03/12/2024
LEO DISEMBA 3 TUNAYAKUMBUKA MAISHA YA MTAKATIFU FRANSISKO KSAVERI, PADRE(1552)
Fransisko Ksaveri alizaliwa Hispania Mwaka 1506 na Wazazi wa Ukoo bora.
K**a angalitaka angaliwaza kujipatia ukuu mbele za watu lakini siku moja, alipokuwa akisoma huko Paris (Ufaransa) Mtakatifu Inyasi wa Loyola (tunayemkumbuka 31 Julai) alimwambia Ksaveri, Ksaveri, yafaa nini kwa mtu kupata ulimwengu wote akipoteza roho yake?.
Baada ya siku za Mafungo Ksaveri na Mtakatifu Inyasi pamoja na wenzake watano Wayesuiti wakafunga Nadhiri ya kwenda katika nchi Takatifu ili kuwatunza Wakristo waliokuwa wakilalama utumwani wa Waislamu, kwa kuwa hawakufaulu kwenda huko badala yake walisafiri kwenda Roma (Italia) wakaonane na Papa ili afanye nao jinsi apendavyo pale Italia, Ksaveri alipewa Upadre Mwaka 1537.
Mwaka 1540, Inyasi na Ksaveri walikuwa Roma kwa Kupewa Kibali rasmi cha Shirika lao Jipya, zamani hizo Mfalme wa Ureno alimwomba Mtakatifu Inyasi apeleke Mapadre wa Shirika lake Kuhubiri Injili katika India.
Fransisko Ksaveri akatumwa kwenda huko pamoja na Mapadre wawili wengine katika Mwaka 1541 Alijipakia na kushuka baada ya miezi kumi na mitatu, katika pwani ya Goa(India)huko Fransisko aliizungukia nchi yote akiwakusanya Watoto na Watumwa ili waje kufundishwa naye Katekisimu akisaidiwa na mkalimali.
Watu wengi hawakukawia kuongoka Miaka miwili baadaye alihamia sehemu ya kusini ya India akiwafundisha hasa Wavuvi wa Pwani na Visiwani dini ya Yesu Kristo, alitenda miujiza mingi hata aliwafufua watu wange na walipoona mwujiza huo walitaka kubatizwa.
Baada ya kuwapatia wenyeji wa huko Mapadre alisafiri tena akafika katika Ufalme wa Trevankor (srilanka) dini katika visiwa vya Moluk, Amboins na Ternate akapata Wakristo wapya wengi alitengeneza Katekisimu ndogo katika lugha ya Ki-Malayan.
Mwaka 1549 alishuka katika Pwani ya Japan ambamo alikaa kwa muda wa miaka miwili, makasisi wao walimchongea kwa Mfalme na hatimaye wakamfukuza katika nchi yao alirudi Goa lakini hakukaa sana, kwani alitamani kupeleka Injili katika nchi ya china.
Alipofika Kisiwani Sanchian akaugua, wakamwacha huko Mreno mmoja alimhurumia akampokea kibandani mwake alikufa Disemba 2, mwaka 1552 katika kisiwa cha sanchian huko china katika muda wa miaka kumi mmisionari huyu aliwabatiza watu wengi ajabu miezi miwili na nusu baada ya kufa kwake waliukuta mwili wake haujaoza bado, ingawa alizikwa katika chokaa isiyozimka kusudi upate kuteketea upesi, ukapelekwa kwa heshima kubwa huko Goa (India) ambako umehifadhiwa hadi hii leo.
Nirahisi kuzitaja na kuziorodhesha nchi alizokuwa amefanya kazi, bali siyo rahisi sana kupata picha halisi ya uzito wa shughuli zile nyingi alizozifanya wakati wa miaka ile kumi na mmoja tangu aondoke Ulaya, mbali na safari mbili za kwenda Japan kutoka India na baadaye kuvuka bahari kuelekea kisiwa cha Sanchian alizifanya safari zake kwa miguu akitembea kilometa nyingi katika hali ya uchovu, Ugonjwa, ugumu wa kazi na kadhalika kweli Mtakatifu Fransisko alikuwa ni mtu hodari sana aliyesukumwa na Upendo wake kwa Bwana ili utawala wake uzidi kuenea mioyoni mwa watu na watu wengi zaidi wapate kumpenda na Kumtumikia.
Katika Barua mojawapo aliyomwandikia mkuu wake Mtakatifu Inyasi alisema Tangu nifike hapa sijapumzika nimekitembelea kila Kijiji nikawaosha Watoto wote wasiobatizwa bado kwa maji Matakatifu hivyo kuna Idadi kubwa sana ya Watoto niliwaondolea dhambi ya asili Watoto hawaniachii nafasi ya kusali breviary kula usingizi kabla ya kuwafundisha.
Lakini walau sala fulani hapo nimepata kungโamua kwamba Ufalme wa mbinguni ni kwa ajili ya hao,
Mtakatifu Fransisko Ksaveri alitajwa Mtakatifu Mwaka 1622 na Mwaka 1927 aliwekwa kuwa Mlinzi wa Wamisionari popote Duniani siku ya leo yafaa sana kuwaombea kwa maombezi ya Mtakatifu Fransiko Ksaveri wale wote wenye kujitahidi kulitangaza kwa namna yoyote ili neno la Mungu.
MTAKATIFU FRANSISKO KSAVERI PADRE UTUOMBEE.