13/12/2021
Happy birthday imamu.
Heri ya siku ya kuzaliwa maamuma.
KUMBUKA ULIKOTOKA, naam ULIPOZALIWA
Ukija Zanzibar utawakuta ng'ombe wanabeba mizigo k**a punda wa kule Singida, lakini heshima ya hawa ng'ombe sio k**a ya punda maana hawaitwi punda,wanaitwa ng'ombe. Je,wewe unaitwa nani? na Je,Wewe ni nani?
Uasili wako ni nguvu naam nguvu ya upendo,nguvu yenye mvuto ikavutika na ikavutia. Ulilivutia yai na ukavutika kwalo kwa kuwa ni wa mfanano wa asili, ukauvaa mwili ili ukusaidie kuiishi asili yako ya upendo pamoja na wenye miili katika ulimwengu wa mwili,ukazaliwa kwetu. Tukakupokea, tukaanza mchakato wa kukuvua uasili wako ili usiweze kuishi kwa nguvu yako ya upendo, naam kuvutia na kuvutika.Tuliyafanya haya yote pasipo kukusudia kwa kuwa hata sisi tulifanyiwa na waliofanyiwa pasipo kukusudia. Tukakuita majina,majina yaliyokufanya ujione bora dhidi ya akina fulani au duni zaidi yao, hivyo ukaanza kuvuta badala ya kuvutia na ukaruhusu kuvutwa badala ya kuvutika. Tulikuita Baraka,tulikuita mwanaume,tulikuita mkatoliki, tulikuita mmatengo,tulikuita mweusi,tulikuita mtoto wa kwanza,tulikuita mtoto wa mwalimu, tulikuita .....nakadhalika nakadhalika. Majina haya kila yaliporudiwa kuitwa masikioni mwako,yalitengeneza mawazo,mtazamo,imani na utamaduni kwako na kukuzidi kukusahaulisha uasili wako kiasi cha wewe kuamini hivyo tunavyokuita ndivyo ulivyo na ndio utofauti wako na watu/viumbe wengine wote unavyochangamana navyo hapa ulimwenguni. Hatukuishia hapo tu,tulikupa tafsiri ya kila kionekanacho na kisichoonekana ulimwenguni naam tafsiri zilizoathiri mtazamo wako kwenye kila ulichokiona,kihisi,kionja,kisikia na kukinusa,Milango uliyopewa kukupa ufahamu ikageuka kukufumba ufahamu. Tuliamua usome wapi,usome nini,uwe nani,ili ufanye nini na kwa manufaa ya nani. Naam umekuja tukiwa tumeshaandaa mfumo tayari wa wewe kuufuata utake au usitake, Umeazaliwa kutumika, naam wewe ni mtumishi na mtumwa linganifu na tafsiri na majina tuliyokupa. Tumekufundisha kuvuta kupitia nguvu tulizokuaminisha unazo,tumekufanya uvutwe kupitia udhaifu tuliokuaminisha kuwa unao. Tafsiri ya hisia zako na uhalisia wa mambo pasipofahamu uasilia wake vimekufanya uwe imamu zumbukuku machoni mwa maamuma. (Ahsante kwa ujumbe kwaiyo nifanye nini?) Jibu:Ukija Zanzibar utawakuta ng'ombe wanabeba mizigo k**a punda wa kule Singida, lakini heshima ya hawa ng'ombe sio k**a ya punda maana hawaitwi punda,wanaitwa ng'ombe. Je,wewe unaitwa nani? na Je,Wewe ni nani?
UKIIJUA KWELI UTAKUWA HURU KWELI KWELI. Kujitambua ni Kujikomboa.
AmkaBeAwareBeAlive