18/11/2022
WAZA JAMBO HILI
K**a ni kwa lugha ya Kiingereza, basi mtu angeweza kusema “Imagine this”.
Wakati wa kuzaliwa kwako, katika chumba cha kuzalia kulifanyika kosa la kukubadilisha wewe na kichanga kingine. Ni kwa kiasi gani maisha yako yangekuwa tofauti na yalivyo sasa? Ingekuaje k**a familia uliyopelekwa kimakosa ni familia ya kimaskini sana, ama familia uliyopelekwa kimakosa ni familia tajiri sana.
Ni kwa kiasi gani kosa hilo lingeathiri maendeleo yako katika shule uliyopelekwa kujifunza? Lingeathiri huduma za kiafya ambazo ungekuwa unapatiwa? Uwezekano wa miito yako ya kazi baada ya kuhitimu mafunzo yote uliyopitia?
Endapo ungekuwa umelelewa katika dini tofauti, ama dhehebu tofauti la dini uliyopo sasa, jambo hilo lingeathiri kwa namna gani Imani yako, desturi yako, na mtazamo wako? Lakini ebu fikiria tena Zaidi, ingekuaje k**a ungezaliwa katika jinsi tofauti na uliyo nayo sasa, au utaifa ulionao sasa?
Naamini kwa kusoma maelezo hayo hapo juu, umeweza kubaini jambo, lakini lengo la maelezo yote hayo ni kuonesha aina ya stadi inayotumika kuisoma jamii ya watu. Somo maalum linaitwa SOSHOLOJIA, ni somo ambalo limejikita katika namna ya kubadili ukweli alionao mtu kuhusu jamii au watu wengine anaokutana nao katika maisha yake.
Kubadili kwa namna njema kile alichokuwa nacho mawazoni, kuhusu familia yake, nafasi yake katika jamii, elimu yake, dini yake, jinsi, na utaifa wake. Kila kimoja kina mchango mkubwa sana katika kukuunda vile ulivyo sasa.
ELIMU HAINA MWISHO, KILA SIKU YAFAA KUENDELEA KUJIFUNZA, HATA KWA KUSOMA MAKALA ZIANDIKWAZO KATIKA MITANDAO YA KIJAMII.
Credit: Mwal. Adrian kansela Mkoba.