07/05/2026
๐๐ผ๐๐๐๐ผ ๐๐ผ ๐ฟ๐๐ผ๐๐ฝ๐
๐
๐ ๐ ๐ช๐ฃ๐ ๐ฉ๐ค๐๐๐ช๐ฉ๐ ๐ฎ๐ค๐ฎ๐ค๐ฉ๐ ๐ ๐๐ฉ๐ ๐ฎ๐ ๐๐๐ ๐ค๐จ๐ ๐ฃ๐ ๐ฟ๐๐๐ข๐๐?
Ungana nami tutafakari pamoja maandiko matakatifu;
Makosa ni vitendo vinavyotokea kwasababu ya Udhaifu wa kibinaadamu/kwa kutojua na wakati mwingine kwa kutokuwa makini,
Mfano mzuri ni huu wa habari y Martha:
Luka 10:40-42
[40]Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie.
[41]Bwana akajibu akamwambia, Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi;
[42]lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa.
Wakati wenzake wanasikiliza hekima na maarifa ya ufalme wa mbinguni, yeye Martha alikuwa anahangaika kuandaa chakula kwa ajili ya wageni waliomtembelea [Yesu na Watu wake].
Martha akazipa kipaumbele kazi zake akasahau kwamba kilicho muhimu ni kutambua siri za ufalme wa Mungu uletao uzima.
Hii haikuwa dhambi ya moja kwa moja, bali ni kosa la kushindwa kusoma alama za majira na nyakati. Alishinda kutambua nini afanye na kwa wakati gani?
Dhambi ni kukosa kwa makusudi huku ukijua sio sahihi na bado unatenda.
Mfano watu waliofanya dhambi ni Adam na Eva walijua fika kwamba Mungu aliwakataza wasile wala wasiyaguse matunda ya mti ulio katikati ya bustani lakini wao wakala,
Mfano mwingine ni Daudi kuzini na Bath-sheba mke wa Uria na kupanga mbinu za kumuua mume wake ili kuuficha uovu wake, hii ni Dhambi ya makusudi.
Kitendo cha kutambua kwamba hairuhusiwi kufanya hivi na bado ukafanya hiyo ndiyo inaitwa kutenda dhambi.
Ni kukusudia, kudhamilia kufanya jambo fulani ambalo kiuhalisia unatambua kwamba si haki.
Mwisho ni Uovu.
Uovu ni ile dhambi inayojirudia mara kwa mara kwenye maisha ya Mtu na kuwa k**a tabia ya kawaida.
Mfano Mtu mwongo, atongopa leo kwenye neno hili kesho lingine na siku zingine hivyo hivyo...
Mtu mwizi leo atamwibia huyu, kesho yule na siku zingine wizi Utaendelea
Kitendo cha dhambi moja kujirudia rudia ndicho kinazaa uovu. Uovu ni dhambi iliyokomaa na kuzoeleka kwenye maisha ya Mtu kiasi cha kuifanya mara kwa mara.
Lakini katika yote Mungu ameachilia neema na msamaha kwa yeyote anayetambua, kukiri kutenda dhambi na kutubu kweli k**a maandiko matakatifu yasemavyo hapa chini;
1 Yohana 1:8-9
[8]Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.
[9]Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.
Ni kweli tunatenda dhambi, lakini toba inatupa nafasi nyingine ya kumrudia Mungu na kufanyika wana wake tena, kwa ubora uleule akiturejesha kwenye nafasi ile tuliyoipoteza hapo awali.
Mungu atubariki sote.
๐ฌ๐๐
๐๐๐๐ ๐๐๐๐๐๐๐๐๐ ๐๐๐๐๐๐๐ ๐๐๐๐ ๐ญ๐๐๐๐๐๐๐ (๐ด๐๐๐๐๐ ๐๐ ๐ฉ๐๐๐๐๐) ๐๐๐๐๐๐๐๐ ๐๐๐๐๐๐
๐๐๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐ ๐๐ ๐ด๐๐๐๐ ๐๐๐๐๐ ๐๐๐๐๐๐๐.
ยฎ๏ธ ๐ณ๐๐๐๐๐๐๐ ๐ฎ๐๐๐๐๐
๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐@๐๐๐๐๐.๐๐๐
+๐๐๐ ๐๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