Efatha Church Matunda

Efatha Church Matunda we connect people to Jesus Christ our saviour through media. He is the way the truth and the life

NENO LA SIKUNa, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira – Kanisa la EfathaTAREHE: 02/06/2026SOMO: YESU NDIYE MLANGOYohana...
02/06/2026

NENO LA SIKU
Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira – Kanisa la Efatha
TAREHE: 02/06/2026
SOMO: YESU NDIYE MLANGO
Yohana 10:9 “Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.”
Unaponena kwa lugha mpya ndipo unakuwa unaingia na unapomaliza kuchukua kile unachochukua katika Roho ndipo unatoka. Kutoka ni kwenda kuishi na kutenda katika ulimwengu ukiwa umebeba kile ulichopokea mbele zake.
Popote ulipo, iwe ni nyumbani, kazini au kwenye biashara yako, nguvu hiyo hukuwezesha kutawala, kushinda vikwazo na kumfukuza ibilisi katika eneo lako la mamlaka.
Huwezi kumiliki pasipo hiyo nguvu. K**a unataka kumiliki biashara kubwa na biashara hiyo ina ushindani mwingi hakikisha una hii nguvu ya Mungu kwa sababu wengine watatumia nguvu ya za giza, hivyo lazima watakutoa nje.
Unapohitaji jambo fulani hakikisha una hiyo mamlaka na tangaza kile unachofahamu ili uweze kumfukuza ibilisi.
Je! una nguvu ya kupambana na hao wanaomiliki upande wa pili? Hakikisha una Mungu anayemiliki dunia na vyote ili uweze kuingia na kutoka. See less

ZONE DAY.
02/06/2026

ZONE DAY.

NAIBARIKI JUMANNE YANGU. BWANA yu mbele yangu daima; Kwetu kutakuwa Kwema, hakutakuwa na magomvi wala magonjwa wala vifo...
02/06/2026

NAIBARIKI JUMANNE YANGU.
BWANA yu mbele yangu daima; Kwetu kutakuwa Kwema, hakutakuwa na magomvi wala magonjwa wala vifo, wala ukata.
Haleluya, YESU ni Mzuri. See less

NENO LA SIKUNa, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira – Kanisa la EfathaTAREHE: 01/06/2026SOMO: WAZALIWA WA MWEZI WA SI...
01/06/2026

NENO LA SIKU
Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira – Kanisa la Efatha
TAREHE: 01/06/2026
SOMO: WAZALIWA WA MWEZI WA SITA
Wazaliwa wa mwezi wa sita ni watu wenye mvuto wa kipekee, wenye upendo, uaminifu na uwezo wa kuvutia watu wengi. Mara nyingi hupata marafiki wengi na wana neema ya kufanikiwa katika biashara na shughuli mbalimbali za maisha.
Mungu ameahidi kuwarejeshea yote yaliyopotea na kuwafungulia milango ya baraka na mafanikio. Hata wanapopitia changamoto au hasara, wana neema ya kuinuka tena na kurejesha walichopoteza kwa muda mfupi. Hivyo wanapaswa kumtumaini Mungu na kuepuka kulipa kisasi.
Yoeli 2:25 “Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige…”
Jambo la muhimu kwao ni kuheshimu wazazi na watumishi wa Mungu. Heshima na utiifu huwalinda katika kibali walichopewa na Mungu na huwafungulia milango ya mafanikio na baraka katika maisha yao.
Waebrania 7:7 “Wala haikanushiki kabisa kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa.” See less

HERI YA MWEZI MPYA JUNIKaribu mwezi wa Juni! Tunamshukuru Mungu kwa kutuvusha salama na kutuingiza katika mwezi mpya. Mw...
01/06/2026

HERI YA MWEZI MPYA JUNI
Karibu mwezi wa Juni! Tunamshukuru Mungu kwa kutuvusha salama na kutuingiza katika mwezi mpya.
Mwezi huu wa Juni ni Mwezi Wako wa Kudunda, Kufanikiwa, Kustawi, Kushinda na Kuvuna, hivyo Ninaamuru Muujiza wako ukujie sasa, ustawi wako ukujie sasa, Mafanikio yako yakujie sasa, ili upate kumchezea Yesu.
Mwezi Huu utapokea Muujiza wako, Uponyaji wako, Ukombozi wako, Mafanikio yako na Utajiri wako katika Jina la Yesu. See less

JUMATATU YANGU IMEBARIKIWA NA BWANAMimi nitailinda Imani yangu kwa maana  Mimi ni wa juu, Kila nifanyalo litastawi, Mimi...
01/06/2026

JUMATATU YANGU IMEBARIKIWA NA BWANA

Mimi nitailinda Imani yangu kwa maana Mimi ni wa juu, Kila nifanyalo litastawi, Mimi ni Bora na ninalindwa na Baba yangu

Asante Yesu kwa kunipenda kwanza.

