Scripture Union Tanzania

Scripture Union Tanzania SERVING CHILDREN,YOUTH TO TRANSFORM FAMILIES AND WHOLE COMMUNITY

Masomo ya maadili yameanza rasmi kufundishwa katika Shule ya Sekondari Iyunga, yakiwa na lengo la kuwalea wanafunzi kati...
21/05/2026

Masomo ya maadili yameanza rasmi kufundishwa katika Shule ya Sekondari Iyunga, yakiwa na lengo la kuwalea wanafunzi katika misingi ya tabia njema, heshima, uwajibikaji, na kumcha Mungu.

Somo la kwanza lililofundishwa ni usafi, likigusa usafi wa mwili, mazingira, pamoja na usafi wa rohoni ili kuwajenga wanafunzi kuwa na maisha safi ndani na nje.

Tunapoishi katika usafi wa mwili na rohoni, tunajenga jamii yenye afya, amani, na maadili mema.




Mwendelezo wa huduma mashuleni Katika Shule ya Sekondari Forest. Tunaamini katika kumlea mwanafunzi kwa ukamilifu kimwil...
20/05/2026

Mwendelezo wa huduma mashuleni Katika Shule ya Sekondari Forest.

Tunaamini katika kumlea mwanafunzi kwa ukamilifu kimwili, kiakili, na kiroho. Somo la usafi limetukumbusha ukweli mmoja mkubwa: Maji na sabuni husafisha mwili, lakini toba, upendo, na neno la Mungu husafisha roho.

​Haina maana kuwa nadhifu kwa nje ikiwa ndani kuna chuki au kinyongo. Sote kwa pamoja tujitahidi kung'aa kwa nje na kutakata kwa ndani ili maisha yetu yawe dhabihu inayompendeza Mungu na jamii inayotuzunguka.




Katika Shule ya ST Merry Secondary school tulipata nafasi ya kufundisha somo la usafi likilenga si tu mazingira na miili...
20/05/2026

Katika Shule ya ST Merry Secondary school tulipata nafasi ya kufundisha somo la usafi likilenga si tu mazingira na miili yetu, bali pia usafi wa kiroho mbele za Mungu.

Usafi wa mwili hutulinda dhidi ya magonjwa na hutuwezesha kujifunza kwa bidii, lakini usafi wa kiroho hututengeneza kuwa na mioyo safi, tabia njema, na uhusiano mzuri na Mungu na wengine.

Tukumbuke: mwili safi + moyo safi = maisha yenye baraka na mafanikio.

Tujitahidi kuwa mfano wa usafi kila siku katika vitendo, mawazo, na roho zetu.



Sifa na utukufu ni kwa Bwana Yesu Kristo kwa neema yake kuu aliyemtumia MCH. Samweli pamoja na mke wake kuhubiri na kufa...
20/05/2026

Sifa na utukufu ni kwa Bwana Yesu Kristo kwa neema yake kuu aliyemtumia MCH. Samweli pamoja na mke wake kuhubiri na kufanya ibada yenye baraka katika Shule ya Sekondari Mwasanga.

Katika ibada hiyo, wanafunzi zaidi ya 23 walimpokea Yesu Kristo k**a Bwana na Mwokozi wa maisha yao. Tunamshukuru Mungu kwa mavuno haya makubwa ya roho.

Pia tunatoa shukrani za dhati kwa Mkuu wa Shule kwa moyo wake wa kipekee wa kuipa nafasi kazi ya Mungu. Hakika Mungu akubariki sana.

Kupitia kulisikia Neno la Mungu, wanafunzi wa imani zote wanapata mwongozo unaowaleta kwenye mabadiliko ya kweli ya tabi...
15/05/2026

Kupitia kulisikia Neno la Mungu, wanafunzi wa imani zote wanapata mwongozo unaowaleta kwenye mabadiliko ya kweli ya tabia na mwenendo.

Neno hili linawajengea msingi imara wa maadili na ujasiri wa kusimama kwenye haki na kushinda kila vishawishi vya ujana.

​Ungana nasi tunapozifikia shule zetu na kugusa mioyo ya vijana kwa ujumbe wa amani na tumaini.




