22/09/2019
SAFARI YA KUMILIKI
Neno la Msingi:
Kumbukumbu 2:24
“Ondokeni, mshike safari yenu, mvuke bonde la Arnoni; tazama, nimemtia Sihoni Mwamori mfalme wa Heshboni mkononi mwako, na nchi yake; anzeni kuimiliki, mshindane naye katika mapigano.
Watu wengi hawaelewi juu ya safari ya kumiliki inavyokuwa. Wanafikiri baada ya kuambiwa juu ya ahadi fulani ya mafanikio au unabii fulani wa mafanikio basi kumiliki hayo kutakuja "automatic" bila kutoa jasho lolote wala jitihada zozote binafsi, huko ni kujidanganya. Safari ya mafanikio ni Safari ndefu ya kuvuka mabonde, kupanda na kushuka vilima na milima. Hakuna kitu chochote ya kumiliki ambacho utakipokea kwa mteremko hata k**a neno la Mungu limesema kuhusiana na hicho.
Kumbukumbu 2:1-3
“Ndipo tukageuka, tukashika safari yetu kwenda jangwani kwa njia ya Bahari ya Shamu, k**a alivyoniambia BWANA; tukawa kuizunguka milima ya Seiri siku nyingi. BWANA akanena, akaniambia, Mlivyouzunguka mlima huu vyatosha; geukeni upande wa kaskazini.”
MAANA YA KUMILIKI
Kumiliki ni kutawala vitu fulani k**a nyumba, mashamba, mali n.k.
Mmiliki ni mtu anayemiliki vitu k**a nyumba, mashamba, mali n.k.
Mithali 8:15-16
“Kwa msaada wangu wafalme humiliki, Na wakuu wanahukumu haki. Kwa msaada wangu wakuu hutawala, Na waungwana, naam, waamuzi wote wa dunia.”
Kumbukumbu 1:8
“Angalieni, nimewawekea nchi mbele yenu, ingieni mkaimiliki nchi BWANA aliyowaapia baba zenu, Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kwamba atawapa na uzao wao baada yao.”
SAFARI YA KUMILIKI
Safari ya kumiliki ina mambo mengi ya kuyafanya na kufuatilia. Ili uone kumiliki kunafanyika katika maisha yako lazima ufahamu kwamba kumiliki ni Safari. Safari inachukua muda, umbali, nguvu, uelekeo, utofauti wa mazingira, hali ya hewa, uono wako n.k.
Kumbukumbu 2:24-25
“Ondokeni, mshike safari yenu, mvuke bonde la Arnoni; tazama, nimemtia Sihoni Mwamori mfalme wa Heshboni mkononi mwako, na nchi yake; anzeni kuimiliki, mshindane naye katika mapigano. Hivi leo nitaanza mimi kutia utisho wako na kuhofiwa kwako juu ya watu walio chini ya mbingu kila mahali, watakaosikia uvumi wako, na kutetemeka, na kuingiwa na uchungu kwa sababu yako.”
I. Ahadi
Biblia ni kitabu kilichojaa ahadi za Mungu kwetu watoto wake. Mungu ameahidi kutumilikisha mambo mengi katika maisha yetu. Uzuri wa Mungu hasemi uongo kile ambacho amekisema at akitimize bila shaka. Mungu alitoa ahadi juu ya Taifa la Israeli la kumiliki nchi NJEMA, PANA iliyojaa MAZIWA na ASALI. Lakini katika hiyo nchi kulikuwa na watu wanaoimiliki. Mataifa makubwa ambayo ukilinganisha na Taifa la Israeli wal ionekane ni watu wasio na uwezo tens walikuwa wachache.
Kutoka 3:7-8
“BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.”
II. Mipango
Ahadi yoyote lazima iambatane na mipango mikakati wa kutaka kutimia kwa ahadi hiyo. Mpango unasaidia kutembea katika malengo ambayo umejiwekea. Macho yako yanatakiwa kuangalia mpango ambao huko mbele yako.
Mithali 16:1, 3
“Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa BWANA.
Mkabidhi BWANA kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika.”
Usiache macho yako kuangalia mpango wako ulionao. Usiruhusu kutoka katika lengo lako ambalo unaloliendea. Uwe king'ang'anizi katika kile ulichokipanga.
Mithali 4:25
“Macho yako yatazame mbele, Na kope zako zitazame mbele yako sawasawa.”
III. Ondoka/Chukua hatua
Kuondoka ni kuchukua hatua ya kutoka hapo ulipo na kwenda kwenye hatua nyingine kuelekea ndoto au mpango wako. Hauwezi kumiliki ikiwa hautakubali mabadiliko chanya katika maisha yako.
Wafilipi 2:13
“Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.”
IV. Shika Safari
Kushika Safari ni kuendelea kutembea katika mpango wako wa kumiliki bila kuangalia mazingira yanayokuzunguka. Mazingira yanaweza kukukatisha tamaa lakini wewe endelea kushika Safari yako.
Mwanzo 13:17-18
“Ondoka, ukatembee katika nchi hii katika mapana yake, na marefu yake, maana nitakupa wewe nchi hiyo. Basi Abramu akajongeza hema yake, akaja akakaa kwenye mialoni ya Mamre, nayo ni miti iliyoko Hebroni, akamjengea BWANA madhabahu huko.”
Waebrania 11:8-10
“Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, k**a katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.”
V. Vuka Bonde
Kuna wakati wa kuvuka bonde. Siyo kila wakati ni tambarare kwingine kuna bonde la kulivuka. Unapoelekea kumiliki kuna wakati unatakiwa uvuke bonde. Bonde inaweza ikawa ni kukosa mtaji, Ada ya shule, kukosa msaada kwa watu wako wa karibu, kuumwa au kuuguliwa n.k.
Zaburi 23:4
“Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.”
VI. Mtambue Adui aliyek**ata nchi yako
Lazima uweze kumtambua Adui yako. Yule ambaye ameshikilia Uchumi au Afya yako. Adui ambaye amekamta kitu chako cha kukimiliki.
Mathayo 13:24-25
“Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake; lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.”
VII. Shindana na Adui
Ukishamfahamu adui hautakiwi kumchekea Bali ushindane naye katika mapigano. Unajua ni roho ya umaskini au roho ya kukurudisha nyuma kimaendeleo au ni roho ya chuma ulete ni lazima ushindane nayo hadi kieleweke.
Luka 11:21-22
“Mtu mwenye nguvu aliyejifunga silaha zake, alindapo nyumba yake, vitu vyake vi salama; lakini mtu mwenye nguvu kuliko yeye atakapomwendea na kumshinda, amnyang’anya silaha zake zote alizokuwa akizitegemea, na kuyagawanya mateka yake.”
VIII. Anza kumiliki
Kumiliki kunaanzia ndani ya nafsi yako. Unaanza kuona mafanikio, baraka, ushindi ndani ya nafsi kabla ya kuona kiuhalisia. Maadui unawaona wamekwishaachia baraka zako.
Mithali 23:7
“Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. Akuambia, Haya, kula, kunywa; Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.”
Hesabu 14:6-9
“Na Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao; wakanena na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu. Ikiwa BWANA anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali. Lakini msimwasi BWANA, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye BWANA yu pamoja nasi; msiwaogope.”
Bishop Emmanuel Mbagwile (+255 715 136868)