Efatha Church Mazizini

Efatha Church Mazizini The official Efatha Church Mazizini page. YouTube: youtube.com/efathachurchmazizini.

31/05/2026

simama na mume wako

MEZA YA BWANAMungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yak...
31/05/2026

MEZA YA BWANA

Mungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yako ndipo dhambi, magonjwa, shetani wachawi, njaa na hata dhiki zitakukimbia na ndipo utakapoona mema yakikujilia. Ayubu anasema utakusudia neno nao litatimia. Ukilinda imani yako isiyumbe hautasikia njaa wala kiu, maana yake mahitaji yako yatatimizwa.

Haya yote yatatokea kwako k**a utalinda imani yako. Tunapomega mkate na kunywa mvinyo, yale yaliyoshindikana yakawezekane, Biblia inasema “Imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo” mwana wa Mungu Neno hili litatimia kwako, hutaona kiu wala njaa maana mahitaji yako yatatimilizwa, unaenda kula na kunywa vile vitamanikavyo.

Biblia inasema Mungu ndiye uzima wako, baada ya kula na kunywa (meza ya Bwana) ule ugonjwa uliyokukandamiza utaondoka. Kwa mamlaka niliyonayo utaenda kutamka Neno leo na litakwenda kutimia, yule mgonjwa aliyekuwa kitandani kwamba ni mkubwa au mdogo anakwenda kuinuka, kwamba ulikuwa unaumwa na kansa, TB, presha, kisukari au aina yoyote ya ugonjwa leo huo ugonjwa umeondolea maana Bwana amesema amekuja ili sisi tuwe na uzima tele, leo unakwenda kuwa na uzima tele. K**a umekuja hapa ulikuwa na maswali yanayokusumbua umepata majibu yake. Mwanangu wacha ikawe hivyo kwako.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

MATUKIO KATIKA PICHA  IBADA YA JUMAPILI TAREHE 31/5/ 2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MAZIZINI UKONGA  DAR ES SALAAM TANZANI...
31/05/2026

MATUKIO KATIKA PICHA IBADA YA JUMAPILI TAREHE 31/5/ 2026 KATIKA KANISA LA EFATHA MAZIZINI UKONGA DAR ES SALAAM TANZANIA

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa...
31/05/2026

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

Baba anabeba mizigo yote inayohusu watoto, maumivu yote ya watoto, huu ndiyo ubaba; anasimama kwa ajili ya familia yake. Yesu aliye baba wa milele kwetu, alichukua mizigo yetu, maumivu yetu na changamoto zetu zote na akafa nazo msalabani na huu ndiyo ubaba.

Wakolosai 2:14-15 “akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutush*taki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani; akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.”

Yesu k**a baba aliyabeba haya yote kwa ajili yetu mimi na wewe, halafu kuna mtu anasahau kile Yesu Kristo amefanya pale msalabani? Aliyoyafanya Yesu ni kwa ajili yetu.

Wakolosai 2:13 “Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;”
Tulikuwa tumekufa lakini kwa ajili yake leo hii tupo hai.

Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Pasipo Imani hauwezi kumpendeza Mungu, k**a haumpendezi YEYE inamaana kuwa unamkosea; utajuaje hivyo? Kwa maana Biblia inasema “huwapa thawabu wale wamtafutao.”

Wale wanaompendeza Mungu YEYE huwapa mahitaji yao, hii ina maana kuwa wale wasiyompendeza wanateseka na kuzunguka sana, wanaishi na njaa na katika uhitaji ingawa wamezaliwa mara ya pili (wameokoka) kwa nini wanaishi hivyo? Ni kwa sababu hawampendezi YEYE.

Biblia inasema “Kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Hivyo kwanza unapaswa kuelewa kuwa YEYE yupo hai, anakuona na kukutazama, hivyo atatazama kila unachofanya, kile unachokifanya kikimpendeza YEYE anakupa mahitaji ili kukufanya wewe uende mbele, k**a ukifanya vizur

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Nay...
31/05/2026

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”

Kwa ajili yetu, na kwa faida yetu na kwa ajili ya maisha yetu mtoto amezaliwa, siyo kwa ajili ya Mungu, la! bali ni kwa ajili yetu, usisahau hilo. Watu wanaishi maisha haya ya wokovu k**a vile kamwe hawatakaa wafe, kwamba wataishi duniani milele, la! Lazima ufe, labda tu Yesu aje mapema, lakini k**a sivyo kufa utakufa tu, lakini lazima uelewe unakufaje, kwamba unakufa na utukufu au laana.

