01/08/2024
UNIONYESHE NJIA ZAKO, NIPATE KUKUJUA
Moja ya sababu kubwa ya watu wengi kutokuona utendaji wa Mungu wa kudumu ni ile hali ya kutaka mambo yatokee haraka haraka bila kukubali au kupitia mchakato.
Namanisha kutaka sana MATENDO ya Mungu na sio NJIA ZA MUNGU.
Ni kweli Mungu anayo MATENDO (MIUJIZA) lakini utendaji wake wa kudumu ni wa KIMCHAKATO (njia) zaidi; au naweza kusema msingi wa utendaji wa Mungu ni kupitia MCHAKATO na sio MATUKIO/MATENDO/MIUJIZA... Naamini ukiendelea kusoma mpaka mwisho utanielewa vizuri.
Watu wengi hupenda BIG RESULTS NOW (MATOKEO MAKUBWA SASA AU HARAKA), lakini hawapendi KUFUATA AINA YA MAISHA (LIFESTYLE) AMBAYO ITAZALISHA MATOKEO YA KUDUMU...
Angalia hili andiko utanielewa zaidi 👇👇
Zaburi 103:7
[7]Alimjulisha Musa NJIA ZAKE,
Wana wa Israeli MATENDO YAKE.
He made known his ways unto Moses, his acts unto the children of Israel.
Hilo andiko limetaja vitu viwili:-
1. NJIA ZA MUNGU
2. MATENDO YA MUNGU
Sasa Mungu anavyo vyote, MATENDO na NJIA, lakini hufanya kazi na waliokubali NJIA zake na sio wanaotafuta matendo yake tu...
Ukipewa MATENDO unaanza kushangilia (to celebrate immediately), lakini ukipewa NJIA hauishangilii muda huo bali UNAANZA KUIENDEA kwa umakini...
Kwa mfano, Mtu anayepewa gari, amepewa matendo, anaanza kuliendesha lakini anayepewa WAZO LA BIASHARA NA NAMNA YA KUIFANYA AMBAYO MWISHO INAWEZA KUMPATIA MAGARI, huyo hataanza kushangilia na kuendesha gari, bali atajikuta ANATAKIWA KUWA COMMITTED KWENYE BIASHARA ALIYOPEWA WAZO...
Mwanzoni mwenye matendo ni k**a amepata zaidi, lakini baada ya muda mwenye njia ndio atakuwa na matokeo ya kudumu...
Ukipewa gari haujui namna ya kupata hela ya mafuta na service, hiyo furaha ya gari ni ya muda tu, lakinj, Ukipewa njia ikakufikisha kupata gari, kulihudumia haiwezi kuwa changamoto...
Mfano huo ni mzuri sana kutusaidia kujua tofauti ya NJIA ZA MUNGU NA MATENDO YA MUNGU...
LINAPOKUJA SUALA LA NJIA, MTU HUJULISHWA, HUONESHWA, HUFUNDISHWA, NA ZAIDI SANA MTU UHUSISHWA KATIKA MCHAKATO, LAKINI MATENDO HUTENDEWA NA KUPOKEA...
Matendo ya Mungu sio lazima yamuhusishe mtendewa...
NJIA INAHITAJI WATU COMMITTED, K**A HAUTAAMUA KUWA COMMITTED NA MUNGU HUWEZI KUJULISHWA NA KUHUSISHWA KATIKA NJIA ZA MUNGU... HUWEZI KUPEWA STRATEGIES (MBINU)...
NJIA NI KWA AJILI YA MARAFIKI, NJIA NI USHIRIKA NI PARTNERSHIP
ANGALIA MAOMBI YA MUSA👇👇
Kutoka 33:13
[13]Basi, sasa nakuomba, ikiwa nimepata neema mbele zako, UNIONYESHE NJIA ZAKO, NIPATE KUKUJUA, ili NIPATE NEEMA mbele zako; ukakumbuke ya kuwa taifa hilo ndilo watu wako.
Neema ya kwanza ilimpa Musa nafasi kumuendea Mungu na hapa anaitumia nafasi hiyo kumuomba Mungu AMUONYESHE NJIA ZAKE... Hapa Musa alishaona MATENDO YA MUNGU YA KUTOSHA TU, LAKINI ANAOMBA MUNGU AMUONYESHE NJIA ZAKE...
Halafu anasema MATOKEO YA NJIA ZA MUNGU NI KUMJUA MUNGU ndio maana anasema "nakuomba, ikiwa nimepata neema mbele zako, UNIONYESHE NJIA ZAKO, NIPATE KUKUJUA"...
Kisha anaendelea kusema "ili NIPATE NEEMA MBELE ZAKO"
Hii Neema ya pili sio Neema ya kwanza, Neema ya kwanza ilimpa nafasi Neema ya pili ni matokeo ya KUTEMBEA KATIKA NJIA ZA MUNGU NA KUMJUA MUNGU ZAIDI...
