21/05/2026
Masomo ya maadili yameanza rasmi kufundishwa katika Shule ya Sekondari Iyunga, yakiwa na lengo la kuwalea wanafunzi katika misingi ya tabia njema, heshima, uwajibikaji, na kumcha Mungu.
Somo la kwanza lililofundishwa ni usafi, likigusa usafi wa mwili, mazingira, pamoja na usafi wa rohoni ili kuwajenga wanafunzi kuwa na maisha safi ndani na nje.
Tunapoishi katika usafi wa mwili na rohoni, tunajenga jamii yenye afya, amani, na maadili mema.