18/06/2026
English/Swahili
Picha hizi zinatukumbusha hatua ya tatu ya ujenzi wa jengo la Kanisa la Mji wa Mashujaa (DCI Dar) jijini Dar es Salaam miaka mitatu iliyopita.
Kile kilichoonekana kuwa ndoto ya mbali kilianza kuchukua sura na kuvutia. Tulijenga jengo hili katikati ya changamoto, majaribu, na wakati mwingine maumivu makali, lakini kwa rehema kuu za Mungu, jengo hili limechukua sura mpya hapa Goba, hatua chache tu kutoka barabara ya lami. Huu ni ushahidi wa mkono wa Mungu.
Zaburi 118:23 "Hii ni kazi yake Mwenyezi Mungu; nayo ni ya ajabu sana kwetu."
These photos remind us of the third phase of the City of Heroes (DCI Dar) project in Dar es Salaam three years ago. What once seemed like a distant dream began to take shape and command beauty. We built this structure through trials, setbacks, and hardships, yet by the sheer grace of God, we now stand in our own church building here in Goba, just a few meters from the tarmac. This is a true testament to God’s faithfulness.
Psalms 118:23 The Message Bible - "This is God's work. We rub our eyes - we can hardly believe it."