Mwovu hataweza kukugusa mpaka pale utakapoilinda imani yako, ni lazima ujue umeipataje imani yako, watu wengi wanalinda ...
31/05/2026

Mwovu hataweza kukugusa mpaka pale utakapoilinda imani yako, ni lazima ujue umeipataje imani yako, watu wengi wanalinda magari yao, nyumba zao, wake au watoto wao lakini hawalindi imani zao, uko sawa wewe? Linda imani yako kuliko chochote ukilindacho maana ndipo ilipo chemchemi ya uzima wako, linda yale yaliyofanya wewe uitwe mlokole na uwe na nguvu za Mungu linda hicho usiku na mchana.

Waefeso 4:27 “wala msimpe Ibilisi nafasi.”

Wala msimpe Ibilisi nafasi.” tambua kuwa ukimpa tu ibilisi nafasi amekumaliza, unawezaje kumzuia ibilisi asipate nafasi kwako? Kwa kulinda imani yako.

Warumi 8:28 “ Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.”

Watu gani wanampenda? Ni hao wenye imani, hauwezi kumpendeza Mungu k**a hauna imani na imani ni kujua kuwa ulikuwa mwenye dhambi na sasa umeokoka na Je! umeokokaje? Hicho ndicho unapaswa kukilinda. Mungu anafanya kazi na hao wanaompenda ili nini? Ili awape mema.

TANGAZO: Nakutangazia Mungu akakupe mema.

Ukishajua wewe ni nani na uko tayari kufanya kazi na YEYE; ndipo anakuwa tayari kukupa wewe mali.

1 Petro 2:9 “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;”

Lazima uelewe kuwa wewe umechaguliwa na siyo umekataliwa, la! Hata watu wakikusengenya wala usiumie bali jipongeze kwa maana wameona kuna kitu cha tofauti kwako. Mwana wa Mungu wewe umeandaliwa kumiliki yaliyo ya Bwana.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Waamini walio wengi hawaelewi wokovu wao; kwa nini wameokoka? Ni k**a vile umemuajiri mtu katika nafasi fulani na huyo m...
31/05/2026

Waamini walio wengi hawaelewi wokovu wao; kwa nini wameokoka? Ni k**a vile umemuajiri mtu katika nafasi fulani na huyo mtu haelewi wajibu wa hiyo nafasi, ingawa anafanya kazi kila siku. Hiki ndicho kinachowakuta watu wengi ambao wameokoka; ibilisi anawapiga huku na kule maana hawaelewi nafasi zao, kwa nini wameokoka.

1 Yohana 5:18 “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.”

Yohana 16:8 “Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu. Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi;”

Dhambi ni nini? Ni kutokumwamini YEYE, tendo lolote linaloitwa dhambi ni matokeo ya kutokujua chanzo cha imani. Ukiwa na imani hata dhambi yoyote itakayokutokea kwa sababu una imani ni rahisi kuiondoa hiyo dhambi pasipo mtu yeyote kuja kukwambie tubu maana unajua umekosea, lakini k**a haujui utaendelea kuitenda hiyo dhambi.

Biblia inasema “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.” Ilinde imani yako kuliko unavyoilinda afya, fedha zako au kuliko kitu kingine unachokijua kwa sababu imani yako ndiyo kila kitu. Ibilisi hana haja na nyumba yako wala fedha zako maana anazo nyingi, bali anashida na imani yako kuliko kitu kingine chochote kile, maana akifanikiwa kuitoa imani yako amekushinda wewe. Yesu alikuja na akafa msalabani kwa ajili yetu, usisahau hilo.

1 Yohana 5:18 “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.”

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Nay...
31/05/2026

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”

Kwa ajili yetu, na kwa faida yetu na kwa ajili ya maisha yetu mtoto amezaliwa, siyo kwa ajili ya Mungu, la! bali ni kwa ajili yetu, usisahau hilo. Watu wanaishi maisha haya ya wokovu k**a vile kamwe hawatakaa wafe, kwamba wataishi duniani milele, la! Lazima ufe, labda tu Yesu aje mapema, lakini k**a sivyo kufa utakufa tu, lakini lazima uelewe unakufaje, kwamba unakufa na utukufu au laana.

Biblia inasema “Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani” tulipewa mtoto mwanaume ambaye alikuwa na majina manne:-

Mshauri wa ajabu; akikushauri, akikusaidia na kukuongoza wewe, akikunyoosha ili uende kule Mungu anataka uwe.

Mungu mwenye nguvu; hii ina maana kuwa kuna miungu mingine lakini Mungu huyu ni Mungu mwenye nguvu, kwa nini mwenye nguvu? Ili kukusababisha wewe uweze kushinda, ili aweze kushinda miungu mingine yote kwa ajili yako. Mungu anapokupa mtu kusimama kwa ajili yako kumbuka anampa huo uweza ili akukomboe kutoka kwenye miungu mingine.

Baba wa milele: hii ina maana kuwa ubaba wake hauna mwisho, Mungu anapokupa baba wa kiroho huo ubaba kamwe hautakaa uishe, kwamba amekufa au yupo hai. Ndiyo maana hata unaposoma biblia Waebrania wote walikuwa wanamuita Ibrahimu baba, kwa nini? Kwa sababu ubaba wa Ibrahimu hautakaa uishe japokuwa yeye amekufa lakini ubaba upo maana huo ubaba ni agano kati ya Mungu na Ibrahimu na huo ubaba utaendelea kuwepo milele. Mungu anapokupa baba wa kiroho unapaswa kujua kuwa huo wajibu hautakaa uishe kwa maana siku tutakapofika mbinguni ni Yeye baba wa kiroho atakayesimama kwa ajili yako.

Mfalme wa Amani: Yeye amebeba mambo yote yanayohusu amani, maana yake ni pamoja na mafanikio yako. Yesu alizaliwa katika ushindi wa namna hii akibeba majina haya, kwa nini? Kwa sababu alikuwa kwa ajili yetu.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa...
31/05/2026

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

Baba anabeba mizigo yote inayohusu watoto, maumivu yote ya watoto, huu ndiyo ubaba; anasimama kwa ajili ya familia yake. Yesu aliye baba wa milele kwetu, alichukua mizigo yetu, maumivu yetu na changamoto zetu zote na akafa nazo msalabani na huu ndiyo ubaba.

Wakolosai 2:14-15 “akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutush*taki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani; akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.”

Yesu k**a baba aliyabeba haya yote kwa ajili yetu mimi na wewe, halafu kuna mtu anasahau kile Yesu Kristo amefanya pale msalabani? Aliyoyafanya Yesu ni kwa ajili yetu.

Wakolosai 2:13 “Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;”
Tulikuwa tumekufa lakini kwa ajili yake leo hii tupo hai.

Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Pasipo Imani hauwezi kumpendeza Mungu, k**a haumpendezi YEYE inamaana kuwa unamkosea; utajuaje hivyo? Kwa maana Biblia inasema “huwapa thawabu wale wamtafutao.”

Wale wanaompendeza Mungu YEYE huwapa mahitaji yao, hii ina maana kuwa wale wasiyompendeza wanateseka na kuzunguka sana, wanaishi na njaa na katika uhitaji ingawa wamezaliwa mara ya pili (wameokoka) kwa nini wanaishi hivyo? Ni kwa sababu hawampendezi YEYE.

Biblia inasema “Kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Hivyo kwanza unapaswa kuelewa kuwa YEYE yupo hai, anakuona na kukutazama, hivyo atatazama kila unachofanya, kile unachokifanya kikimpendeza YEYE anakupa mahitaji ili kukufanya wewe uende mbele, k**a ukifanya vizuri anakupa uzuri ili aweze kukushawishi wewe uende mbele. Vile unavyofanya vizuri inamfurahisha YEYE na YEYE akifurahi anakupa wewe zaidi na zaidi na ndivyo unavyozidi kuwa na kila kitu katika maisha yako, yaani (unakuwa tajiri).

Mwanamke muombe Mungu akupe kuolewa na mwanaume mwenye akili nzuri maana mtu mwenye akili nzuri mara zote anatafuta kumpendeza Mungu. Anaweza kuwa leo hii hana kitu lakini k**a akili yake ni nzuri basi utajua kuwa huyu ana uhakika na anajua wapi anaenda. Mwanaume mwenye imani hata k**a ataanguka lakini Bwana Yesu atamuinua na atampa kusonga mbele.

Wewe mama muangalie mumeo Je! Akianguka anainuka? Ukimuona anaamka na kwenda kanisani usiangalie alichokosea lakini angalia nia aliyonayo, biblia inasema “ataanguka mara saba lakini atainuka,” mwanamke usimkatishe mumeo tamaa maana ana safari na atafika. Mimi k**a baba yao nimeamua kusimama na wababa na sitakaa kimya mpaka wafike wanakotakiwa kufika.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Matunda posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share