa namna hii huwa wanakuombea ufanikiwe ata kuwazidi wao. Watu wa namna hii ni wachache sana na k**a unao wawili ama watatu katika maisha yako, basi wewe umebarikiwa. Unamkumbuka Ruthu kwa Naomi katika kitabu cha Ruthu??? Ngoja nikupe maandiko machache uone, Ruthu 1:16-17 "16 Naye Ruthu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu;
17 Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo hapo nitazikwa; BWANA anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga wewe nami." Hayo ni maneno ya Ruthu kwa mama mkwe wake Naomi.

2.WASHIRIKA: Hii ni aina ya watu ambao hawapo kwa ajili yako, bali kwa ajili ya kile ulichonacho chenye faida kwao. Ilimladi una kile wanachokitaka basi watakuwa na wewe kwa hali na mali, watafanya kazi na wewe yamkini wanajua kuna kitu watafaidika. Watu wa namna hii wakikutana na mtu ambaye anaweza kuwapatika kile wanachokitaka kwako kwa ubora ama ukubwa zaidi yako uwe na uhakika wataachana na wewe. La msingi ni kutambua watu wa namna hii hawapo kwa ajili yako bali ulichonacho/wanachokipata kwako, na usipokuwa makini unaweza kuwachanganya na wasiri. Ukikwama kiuchumi ama kimaisha utawatambua vizuri, hata mmoja hautamuona na wataishia kukuumiza moyo wako. Unawakumbuka wale makutano waliokula mikate na samaki mpaka wakavimbiwa??? Baada ya siku kadhaa walimsaka tena Yesu, unajua kilichowafanya wamsake?? Ebu ona kilichowafanya wamsake tena Yesu, Yohana 6:24-26 "24 Basi mkutano, walipoona ya kuwa Yesu hayuko huko wala wanafunzi wake, waliingia mashuani wenyewe, wakaenda Kapernaumu wakimtafuta Yesu.
25 Hata walipomwona ng’ambo ya bahari, walimwambia, Rabi, wewe umekuja lini hapa?
26 Yesu akawajibu, akasema, Amin, amin, nawaambieni, Ninyi mnanitafuta, si kwa sababu mliona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba." Sasa hawa ndo aina ya waumini wengi walioko makanisani, wanamtafuta Yesu kwa sababu wameskia anaweza kutatua shida zao, wakifanikiwa huwaoni tena makanisani. Wakristo wengi wapo kanisani si kwa sababu wanampenda Mungu, bali wapo kanisani kwa sababu Mungu anaweza kujibu maitaji yao, hawapo kwa ajili ya Mungu bali wanachoweza kupata kutoka kwa Mungu.

3. WAPINZANI WENZA: Watu wa namna hii hawapo kwa ajili yako wala kwa ajili ya wanachoweza kufaidika kutoka kwako, bali watu wa namna hii wapo kwa ajili ya kile ambacho upo kinyume nacho. K**a upo kinyume na jambo fulani, basi ata wao watakuunga mkono kwa sababu wapo kinyume na jambo hilo pia, ikiwezekana ata kifedha watakuwezesha ili ushindi upatikane. Mara nyingi watu wa namna hii uwa hawapendi wajulikane wapo upande gani, ujificha nyuma ya kivuli chako ili wasionekane. Wakati mwingine wataungana na wewe kwa hali na mali ili wakusaidie umpige adui yako. Sasa usichanganyikiwe na muungano wao, watakuwa na wewe mpaka ushindi upatikane, wapo kwa ajili ya kutimiza kusudi na likitimia hutawaona tena. Usivunjike moyo wakiondoka maana kusudi lao litakuwa limetimia. Urafiki wa namna hii mara nyingi unafanyika kati ya mtu na mtu, nchi na nchi, kabila na kabila, ukanda na ukanda, nk. Mwanamke huyu na mwanamke huyu wanaungana kwa ajili ya kumchamba mwanamke fulani kisa wote hawampendi. Unaikumbuka vita kati ya Shinari, Elasari, Elamu, Goimu na Sodoma, Gomora, Adma, Seboimu, Soari??? Wafalme wa hizo nchi waliungana kulingana na ukanda wao kupigana kwa sababu tu ukanda mmoja hauelewani na mwingine (Mwanzo 14:1-12). Unamkumbuka Mfalme Sauli na Daudi walipoungana kwa sababu tu ya adui Goliati?? Baada ya hapo kilichoendelea ni nini? Uhasama baina yao wawili, mifano ipo mingi kwenye biblia ila kwa leo ngoja niishie hapo.

