Eagt kilimani

Eagt kilimani Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Eagt kilimani, Religious organisation, Mbezi Juu Kwa Sanya, Dar es Salaam.

05/02/2026
Siku ya nne ya Maombi ya Kufunga.Karibuni sana kanisa la EAGT Kilimani,Mbezi juu Kayuni.
04/02/2026

Siku ya nne ya Maombi ya Kufunga.
Karibuni sana kanisa la EAGT Kilimani,Mbezi juu Kayuni.

Tutaomba mpaka mbingu Iseme WOTE mnakaribishwa  KARIBU KATIKA KANISA LA E.A.G.T- KILIMANIMpendwa mtu wa Mungu, tafadhali...
02/02/2026

Tutaomba mpaka mbingu Iseme
WOTE mnakaribishwa
KARIBU KATIKA KANISA LA E.A.G.T- KILIMANI

Mpendwa mtu wa Mungu, tafadhali ungana nasi kusikiliza neno la Mungu mubashara kutoka hapa kanisani E.A.G.T - KILIMANI CHURCH lililopo MBEZI JUU, KAYUNI, Dar es Salaam

Tunazidi kumshukuru na kumtukuza Mungu kwa mema na makuu aliyotutendea mwaka wote huu. Asante sana kwa kujumuika nasi. Mualike na mwingine hapa na ndelea kufuatilia mafundisho mubashara.

USISAHAU KU-SUBSCRIBE NA KU-SHARE HABARI HIZI NJEMA


Pia unaweza kufuatilia mafundisho yetu kupitia facebook kwa jina la KILIMANI CHURCH EAGT

IBADA KUU YA KANISA LA E.A.G.T KILIMANI 25/01/2026karibuni katika Kanisa la Kilimani Church E.A.G.T Mbezi juu Dar-es-sal...
25/01/2026

IBADA KUU YA KANISA LA E.A.G.T KILIMANI 25/01/2026
karibuni katika Kanisa la Kilimani Church E.A.G.T Mbezi juu Dar-es-salaam
KWA SADAKA NA MATOLEO MBALIMBALI
LIPA NAMBA M-PESA : 350295389 JINA EAGT KILIMANI CHURCH NA KWA NAMBA YA SIMU NI 0752-354-109 JINA EAGT KILIMANI CHURCH

π‰π”πŒπ€ππˆπ‹πˆ π˜π€ 𝐓𝐀𝐑 πŸπŸ”/𝟏𝟏/πŸπŸŽπŸπŸ“πŒπšπ‘πšπ₯𝐒: Kanisa la EAGT Kilimani Mbezi juu𝐍𝐚:  Mch George Mgoyela𝐒𝐨𝐦𝐨: π’πˆπ’πˆ π’πŽπ“π„ 𝐍𝐈 π€π’πŠπ€π‘πˆ 𝐖𝐀 𝐘...
17/11/2025

π‰π”πŒπ€ππˆπ‹πˆ π˜π€ 𝐓𝐀𝐑 πŸπŸ”/𝟏𝟏/πŸπŸŽπŸπŸ“
𝐌𝐚𝐑𝐚π₯𝐒: Kanisa la EAGT Kilimani Mbezi juu
𝐍𝐚: Mch George Mgoyela
𝐒𝐨𝐦𝐨: π’πˆπ’πˆ π’πŽπ“π„ 𝐍𝐈 π€π’πŠπ€π‘πˆ 𝐖𝐀 π˜π„π’π”(SIFA ZA ASKARI KAMILI WA YESU)

π„πŸπžπ¬π¨ πŸ”:πŸπŸ’-πŸπŸ–
Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani
zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote

Sisi ni Askari wa Yesu hivyo lazima tuzivae silaha zote za vita ili tuweze kushinda vita vya Ibilisi.
Paulo alitumia uvaaji wa vazi la Askari wa Kirumi

Paulo katika Timotheo anasema nimevipiga vita vilivyo vizuri,mwendo nimeumaliza na Imani nimeilinda
Kwa hiyo na sisi mwisho wa safari yetu inabidi ushinde vita
Na ili ushinde inabidi uzivae silaha zote za MUNGU
Mwanajeshi wa kirumi anapoenda vitani alihakikisha anavaa kofia ya chuma ili kujikinga kichwa
1.Iliitwa chapeo yani silaha namba moja
2.Kifuani alikuwa anavaa mkanda wa chuma,siku hizi wanaita (bullet proof)
Ili kujikinga na silaha yoyote isiufikie moyo
Iliitwa Dirii
3.Kiunoni wanafunga mkanda ambao wanaweza kuweka silaha zao
4. Kiatu cha chuma ili ukipita popote usipate madhara mfano miba

