Efatha Ministry Matosa

Efatha Ministry Matosa This is officially Facebook account for Efatha Church Matosa. Karibu ukutane na Uponyaji na Ukombozi kwa Damu ya Yesu. YESU ANAKUPENDA.

Safari hii kila utakachoomba kwa MUNGU unakwenda kupolea katika jina la YESU
12/05/2026

Safari hii kila utakachoomba kwa MUNGU unakwenda kupolea katika jina la YESU

MATUKIO KATIKA PICHA IBADA YA MFUNGO LEO JUMATATU YA TAREHE 11/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA DAR ES SALA...
11/05/2026

MATUKIO KATIKA PICHA IBADA YA MFUNGO LEO JUMATATU YA TAREHE 11/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA DAR ES SALAAM TANZANIA.

MAOMBI- Bwana Yesu naomba unisamehe pale ambapo tulijijari wenyewe na hatukujari wengine, naomba utupe roho ya umoja na ...
11/05/2026

MAOMBI

- Bwana Yesu naomba unisamehe pale ambapo tulijijari wenyewe na hatukujari wengine, naomba utupe roho ya umoja na wengine.

- Bwana Yesu nami natangaza msamaha kwa yote alienikwaza ninamsamehe Bwana

- Bwana Yesu naomba uniumbie roho ya Kujali wengine kuliko hata ninavyojijali mimi naomba uniumbie roho ya umoja jambo linalompata mwingine liwe langu

- Kila tabia iwe ya kurithi au kujifunza inayofanya niwa dharau wengine nina itoa leo toka ndani yangu

- Bwana Yesu popote waliposimama wanaotaka nijitenge na watakatifu wako nawapinga katika Jina la Yesu k**a wanapita usiku au mchana hatawano nena juu ya afya yangu nawapinga

- Bwana Yesu mjumbe yoyote anakuja kinyume kwe Biashara, watoto, Shambani, kazini kwangu anaeachia hofu mbaya kabla afike namtengua

- Bwana Yesu wale wajumbe wema popote walipo dhuhiliwa naondoa hicho kizuizi popote ulipo watuma ili waje nyumbani mwangu hapa kanisani naondoa hiyo vizuizi

IBADA YA MFUNGO LEO JUMATATU YA TAREHE 11/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA DAR ES SALAAM TANZANIA.

SOMO: UMOJAWafilipi 2:2 - 4 "ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia ...
11/05/2026

SOMO: UMOJA

Wafilipi 2:2 - 4 "ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja. Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine."

Mwili unatunzwa na mwenywe Mwili na mwenye Mwili ni Kristo kwahiyo anae umilki ni kristo.

Kanisa sio mali ya mwanadamu kanisa ni mali ya Kristo ni Mwili wa Kristo. Anaetunza Mwili huo
Anaekupa chakula, anaekupa mavazi, anaekupa vitu ni kristo.

Mwili ili uwe Kamili una viungo mbalimbali ambavyo vinaufanya Mwili uwe kamili.
Unakuta mtu amepewa Uwezo wa kuona mambo ya rohoni mwingine anaweza kuwa sikio kusikia mambo ya rohoni.

Mwili wa kristo umeumbwa katika umoja hivyo tukiwa hapa Kanisani tunatakiwa tuwe na umoja pasiwe na mabishano tunatakiwa tuwe katika nia moja na Kwa umoja.

Wakolosai 3:10 - 12 "Mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba. Hapo hapana Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, mgeni wala mshenzi, mtumwa wala mwungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote.Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba."

Mungu anatutaka tuamke ili ule wokovu ambao yesu alitupa uwe halisi na ndipo ibada yako ya maombi inakuwa na maana kwa kutofanya yale yote ambao bwana amekataza.

Utampendeza Mungu k**a ukifanya mambo yake na sio kudili na mambo ya wengine.

Unyenyekevu unakufanya umuelewe mtu
Unyenyekevu sio unyonge ni kufanya vitu kwa usahihi sawa sawa neno linavyosema
Unyenyekevu ni kuangalia kile Mungu anasema
Unyenyekevu ni kufanya kwa usahihi nakufuata maagizo ya Bwana

Kuna gharama yakulipa ili kupata nguvu ya Mungu lakini ukilipa faida ni yako maana wale wanaomcha Bwana wanatimiza siku zao.

IBADA YA MFUNGO LEO JUMATATU YA TAREHE 11/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA DAR ES SALAAM TANZANIA.

11/05/2026

Zaburi 29:2 "Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu."