14/05/2026

Watoto wa Shule ya Msingi Amani wakiabudu Mungu kwa moyo wote, wakiwa wadogo bado. Ni baraka kuwaona wakikua katika imani.
Hakika ni baraka kuwaona wakikua katika kumjua Mungu tangu wakiwa wadogo.



14/05/2026

Katika Shule ya Msingi Amani watoto wakiwa kwenye ibada wakijifunza somo la "Usafi hufikiri mawazo mazuri"




Tunamrudishia sifa, utukufu na heshima Mungu Pekee yake kwa neema na ulinzi wake unaoendelea katika huduma ya kuwafikia ...
13/05/2026

Tunamrudishia sifa, utukufu na heshima Mungu Pekee yake kwa neema na ulinzi wake unaoendelea katika huduma ya kuwafikia watoto kwa mafundisho yenye kujenga maisha yao ya kila siku.

Tulipata nafasi ya kuwa katika Shule ya Msingi Amani tukifundisha masomo ya maadili, ambapo somo lililofundishwa lilikuwa “Usafi hufikiri mawazo mazuri.”

Tunaamini kuwa kupitia mafundisho haya watoto wataendelea kukua katika maadili mema, usafi na fikra chanya kwa ajili ya maisha yao ya sasa na ya baadaye. Tuendelee kuwaombea watoto hawa pamoja na kuiombea huduma ya SU ili Mungu azidi kuitumia kuleta mabadiliko mema katika jamii.




Scripture Union Tanzania Kanda ya Kati tulibarikiwa kuwa na Semina ya Watumishi na Wachungaji yenye somo lililosema “Umu...
07/05/2026

Scripture Union Tanzania Kanda ya Kati tulibarikiwa kuwa na Semina ya Watumishi na Wachungaji yenye somo lililosema “Umuhimu wa Maombi”

Kupitia semina hiyo, watumishi wa Mungu walikumbushwa nguvu, nafasi, na umuhimu wa maombi katika huduma na maisha ya kila siku. Tunaamini Mungu ataendelea kuwatia nguvu na kuwajaza hekima katika kulitumikia kanisa lake.

Asanteni wote mliohudhuria na kuungana nasi katika semina.

Kujenga kizazi kinachoishi katika ukweli! Timu ya Scripture Union Tanzania Kanda ya Kati ikiongozwa na Mwalimu Dinna Mre...
07/05/2026

Kujenga kizazi kinachoishi katika ukweli!

Timu ya Scripture Union Tanzania Kanda ya Kati ikiongozwa na Mwalimu Dinna Mremi walitembelea Shule ya Msingi Iyumbu kwa ajili ya kufundisha somo la Ukweli

Kupitia mafundisho hayo, wanafunzi walihimizwa kuwa waaminifu, kusema kweli, na kuishi maisha yenye maadili mema katika jamii. Tunamshukuru Mungu kwa nafasi ya kuwafikia watoto na kupanda mbegu njema za tabia.



SCRIPTURE UNION TANZANIA – KANDA YA KASKAZINI Watoto ni hazina ya taifa na msingi wa kesho iliyo bora Karibu katika Kamb...
07/05/2026

SCRIPTURE UNION TANZANIA – KANDA YA KASKAZINI

Watoto ni hazina ya taifa na msingi wa kesho iliyo bora
Karibu katika Kambi ya Watoto kwa watoto wenye umri wa miaka 5–15, mahali pa kujifunza, kukua kiroho, na kujengwa katika maadili mema.

Masomo yatakayofundishwa ni pamoja na:
✓Self-control
✓Forgiveness
✓Purity of Heart
✓Truth
✓Academic Excellence
✓Career Guidance and Counseling

Kupitia michezo, mafundisho, ushauri, na ushirika wa pamoja, watoto watapata nafasi ya kujifunza na kufurahia mazingira salama na yenye kujenga maisha yao ya sasa na ya baadaye.

Usikose kumleta mtoto wako kwenye kambi hii yenye baraka na mafundisho yenye kujenga tabia na kumkaribisha karibu na Mungu.

Address

Kalenga Street Upanga Dar Es Salaam Tz
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Scripture Union Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Scripture Union Tanzania:

Share