Ni maombi yangu kwa Mungu somo hii lizae matunda ndani yako, uweze kuwatambua aina ya watu waliokuzunguka.

Mungu akubariki.

10/11/2018

SOMO: MAMBO 12 YANAYOWEZA KUKUSAIDIA KUONGEZA NGUVU YA KUJIBIWA KWA MAOMBI YAKO.

Sehemu ya nne na mwisho.

Na Mwl Ansbert Justus
+255759947276/+255716797470

Shalom shalom shalom watu wa Mungu, amani ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja navyi kadri ya utukufu ulio juu yenu. Nawasalimu kwa jina la Mfalme wa wafalme, Bwana wa mabwana..... Bwana Yesu asifiwe. Ni hakika yangu mu wazima wa afya kiroho na kimwili. Namtukuza Mungu kwa kutupa nafasi nyingine ya kuweza kujifunza neno lake, utukufu una yeye milele na milele........ Amen

K**a ni mara yako ya kwanza kufuatilia somo hili, napenda nikujulishe kuwa hii ni sehemu ya nne na ya mwisho ya somo hili, tulianza sehemu ya kwanza, ya pili na ya tatu, kwa hiyo nakushauri fuatilia hapa hapa kwenye huu ukurasa utapata, soma tena na tena, ni somo muhimu sana litakusaidia kujenga uhusiano wako wa karibu sana na Mungu.

Katika sehemu zilizopita tuliweza kujifunza mambo 8 kati ya 12 ambayo yanaweza kukusaidia kuongeza nguvu ya kujibiwa kwa maombi yako. Tulijifunza kuhusu toba na utakaso, maana ya kuomba, muda, kuwa na neno, kuomba Mungu akupe masikio ya kusikia, kuombea mwili wako, kuomba upako wa kuomba na kuomba kwa Imani. Leo tutamalizia mambo 4 yaliyobaki.

9. ONGEZA NGUVU ITATENDAYO KAZI NDANI YAKO: Ukisoma Waefeso 3:20 utaona kitu cha ajabu pale. Mungu anasema “Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuwayazayo, na kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu.” Hapa Mungu anatuambia anajibu zaidi ya tunayoomba lakini pia anasema kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu. Hivyo moja ya njia ya kuongeza kujibiwa ni kuongeza nguvu ya Mungu ndani yako. Nguvu inayoongelewa ni upako wa Roho Mtakatifu kwani ndo nguvu pekee ambayo inatenda kazi ndani yetu. Ndo maana k**a unataka kuongeza nguvu katika maombi yako huwezi kukwepa kujua aina mbali mbali za upako wa Roho Mtakatifu za kukusaidia wewe.

10. MATEGEMEO: Unapoenda mbele za Mungu kuomba unategema nini? Lazima uwe na mategemeo fulani katika maombi yako. K**a hutegemi chochote kutoka kwa Mungu, kwa nini unaomba? Kuna mambo tunatakiwa kuyategemea tunapokuwa tunaomba lakini kuna mambo hatutakiwi kuyategemea. Tegemeo kubwa juu ya maombi ni kwamba “na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake” (1 Yohana 3:22). Kwa hiyo lazima tuzishike kwanza amri za Mungu. Pia katika maombi utegemee kupata maarifa na roho ya ufaham (Wakolosai 1:9). Kuna mambo mengi zaidi ambayo unaweza kutegemea kwenye maombi. Lakini pia kuna mambo ambayo usiyategemee.

Kwanza usitegemee tu kila kitu kitakuwa rahisi. Omba kwa imani lakini usitegemee kuwa kila kitu kitaenda kirahisi k**a unavyotaka wewe. “Kwa hiyo tulitaka kuja kwenu, naam, mimi Paulo, mara ya kwanza, na mara ya pili, na Shetani akatuzuia” (1 Wathesalonike 2:18). Daniel maombi yake yalizuiliwa siku 21 (Daniel 10:13). Kuna kipindi shetani anaweza kuzuia hivyo lazima ujue kuwa kuna wakati unapoomba unaenda kupambana. Uwe na imani ya kushinda lakini usiende kwa kutegemea kila kitu ni rahisi. Na level fulani ya maombi unatakiwa ku-bypass radar ya shetani. Njia mojawapo ni kunena kwa lugha (1 Wakorintho 14:2).

