02/08/2025
*NI AGOSTI ,LAKINI HAUELEWI !*
Ni mwezi mwingine ikiwa imebaki miezi michache KWENDA 2026.
Unavaa unapendeza,unacheka na watu, lakini moyoni unajua kuna kitu hakiko sawa.
Unaendelea kurudia mambo uliyosema utayaacha Toka 2020.
✍️Siyo kwamba huna nguvu ,Na sio kwamba hausomi neno,na sio kwamba hauna juhudi,ni kwamba umekataa YESU asiwe dereva wa Maisha Yako!
Hivyo umejaribu kujikamilisha Kila kitu mwenyewe.
Elimu Yako, marafiki, mahusiano ,uchumi,
Mwili wako ,vyote umeamua kusimamja bila kumpa MHANDISI MKUU (YESU).
Sikiliza rafiki,Maisha Yako hayatasimama kamwe kwa kumuweka Yesu k**a ziada,unamwitaji yeye ndiye mwanzo na mwisho,alikuwepo,yupo ,na milele ataishi.
Jiulize,Je, unamwitaji kweli?
Ama unataka tu upone maumivu yako bila kubadilisha maisha yako?
Ukweli ni huu: hautaweza kumaliza safari hii bila Yeye.
Maisha si maisha, k**a hayana YESU.
Ellen G. White aliwahi kusema:
"Hatuwezi kuishi maisha ya kiroho bila kujikana nafsi kila siku, k**a Yesu alivyoishi."
✍️Sasa ni wakati wa kuachia usukani.
Bado una hofu,kiburi,dharau ,majivuno ,wivu ,manung'uniko,tamaa,
hasira,vilio..nk
Yesu hajakuchoka, Bado anakupa mwezi huu mpya Agosti ,k**a nafasi ya kuanza tena.
Si kwa nguvu zako Si kwa akili zako
Ni kwa Neema Yake,na kwa kwa kutegemea yeye.
_MUNGU akusaidie sana unapofanya maamuzi magumu,huhitaji pesa nyingi,huhitaji mpenzi,huhitaji kitu kingine chochote ,unamuhitaji YESU_
🙏BARIKIWA
WITH YOUR FRIENDS
https://www.facebook.com/profile.php?id=61562290635752