Biblia inasema “Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani” tulipewa mtoto mwanaume ambaye alikuwa na majina manne:-

Mshauri wa ajabu; akikushauri, akikusaidia na kukuongoza wewe, akikunyoosha ili uende kule Mungu anataka uwe.

Mungu mwenye nguvu; hii ina maana kuwa kuna miungu mingine lakini Mungu huyu ni Mungu mwenye nguvu, kwa nini mwenye nguvu? Ili kukusababisha wewe uweze kushinda, ili aweze kushinda miungu mingine yote kwa ajili yako. Mungu anapokupa mtu kusimama kwa ajili yako kumbuka anampa huo uweza ili akukomboe kutoka kwenye miungu mingine.

Baba wa milele: hii ina maana kuwa ubaba wake hauna mwisho, Mungu anapokupa baba wa kiroho huo ubaba kamwe hautakaa uishe, kwamba amekufa au yupo hai. Ndiyo maana hata unaposoma biblia Waebrania wote walikuwa wanamuita Ibrahimu baba, kwa nini? Kwa sababu ubaba wa Ibrahimu hautakaa uishe japokuwa yeye amekufa lakini ubaba upo maana huo ubaba ni agano kati ya Mungu na Ibrahimu na huo ubaba utaendelea kuwepo milele. Mungu anapokupa baba wa kiroho unapaswa kujua kuwa huo wajibu hautakaa uishe kwa maana siku tutakapofika mbinguni ni Yeye baba wa kiroho atakayesimama kwa ajili yako.

Mfalme wa Amani: Yeye amebeba mambo yote yanayohusu amani, maana yake ni pamoja na mafanikio yako. Yesu alizaliwa katika ushi

SOMO: KUFANYA MAPENZI YA MUNGUIsaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kif...
31/05/2026

SOMO: KUFANYA MAPENZI YA MUNGU

Isaya 9:6
“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”

Kwa ajili yetu, na kwa faida yetu na kwa ajili ya maisha yetu mtoto amezaliwa, siyo kwa ajili ya Mungu, la! bali ni kwa ajili yetu, usisahau hilo. Watu wanaishi maisha haya ya wokovu k**a vile kamwe hawatakaa wafe, kwamba wataishi duniani milele, la! Lazima ufe, labda tu Yesu aje mapema, lakini k**a sivyo kufa utakufa tu, lakini lazima uelewe unakufaje, kwamba unakufa na utukufu au laana.

Biblia inasema “Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani” tulipewa mtoto mwanaume ambaye alikuwa na majina manne:-

Mshauri wa ajabu; akikushauri, akikusaidia na kukuongoza wewe, akikunyoosha ili uende kule Mungu anataka uwe.

Mungu mwenye nguvu; hii ina maana kuwa kuna miungu mingine lakini Mungu huyu ni Mungu mwenye nguvu, kwa nini mwenye nguvu? Ili kukusababisha wewe uweze kushinda, ili aweze kushinda miungu mingine yote kwa ajili yako. Mungu anapokupa mtu kusimama kwa ajili yako kumbuka anampa huo uweza ili akukomboe kutoka kwenye miungu mingine.

Baba wa milele: hii ina maana kuwa ubaba wake hauna mwisho, Mungu anapokupa baba wa kiroho huo ubaba kamwe hautakaa uishe, kwamba amekufa au yupo hai. Ndiyo maana hata unaposoma biblia Waebrania wote walikuwa wanamuita Ibrahimu baba, kwa nini? Kwa sababu ubaba wa Ibrahimu hautakaa uishe japokuwa yeye amekufa lakini ubaba upo maana huo ubaba ni agano kati ya Mungu na Ibrahimu na huo ubaba utaendelea kuwepo milele. Mungu anapokupa baba wa kiroho unapaswa kujua kuwa huo wajibu hautakaa uishe kwa maana siku tutakapofika mbinguni ni Yeye baba wa kiroho atakayesimama kwa ajili yako.

Mfalme wa Amani: Yeye amebeba mambo yote yanayohusu amani, maana yake ni pamoja na mafanikio

Leo ni siku yako, furahi kwa maana Bwana ameamua ufurahi, hakuna kitakachokuzuia usifurahi kwa sababu Mungu ameamuru ufu...
31/05/2026

Leo ni siku yako, furahi kwa maana Bwana ameamua ufurahi, hakuna kitakachokuzuia usifurahi kwa sababu Mungu ameamuru ufurahi, katika Jina la Yesu naamuru ufurahi.

