08/05/2026
Kwa kipindi kirefu, Jumuiya ya Kibaha’i ulimwenguni kote imeendelea kushiriki kikamilifu katika mijadala mbalimbali inayolenga maendeleo na uboreshaji wa jamii wa wanadamu, ikiwemo suala la usawa kati ya wanawake na wanaume, kuendeleza upatano kati ya dini na sayansi, pamoja na kuchangia jitihada za kuleta Amani Kuu ya ulimwengu.
Kwa muda wa siku tano, wawakilishi wa Ofisi za Mambo ya Nje za Jumuiya ya Kibaha’i (EAO) kutoka ukanda wa Afrika Mashariki walikutana nchini Kenya kwa ajili ya kujifunza kwa pamoja, kushauriana, na kujadili kwa kina masuala mbalimbali yanayohusiana na utendaji wa ofisi hizo.
Katika kipindi cha mkutano huo, pia yaliandaliwa mazingira ya kukutana na wadau mbalimbali wa kijamii ili kushiriki katika mazungumzo yenye maana na yainuayo, yaliyoangazia masuala muhimu ya kijamii yanayochangia katika ustawi na uboreshaji wa ulimwengu.
Baha'i Tanzania www.bahai.or.tz