26/05/2026
Si msalaba tu bali msalaba wa katikati. Si msalaba tu wa katikati bali aliyeko juu ya huo msalaba. Yesu aliungana na wenye dhambi katikati ya dhambi zao, wakijitahidi kulipia makosa yao. Mmoja akaona msalaba wa Yesu kuwa wokovu.. Mwingine akaudharau.. akafa kwenye jitihada zake. Na hakusaidika. Wewe unashikilia jitihada zako au unaitazama kazi ya Mwokozi? Yesu anataka kukutakasa uko busy unajitakasa. Anataka kukuhesabia haki bure uko busy kulipia dhambi zako. Ukishachoka sema usaidiwe...
— Global Family Gatherings
"God's Standards"