Baha'i Tanzania

Baha'i Tanzania Ukurasa rasmi wa Jumuiya ya Wabaha'i, Tanzania

Kwa kipindi kirefu, Jumuiya ya Kibaha’i ulimwenguni kote imeendelea kushiriki kikamilifu katika mijadala mbalimbali inay...
08/05/2026

Kwa kipindi kirefu, Jumuiya ya Kibaha’i ulimwenguni kote imeendelea kushiriki kikamilifu katika mijadala mbalimbali inayolenga maendeleo na uboreshaji wa jamii wa wanadamu, ikiwemo suala la usawa kati ya wanawake na wanaume, kuendeleza upatano kati ya dini na sayansi, pamoja na kuchangia jitihada za kuleta Amani Kuu ya ulimwengu.
Kwa muda wa siku tano, wawakilishi wa Ofisi za Mambo ya Nje za Jumuiya ya Kibaha’i (EAO) kutoka ukanda wa Afrika Mashariki walikutana nchini Kenya kwa ajili ya kujifunza kwa pamoja, kushauriana, na kujadili kwa kina masuala mbalimbali yanayohusiana na utendaji wa ofisi hizo.
Katika kipindi cha mkutano huo, pia yaliandaliwa mazingira ya kukutana na wadau mbalimbali wa kijamii ili kushiriki katika mazungumzo yenye maana na yainuayo, yaliyoangazia masuala muhimu ya kijamii yanayochangia katika ustawi na uboreshaji wa ulimwengu.
Baha'i Tanzania www.bahai.or.tz

MKUTANO MKUU WA KITAIFA WA 63 – JUMUIYA YA WABAHÁ’Í WA TANZANIAMkutano Mkuu wa Kitaifa wa 63 wa Jumuiya ya Wabahá’í wa T...
29/04/2026

MKUTANO MKUU WA KITAIFA WA 63 – JUMUIYA YA WABAHÁ’Í WA TANZANIA
Mkutano Mkuu wa Kitaifa wa 63 wa Jumuiya ya Wabahá’í wa Tanzania ulifanyika kwa mafanikio makubwa tarehe 24–26 Aprili 2026 katika Kituo cha Wabahá’í, (Baha’i center) Upanga – Dar es Salaam.
Zaidi ya Marafiki 80 walihudhuria mkutano huu, wakiwemo wawakilishi kutoka jamii mbalimbali, Mshauri wa Bara Bw. Agustino Ibrahimu, Washauri Wasaidizi pamoja na wageni waalikwa.
Kati ya wawakilishi 57 waliochaguliwa katika hatua za awali za mchakato wa uchaguzi, asilimia 98 walishiriki kikamilifu katika upigaji kura, jambo linaloashiria kiwango cha juu cha ukomavu katika michakato ya uchaguzi.
Mkutano huu ulishuhudia tukio muhimu la uchaguzi wa wajumbe wa Baraza la Kiroho la Kitaifa la Wabahá’í wa Tanzania kwa kipindi cha 2026–2027. Wajumbe waliochaguliwa ni:
1. Bw. Dunstan Ruta
2. Bw. Geofrey Nduke
3. Bw. Christopher Stevenson
4. Bi. Ester Mtisya
5. Dkt. Ola Johnpour
6. Bw. Gershom Mpumbiye
7. Bi. Suzan Kyando
8. Bw. Cleophace Ndaro
9. Bw. Samson Rutebuka
Aidha, washiriki walipata fursa ya kusoma na kujadiliana kwa kina Ujumbe wa Riḍván 2026 pamoja na barua ya tarehe 31 Desemba 2025 kutoka Nyumba ya Haki ya Ulimwengu, zinazohitimisha awamu ya kwanza ya Mpango wa Miaka Tisa na kufungua awamu ya pili ya mpango huo. Mkutano pia ulipokea na kujadili ripoti ya utendaji ya mwaka 2025–2026 iliyowasilishwa na Katibu wa Baraza la Kiroho la Kitaifa.
Tunawapongeza wajumbe wote waliochaguliwa na tunawatakia mafanikio mema katika utekelezaji wa majukumu yao kwa uadilifu, bidii na moyo wa huduma kwa jamii ya wanadamu.

Baha'i Tanzania
www.bahai.or.tz

Address

Makongo Juu
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Baha'i Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share