Baha'i Tanzania

Baha'i Tanzania Ukurasa rasmi wa Jumuiya ya Wabaha'i, Tanzania
Tovuti: https://www.bahai.or.tz
WhatsApp: https://wa.link/5uyhnu
Simu: +255 685 637 422

Je tunawezaje kumjua Mungu?Karibu tujifunze pamoja.
23/08/2026

Je tunawezaje kumjua Mungu?
Karibu tujifunze pamoja.

Ni yapi baadhi ya mafundisho ya Imani ya Kibaha'i? Endelea kutembelea tovuti yetu www.bahai.or.tz pamoja na kurasa zetu ...
23/08/2026

Ni yapi baadhi ya mafundisho ya Imani ya Kibaha'i?
Endelea kutembelea tovuti yetu www.bahai.or.tz pamoja na kurasa zetu za mitandao ya kijamii Baha'i Tanzania ili kujifahamisha zaidi.

Kuendelea kujifunza zaidi tafadhali tembelea tovuti yetu.www.bahai.or.tz
22/08/2026

Kuendelea kujifunza zaidi tafadhali tembelea tovuti yetu.

www.bahai.or.tz

KONGAMANO LA WANAWAKE - ZIWA MASHARIKIKatika kujenga maendeleo ya kweli ulimwenguni, usawa kati ya mwanamke na mwanaume ...
12/07/2026

KONGAMANO LA WANAWAKE - ZIWA MASHARIKI
Katika kujenga maendeleo ya kweli ulimwenguni, usawa kati ya mwanamke na mwanaume ni msingi usioweza kupuuzwa. Kadiri jamii inavyoendelea kutambua na kuthamini nafasi ya mwanamke, ndivyo uwezo wake wa kuchangia maendeleo ya familia na jamii unavyozidi kuonekana.
Kwa siku tatu, wanawake walikutana katika kongamano maalumu la kutafakari, kujifunza na kushauriana kuhusu namna wanavyoweza kuongeza mchango wao katika maendeleo ya jamii. Katika kipindi chote cha kongamano, washiriki walijifunza na Maandiko Matakatifu na jumbe za Nyumba ya Haki ya Ulimwengu kuhusu nafasi ya wanawake katika maendeleo ya familia na jamii.
Mojawapo ya uelewa uliojitokeza kwa kina ni kwamba familia ndiyo msingi wa kujenga jamii yenye maadili, umoja na maendeleo endelevu. Ilisisitizwa kuwa kila nyumba inaweza kuwa kitovu cha ibada, mazungumzo yenye kujenga, huduma kwa wengine na shughuli mbalimbali za kielimu zinazotolewa kupitia taasisi za mafunzo.
Washiriki pia walitafakari umuhimu wa makundi ya familia k**a njia madhubuti ya kupanua ushiriki wa watu binafsi na familia katika mchakato wa kujenga jumuiya amirifu. Kupitia makundi haya, familia huimarisha urafiki, hujifunza pamoja na kushiriki katika shughuli zinazokuza maendeleo ya kiroho na kijamii.
Aidha, kongamano lilisisitiza nafasi ya akina mama k**a walimu wa kwanza wa watoto. Ilibainika kuwa wanawake wana mchango wa kipekee katika kujenga msingi wa maadili mema, tabia njema na maisha ya kiroho ya watoto na vijana. Uelewa huu umeongeza dhamira ya kuendeleza programu za kielimu na kuimarisha ushiriki wa familia katika malezi ya kizazi kijacho.
Mwisho wa kongamano, washiriki waliondoka wakiwa na hamasa mpya ya kuendelea kuimarisha familia zao, kushiriki kikamilifu katika shughuli za kujenga jumuiya na kuwa chachu ya maendeleo katika maeneo wanayoishi. Ujifunzaji uliopatikana umeweka msingi imara wa kujenga jamii zenye umoja, maadili na uwezo wa kuwalea watoto na vijana katika mazingira yanayokuza utu, huduma kwa wengine na maendeleo endelevu.
Baha'i Tanzania www.bahai.or.tz

Miongoni mwa kanuni muhimu za Imani ya Kibahá’í ni umoja wa dini. Kanuni hii inafundisha kwamba dini zote kuu duniani zi...
07/06/2026

Miongoni mwa kanuni muhimu za Imani ya Kibahá’í ni umoja wa dini. Kanuni hii inafundisha kwamba dini zote kuu duniani zinatoka kwa Mungu mmoja na kwamba zinawakilisha hatua tofauti za maongozi ya Mungu kwa wanadamu katika nyakati mbalimbali.
Wabahá’í wanaamini kuwa manabii na waanzilishi wa dini mbalimbali, k**a vile Abraham, Moses, Buddha, Yesu Kristo, Muhammad na Bahá’u’lláh, walitumwa na Mungu katika vipindi tofauti vya historia ili kukidhi mahitaji ya jamii za wakati wao.
Kwa mujibu wa mafundisho ya Kibahá’í, tofauti zinazojitokeza kati ya dini hizi zinatokana na mazingira, nyakati na mahitaji tofauti ya wanadamu waliokuwa wakiongozwa, na si kwa sababu chanzo cha dini hizo ni tofauti. Hivyo, dini zote zinachukuliwa kuwa sehemu za mpango mmoja wa Mungu wa kuwaongoza wanadamu kuelekea maendeleo ya kiroho na kijamii.