Pili usitegemee muujiza. Watu wengi wanapenda kuomba wakitegemea muujiza. Maandiko hayasemi tutaishi kwa muujiza bali kwa neno (Matayo 4:4). Sina maana kuwa maombi hayawezi kukuletea muujiza lakini usiwe unaenda mbele za Mungu kuomba kwa mategemeo ya muujiza. Miujiza ipo lakini kumbuka kila muujiza una sababu yake kuwepo na wakati wake kuwepo. Sababu na wakati wa kuwepo muujiza ikiondoka na muujiza huondoka (1 Waflme 17:14). Mungu mwenyewe anajua kipindi unahitaji muujiza. Hivyo mategemeo yako yasiwekwe kwenye muujiza bali yawekwe neno la Mungu. Kikubwa na cha msingi ni kwamba “twaenenda kwa imani, si kwa kuona” (2 Wakorintho 5:7).

11. PIMA NGUVU YA MAOMBI YAKO: Utajuaje k**a maombi yako yana nguvu au hayana? Nguvu ya maombi haipimwi kwenye muda ambao unautumia kuomba bali kwenye matunda unayoyapata unapoomba. Maandiko yanasema “kwa matunda yao mtawatambua” (Matayo 7:16). Kwa lugha nyingine nguvu ya maombi yako inapimwa kwenye ongezeko la imani yako. Maombi yanatakiwa yakuze imani yako kwa Kristo na imani yako inapokua hata kujibiwa kwako na kiwango cha maisha kinaongezeka.

Lakini kumbuka kuwa “tunaishi kwa imani”(Warumi 1:17) na wala “hatuishi kwa maombi.” Jinsi nguvu yako ya maombi inavyongezeka ndivyo kujibiwa kutaongezeka na utaweza kuomba kwa muda mrefu. Ila kumbuka urefu wa maombi siyo nguvu ya maombi. Nguvu ya maombi iliyoko ndani yako siyo nguvu yako ila ni nguvu ya Roho Mtakatifu ifanyayo kazi ndani yako. Unaweza kuomba maombi marefu yasiyo na nguvu na pia unaweza kuomba maombi mafupi yakawa na nguvu. Hii inategemea na nguvu itendayo kazi ndani yako.

12. MAOMBI YA KUFUNGA: Kuna level fulani ya maombi ambayo unahitaji kufunga na kuomba. Kuna mambo mengine ambayo Mungu hawezi kufanya mpaka umefunga na kuomba. “Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga” (Matayo 17:21). Maombi ya kufunga ni maombi ambayo yana nguvu sana. Unapofunga unatakiwa uombe Roho Mtakatifu akuongoze mambo gani ufunge. Wengi huwa wanafunga kwa kuunyima mwili chakula na maji. Kwa mfano mtu hali asubuhi mpaka jioni.

Lakini wakati mwingine unatakiwa uinyine nafsi pia na hapa ndo huwa pagumu. Nafsi inalishwa kwa kuhisi, kuona, kusikia, kuonja na kunusa. Kwa wengine kufunga kwenye nafsi ni kugumu zaidi ya kufunga kwa mwili. Kuna watu wengine anaweza kufunga chakula siku mbili bila shida ila hawezi kuacha kutumia simu, kuangalia TV, au kusikia mziki. Wakati mwingine unaweza kufunga kwa ajili ya nafsi pia kwani lengo kubwa la kufunga nikujinyima vile mwili na nafsi inahitaji ili kuilisha roho. Soma Isaya 58 juu ya kufunga. Kuna sababu nyingi mtu anaweza kufunga na chache ni hizi:

Kufunga ili kutafuta msaada na mwongozo wa Mungu (Ezra 8:21—23).

Kufunga ili Mungu asikie maombi kilio na maombi yako (Esther 14:6; Nehemia 1:4—11).

Kufunga ili ushinde majaribu (Matayo 4).

Kufunga ili kuwa na upako wa huduma (Matendo 13:3).

MUHIMU: Maombi ni muhimu sana katika maisha ya kila anayeamini. Lakini usijaribu kuishi kwa maombi ila hakikisha unaishi kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu (Matayo 4:4). Watu wengi wameweka imani yao katika maombi kuliko katika neno. Matokeo yake wanakua katika maombi lakini hawakui katika kumjua Kristo kupitia neno lake.