Mungu alimuamuru Yesu afe kwa ajili yetu ili mimi na wewe tupate kupatikana, ili wewe uweze kukombolewa, ulipitia maumivu mengi hata haujajua ulikuwa wapi, nguvu za giza, uchawi zilikuwepo ili kukuangamiza, lakini ile nguvu ya mbinguni ikapita kupitia mimi na wewe ukakombolewa, tafadhali usilisahau hilo, kwa maana k**a ukisahau usifikiri utaingia mbinguni; kwa sababu ilimfanya Yesu Kristo afe ili wewe ukombolewe. Yesu hayupo hapa duniani lakini nguvu ile ile iliyomfanya Yesu afe akaniamuru mimi nikombolewe na akanipa hiyo nguvu ili kukufanya wewe ukombolewe, ukisahau hilo kuzimu hakutakuacha salama. Tafadhali haijalishi nini kitatokea usisahau hilo.

Kwa nini Mungu alimtumia Yesu Kristo na siyo Adamu, Musa, wala Eliya, lakini kwa nini Yesu? kwa sababu ni mwana wa Mungu. Nawaona watu wengi wana uchezea wokovu na mpaka wakitambua hilo watakuwa wameshachelewa. Watu wengi wakati walipokuwa wanaokoka wanalia kwa machozi na kusema sitasahau wokovu Bwana, lakini baada ya kitambo kidogo wanasahau na wanaanza kumdhihaki yule aliyewakomboa.

Watu huwa hawaelewi nini maana ya kumdhihaki Roho Mtakatifu, tendo hilo ni la hatari sana zaidi ya kuua, aliyeua anaweza kusamehewa, anayefanya uasherati atasamehewa lakini kumdhihaki Roho Mtakatifu hakuna msamaha. Kwa nini? Kwa sababu wokovu ni kazi ya Roho Mtakatifu ndani ya mtu fulani. Mungu hamtumii malaika, la! Bali anamtumia mtu ambaye alichaguliwa kabla hajazaliwa ili abebe jukumu hilo ili anaposimama anaibeba ile nguvu yote na kuachia vizazi na vizazi, na wale wanayoipokea hiyo nguvu wanaenda na hiyo nguvu na wanaposahau walipotoka hapo ndipo hatari inaanzia. Roho ya mazoea itakupelekea wewe kumkufuru Roho Mtakatifu na hiyo roho ni hatari sana kwako.

OMBI: Bwana nisaidie nitoke katika roho ya mazoea maana nataka nifike mbinguni.

©️ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWI

NENO LA SADAKA Zaburi 100:1-5 “Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa ku...
31/05/2026

NENO LA SADAKA

Zaburi 100:1-5
“Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba; Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake; Kwa kuwa Bwana ndiye mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake vizazi na vizazi.”

Tumfanyie Bwana shangwe maana YEYE ni BABA kwetu. Tuingie nyumbani mwake kwa kushukuru maana ametutendea mema, ndiye anayetupa uwezo na nguvu katika maisha yetu, hajatuacha kamwe katika mwezi huu wa mfungo amekuwa pamoja nasi.

Mshukuru Mungu kwa kumtoa mwanaye mpendwa Yesu Kristo kwa ajili yetu lakini pia akatubariki; kwa maana Yeye ndiye anayetupa nguvu za kufanikiwa.

©️ MTUME ELIAKUNDA MWINGIRA

Hivi umeshawahi kujiuliza, k**a sio Yesu kutufia msalabani mimi na wewe tungekuwaje leo hii?Tunapaswa kumshukuru sana Mu...
31/05/2026

Hivi umeshawahi kujiuliza, k**a sio Yesu kutufia msalabani mimi na wewe tungekuwaje leo hii?Tunapaswa kumshukuru sana Mungu kwa kumtoa mwanaye mpendwa Yesu Kristo kwa ajili yetu.

Liko jambo jipya kwa ajili yako leo hii mwana wa Mungu, kuwa makini na msikivu utapokea haja ya moyo wako.

Leo ni siku ambayo utaona Utukufu wa Bwana na tarajia siku mpya na jambo jipya maana utamwona Mungu maana anakusudi na wewe.

Isaya 43:19a “Tazama, nitafanya jambo jipya; sasa litatokea; je, hamtalijua?"

© MTUME MARGETH ILOMO

Address

Mazizini
Dar Es Salaam
MAZIZINI

Telephone

+255622579421

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Mazizini posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Mazizini:

Share