Endelea kutembelea kurasa zetu Baha'i Tanzania BahaiTeachings.org www.bahai.or.tz

Kwa kipindi kirefu, Jumuiya ya Kibaha’i ulimwenguni kote imeendelea kushiriki kikamilifu katika mijadala mbalimbali inay...
08/05/2026

Kwa kipindi kirefu, Jumuiya ya Kibaha’i ulimwenguni kote imeendelea kushiriki kikamilifu katika mijadala mbalimbali inayolenga maendeleo na uboreshaji wa jamii wa wanadamu, ikiwemo suala la usawa kati ya wanawake na wanaume, kuendeleza upatano kati ya dini na sayansi, pamoja na kuchangia jitihada za kuleta Amani Kuu ya ulimwengu.
Kwa muda wa siku tano, wawakilishi wa Ofisi za Mambo ya Nje za Jumuiya ya Kibaha’i (EAO) kutoka ukanda wa Afrika Mashariki walikutana nchini Kenya kwa ajili ya kujifunza kwa pamoja, kushauriana, na kujadili kwa kina masuala mbalimbali yanayohusiana na utendaji wa ofisi hizo.
Katika kipindi cha mkutano huo, pia yaliandaliwa mazingira ya kukutana na wadau mbalimbali wa kijamii ili kushiriki katika mazungumzo yenye maana na yainuayo, yaliyoangazia masuala muhimu ya kijamii yanayochangia katika ustawi na uboreshaji wa ulimwengu.
Baha'i Tanzania www.bahai.or.tz

MKUTANO MKUU WA KITAIFA WA 63 – JUMUIYA YA WABAHÁ’Í WA TANZANIAMkutano Mkuu wa Kitaifa wa 63 wa Jumuiya ya Wabahá’í wa T...
29/04/2026

MKUTANO MKUU WA KITAIFA WA 63 – JUMUIYA YA WABAHÁ’Í WA TANZANIA
Mkutano Mkuu wa Kitaifa wa 63 wa Jumuiya ya Wabahá’í wa Tanzania ulifanyika kwa mafanikio makubwa tarehe 24–26 Aprili 2026 katika Kituo cha Wabahá’í, (Baha’i center) Upanga – Dar es Salaam.
Zaidi ya Marafiki 80 walihudhuria mkutano huu, wakiwemo wawakilishi kutoka jamii mbalimbali, Mshauri wa Bara Bw. Agustino Ibrahimu, Washauri Wasaidizi pamoja na wageni waalikwa.
Kati ya wawakilishi 57 waliochaguliwa katika hatua za awali za mchakato wa uchaguzi, asilimia 98 walishiriki kikamilifu katika upigaji kura, jambo linaloashiria kiwango cha juu cha ukomavu katika michakato ya uchaguzi.
Mkutano huu ulishuhudia tukio muhimu la uchaguzi wa wajumbe wa Baraza la Kiroho la Kitaifa la Wabahá’í wa Tanzania kwa kipindi cha 2026–2027. Wajumbe waliochaguliwa ni:
1. Bw. Dunstan Ruta
2. Bw. Geofrey Nduke
3. Bw. Christopher Stevenson
4. Bi. Ester Mtisya
5. Dkt. Ola Johnpour
6. Bw. Gershom Mpumbiye
7. Bi. Suzan Kyando
8. Bw. Cleophace Ndaro
9. Bw. Samson Rutebuka
Aidha, washiriki walipata fursa ya kusoma na kujadiliana kwa kina Ujumbe wa Riḍván 2026 pamoja na barua ya tarehe 31 Desemba 2025 kutoka Nyumba ya Haki ya Ulimwengu, zinazohitimisha awamu ya kwanza ya Mpango wa Miaka Tisa na kufungua awamu ya pili ya mpango huo. Mkutano pia ulipokea na kujadili ripoti ya utendaji ya mwaka 2025–2026 iliyowasilishwa na Katibu wa Baraza la Kiroho la Kitaifa.
Tunawapongeza wajumbe wote waliochaguliwa na tunawatakia mafanikio mema katika utekelezaji wa majukumu yao kwa uadilifu, bidii na moyo wa huduma kwa jamii ya wanadamu.

Baha'i Tanzania
www.bahai.or.tz

Address

Makongo Juu
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Baha'i Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share