Maombi yana nafasi yake lakini muhimu zaidi hakikisha una neno ili uweze kujenga imani yako. Ukisoma misingi 12 ya imani utakuta maombi siyo moja ya msingi. Umewahi kujiuliza kwa nini watu wengi wanaweza kuomba kila siku lakini hawawezi kusoma neno kila siku? Umewahi kujiuliza kwa nini watu wengi wakiwa wanaumwa au wanashida kitu cha kwanza watasema ni “ninahitaji maombi.” Ni wachache watasema “ninaumwa ninahitaji neno.” Maandiko yanatuambia Mungu hutuma neno la uponyaji (Zaburi 107:20). Hivyo unavyozidi kuongeza nguvu yako katika kuomba, kumbuka kuwa tunaishi kwa neno na siyo kwa maombi.

Ni hakika yangu kuwa somo hili limekusaidia kujenga uhusiano wako wa kimaombi na Mungu. Usikose somo jingine wiki ijayo.

Mungu awabariki.

07/11/2018

SOMO: MAMBO 12 YANAYOWEZA KUKUSAIDIA KUONGEZA NGUVU YA KUJIBIWA KWA MAOMBI YAKO.

Sehemu ya Tatu

Na Mwl Ansbert Justus
+255759947276/+255716797470

Halleluyah watu wa Mungu. Nawasalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo aliyetukomboa kwa kuutoa uhai wake msalabani. Katika yeye tunaishi, tunakwenda na kuwa na uhai. Ni matumaini yangu kuwa mu wazima wa afya kiroho na kimwili. Basi jina lake libarikiwe, utukufu na heshima ni vyake nasi hatustahiri kugusa ata tone la ufalme wake....amen

Katika sehemu ya pili ya somo letu wiki iliyopita tulipata kujifunza mambo manne muhimu kati ya mambo kumi na mbili yanayoweza kukusaidia kuongeza nguvu ya kujibiwa kwa maombi yako, ambapo tulijifunza Toba na utakaso, kujua maana ya maombi, muda na kuwa na neno. K**a hukufanikiwa kujifunza, tafuta sehemu ya pili ya somo hili hapa hapa kwenye ukurasa utalipata, soma litakusaidia sana.

Leo nataka tujifunze mambo mengine manne muhimu pia yatakayokusaidia kuongeza nguvu za kujibiwa maombi yako;

5. OMBA MUNGU AKUPE MASIKIO YA KUSIKIA: Hiki kipengele kinaweza kuunganishwa na cha 4. Ili maombi yako yakue, unahitaji kuwa na neno la Kristo. Warumi 10:17 inasema “basi imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo.” Kwa hiyo muombe Mungu akupe masikio ya kusikia ili uweze kusikia sauti ya neno lake. Siongelei masikio ya nje bali masikia ya ndani ambayo yanasikia kile ulichosikia. Matayo 13:13 inasema “wakisikia hawasikii wala kuelewa.” Kwa hiyo unaweza kusikia na usisikie kile ulichosikia. Lakini ukimuomba Mungu akupatie masikio ya kusikia itaongeza neno la Mungu ndani yako na kufanya maombi yako yawe na nguvu.

6. JIFUNZE KUUOMBEA MWILI WAKO: Kuomba ni jambo la rohoni na Mungu wetu anapenda tuwe tunaomba. Kwa sababu mwili na roho mara zote vinapingana (Wagalatia 5:17), mwili hautaki kabisa maombi. K**a unabisha siku moja fanya jaribio hili: Andaa maombi ya saa moja halafu mpigie simu rafiki yako mpendwa na umwambie mambo yote unataka kumwambia Mungu. Utakuta unaweza kumwambia rafiki yako kwa muda wa saa moja bila kuchoka. Sasa chukua hayo maombi halafu nenda mbele za Mungu kwa lengo la kuomba, utaona mwili unakugomea. Kwa hiyo ili uweze kuwa na maombi effective, lazima uushinde kwanza mwili.

Maandiko yanasema “Basi ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana” (Warumi 12:1). Kumbuka dunia, mwili, na shetani vinafanya kazi pamoja katika utatu wa uovu kwa ajili ya kupinga chochote kile cha Mungu k**a kuomba. Hivyo kuwa na tabia ya kuuombea mwili wako kila siku. K**a unataka kuomba kwa saa moja, omba kwanza na kuukabidhi mwili wako kwa Mungu ili uweze kukubali maombi ya saa moja. Ukianza kuomba utaona mwili unakataa lakini unavyoendelea kuomba, eventually unaushinda na utashangaa unaomba kwa urahisi sana. Uombee mwili wako kila siku.

