05/04/2026
Mpendwa, wakati tunakaribia mwisho wa mwezi huu, leo tena nakuja na Habari kutoka kwa Mungu! Je kuna hali au kitu kimekumeza? Je umebanwa kwenye eneo fulani la maisha toka siku nyingi? Je uko mahali pa giza hauoni njia ya kutoka? Mungu anataka kusema na hiyo hali ili ikuachie! Fanya k**a Yona, omba bila mashaka ukiwa na imani! Usikate tamaa! Mungu ni Bwana juu ya kila kitu duniani! Akisema lazima hiyo hali itii neno la Mungu! Kwa hiyo uwe tayari kutoka, Bwana ananena na samaki ili akutapike; atapike ndoa yako, atapike cheo yako, atapike watoto wako, atapike pesa yako, nk.
Fanya maombi haya:
Mungu, nena na samaki ili atapike baraka zangu zote kwa jina la Yesu Kristo !!!
Christ in Us, Hope of Glory