Sasa hapa kwenye Neema tusiingie ndani, titapaongelea Mungu akitupa nafasi... Tuendelee na NJIA ZA MUNGU
Kumbe matendo ya Mungu hayatoshi kumfanya mtu kumjua Mungu...
Unapaswa kufahamu kwamba, MUNGU akikutendea hataki uweke kituo hapo, anataka UMUENDEE KUMTAFUTA ZAIDI ILI AKUONYESHE NJIA ZAKE NA UPATE KUMJUA ZAIDI...
NJIA NI MATOKEO YA MAHUSIANO IMARA NA MUNGU... NA MAHUSIANO SIO TUKIO NI MCHAKATO, NJIA NI MCHAKATO
Njia ZINATAFUTWA, ZINADAIWA, ZINAOMBWA... Hutazijua NJIA ZA MUNGU ikiwa HAUTAWEKA UHITAJI KUANZIA MOYONI MWAKO (YOU SHOULD PRESS A DEMAND FOR HIS WAYS)...
Usitulie kwa kidogo (matendo), tafuta NJIA... Do not settle for less
NJIA ZA MUNGU ZITAKUPELEKEA KUMJUA MUNGU NA KUMJUA MUNGU ZAIDI KUTAKUPEKEKEA KUZIJUA ZAIDI NJIA ZAKE NA HAPO NDIPO UKUAJI UENDELEVU KATIKA MUNGU UTATOKEA
Watu wengi UKIMUONA ANAOMBA NI KWA SABABU ANATAFUTA MATENDO YA MUNGU, NI KWELI MUNGU ANAWEZA AKAKUONYESHA MATENDO YAKE UKIOMBA, LAKINI UKIISHIA KWENYE MATENDO YA MUNGU, BAADA YA MUDA UTARUDI KUWA EMPTY NDANI YAKO NA HATA UTAJIKUTA UNERUDI NYUMA WAKATI UNAJUA WAZI MUNGU ALIKUTENDEA...
Kutendewa Matendo mengi hakumkuzi mtu kiroho wala hakumpia mtu kumjua Mungu (aliyeyatenda hayo), na Hilo ndio liliwakuta Wana wa Israeli, walikuwa wanatendewa muujiza, wanafurahia sana lakini baada ya muda wanarudi nyuma, kwa sababu WALIPATA MUUJIZA LAKINI HAWAKUWA NA MAHUSIANO NA MTENDA MIUJIZA...
Kila utendewapo muujiza, usiweke kituo, bali uchukue k**a WITO WA KUMJUA MUNGU ZAIDI... Hii ndio sababu maandiko yanaiita miujiza ni ISHARA (SIGNS)... ISHARA MAANA YAKE ZINAONYESHA MAHALI FULANI... ISHARA SIO MWISHO (SIGNS ARE NOT DESTINATION)
SIGNS ARE NOT TARGET, OUR TARGET IS GOD
ACHA KUFANYA VITU (KUFUNGA, KUOMBA, KUJIFUNZA, NK) KWA AJILI YA KUPATA KITU (MATENDO), ANZA KUFANYA KWA AJILI YA KUMJUA MWENYE VITU...
Kuanzia leo ACHA KUFANYA VITU KWA AJILINYA ISHARA, ANZA KUFANYA VITU KWA AJILI YA MWENYE ISHARA, KWA AJILI YA KUMJUA MUNGU...
Paulo anasema "ILI NIMJUE YEYE" Wafilipi 3:10
Musa anasema "Unionyeshe NJIA ZAKO NIPATE KUKUJUA"
Yesu anasema "Na uzima wa milele ndio huu, WAKUJUE WEWE"
HIKI NDIO KILIO NA SHAUKU YA MOYO WANGU, "MUNGU NIPE KUKUJUA WEWE ZAIDI NA ZAIDI, UNIONYESHE NJIA ZAKO NIPATE KUKUJUA"
Mungu akupe ILE SHAUKU YA KUTOKA NDANI YA KUZIJUA NJIA ZAKE NA KUMJUA YEYE, AMBAYO NDIO ITAKUWA DRIVING FORCE YA KILA UNACHOKIFANYA...
HII ITAPELEKEA KUMJUA MUNGU NA NJIA ZA MUNGU, ITAIMARISHA MAHUSIANO YAKO NA MUNGU NA WAKATI HUO HUO UKIENDELEA KUFURAHIA MATENDO YA MUNGU KWA KUDUMU SIO KWA MATUKIO...
Ayubu 22:21
[21]Mjue sana Mungu, ili uwe na amani;
Ndivyo mema yatakavyokujia.
Acquaint now thyself with him, and be at peace: thereby good shall come unto thee.
Zaburi 63:1-2
[1]Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,
NAFSI YANGU INAKUONEA KIU,
MWILI WANGU WAKUONEA SHAUKU,
Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.
[2]Ndivyo NILIVYOKUTAZAMA KATIKA PATAKATIFU,
NIZIONE NGUVU ZAKO na UTUKUFU WAKO.
Umebarikiwa
Mwl. Francis M. Langula
WhatsApp: +255754711247
TELEGRAM: