02/06/2026
NENO LA SIKU
Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira – Kanisa la Efatha
TAREHE: 02/06/2026
SOMO: YESU NDIYE MLANGO
Yohana 10:9 “Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.”
Unaponena kwa lugha mpya ndipo unakuwa unaingia na unapomaliza kuchukua kile unachochukua katika Roho ndipo unatoka. Kutoka ni kwenda kuishi na kutenda katika ulimwengu ukiwa umebeba kile ulichopokea mbele zake.
Popote ulipo, iwe ni nyumbani, kazini au kwenye biashara yako, nguvu hiyo hukuwezesha kutawala, kushinda vikwazo na kumfukuza ibilisi katika eneo lako la mamlaka.
Huwezi kumiliki pasipo hiyo nguvu. K**a unataka kumiliki biashara kubwa na biashara hiyo ina ushindani mwingi hakikisha una hii nguvu ya Mungu kwa sababu wengine watatumia nguvu ya za giza, hivyo lazima watakutoa nje.
Unapohitaji jambo fulani hakikisha una hiyo mamlaka na tangaza kile unachofahamu ili uweze kumfukuza ibilisi.
Je! una nguvu ya kupambana na hao wanaomiliki upande wa pili? Hakikisha una Mungu anayemiliki dunia na vyote ili uweze kuingia na kutoka. See less