5.Mkono wa kushoto anashika ngao ili kujilinda
6.Mkono wa kulia anashika panga la kushambulia
Kwa hiyo Paulo anamfananisha Mwanajeshi huyo na Mtu wa Mungu
Je Mtu wa Mungu k**a Askari umezivaa silaha hizo na umezibeba kila wakati maana adui yeye halali wakati wote yupo vitani
1.Silaha namba moja yani chepeo ni wokovu
Je umetubu na kumgeukia Mungu na kuishi maisha matakatifu yenye kumpendeza Mungu
Hakikisha wokovu wako umesimama imara na misingi ya kiroho umeishikiria

Misingi hiyo ni
A) Kumjua sana Yesu
Ayubu 22:21
Mjue sana Mungu, ili uwe na amani Ndivyo mema yatakavyokujia.
Mema hayawezi kukujulia k**a humjui sana Yesu
😎 Kumuamini Yesu
Je unamuamini Yesu kweli kweli?
C) Kumtegemea Yesu
Katika mambo yako yote mtegemee Bwana Yesu
D) Kumtumikia Yesu
Je unamtumikia Yesu kwa kiwango kipi
Jipime je wokovu wako umejikita katika Misingi hii
Fanya juhudi uwezavyo kumtumikia Bwana Yesu maana kwa kufanya hivyo unahesabiwa taji yako

Hakikisha hii misingi minne ya kiroho unaishikilia kweli kweli

2.SILAHA NAMBA MBILI NI DIRII AMBAYO NI HAKI
Lazima utembee kwa haki zote upasazo,
Tunza usafi wako wewe uliyekoka kwa maadili yapasayo mwana wa Mungu kuishi
Haki inainua nchi palipo na haki utulivu unapatikana
Sisi ni watetezi wa Yesu inabidi hata mtu akikuona tu ajue huyu ameokoka kusiwe na sababu ya Yesu kusemwa vibaya kwa sababu yako
Tuonekane k**a chumvi na nuru mbele ya macho ya watu
Watu washuhudie kuwa wewe ni mwanafunzi wa Yesu.
Maneno yako yawe ya kumjenga Yesu na kuleta watu kwa Yesu
Pia matendo yako yawe ni nuru yenye mfano mzuri wa Yesu

3.SILAHA YA TATU NI MKANDA AMBAO NI KWELI
je unaulinda utu wako wa ndani kwa kutembea na kweli
Hebu ifahamu sana hiyo kweli na ukishaifahamu itakuweka huru
Soma sana neno la Mungu ili uifahamu kweli
Hata ibilisi atakapokujia hatakushunda
Kweli tunaipata kwa kusoma sana neno la Mungu

Kuna kanuni za kiroho ili ufanikiwe:
A) Kulisoma neno la Mungu
Ili kuifahamu kweli nayo ituweke huru
😎 Imani
C) Maombi
D) Sadaka
Tuwe wasomaji sana wa neno la Mungu

4.SILAHA YA NNE Ni KIATU CHA CHUMA
Ni kuhubiri Injili ya Amani
Inapendeza mno miguu ya watu wanaohubiri injili
Tuishuhudie injili popote pale tunapokuwepo

5.SILAHA YA NGAO INAYOZUIA MASHAMBULIZI MBALIMBALI NI IMANI
Tutembee kwa Imani ,na kuishika imani tuliyonayo,imani yetu inatokana na neno la Mungu
Wewe shikilia neno la Mungu k**a linavyosema maana imani ni kuwa na uhakika wa neno la Mungu
Kila hatua au silaha inayokuja inabidi ikutane na Imani nayo itaanguka

6.SILAHA YA SITA NI UPANGA
HILI NI neno la Mungu
Ibilisi akija unamshambulia kwa neno la MUNGU naye anaanguka chini k**a ambavyo Yesu alivyojaribiwa na Ibilisi alimshinda kwa neno la Mungu kwa sababu alikuwa na neno ndani yake
Hivyo nasi tunaposhambuliwa lazima tuwe na neno la Kumshinda shetani.

Tunapaswa kuvaa silaha zote za Mungu ili kushinda vita
Kuomba na kuombeana ni kitu kikubwa sana na unapoingia kwenye maombi ujue kabisa umeingia katika vita ambayo lazima ushinde
Tumefundishwa juu ya upendo
Kwamba mtangulize ndugu yako kabla yako,katika shida yake wewe uwe wa kwanza kuibeba na kumsaidia

Hivyo mwana Wa Mungu ujichunguze k**a una hizi silaha na k**a umepungukiwa muombe roho mtakatifu akusaidie

KARIBUNI SANA NYUMBANI MWA BWANA.
22/07/2024

KARIBUNI SANA NYUMBANI MWA BWANA.

BAADHI YA MATUKIO KATIKA IBADA YETU LEO 21/07/2024
21/07/2024

BAADHI YA MATUKIO KATIKA IBADA YETU LEO 21/07/2024

IBADA KUU LEO 21/07/2024
21/07/2024

IBADA KUU LEO 21/07/2024

Address

Mbezi Juu Kwa Sanya
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Eagt kilimani posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share