04/09/2026
MCHUNGAJI ; LABANI LUTUFYA
SOMO: MAANDALIZI YA KUKUTANA NA BWANA KUPITIA KUSANYIKO LA WANA WA MUNGU
-kukusanyika ni agizo la Mungu, Mungu anapowakusanya watoto wake anakuwa na NENO , agizo kwa ajili yao
Mungu anapotaka tukusanyike ni kwa faida yetu maana ana jambo JIPYA kwa ajili yetu
SWALI: Je Mungu anapokuita kwenye KUSANYIKO lake UNAKUWA umejiandaa kwa namna gani? Hakuna msafiri ambaye haandai safari yake na sisi tuna safari yetu ya kwenda mbele za Baba yetu wa Mbinguni ni kwa namna gani tumejiandaa ili turudi na ushuda? Kila anayesafiri anaporudi baada ya safari yake anakuwa na ushuhuda .
Mithali 16:1
Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu;
Bali jawabu la ulimi hutoka kwa BWANA.
Jukumu la kuandaa moyo wako ili Bwana aweze kukupa HAZINA zake ni la kwako mwenyewe si la mchungaji au mtumishi yoyote qnayesimama mbele Yako . Mtumishi wa Mungu inawezekana akanyimwa kufunuliwa Yale unayopita nayo ila wewe unajua yake unayoyapitia na Mungu mwenyewe,huu ni wakati wa kumwambia Baba ninaenda mahali AMBAPO unasema kasema na mimi kuhusu maisha yangu naenda mahali unapojibu kanijibu mimi kuhusu mambo yangu ,uandae moyo wako vizuri kupokea matakatifu ya Mungu aliye Baba Yako
Kutoka 19:10
BWANA akamwambia Musa, Enenda kwa watu hawa, ukawatakase leo na kesho, wakazifue nguo zao,
-usijishughurishe na mambo mengi katika KIPINDI HIKI CHA maandalizi kwa ajili ya KUSANYIKO yatakuchelewesha andaa moyo wako .
Pata muda wa kutafakari je ni yepi yanayokuhmiza ,ni yepi yanayokusononesha ni ugonjwa ,ni KUKOSA kipato,ni ndoa ni WATOTO nenda mbele za Baba MWAMBIE Baba mwaka huu ninapoenda mahali pale AMBAPO Kuna uwepo wako mkubwa najiungamanisha na madhabahu ile ili na mimi nirudi na ushuhuda wangu .