7. OMBA UPAKO WA KUOMBA: Maandiko yanasema Roho Mtakatifu ndiye anatusaidia kuomba (Watumi 8:26). Hivyo kila siku muombe Roho Mtakatifu akupe upako wa kukusaidia kuomba unapoanza kuomba. Hii ni sala ambayo unatakiwa uifanye kila siku kwani unahitaji Roho wa Mungu akusaidie katika maombi yako yote. Lakini unapoomba upako wa kuomba, muombe Roho Mtakatifu akuongoze kuomba katika kila kitu ili usiombe kwa tamaa zako, kitu ambacho kinaweza kumfanya Mungu asijibu maombi yako (Yakobo 4:3). Pia muombe Roho Mtakatifu akukumbushe neno (Yohana 14:26) la kukusaidia kuomba. Kumbuka kila unachotaka kufanya cha Mungu, kinahitaji upako wa Mungu. Wapendwa wengine huwa wanashindwa kuomba kutokana na kwamba wanajaribu kutumia nguvu zao kuomba.
8. OMBA KWA IMANI: Hiki ni kipengele muhimu kuliko vyote. Unapokuwa unaomba, weka imani yako kwa Yesu. Wengi wanaweka imani kwenye maombi, kwenye kupokea, kwenye kufunga, au kwenye kujibiwa. Unapoweka imani kwenye maombi halafu Mungu asipojibu, utaanza ku-question maombi yako. Na k**a upo kwenye kikundi cha maombi utaanza kujiuliza juu ya hicho kikundi cha maombi na wengine wanaweza kuhama kikundi. Maana yake wanatoa imani ya maombi kwenye kundi moja na kuihamisha kwenye kundi jingine. Hii ni kuwa na “imani kwenye maombi” na siyo “kuomba kwa imani.” Lakini ukiweka imani yako kwa Yesu na usipojibiwaa maombi yako utamuuliza Yesu shida ipo wapi na atakujibu kwa kukupa neno lake. “Kwa sababu hii nawaambia, yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” (Marko 11:24). Unaweza kutumia msitari huo kumuuliza Mungu kwa nini hujapokea kile umeomba wakati amekuahidi utapokea.

Usikose sehemu ya nne na ya mwisho ya somo hili jumamosi. Ni matumaini yangu umejifunza kitu katika mambo haya.

MUNGU AKUBARIKI.

03/11/2018

SOMO: MAMBO 12 YANAYOWEZA KUKUSAIDIA KUONGEZA NGUVU YA KUJIBIWA KWA MAOMBI YAKO.

Sehemu ya Pili

Na Mwl Ansbert Justus
+255759947276/+255716797470.

Bwana Yesu asifiwe watu wa Mungu. Nawasalimu kwa jina la Yesu Bwana wa utukufu. Kwa kufa kwake tunapata ondoleo la dhambi na kwa kufufuka kwake tunapata uzima tena tunakuwa nao milele. Hatuna jina lingine duniani wala mbinguni litupasalo kuokolewa kwalo isipokuwa jina la Yesu. Utukufu una yeye milele na milele..........Amina.

Katika sehemu ya kwanza ya somo letu la mambo 12 yanayoweza kukusaidia kuongeza nguvu ya kujibiwa maombi yako tuliona utangulizi, tuliweza kujifunza nini maana ya maombi, tukaona pia kuwa maombi yanaboresha uhusiano baina yako na Mungu, pia tukapata kujifunza kuwa kutokuomba ni dhambi halisi.

Leo nataka tuanze kujifunza mambo hayo 12 yanayoweza kukusaidia kuongeza nguvu ya kujibiwa maombi yako;

1. TOBA NA UTAKASO: Kablda ya kuanza kuomba, omba toba kwa ajili yako na yule unamuombea, jisafishe kwa Damu ya Yesu Kristo, na pia takasa eneo ambalo unaomba na kulikomboa katika ulimwengu wa roho. Nguvu yako ya kuomba inaweza kutegemea eneo ulipo. Hujawahi kuona kuna maeneo unaweza kuomba vizuri lakini kuna maeneo zingine ukishaenda nguvu ya kuomba haipo. Wengine akiwa kwenye kikundi cha maombi kanisani anakuwa na nguvu sana ya kuomba lakini akishafika nyumbani, nguvu yote inaisha. Unadhani shida ipo wapi? Eneo ni muhimu sana katika ulimwengu wa roho.