Nakutamkia leo kwajina la Yesu kila kitu ambacho MUNGU anataka usikie kwaajili ya ubadae wako mwema basi ukasiki adui sh...
11/05/2026

Nakutamkia leo kwajina la Yesu kila kitu ambacho MUNGU anataka usikie kwaajili ya ubadae wako mwema basi ukasiki adui shetana asizuie kusikia kwako na kutenda kwako kwa jina la YESU

MATUKIO KATIKA PICHA IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 10/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA  DAR ES SALAAM.
10/05/2026

MATUKIO KATIKA PICHA IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 10/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA DAR ES SALAAM.

SOMO: KUJITAMBUA  Zaburi 139:14 "Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajab...
10/05/2026

SOMO: KUJITAMBUA

Zaburi 139:14 "Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, Na nafsi yangu yajua sana,"

KUJITAMBUA NI NINI?
Kujitambua ni namna ya kujua kuwa wewe ni nani mbele za Mungu,kusudi lake, duniani na namna anavyo paswa kuishi kulingana na mapenzi ya Mungu.

Ukijitambua kuwa wewe ni nani Mbele za watu na mbele za Mungu hakuna mtu yeyote ataye kudhalau katika hali yoyote wala hakuna mazingira ya aina yoyote yatakayo kurudisha nyuma, kwasababu sisi tumeubwa kwa namna ya ajabu.

Usipo jitambua huwezi kuendelea katika mipango yako.

Kitu kibaya katika safari ya wokovu ni kutokujitambua, kwasababu usipo jitambua wokovu wako hauwezi kukua bali utaishia kudumaa siku zote.ili uweze kusonga mbele na wokovu wako uwe ni wa hushuuda ni lazima ukubali KUJITAMBUA.

MCHUNGAJI: ANDREW SANGA

IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 10/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA DAR ES SALAAM.

Naitwa CONSOLATH KIMARONipo mbele yenu kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya mtoto. Kwa muda wa miaka 10 ndani ya ...
10/05/2026

Naitwa CONSOLATH KIMARO
Nipo mbele yenu kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya mtoto. Kwa muda wa miaka 10 ndani ya ndoa yangu nilikuwa sijapata mtoto.

Siku moja kwenye Ibada ya live Mtume na nabii Josephat Mwingira alisema "Nawatuma wachungaji kwenye vituo vyenu muwapokee k**a Yesu kwenye vituo vyenu."

Wakati Mchungaji alipokuwa analetwa katika kanisa hili, niliandika maombi yangu matano nikimuomba Mungu anitendee. Nilisema moyoni mwangu kuwa, “Mchungaji anayekuja amebeba vilivyo vya kwangu, na lazima nivipokee.” na Mchungaji alipofika, alinipa jukumu la kuwa kiongozi wa kiroho. Kwa kweli nilihisi sitaweza kabisa, lakini nilikubali kujigharimu, kwa sababu nilitambua kuwa kila kitu unachokitaka maishani kinahitaji gharama.

Moja ya maombi yangu ilikuwa Mungu anipe kilicho cha kwangu. Nilipewa jukumu la kuongoza ibada ya asubuhi siku ya Jumanne. Kwa kuwa siku hiyo ilikuwa ni siku ya familia, nilimuomba Mungu afanyike baraka katika familia yangu.

Kuna siku nilipokuwa naongoza maombi, nilisikia sauti ikisema, “Tayari wewe ni mjamzito.” Nilipoenda kupima, majibu yalionyesha kuwa kweli nilikuwa mjamzito.

Haikuwa rahisi, kwa sababu hapo mwanzo madaktari waliniambia kuwa siwezi kubeba mimba. Lakini Mungu ameonyesha ukuu wake, na hatimaye leo nimebarikiwa kupata mtoto wa kiume.

IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 10/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA DAR ES SALAAM

UTANGULIZIWafilipi 4:4 "Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini."MTUMISHI: CALORINA NJAUIBADA YA JUMAPILI ...
10/05/2026

UTANGULIZI
Wafilipi 4:4 "Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini."

MTUMISHI: CALORINA NJAU

IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 10/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA DAR ES SALAAM TANZANIA.

1 Yohana 5:14 – "Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia."IBADA Y...
10/05/2026

1 Yohana 5:14 – "Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia."

IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 10/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA DAR ES SALAAM.

Address

Kimara Matosa Michungwani
Dar Es Salaam
....

Telephone

+255762937811

Website

Church Matosa?mibextid=ZbWKwL

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Ministry Matosa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share