Abel Molla

Abel  Molla Ukurasa huu ni maalumu kabisa kwa ajili ya kupata habari za hudumu, mafundisho ya neno la Mungu, na mambo mengine yanayohusika ufalme wa mbinguni.

"Uchungu ni mlango mkubwa sana unaweza kupoteza hamu na nguvu ya kumshukuru Mungu, jitahidi uushinde uchungu kwa damu ya...
09/12/2023

"Uchungu ni mlango mkubwa sana unaweza kupoteza hamu na nguvu ya kumshukuru Mungu, jitahidi uushinde uchungu kwa damu ya Yesu na faraja ya neno la Mungu ili upate hamu na nguvu ya kumshukuru Mungu"

"Tuuimbeje wimbo wa Bwana Katika nchi ya ugeni?" ZABURI 137:4.

# Moyo wa shukrani #

29/12/2022

"The believer can never be more efficient in his Christian experience than he is in his understanding of the scriptures"

30/11/2022

"PENDA KUSOMA UPATE MAARIFA"

"Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu" YOHANA 16:24.

1.Kuna uhusiano katika ya kupata unachokiomba kwa Mungu na "KUOMBA KWA JINA LA YESU"

2. Lakini pia, Kuna uhusiano kati ya "KUWA NA FURAHA TIMILIFU" na "KUPATA UNACHOOMBA KWA MUNGU"

-Wapo watu wengi sana ni waombaji wazuri lakini hawana "FURAHA TIMILIFU NDANI YAO" (ni mwombaji lakini ndani ana malalamiko (Habakuki 1:1...), ndani yake kumejaa huzuni iletayo mauti, n.k,
UKIFUATILIA KWA UNDANI SANA UTAGUNDUA WAPO HIVYO NI KWA SABABU KUNA MAMBO WANAMWOMBA MUNGU LAKINI MPAKA SASA HAWAJAPATA WANACHOMWOMBA MUNGU. Hiyo hali imeondoa kabisa furaha timilifu ndani yao (utamwona kwa nje anacheka Ila moyoni hana furaha, ukitaka kujua hana furaha timilifu ndani yake sikiliza mazungumzo yake; ukimuuliza unaendeleaje? Utasikia ninaendelea hivyo hivyo tu, n.k.

-Kuomba kwa jina la Yesu ni zaidi ya KUOMBA, "KUOMBA kwa JINA la YESU ni kuomba kwa Imani, ukitumia jina la Yesu ukijua ndani ya hilo jina kuna nguvu ambayo ina uwezo wa kuleta majibu ya maombi yako"

-Kila wakati ukiwa unaomba hivyo utakuwa unapata mambo makubwa mawili;
1. Utakuwa umelitumia jina la Yesu kwa Imani, matokeo yake utapata furaha timilifu ndani hata k**a haujapata unachokiomba ila IMANI itakupa tumaini la kupata hicho kitu.
2. Lakini pia, nguvu iliyopo ndani ya jina la Yesu itafanya upate majibu ya maombi yako maana ndani jina la Yesu kuna nguvu endapo jina la Yesu limetumika kwa IMANI.

Siku njema.

19/11/2022

"Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni"
Mathayo 5:16

26/10/2022

"Ukizimia siku ya taabu, Nguvu zako ni chache"

Mithali 24:10.

Penda kusama upate maarifa:"Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika k**a kond...
30/06/2022

Penda kusama upate maarifa:

"Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika k**a kondoo wasio na mchungaji. Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake"
MATHAYO 9:36-38

-Watenda kazi wanahitaji sana shambani mwa Bwana (PATA MUDA UTAFAKARI NI ENEO GANI MUNGU AMEKUITA UKAITENDE KAZI YAKE)

-Kisha jiulize maswali yafuatayo;
1. JE, UMESHAANZA KUITENDA KAZI SHAMBANI MWA BWANA?
2. JE, MUNGU AKIKUTAKA UMPATIE MATUNDA YA UTENDAJI WAKO, UTAMPATIA KITU GANI?

21/05/2022

"As you are celebrating the years that you have been on the Earth's surface, THINK HOW FAR HAVE YOU MOVED TOWARD FULFILLING THE PURPOSE OF YOUR BEING"

15/03/2022

"MUNGU AKIKUJALIA NEEMA YA KUISHI MIAKA 20 ZAIDI TANGU LEO, MUNGU ATAJIVUNIA NINI KUTOKA KWAKO KWA AJILI YA HIYO MIAKA ULIYOISHI"

"Mnawaza nini juu ya Bwana...? NAHUMU 1:9

"Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, TAZAMA, MIAKA MITATU HII NAJA NIKITAFUTA MATUNDA JUU YA MTINI HUU, NISIPATE KITU, UUKATE, mbona hata nchi unaiharibu? Akajibu akamwambia, Bwana, UUACHE MWAKA HUU NAO, hata niupalilie, niutilie samadi; nao ukizaa matunda baadaye, vema! LA, USIPOZAA, NDIPO UUKATE. LUKA13:7-9.

-Mtunzaji wa shamba la mizabibu ALIMWOMBA YESU MWAKA MMOJA TU asipopata matunda ndipo aukate.

NB: USIFIKIRI KWA AJILI YA MUDA ULIOPOTEA (IWE ULIUPOTEZA KWA KUKUSUDIA AU KWA KUTOKUKUSUDIA), FIKIRI KWA AJILI YA BWANA KUANZIA LEO.

ESTABLISH FUCUS FROM TODAY.

13/03/2022

"Tough time come and tough time goes"
"Nyakati ngumu huja, and nyakati ngumu huenda (hupita)"

"Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; MAANA NIMEJIFUNZA KUWA RADHI NA HALI YOYOTE NILIYO NAYO. Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, NIMEFUNDISHWA KUSHIBA NA KUONA NJAA, KUWA NA VIINGI NA KUPUNGUKIWA. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu" WAFILIPI 4:11-13

NB: "STRENGTH UP YOUR FOCUS TOWARDS THE WILL OF GOD IN YOUR LIFE"

11/03/2022

Watu hawachukii au hawapendi unachokifanya Ila wengi sana wanachukia na hawapendi unachokifanya kwa sababu hawajaona faida iliyopo ndani ya kile unachokifanya, siku wakiona faida inayotokana na kile unachokifanya watakupata mkono wa kuume wa shirika (wataacha kukuchukia na watakupa ushirikiano).

NB: Uponaanza jambo si kila mtu atakuelewa na si kila mtu ataona faida ya hilo jambo wakati ndipo linaanza.

"TENA WALIPOKWISHA KUIJUA ILE NEEMA NILIYOPEWA; Yakobo, na Kefa, na Yohana, wenye sifa kuwa ni nguzo, WALINIPA MIMI NA BARNABA MKONO WA KUUME WA SHIRIKA; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara" WAGALATIA 2:9.

BE FOCUSED FROM THE BEGINNING.

26/11/2021

Na hata ijapokuwa binadamu angeinuka akuwinde, na kuitafuta nafsi yako, hiyo nafsi ya bwana wangu itafungwa katika furushi ya uhai pamoja na Bwana, Mungu wako; na nafsi za adui zako ndizo atakazozitupa nje, k**a kutoka kati ya teo.
1Samweli 25:29

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255763438164

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Abel Molla posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Abel Molla:

Share