11/05/2026
SOMO: UMOJA
Wafilipi 2:2 - 4 "ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja. Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine."
Mwili unatunzwa na mwenywe Mwili na mwenye Mwili ni Kristo kwahiyo anae umilki ni kristo.
Kanisa sio mali ya mwanadamu kanisa ni mali ya Kristo ni Mwili wa Kristo. Anaetunza Mwili huo
Anaekupa chakula, anaekupa mavazi, anaekupa vitu ni kristo.
Mwili ili uwe Kamili una viungo mbalimbali ambavyo vinaufanya Mwili uwe kamili.
Unakuta mtu amepewa Uwezo wa kuona mambo ya rohoni mwingine anaweza kuwa sikio kusikia mambo ya rohoni.
Mwili wa kristo umeumbwa katika umoja hivyo tukiwa hapa Kanisani tunatakiwa tuwe na umoja pasiwe na mabishano tunatakiwa tuwe katika nia moja na Kwa umoja.
Wakolosai 3:10 - 12 "Mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba. Hapo hapana Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, mgeni wala mshenzi, mtumwa wala mwungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote.Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba."
Mungu anatutaka tuamke ili ule wokovu ambao yesu alitupa uwe halisi na ndipo ibada yako ya maombi inakuwa na maana kwa kutofanya yale yote ambao bwana amekataza.
Utampendeza Mungu k**a ukifanya mambo yake na sio kudili na mambo ya wengine.
Unyenyekevu unakufanya umuelewe mtu
Unyenyekevu sio unyonge ni kufanya vitu kwa usahihi sawa sawa neno linavyosema
Unyenyekevu ni kuangalia kile Mungu anasema
Unyenyekevu ni kufanya kwa usahihi nakufuata maagizo ya Bwana
Kuna gharama yakulipa ili kupata nguvu ya Mungu lakini ukilipa faida ni yako maana wale wanaomcha Bwana wanatimiza siku zao.
IBADA YA MFUNGO LEO JUMATATU YA TAREHE 11/05/2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MATOSA KIMARA DAR ES SALAAM TANZANIA.