2. IJUE MAANA YA KUOMBA: Kuomba ni njia mojawapo ya kuzungumza na Mungu wetu. Unapomuita Mungu kwa kuomba anakusikiliza (Yeremia 29:12). “BWANA yu karibu kwa wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu”(Zaburi 145:18). Na njia mojawapo ya kumwita Mungu ni kwa njia ya maombi. “Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua”(Yeremia 33:3). Neno “mambo usiyoyajua” tukiliangalia kwa undani tunaona ni “mafunuo ya Mungu.” Kwa hiyo kuomba kunamfanya Mungu akupe mafunuo(revelation). Hivyo dumu katika kuomba (Wakolosai 4:2) kwani maombi ya mwenye haki yana nguvu (Yakobo 5:16).

3. MUDA: Muda/wakati ni muhimu sana katika ulimwengu wa roho hasa katika kuomba. Waefeso 5:16 inasema “tuukomboe wakati.” Maana yake wakati umetekwa na ibilisi. Moja ya silaha ambazo shetani anatumia kuua maombi ni kutumia muda. Akiweza kuuteka muda wako ameuwa maombi yako. Shetani alitumia sheria kujaribu kufunga muda wa maombi kwa kina Daniel siku 30 (Daniel 4). Kwa kuwa sheria sasa imeandikwa katika mioyo yetu Waebrania 10:16), muda unafungwa katika ulimwengu wa roho na matokeo yanatokea katika mwili.

Kuna watu ambao katika ulimwengu wa roho, shetani amefunga muda wao labda masaa 23 kwa siku. Maana yake katika siku huwezi kufanya maombi zaidi ya saa moja. Pia wengine muda wao umefungwa masaa 23 na dakika 45. Maana yake huwezi kuomba effectively zaidi ya dakika 15. Dakika 15 za mwanzo utaomba vizuri ila zikianza kuzidi, utaanza kupata uzito wa ajabu. Na kuna watu muda wao wa kuomba umefungwa masaa 24 kwa siku. Kwa huyu mtu hata kuomba dakika 5 ni kazi na ukianza tu kuomba, hapo hapo unaanza kusikia uzito. Kumbuka muda unafungwa katika ulimwengu wa roho, hivyo ukitaka kuukomboa, lazima uukomboe katika ulimwengu wa roho.

Na ukianza kufanya maombi ya kukomboa wakati sawa na Waefeso 5:16, shetani atakupiga vita. Lakini unaweza kuanza kukomboa kidogo kidogo. Mfano unashangaa ulikuwa huwezi kuomba nusu saa sasa unaweza. Baadae unaenda unaweza kuomba saa moja na kuendelea. K**a ulikuwa huwezi kuomba hata dakika 5 ni vigumu kuanza ghafla tu uweze kuomba kwa masaa 3 mfululizo. Maombi ya kuukomboa wakati ni maombi ya kufanya mara kwa mara.

4. KUWA NA NENO: Moja ya maombi ambayo yana nguvu sana ni maombi kwa kutumia neno la Mungu kwa imani. Unapokuwa unaomba kutumia neno la Mungu unamkumbusha Mungu kuwa yeye ni nani kwako. Neno la Mungu ni agano amefunga na wewe hivyo ukitumia neno unamkumbusha Mungu juu ya agano alilofunga na wewe. Mfano k**a unahitaji uponyaji, unaweza kutumia mistari k**a “kwa kupigwa kwake sisi tumepona” (Isaya 53:5) kwa imani. Mistari ya biblia itabaki k**a mistari usipopata mafunuo kutoka kwa Roho Mtakatifu.

Unapotoa neno k**a hilo kwa imani unampa Mungu kuachilia neno na kukujibu. “Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao” (Zaburi 107:20). Kwa hiyo unapomuomba Mungu kitu fulani hakupi hicho kitu ila anakupa neno lilibeba hicho kitu. Mfano ukiomba uponyaji anakupa neno lilibeba uponyaji na imani yako inakupa kupokea. Ukimuomba hela hakupi hela ila neno ambalo limebeba maarifa ya kupata hela. Ndo maana ni muhimu sana kuwa na neno la Mungu kwani yeye hujibu kwa kutumia neno. K**a huna neno Mungu anaweza kukujibu na usilione jibu lake.

Usikose sehemu ya tatu ya somo hili jumatano ijayo ambapo tutaendelea na jambo la tano. Ni matumaini yangu umepata jambo la kukujenga kupitia mambo haya manne.

Mungu akubariki.

Address

Kinondoni Dar
Dar Es Salaam
011

Telephone

255759947276

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Utukufu Life Ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share