City Light Temple - CLT

City Light Temple - CLT Called to shine in the Darkness. Maarifa sahihi ni uhuru wa mtu, maangamizi yetu ni ujinga tulionao

Rev.Dr Mulenda Omary akimkaribisha mtumishi Yohana Madadi kwa neno
11/05/2026

Rev.Dr Mulenda Omary akimkaribisha mtumishi Yohana Madadi kwa neno

 Tunainama si kwa sababu ya udhaifu, bali kwa heshima ya uwepo wa Mungu
10/05/2026


Tunainama si kwa sababu ya udhaifu, bali kwa heshima ya uwepo wa Mungu

 Kila pumzi ni sababu ya kumsifu Bwana 💙
10/05/2026


Kila pumzi ni sababu ya kumsifu Bwana 💙

  Tunaimba kwa ajili ya utukufu wa Mungu ✨
10/05/2026


Tunaimba kwa ajili ya utukufu wa Mungu ✨

03/05/2026
Heri ya siku ya kuzaliwa, Mchungaji Rev. Dr. Mulenda Omary! Tunakushukuru kwa uongozi wako wa kiroho na moyo wako wa kuj...
03/05/2026

Heri ya siku ya kuzaliwa, Mchungaji Rev. Dr. Mulenda Omary! Tunakushukuru kwa uongozi wako wa kiroho na moyo wako wa kujitoa. Mungu aendelee kukuinua, akujalie afya njema na kukuzidishia hekima katika kila hatua ya huduma yako. Baraka tele juu yako leo na siku zote! 🎉🙏

Hongera ya siku ya kuzaliwa, Mchungaji Rev. Dr. Mulenda Omary! Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai wako na huduma yako...
03/05/2026

Hongera ya siku ya kuzaliwa, Mchungaji Rev. Dr. Mulenda Omary! Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai wako na huduma yako yenye baraka kubwa. Umeendelea kuwa mwanga na nguzo ya imani kwa wengi. Tunaomba Mungu akupe afya njema, hekima zaidi, na neema tele ili uendelee kutumika kwa utukufu wake. Miaka mingi yenye baraka na mafanikio! 🙏🎉

Mungu akuzidishie nguvu na akuinua zaidi katika huduma yako. Heri ya kuzaliwa!

IDARA YA CMF IKIWATEGEMEZA WACHUNGAJI KWA KUJITOA KUMTUMIKIA MUNGU
03/05/2026

IDARA YA CMF IKIWATEGEMEZA WACHUNGAJI KWA KUJITOA KUMTUMIKIA MUNGU

SOMO:NI WAKATI WA KUREJESHA VYOTE1samwel 30-1:191 Ikawa, Daudi na watu wake walipokuwa wamefika Siklagi siku ya tatu, ha...
03/05/2026

SOMO:NI WAKATI WA KUREJESHA VYOTE
1samwel 30-1:19

1 Ikawa, Daudi na watu wake walipokuwa wamefika Siklagi siku ya tatu, hao Waamaleki walikuwa wameshambulia Negebu, na Siklagi, nao wameupiga Siklagi, na kuuchoma moto;
2 nao wamewachukua mateka wanawake waliokuwamo wakubwa kwa wadogo; hawakuwaua wo wote, ila wakawachukua, wakaenda zao.
3 Basi Daudi na watu wake walipoufikilia mji, tazama, ulikuwa umechomwa moto; na wake zao, na watoto wao, waume kwa wake, wamechukuliwa mateka.
4 Ndipo Daudi na watu waliokuwa pamoja naye wakainua sauti zao na kulia, hata walipokuwa hawana nguvu za kulia tena.
5 Na hao wake wawili wa Daudi walikuwa wamechukuliwa mateka, Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, aliyekuwa mkewe Nabali, wa Karmeli.
6 Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.
7 Kisha Daudi akamwambia Abiathari, kuhani, mwana wa Ahimeleki, Tafadhali niletee hapa hiyo naivera. Naye Abiathari akamletea Daudi naivera huko.
8 Daudi akauliza kwa Bwana, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote.
9 Basi Daudi akaenda, yeye na wale watu mia sita waliokuwa pamoja naye, nao wakakifikilia kijito Besori, ambapo wale walioachwa nyuma walikaa.
10 Lakini Daudi akakaza kufuata, yeye na watu mia nne; kwa maana watu mia mbili walikaa nyuma, ambao walitaka kuzimia hata hawakuweza kukivuka hicho kijito Besori.
11 Nao wakamkuta Mmisri mavueni, wakamleta kwa Daudi, na kumpa chakula, naye akala; nao wakampa maji ya kunywa;
12 kisha wakampa kipande cha mkate wa tini, na vishada viwili vya zabibu; naye akiisha kula roho yake ikamrudia; kwa maana alikuwa hakula chakula wala kunywa maji, siku tatu mchana na usiku.
13 Ndipo Daudi akamwuliza, Wewe u mtu wa nani; nawe umetoka wapi? Naye akasema, Mimi ni kijana wa Misri, mtumwa wa Mwamaleki mmoja; bwana wangu aliniacha, kwa sababu tangu siku hizi tatu nalishikwa na ugonjwa.
14 Sisi tulishambulia Negebu ya Wakerethi, na ya milki ya Yuda, na Negebu ya Kalebu; na huo mji wa Siklagi tukauchoma moto.
15 Daudi akamwambia, Je! Wewe utaniongoza chini hata nilifikilie jeshi hilo? Naye akasema, Uniapie kwa Mungu, ya kwamba hutaniua, wala kunitia mikononi mwa huyo bwana wangu, nami nitakuongoza chini hata kulifikilia jeshi hilo.
16 Na hapo alipokuwa amewaongoza chini, tazama, hao walikuwa wametawanyika juu ya nchi yote, wakila na kunywa, na kufanya karamu, kwa sababu ya hizo nyara kubwa walizochukua katika nchi ya Wafilisti, na katika nchi ya Yuda.
17 Naye Daudi akawapiga tangu ukungu wa jioni hata jioni ya siku ya pili; hakuna aliyeokoka, ila vijana mia nne waliopanda ngamia na kukimbia.
18 Daudi akawapokonya wote waliokuwa wamechukuliwa na Waamaleki; naye Daudi akawaokoa wakeze wawili.
19 Wala hawakupotewa na kitu, mdogo wala mkubwa, wana wala binti, nyara wala cho chote walichojitwalia hao; Daudi akavirudisha vyote.

Mchungaji REV.DR MULENDA OMARY akimkabizi madhabau DKT. YOTHAM MACKENZIE kwa neno
03/05/2026

Mchungaji REV.DR MULENDA OMARY akimkabizi madhabau DKT. YOTHAM MACKENZIE kwa neno

Address

Goba, Matosa
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 17:00 - 18:30
Wednesday 16:30 - 18:30
Friday 16:30 - 18:30
Sunday 06:30 - 12:30

Telephone

+255673280229

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when City Light Temple - CLT posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share